NEYO APOKELEWA KAMA MFALME JIJINI MWANZA

NEYO APOKELEWA KAMA MFALME JIJINI MWANZA

May 20, 2016
Msanii wa Kimataifa kutoka nchini Marekani Neyo amewasili jijini Mwanza jioni hii akitokea Dar es Salaam na kupokelewa na umati mkubwa wa wakazi wa jiji hilo kama Mfalme katika Uwanja wa Ndege wa jijini Mwanza.
Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania ndio wadhamini wakuu wa Jembeka Festival 2016 kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Fastjet, SYSCORP Cooperation, CF Hospitals, KK Security, Samsung, EF Outdoor, Lacairo Hotel, Ndege Insurance, Jembe Media Group pamoja na Coca Cola.
Msanii huyo anatarajiwa kutumbuiza katika tamasha hilo kwa kupiga 'Live Music' katika uwanja wa CCM Kirumba ambapo msanii wa kimataifa kutoka nchini, Diamond Platnumz, FID Q, Stamina, Mr. Blue, Ney wa Mitego, Maua Sama, Rubby, Baraka Da Prince, Juma Nature, MO Music na wengine wengi watapanda jukwaa moja na msanii Neyo.
Neyo check out from the hotel Hyatt Regency
Msanii wa Kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo akiondoka katika hoteli ya Hyatt Regency-The Kiliamanjaro kueelekea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa safari ya jiji Mwanza kutumbuiza kwenye Jembeka Festival 2016 ambapo wadhamini wakuu ni Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Fastjet, SYSCORP Cooperation, CF Hospitals, KK Security, Samsung, EF Outdoor, Lacairo Hotel, Ndege Insurance, Jembe FM. Kulia ni Meneja wa Hoteli hiyo, Timothy Mlay.
IMG_5465
Attu Mynah and Neyo
Meneja Masoko wa CFAO Motors Group, Attu Mynah ambao wamedhamini usafiri uliotumika kumwendesha msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo gari aina Mercedes Benz GLE 350 D ya mwaka 2016 katika picha ya kumbukumbu na Msanii huyo kabla ya kuelekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.
Neyo ta Hyatt Regency-The Kilimanjaro
Msanii wa kimataifa Neyo aki-show love na walinzi maalum kabla ya kuelekea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere tayari kwa safari ya Mwanza.
Neyo official car Mercedes Benz GLE 350 D of 2016
Msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo akielekea kwenye gari maalum aina ya Mercedes Benz GLE 350 D ya 2016 lilitolewa na kampuni ya CFAO Motors Group.
Neyo Sorrounded by Tanzanian Bodyguard
Msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Mwalimu JK Nyerere akiwa amezungukwa na walinzi maalum alipokuwa akielekea jijini Mwanza.
Neyo at Julius Nyerere International Airport
Msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere akiwa na mlinzi wake wakielekea jijini Mwanza leo jioni.
Costantine Magavilla and Neyo
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Jembeka Festival 2016, Costantine Magavilla (t-shirt ya blue) na Msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo wakijianda kupanda ndege ya Shirika la Fastjet katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kuelekea jijini Mwanza. Shirika la Ndege la Fastjet ni miongoni mwa wadhamini wa tamasha hilo.
Neyo Crew to Mwanza
Mkurugenzi Mtendaji wa Jembe Media Group, Dr. Sebastian Ndege akiwa na 'crew' iliyoambatana na msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo wakipanda ndani ya ndege ya Shirika la Fastjet ambao ni miongoni mwa wadhamini wa Jembeka Festival 2016 kutokea jijini Dar es Salaam kuelekea jijini Mwanza.
Jembeka Festival 2016 boarding Fastjest Airline
Neyo arrived in Mwanza
Mkurugenzi Mtendaji wa Jembe Media Group, Dr. Sebastian Ndege na Mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo wakishuka kwenye ndege ya Shirika la Fastjet ambao ni miongoni mwa wadhamini wa Jembeka Festival 2016 mara baada ya kutua jijini Mwanza. Kampuni ya simu mkononi Vodacom Tanzania ndio wadhamini wakuu wa Jembeka Festival 2016 kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Fastjet, SYSCORP Cooperation, CF Hospitals, KK Security, Samsung, EF Outdoor, Lacairo Hotel, Ndege Insurance, Jembe Media Group pamoja na Coca Cola.
IMG_5597
Baadhi ya wapiga vyombo waliombatana na msanii wa Marekani, Neyo wakishuka kwenye ndege ya shirika la Fastjet katika uwanja wa ndege wa jijini Mwanza jioni. Kampuni ya simu mkononi Vodacom Tanzania ndio wadhamini wakuu wa Jembeka Festival 2016 kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Fastjet, SYSCORP Cooperation, CF Hospitals, KK Security, Samsung, EF Outdoor, Lacairo Hotel, Ndege Insurance, Jembe Media Group pamoja na Coca Cola.
Costantine Magavilla
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Jembeka Festival 2016, Costantine Magavilla (wa pili kushoto) na Mwanakamati ya Jembeka Festival 2016, