PPF YAKUTANA NA WAFANYAKAZI WA NOKIA JIJINI DAR ES SALAAM

August 21, 2015


 Mwanachama mpya wa PPF, akijaza fomu za mpango wa uchagiaji wa hiari wakati wa utoaji huduma kwa wafanyakazi wa kampuni ya NOKIA pale Mlimani City jijini Dar es Salaam, Agosti 21, 2015. Kulia ni Afisa wa Kanda wa PPF, Upendo Singinika Sasi
 Meneja Masoko wa PPF, Elihuruma Ngowi (kushoto), akimkabidhi zawadi mwanachama wa Mfuko huo, Raymond Ndambo
 Elihuruma (kushoto) na mtaalamu wa mifumo ya comuter wa PPF, (Kulia), wakiangalia jinsi wanachama wa mfuko huo wanavyopata taarifa za michangu yao kupitia simu zao
 Afisa Masoko mwandamizi wa PPF, Nelu Mwalugaja, (kulia), akimpatia maelezo ya huduma za Mfuko huo, Mwanachama wa PPF.
 Meneja Masoko wa PPF, Elihuruma Ngowi, akizungumza na waandishi wa habari.
Msimamizi wa Kanda wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Upendo Walter Mazula, (kulia), akimkabidhi zawadi mwanachama mpya wa PPF, Raymond Ndambo, (katikati), huku Meneja Masoko wa PPF, Elihuruma Ngowi, wakati wa siku ya wafanyakazi wa kampuni ya NOKIA.




 Wataalamu wa mifumo ya computer wa PPF, wakifuatialia taarifa za Mwanachama (wapili kushoto) 
 Afisa wa Kanda wa PPF, Upendo, (kushoto), akimpatia zawadi Mwanachama wa Mfuko huo baada ya kupatiwa huduma
Msimamizi wa Kanda wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Upendo Walter Mazula, (aliyekaa), akimpatia maelezo Mwanachama wa Mfuko huo, (kushoto), wakati wa utoaji huduma kwa wafanyakazi wa NOKIA pale Mlimani City jijini Dar es Salaam
Khalfan Said Photojournalist.

WIZARA YA AFYA YAWANOA WAANDISHI WA HABARI JINSI YA KUKABILIANA NA MAGONJWA YA MLIPUKO DAR

August 21, 2015

Daktari Mwandamizi Dharura na Maafa kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Mary Kitambi akitoa mada jana jijini Dar es salaam wakati wa semina ya waandishi wa habari jinsi ya kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu. 
Mmoja wa waandishi wa habari akiuliza swali jana jijini Dar es salaam wakati wa semina ya waandishi wa habari jinsi ya kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.
Mtaalamu wa Ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt.Vida Mmbaga akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari jinsi ya kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu katika Semina iliyoandaliwa na Wizara hiyo kwa wanahabari. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Gain Marc Van Amengen (kulia) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari(hawapo pichani ) jana jijini Dar es salaam juu ya kuweka madini joto kwenye vyakula. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Michael John.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Michael John(kushoto)  akijibu maswali ya wanahabari (hawapo pichani ) jana jijini Dar es salaam juu ya kuweka madini joto kwenye vyakula. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Gain Marc Van Amengen.
Mkurugenzi Msaidizi huduma ya lishe kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Vincent Assey (kushoto) akifafanua kwa wanahabari juu ya umuhimu wa madini joto jana jijini Dar es salaam .Kulia ni Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Neema Rusibimayila.
Mmoja wa waandishi wa habari David John  swali jana jijini Dar es salaam wakati wa semina ya waandishi wa habari jinsi ya kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.
Picha zote na Anitha Jonas -MAELEZO-Dar es salaam.
MAKONDA AWAHIMIZA WASANII KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA

MAKONDA AWAHIMIZA WASANII KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA

