REDD'S MISS KINONDONI 2014 NI SHIDAAAAH!
Mratibu wa shindano la Redd's miss Kinondoni 2014 Innocent Melleck
katikati akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar Es Salaam juu ya
shindano la kanda ya kinondoni litakalofanyika katika ukumbi wa Escape
One ijumaa kwa kiingilio cha 10,000 kwa viti vya kawaida na 30,000 kwa
VIP huku burudani za Malaika Bend chini ya Chirstian bella na Young Suma
na tayari tiketi zipo mtaani. Baadhi ya warembo wa shoto ni matroni wa kambi hiyo Husna Maulid na
kulia ni Mkuu wa itifaki wa kamati ya Miss Tanzania Albert Makoye
MAHABUSI YA WATOTO TANGA KUPATIWA FEDHA
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
13/08/2014
Serikali
imetenga fedha zitagawiwa kwenye vituo vyote vinavyotoa ushauri nasaha
na kurekebisha watoto walio chini ya umri wa miaka 18 vilivyo chini ya
Idara ya Ustawi wa jamii nchini.
Kauli
hiyo imetolewa na Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
Nsachris Mwamwaja kufuatia habari iliyochapishwa na gazeti la Majira
toleo Na. 7524 Vol.II/5624 la Jumatano Agosti 13, mwaka huu yenye kichwa
cha habari “Mahabusu ya watoto yadaiwa mil. 1/=”.
“Ni
kweli tatizo hilo lipo ndio maana Serikali imetenga fedha tayari ambazo
zitagawiwa kwenye vituo vyote nchi nzima” alisema Mwamwaja.
Mwamwaja alisisitiza kuwa deni hilo litalipwa kweye mahabusi hiyo iliyoko Tanga.
Mahabusi
hiyo ni miongoni mwa vituo kadhaa vilivyo chini ya Idara ya Ustawi wa
Jamii ndani ya Wizara ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
Matumizi
ya fedha hizo ni pamoja na kushughulikia tatizo la maji na uhaba wa
chakula kituoni hapo ili kuendelea kutoa huduma stahiki kwa watoto hao
na kufikia lengo la kuwarekebisha tabia zao ili wawe raia wema nchini.
Aidha,
Mwamwaja aliongeza kuwa fedha zilizotengwa si za Mkoa wa Tanga tu bali
ni kwa ajili ya vituo vya nchi nzima zikiwemo makambi ya wazee
wasiojiweza, mahabusi za watoto na kambi za kutibu wagonjwa wa ukoma.
Mkurugenzi Idara ya Habari( MAELEZO) atembelea vitengo vya Mawasiliano Serikalini
Afisa Habari wa Wizara ya Maji na
Umwagiliaji Bw. Dennis Kiilu akimueleza jambo Mkurugenzi wa Idara ya
Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (hayupo pichani) wakati wa Ziara ya
Mkurugenzi huyo katika Vitengo vya Mawasiliano Serikalini yenye lengo la
kuangalia utendaji kazi na ufanisi wa vitengo hivyo katika utekelezaji
wa majukumu yake ya kila siku leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa
Habari wa Wizara hiyo Bi. Fatuma Malende.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari
(MAELEZO) Bw. Assah Mwambeneakiwaonesha Maafisa Habari wa Wizara ya Maji
(hawapo pichani) namna Matumizi ya Mtandao wa Kijamii wa Twitter
unavyofanya kazi hasa katika nguvu na kasi ya upashaji habari kwenye
jamii, wakati wa Ziara ya Mkurugenzi huyo katika Vitengo vya Mawasiliano
Serikalini yenye lengo la kuangalia utendaji kazi na ufanisi wa vitengo
hivyo katika utekelazaji wa majukumu yake ya kila siku leo Jijini Dar
es Salaam.
Baadhi ya Maafisa Uhusiano Shirika
la Umeme Tanzania (TANESCO) Kutoka kushoto ni Neema Mbuja, Salama
Kasamalu na Henry Kilasila wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Habari
(MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (hayupo pichani) wakati wa Ziara ya
Mkurugenzi huyo katika Vitengo vya Mawasiliano Serikalini Leo Jijini Dar
es Salaam.
[PICHA NA HASSAN SILAYO]
[PICHA NA HASSAN SILAYO]
Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika
la Umeme Tanzania (TANESCO) Bw. Adrian Severin akimueleza jambo
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (hayupo
pichani) wakati wa Ziara ya Mkurugenzi huyo katika Vitengo vya
Mawasiliano Serikalini yenye lengo la kuangalia utendaji kazi na ufanisi
wa vitengo hivyo katika utekelzaji wa majukumu yake ya kila siku leo
Jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Idara ya Habari
(MAELEZO) Bw. Assah Mwambene akieleza jambo kwa Maafisa Uhusiano wa
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) (baadhi hawapo pichani) wakati wa
Ziara ya Mkurugenzi huyo katika Vitengo vya Mawasiliano Serikalini yenye
lengo la kuangalia utendaji kazi na ufanisi wa vitengo hivyo katika
utekelzaji wa majukumu yake ya kila siku leo Jijini Dar es Salaam.
