Na Oscar Assenga, Tanga.
MKUU wa wilaya ya Tanga,Halima Dendego amemtaka mrembo
atakayochaguliwa katika shindano la kumtafuta malkia wa Mkoa wa Tanga,Redd’S
Miss Tanga 2013 kuhakikisha anautangaza vema uzuri wa mkoa wa Tanga na vivutio
vyake ili kuweza kuwapa uelewa wananchi wengine kuufahamu mkoa wa Tanga.
Shindano hilo linatarajiwa kufanyika katika uwanja wa
Mkwakwani Jumamosi ijayo ya June 22 mwaka huu ambalo litasindikizwa na wasanii
nguli wa mziki wa bongofleva hapa nchini.
Dendego alitoa kauli hiyo leo wakati akifanya usafi na
warembo hao katika barabara ya Taifa ambapo warembo wanaowania taji hilo
walishiriki zoezi hilo ambalo hufanyika kila Jumamosi mkoani Tanga lenye lengo
la kuuweka mji katika mazingira mazuri maarufu kama “Kalembo Day”
Alisema ushiriki wao katika zoezi hilo wanaonyesha ni jinsi
gani warembo hao walivyokuwa karibu na jamii ambazo zinawazunguka na kuwataka
kuendelea kuhamasisha na wanajamii wengine ili nao waweze kushiriki katika
usafi kwa ajili ya kuyaweka maeneo yao kwenye muonekano mzuri.
Aidha alisema amefarijika sana kushiriki katika zoezi hilo na
warembo hao na kuelezea kuwa shindano hilo litakuwa na upinzani mkubwa kutokana
na warembo bomba ambao wanawania taji hilo ambalo hufanyika kila mwaka mkoani
hapa.
Mkuu huyo wa wilaya aliwaomba wakazi wa mkoa wa Tanga
kujitokeza kwa wingi kuweza kushuhudia shindano hilo ambalo limesheheni warembo
wakali na kuona jinsi washiriki hao watakavyo fanya maonyesho mbalimbali kabla
ya kuanza kinyang’anyiro hicho.
Kwa upande wake,Mratibu wa Redd’s Miss Tanga 2013,Asha
Kigundula ambaye ni Mkurugezi
wa Kampuni ya DATK Intertaimeint, Asha Kigundula,alimpongeza
Mkuu huyo wa wilaya kwa kuona umuhimu wa kushiriki zoezi hilo na kuwataka
wakazi wa mkoani wa Tanga kutoka wilaya zote kujitokeza kushuhudia shindano
hilo ambalo litakuwa la aina yake.
Kigundula alisema maandalizi ya shindano hilo yanaendelea vizuri
na zawadi za washindi zitatangazwa Jumatano wiki ijayo huku warembo wanaowania
shindano hilo kila mmoja akionekana kutamba kuchukua taji hilo ambalo
linaonekana litakuwa na upinzani mkubwa.
Hawa Ramadhani ambaye ni mmoja kati ya washiriki wa shindano
hilo alisema suala la usafi ni muhimu hasa katika jamii za watanzania na
kuwataka waendelee kuhakikisha wanafanya hivyo kila wakati ili kuyaweka
mazingira yao mazuri na salama kwa wageni na wenyeji.
Kwa upande wake,Mwalimu wa warembo hao,Mariam Bandawe alisema
wameanza kufanya zoezi hilo la usafi ili kuweza kuonyesha mfano kwa wananchi wa
mkoa wa Tanga kwa sababu usafi ni muhimu.
Warembo hao ni Hawa Ramadhan
(18),Hazina Mbaga (19)Like Abdulraman (19), Wahida Hashimu(20), Tatu Athumani (19),
Winfrida Gutram (21)Lulu Mbonela (19) ,Hazina Daniel (19),Lulu
Matawalo(22),Judithi Moleli (21) na Hawa Twaybu(21)
Redd's, Miss Tanga, imedhaminiwa na Dodoma Wine,CXC Africa,Executive Solutions,Busta General Supply, Mkwabi Interprises,Lusindic Investment LTD, Lavida Pub,Jambo Leo,Staa Spoti,Five Brothers Cloud's Media Group, pamoja na Blog Michuzi Media Group,Bongostaz.com, Saluti5,Kajuna, JaneJohn, na Kidevu na assengaoscar.blogspot.com.
Redd's, Miss Tanga, imedhaminiwa na Dodoma Wine,CXC Africa,Executive Solutions,Busta General Supply, Mkwabi Interprises,Lusindic Investment LTD, Lavida Pub,Jambo Leo,Staa Spoti,Five Brothers Cloud's Media Group, pamoja na Blog Michuzi Media Group,Bongostaz.com, Saluti5,Kajuna, JaneJohn, na Kidevu na assengaoscar.blogspot.com.