August 21, 2015

if1
Picha ya Pamoja ya DC Makonda, Viongozi wa BASATA, Viongozi wa NHIF na Wasanii
if2
Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Wasanii waliokabidhiwa kadi za NHIF wakiwa na Mgeni rasmi DC Makonda 
if3
Baadhi ya wasanii wakifuatilia mada
if4
Mkuu wa Wilaya ya Kindondoni akihutubia wasanii
……………………………………………………………………………
Awataka kutumia taaluma yao kuhamasisha wengine kujiunga:
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda amesema wakati sasa umefika kwa wasanii kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, badala ya kuendelea kuchangishana fedha za matibabu kila wanapougua.
Amesema kutokana na kupanda kwa gharama za maisha hivi sasa zikiwemo za matibabu, wasaani wana kila sababu ya kuona umuhimu wa kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili wanapougua watibiwe kwa kutumia kadi badala ya kuhangaika kutafuta fedha taslimu.
Makonda alikuwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina kuhusu huduma za matibabu kupitia mpango maalumu wa bima ya afya kwa wajasiliamali na vikundi vilivyosajiliwa unaojulikana kama KIKOA.
Amesema hivi sasa wasanii wengi wanahangaika kupata matibabu katika mazingira yasiyoridhisha kwa kuwa hawana bima za afya hivyo ni muhimu kwao wachangamke fursa hiyo ambayo itawawezesha kuchangia kabla ya kuugua na hivyo kuwa na uhakika wa kutibiwa hata kama hawana fedha mfukoni.
Naye Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Eugen Mikongoti amesema NHIF imeanzisha utaratibu huo wa kuchangia kwa kundi la wajasiliamali ili kuwapa uhakika wa matibabu wakati wote wanapokua katika shughuli zao za kuelimisha na kuhamasisha jamii katika masuala mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Amesema kwa kuchangia 76,800 mwanachama wa KIKOA atakuwa na uhakika wa kutibiwa mwaka mzima katika vituo vya matibabu zaidi ya 6000 vilivyosajiliwa na Mfuko nchini nzima.
Mikongoti amesema NHIF itawatumia wasanii hao katika kuelimisha umma  ili kuhakikisha kuwa ujumbe wa umuhimu wa wananchi  kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya unaenea nchini nzima.
Katika semina hiyo iliyoandaliwa kwa pamoja na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na Baraza la Wasanii Tanzania (BASATA), viongozi wanne wa Shirikisho la Wasanii walikabidhiwa kadi zao za bima ya afya zinazowawezesha kupata matibabu wakati wowote watakapougua.
Mpango wa bima ya afya kwa wajasiliamali – KIKOA- unawalenga wajasiliamali walio katika vikundi vilivyosajiliwa, ambapo hadi sasa zaidi ya vikundi mia moja vyenye wanachama zaidi ya elfu ishirini vimejiunga na Bima ya Afya.

MKURUGENZI MKUU WA AGPAHI AAGANA RASMI NA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA

August 21, 2015

 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika lisilo la Kiserikali la Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI), Laurean Bwanakunu aliyekwenda kumuaaga ofisini kwake baada ya Rais Jakaya Kikwete kumteua kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD). (Picha na Francis Dande)
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga (katikati) akizungumza na uongozi wa Shirika lisilo la Kiserikali la AGPAHI uliokwenda ofisini kwake wakati Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo alipokwenda kumuaga. 
 Meneja Miradi wa Shirika la AGPAHI kwa Mikoa ya Shinyanga & Simiyu, Dk. Gastor Njau (kushoto) akifafanua jambo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la AGPAHI anayemaliza muda wake, Laurean Bwanakunu akifafanua jambo.
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga akisisitiza jambo.... 
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Mkuu wa AGPAHI akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga. 
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga akifafanua jambo wakati uongozi wa Shirika la AGPAHI ulipomtembelea ofisini kwake. 
 Mkurugenzi Mkuu wa AGPAHI anayemaliza muda wake.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la AGPAHI, Laurean Bwanakunu (kushoto) akimkabidhi cheti cha shukrani Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga, wakati alipokwenda kumuaga ofisini kwake baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD). 
BALOZI MTEULE MAKAKALA WA NCHINI ZIMBABWE AKUTANA NA DR.SHEIN

BALOZI MTEULE MAKAKALA WA NCHINI ZIMBABWE AKUTANA NA DR.SHEIN

August 21, 2015

ba1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Zimbabwe Lt.Gen.Mstaafu Charles Makakala alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kujitambulisha leo,[Picha na Ikulu.]
ba2
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akifuatana  na Balozi mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Zimbabwe Lt.Gen.Mstaafu Charles Makakala baada ya mazungumzo yao leo alipofika  Ikulu Mjini Zanzibarkujitambulisha   ,[Picha na Ikulu.]
ba3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Balozi mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Zimbabwe Lt.Gen.Mstaafu Charles Makakala alipofika kujitambulisha Ikulu Mjini Zanzibar  leo,[Picha na Ikulu.]

