IMEWEKWA DESEMBA 23 2013
Na. Cliford Mario Ndimbo.
Timu ya Yanga imetangaza rasmi kumtimua kocha wake mkuu raia wa Uholanzi Ernie Brandts ikiwa ni siku chache baada ya kula kibano cha mabao 3-1 kutoka kwa mahasimu wao Wekundu wa Msimbazi Simba kwenye mchezo wa hisani wa Nani Mtani Jembe.
Akitangaza maamuzi magumu yaliyofikiwa na kamati ya utendaji Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya klabu hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya usajili Abdallah Binkleb amesema wamefikia uamuzi wa kumtimua kazi Brandts kwakuwa tayari uwezo wake ulifikia mwisho.
Timu ya Yanga imetangaza rasmi kumtimua kocha wake mkuu raia wa Uholanzi Ernie Brandts ikiwa ni siku chache baada ya kula kibano cha mabao 3-1 kutoka kwa mahasimu wao Wekundu wa Msimbazi Simba kwenye mchezo wa hisani wa Nani Mtani Jembe.
Akitangaza maamuzi magumu yaliyofikiwa na kamati ya utendaji Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya klabu hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya usajili Abdallah Binkleb amesema wamefikia uamuzi wa kumtimua kazi Brandts kwakuwa tayari uwezo wake ulifikia mwisho.