Kushoto ni Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika hilo Bw. Adrian Severin na
katikati ni Afisa Uhusiano wa Shirika hilo Bw. Henry Kilasila.
MWANAFUNZI ALIWA NA MBWA KARIBU NA IKULU
Jeneza la Mwili wa Marehemu Iblahim Faraja Chipungahelo likiteremshwa makaburini kwa ajili ya mazishi.
Mchungaji akiendesha ibada ya mazishi ya Marehemu Iblahim Faraja Chipungahelo
Waomboleaji wakiuzika mwili wa marehemu Iblahim Faraja Chipungahelo
Mmoja wa Mbwa wanaodaiwa kumuua marehemu Iblahim Faraja Chipungahelo ameuwawa.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kushuhudia tukio hilo.
…………………………………………………………………………………………………………….
Na Bazil Makungu Ludewa
MWANAFUNZI
wa shule ya msingi Ludewa mjini katika mkoa wa Njombe Iblahim Faraja
Chipungahelo ameuawa na kisha kuliwa nyama na mbwa wanaosadikika kuugua
kichaa kwa kukosa chakula kwa muda mrefu.
Tukio
hilo la kusikitisha na lililoleta simanzi kubwa kwa wakazi wa Ludewa
mjini lilitokea August 8 mwaka huu majira ya saa saba mchana katika eneo
la Ikulu ambapo marehemu Chipungahelo pamoja na wenzake walikuwa
wakipita njia karibu na nyumba ya mtu aliyejulikana na kwa jina la Bosco
Lingalangala kwenda kuchuma mapera kama ilivyo destuli yao.
Mashuhuda
wa tukio hilo mama Kumba na mama Haule wakazi wa kitongoji cha Ibani
katika kata ya Ludewa kwa pamoja walieleza kuwa wakiwa nyumba walisikia
kelele za watoto jirani huku wakimwita mwenzao marehemu bila mafanikio.
‘’’’ Tulipowauliza
walisema kuwa mwenzao Ibrahim amekamatwa na mbwa na ndipo
tulipokusanyika na kwenda kumwokoa mtoto lakini tulipofika eneo la tukio
tulimkuta mbwa wakiendelea kumla marehemu huku amelala kifudifudi
lakini tulishindwa kumwokoa na ndipo tukakimbia kutoa taarifa kituo cha
polisi.””” walisema akina mama hao kwa uchungu
Kwa
mujibu wa taarifa ya daktari Sira Rajabu wa Hospitali ya wilaya ya
Ludewa aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu alisema mtoto Ibrahim
alikuwa na majeraha makubwa mwili mzima huku paja la mguu wake wa kulia
likiwa limeliwa na kuondolewa nyama.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Njombe Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi
Fulgensi Ngonyani alikiri kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa
upelelezi unaendelea ikiwa ni pamoja na kuwahoji watu mbalimbali akiwemo
mmiliki wa mbwa hao ambaye inasadikika kuwa ananishi jijini Dar es
salaam.
Akizungumza
na mwandishi wetu mganga wa mifugo Simoni Haule alisema kuwa mbwa hao
wa bwana Bosco Lingalangala hawajapata chanjo zaidi ya miaka miwili sasa
kwa hiyo tayari mbwa hao wanaugua ugonjwa wa kichaa ambacho hawawezi
kupona tena na dawa iliyobaki ni kuuawa tu.
Mmiliki wa mbwa hao Bosco lingalangala hakupatikana ili kuzungumzia suala hilo kwa sababu simu yake ya mkononi haikupatikana.
Hata
hivyo akiwa makaburini diwani wa Kata ya Ludewa Monica Mchiro
aliwaambia na kuwatahadharisha waombolezaji na wananchi waliohudhuria
mazishi kuwa mawasiliano yamefanywa kati yake na mmiliki wa mbwa hao
lakini majibu aliyoyatoa hayana ushirikiano kwa sababu ameahidi kuchukua
hatua za kisheria kwa yeyote atakaye husika kuwadhuru mbwa wake.
Hata
hivyo habari kutoka kwa majirani ambao hawakupenda kutaja majina yao
walisema mbwa hao hufungiwa kwenye banda na hupewa nyama mbichi kwa
kurushiwa na wahudumu lakini siku hiyo walifunguliwa na kuanza kuzagaa
kwa nia ya kujitafutia chakula wenyewe baada ya kukosa kwa muda mrefu.
Subscribe to:
Posts (Atom)