TANZANIA NA INDIA KUJA NA MAPINDUZI MAKUBWA KWENYE UTAMADUNI

June 17, 2022

 


Na John Mapepele.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema  kuwa Tanzania na India zinakwenda kupitia na kuboresha mikataba ya mashirikiano ya awali  kwenye eneo la Utamaduni na Sanaa iliyojiwekea  mwaka 1984 ili  kuiboresha iweze kuleta mapinduzi makubwa na ya haraka kwa faida ya pande zote.

Mhe, Mchengerwa ameyasema haya leo Juni 17, 2022 akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Hassan Abbasi wakati alipotembelewa ofisini kwake na Balozi wa India nchini Mhe.  Binaya Srikanta Pradhan na kufanya mazungumzo ya kuendeleza mashirikiano kwenye sekta hizo.

Aidha, amesema mambo mengi yalikubalika   baina ya nchi zote mbili hususan  kuendelea kwa tamaduni  pia  kumekuwa na mambo mengi ambayo yameandikwa ambayo kuna haja ya kufanya mapitio.


Ameongeza  kuwa katika maongezi hao  wamekubaliana kuwa  na kituo maalum cha kuandaa filamu ambacho kitatumika kwa nchi za Afrika mashariki ambapo  baadhi ya wasanii kutoka India  watashiriki moja kwa moja kwenye eneo hili.


Pia amesema eneo jingine  kubwa ambalo wamejadili  ni kuhusu umuhimu wa  wa kufanya mkutano mkubwa kuhusu bahari ya Hindi ambao utajumuisha nchi hizo  mbili.

Amesema tamasha hilo litasaidia kuonyesha historia za nchi zote zilikotoka zilipo na zinakoelekea

Aidha, amesema  bahari ya Hindi imebeba historia kubwa ambayo tayari watafiti kutokana  India na Tanzania wamefanya utafiti hivyo ni muhimu  kuutumia utafiti huo kwa faida ya nchi zote.

Naye  Mtaalam  na Mtafiti  Arindam Mukherjee ambaye ameambatana  na Mhe. Balozi amefafanua kuwa tafiti zinaonesha kuwa  Bahari ya Hindi ilikuws ikitumika kwa miaka mingi kufanya biashara  ambapo yapo baadhi ya maeneo ambayo yamethibitika yamekuwa yakikaliwa na waswahili na pia kumekuwa na mfanano wa maneno ya kiswahili.

SOUTHAMPTON KUWANOA MAKOCHA WA TANZANIA -WAZIRI MCHENGERWA

June 17, 2022

Na John Mapepele.


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema  Tanzania inakwenda  kushirikiana na klabu ya Soka ya Southampton  kuwandaa makocha wa soka ili wawe kwenye kiwango cha kimataifa.

Mhe. Mchengerwa amesema haya leo juni 17, 2022 ofisini kwake akiambatana na Katibu Mkuu wa Wizara yake, Dk. Hassan Abbasi wakati alipokutana na ujumbe wa Klabu hiyo ulioongozwa na Afisa Biashara  Mkuu wa Klabu hiyo David Thomas. 


Amesema dhamira ya Serikali ni kuona kuwa michezo mbalimbali inasimamiwa  kisayansi ili kuleta tija ikiwa ni pamoja na kuwa na makocha ambao watasaidia kufundisha  timu za micherzo ili kufuka kwenye kiwango cha kimataifa.


Katika kikao hicho  wamekubalina kuwa Timu ya soka  ya ya Wanawake chini ya Miaka 17 (Serengeti Girls)  itakwenda kupatiwa mafunzo maalum   kwenye Klabu hiyo ikiwa ni maandalizi ya kwenda kwenye  mashindano ya kombe la dunia nchini India.

Katika tukio hilo ujumbe wa timu hiyo ulimzawadia jezi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe Samia Suluhu Hassan ikiwa ni kuthamini mchango wake mkubwa anaoutoa kuendeleza michezo nchini.

MNDOLWA AONGOZA MAPITIO YA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO WA TUME YA TAIFAYA UMWAGILIAJI

June 17, 2022

 

MkurugenziMkuu, Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Raymond Mndolwa akifungua kikao kazi cha mapitio ya mpango mkakati wa miaka mitano wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Jijini Dodoma.

Mhandisi wa Umwagiliaji wa Mkoa wa Singida William Kadinda akielezea namna mpango mkakati utakavyorahisisha utekelezaji kiutendaji katika maeneo husika.


Baadhi ya Wataalam wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakijadiliana kwa lengo la kuboresha Mpango Mkakati wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.

Picha ya pamoja kati ya Menejimenti ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Wahandisi wa Umwagiliaji wa Mikoa.




Na; MwandishiWetu - Dodoma

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Raymond Mndolwa, ameongoza kikao kazi cha mapitio ya mpango mkakati wa miaka mitano wa Tume ya Taifa ya umwagiliaji, uliohusisha wataalam na wahandisi wa Umwagiliaji nchini, mapema leo Jijini Dodoma.

Bw. Mndolwa alisema kuwa,kuna umuhimu wakufanya mapitio ya mpango mkakati huo kwa pamoja tofauti kwa kuwa Mpango mkakati huo ni Dira ya Taasisi hivyo ni muhimu kila mtumishi katika taasisi anatakiwa kuifahamu kwani ndiyo zana inayotumika katika utekelezaji wa kazi za kila siku.

“Nimeona kuna Umuhimu wa kupitia kwa pamoja ili pale ambapo patakuwa na marekebisho turekebishe kwa pamoja, na kuwe na ushiriki kwa hoja katika kazi hii.” AlifafanuaMndolwa.

Kwa upande wake Mhandisi wa Umwagiliaji wa Mkoa wa Singida William Kadinda amesema, kikao kazi hiki kinatoa fursa ya mpango wa miaka mitano ambao unajumuisha shughuli zinazofanyika, pia kinaangalia maslahi ya watumishi katika upande wa mafunzo na kuona mahitaji yao, nakuweza kuwaongezea uwezo kiutendaji.

Kukamilika kwa mpango mkakati huo ni hatua muhimu kwa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakati huu,ikiwa na jukumu kubwa la ukarabati na ujenzi wa Skimu za umwagiliaji pamoja na Mabwawa kwa ajili ya umwagiliaji. Lengola serikalini kufikia Hekta 1,200,000 za umwagiliaji mwaka 2025.