MAONESHO YA BIASHARA YA AFRIKA MASHARIKI 2016 KUFANYIKA ROCK CITY MALL JIJINI MWANZA.

August 19, 2016
Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA mkoani Mwanza, Leopard Lema (wa pili kushoto), akitoa ufafanuzi hii leo Jijini Mwanza kuhusiana na Maonesho ya Wafanyabiashara Afrika Mashariki yanayotarajiwa kuanza Agost 26,2016 hadi Septemba 04,2016 katika viwanja vya Rock City Jijini Mwanza.

Wengine ni, Hassan Karambi ambaye ni Katibu Mtendaji wa TCCIA Mwanza (wa kwanza kushoto), Tungu Misululu, Makamu Mwenyekiti TCCIA kitengo cha Biashara mkoani Mwanza (wa pili kulia) na Majid Igangula (wa kwanza kulia), kutoka bodi ya Washauri TCCIA.
Makampuni pamoja na wajasiriamali mbalimbali katika nchi za Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania, yametakiwa kutumia Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki katika kutangaza na kuuza bidhaa zao.

Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA mkoani Mwanza, Leopard Lema, ametoa rai hiyo leo Jijini Mwanza, wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na Maonesho hayo.

"Maonesho haya yanatoa fursa kwa makampuni mbalimbali Afrika Mashariki kujitangaza, kukutana na wateja wao, kutafuta wabia wapya wa kibiashara pamoja na kufanya utafiti wa kimasoko". Ametanabaisha Lema.

Maonesho hayo yanatarajiwa kuanza agost 26,2016 hadi Septemba 04,2016 katika viunga vya Rock City Mall Jijini Mwanza na yanatarajiwa kushirikisha wafanyabiashara kutoka mataifa ya Afrika Mashariki na nje ya Afrika Mashariki.
Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA mkoani Mwanza, Leopard Lema (katikati), akiwa katika mkutano na wanahabari (hawapo pichani) kuhusiana na Maonesho ya Wafanyabiashara Afrika Mashariki yanayotarajiwa kuanza Agost 26,2016 hadi Septemba 04,2016 katika viwanja vya Rock City Jijini Mwanza.

Wengine ni, Hassan Karambi ambaye ni Katibu Mtendaji wa TCCIA Mwanza (kushoto), Tungu Misululu, Makamu Mwenyekiti TCCIA kitengo cha Biashara mkoani Mwanza (kulia).
Wanahabari Jijini Mwanza, wakiwa katika Mkutano wa TCCIA kuhusu Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki Jijini Mwanza, uliofanyika leo.
Wanahabari wakiwa katika mkutano huo
Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA mkoani Mwanza, Leopard Lema, akitoa ufafanuzi kwa wanahabari.
Taswira ya Mkutano wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA, na Wanahabari ulioketi hii leo Jijini Mwanza, kuhusu Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashari yanayotarajiwa kuanza Agost 26 mwaka huu viwanja vya Rock City Mall Jijini Mwanza.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo @BMG

WAZIRI ANGELLAH KAIRUKI AFUNGUA MKUTANO WA KAZI WA MFUKO WA TASAF MKOANI ARUSHA

August 19, 2016


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,Angellah Kairuki akiwaongoza Wakuu wa mikoa kutoka kushoto,Mhandisi Mathew Mtigumwe(Singida),Dk Joel Bendera(Manyara),Said Meck Sadick(Kilimanjaro)na Martine Shighela(Tanga).

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,Angellah Kairuki akifungua mkutano wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(Tafas)walioketi ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo,Ladislaus  Mwamanga na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck Sadick.

Wakuu wa wilaya kutoka mikoa mitano ya Singida ,Manyara,Arusha,Kilimanjaro na Tanga wakiwa kwenye mkutano wa Kazi wa kupata uelewa zaidi wa mfuko wa Tasaf.

Wakuu wa mikoa Mhandisi Mathew Mtigumwe wa Singida,Dk Joel Bendera wa Manyara(katikati) na Martine Shighela wa Tanga.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Tasaf ,Ladislaus  Mwamanga akizungumza katika mkutano huo.

Mkuu wa wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha akizungumza jambo katika mkutano huo.

Mkuu wa wilaya ya Handeni mkoa wa Tanga,Godwini Gondwe  akizungumza  katika mkutano huo.

Mkuu wa wilaya ya Moshi mkoa wa Kilimanjaro,Kippi Warioba  akizungumza  katika mkutano huo.