RAIS KIKWETE APOKEA HATI YA UTAMBULISHO WA BALOZI WA DENMARK NCHINI

August 21, 2015

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (kushoto) akipokea hati ya utambulisho ya Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (kulia) leo Ikulu jijini Dar es salaam wakati alipokwenda kujitambulisha.
Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen akisaini kitabu cha wageni wakati alipokuwa anaenda kukabidhi hati ya utambulisho na kujitambulisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (kushoto) akisalimiana na Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (kulia) wakati alipokwenda kujitambulisha na kukabidhi hati ya utambulisho leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (kulia) akisalimiana na Balozi wa Denmark (kushoto) nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen mara baada ya kukabidhi hati ya utambulisho leo Ikulu jijini Dar es salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (kulia) akibadilishana mawazo na Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (kushoto) wakati alipokwenda kujitambulisha na kukabidhi hati ya utambulisho leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (kulia) akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Maadhi Juma Maalimu (wa pili kushoto) leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (katikati mstari wa mbele) akiwa amesimama wakati nyimbo za taifa za Tanzania na Denmark zikiimbwa leo Ikulu jijini Dar es salaam alipokwenda kujitambulisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete.
 Bendi ya Jeshi la Polisi nchini ikipiga nyimbo za taifa za Tanzania na Denmark wakati Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (katikati mstari wa mbele) alipokuwa anakwenda kujitambulisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete.
(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
PINDA ATETA NA WAZIRI MKUU WA UGANDA

PINDA ATETA NA WAZIRI MKUU WA UGANDA

August 21, 2015

download (6)
*Asema Tanzania kuadhimisha miaka 100 ya Maskauti mwaka 2017
……………………………………………………………
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amekutana na Waziri Mkuu wa Uganda, Dk. Ruhakana Rugunda na kufanya naye mazungumzo kuhusiana na masuala mbalimbali yahusuyo nchi hizi mbili.
Akizungumza na mwenyeji wake jana jioni (Alhamisi, Agosti 20, 2015), kwenye kikao kilichofanyika Ofisi ya Waziri Mkuu wa Uganda jijini Kampala, Waziri Mkuu alisema amefurahishwa na juhudi zinazofanywa kwenye mipaka ya nchi hizo mbili na hasa mpaka wa Mutukula.
“Nimearifiwa kwamba juhudi za ujenzi wa one-border-post pale Mtukula zinaendelea vizuri. Tunachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuangalia kwa kiasi gani tunaweza kutumia kituo hiki kama fursa ya kukuza biashara baina ya nchi zetu mbili,” alisema.
Alisema masuala ya kuimarisha uchumi ni ya msingi na hayana budi kupewa kipaumbele katika kipindi hiki cha sasa. “Kikubwa ni kwa nchi zetu kuendelea kuimarisha amani iliyopo kwa faida ya wananchi wake, maana bila amani hakuna kitakachofanyika,” alisema.
Waziri Mkuu Pinda alitumia fursa hiyo kumtakia heri yeye na wananchi wa Uganda wakati wakijiandaa kufanya Uchaguzi Mkuu ujao unaotarajiwa kufanyika Februari, 2016.
Pia alimwalika Waziri Mkuu wa Uganda aje kutembelea Tanzania pindi apatapo nafasi ya kufanya hivyo.
Naye Waziri Mkuu wa Uganda, Dk. Rugunda alisema nchi yake bado inatambua na inathamini mchango wa Tanzania katika kuleta amani nchini mwao.
“Tanzania itaendelea kukumbukwa na Waganda kwa mchango mlioutoa katika harakati za kuikomboa Uganda kutoka kwenye makucha ya Iddi Amin Dada. Maneno aliyokuwa akiyasema mwalimu Nyerere bado yamo akilini mwetu na yanaendelea kuishi mioyoni mwa Waganda wengi,” alisema.
“Waganda wengi wanaiona Tanzania kama ni nyumba yao ya pili (second home) na wanafurahia wanapokuja huko akiwemo Rais wetu, Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni. Sote tunathamini mchango wa Tanzania na tutaendelea kuuezi,” alisema Dk. Rugunda.
Alisema yeye binafsi anafurahi kwamba Tanzania na Uganda zimeunganishwa kwa njia ya kieletroniki (mtandao na mawasiliano ya simu); lakini akaongeza kuwa kiasili, nchi hizo zimeunganishwa kwa njia ya barabara na maji kupitia Ziwa Victoria na kwamba ana imani uhusiano uliopo utaendelea kudumu vizazi na vizazi.
Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema Tanzania itaadhimisha miaka 100 ya Chama cha Maskauti cha Tanzania ifikapo Agosti, 2017. “Hivi sasa tunao maskauti wapatao 800,000 nchi nzima lakini lengo letu ni kufikisha maskauti milioni moja ifikapo mwaka 2017 kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 100 nchini kwetu,” alisema.
Waziri Mkuu Pinda aliwasili nchini Uganda Jumatano usiku kwa ziara ya siku moja akimwakilisha Rais Jakaya Kikwete kwenye maadhimisho ya miaka 100 ya Chama cha Maskauti cha Uganda (Uganda Scouts Association – USA). Amerejea nchini jana usiku.
Rais Yoweri Museveni ndiye mlezi wa chama hicho na alikuwa amemwalika Rais Kikwete kwenye maadhimisho hayo.