MAFURIKO TANGA PICHA

June 03, 2015


 Wanafunzi wa shule ya msingi ya Donge  kata ya Mabawa  Tanga, wakiangalia nyumba zilizozingirwa na maji kufuatia mvua kubwa zilizoanza kunyesha toka juzi mfululizo.




ZIARA YA ACCESSS BANK KWA VYOMBO VYA HABARI

June 03, 2015

 Meneja Masoko wa AccessBank Ndugu Muganyizi Jonas Bisheko  (katikati ) akiwa Azam tv  Pamoja na Watangazaji wa Kipindi cha alasiri ndugu Andrian (kushoto) pamoja na wasiwasi Mwabulambo  kwenye  ziara kubwa ya Meneja kwenye Vyombo Mbalimbali vya Habari  Kutoa Elimu kwa Jamii juu ya Mambo mbalimali ya Kiuchumi ikiwemo Tatizo la Ajira ,Namna ya Kujiajiri na Nidhamu utawala wa Rasilimali fedha.

HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA(TANAPA) KUPITIA UJIRANI MWEMA WAKABIDHI MRADI WA MAJI KATIKA KIJIJI CHA ASHIRA WILAYA YA MOSHI

June 03, 2015

Mkuu wa mkoa wa Kilimajaro,Leonidas Gama
akikaribishwa na Mhifadhi Mkuu Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro
(KINAPA)Erastus Rufungulo katika makabidhiano ya mradi wa maji wa
ujirani Mwema uliotolewa na hifadhi za taifa nchni
TANAPA.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akikata utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi katika tanki la maji la mradi wa ujirani mwema uliotolewa na TANAPA kwa wananchi katika kijiji cha Ashira wilaya ya Moshi vijijini.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama
akisoma kilichoandikwa katika vibao mara baada ya uzinduzi wa mradi
huo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama
kuashiria uzinduzi rasmi wa mradi huo.
RC ,Gama akinywa maji kwa kutumia mkono mara
baada ya kufungua bomba la maji katika kijiji cha Ashira wilaya ya
Moshi vijijini.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,akimtwisha ndoo
ya maji mmoja wa wakazi wa kijiji cha Ashira katika wilaya ya Moshi
ikiwa ni ishara ya kukabidhi mradi huo wa maji ulifadhiliwa na TANAPA
kupitia mradi wa ujirani mwema.
Tanki la Maji la mradi wa ujirani mwema
uliofadhiliwa na Hifadhi za Taifa ,Tanzania (TANAPA).
Mhifadhi mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima
Kilimanjaro (KINAPA) Erastus Rufungulo akiwasalimia wananchi katika kijiji cha Ashira wilaya ya Moshi wakati wa kukabidhi mradi wa maji wa ujirani mwema uliofadhiliwa na TANAPA.
Baadhi ya wananchi katika kijiji cha Ashira
wilaya ya Moshi vijijini.
Meneja Ujirani mwema wa Hifadhi za Taifa
,Tanzania(TANAPA) Ahmed Mbugi akizungumza kuhusu miradi ya ujirani mwema ambayo TANAPA imekuwa ikiitoa kwa jamii katika kijiji cha Ashira wilaya ya Moshi vijijini.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Ashira
katika wilaya ya Moshi .
Kaimu Mkurugenzi mkuu TANAPA,Ibrahim Musa
akitoa taarifa mbele ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama
kuhusu ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Ashira wilaya ya
Moshi ,
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga
akizungumza wakati wa makabidhiano ya mradi wa maji uliofadhiliwa na
TANAPA kwa ajili ya wananchi wa kijiji cha Ashira wilaya ya
Moshi.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akiwahutubia wananchi waliofika katika makabidhiano ya mradi wa maji
katika kijiji cha Ashira wilaya ya Moshi ,uliofadhiliwa na hifadhi za
taifa Tanzania (TANAPA) .

Na Dixon Busagaga wa Globu ya
Jamii,Kanda ya Kaskazini, 

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO LEONIDAS GAMA AZINDUA DUKA JIPYA LA KAMPUNI YA SIMU ZA MKONONI YA TIGO.

June 03, 2015

Duka jipya la kampuni ya mawasiliano ya simu
za mkononi,Tigo lafunguliwa mjini Moshi.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa duka jipya la kampuni ya simu za mkononi ya Tigo.wengine wanaoshuhudia toka kulia ni mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga,Meneja huduma kwa wateja kanda ya
kaskazini,Gwamaka Mwakilembe na kushoto ni Meneneja wa Ubora wa Huduma ka wateja ,Mwangaza Matotola.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka jipya la kampuni ya simu za mkononi ya Tigo lililozinduliwa mjini Moshi.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga
akifuatilia kwa makini shughuli za uzinduzi wa duka la Tigo katika mji
wa Moshi.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu za
mkononi ya Tigo,wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas
Gama wakati wa uzinduzi wa duka jipya la kampuni hiyo mjini
Moshi.
Meneja huduma kwa wateja kanda ya
Kaskazini,Gwamaka Mwakilembe akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama wakati akitembelea vitengo mbalimbali ndani ya duka hilo.
Wafanyakazi wa kampuni ya Tigo wakiwa kazini.
Uuzaji wa simu za aina mbalimbali pia ulikuwa ukifanyika katika duka hilo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
,akifurahia jambo mara baada ya kutembelea ndani ya duka hilo na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo ya Tigo.
Meneja huduma kwa wateja Kanda ya
Kaskazini,Gwamaka Mwakilembe akitoa neno la shukurani kwa mkuu wa mkoa
wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama (hayupo pichani)mara baada ya uzinduzi
wa duka jipya la kampuni ya Tigo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kampuni ya Tigo muda
mfupi mara baada ya uzinduzi wa duka hilo.
………………………………………….
Na Dixon
Busagaga wa Globu ya jamii Kanda ya Kaskazini.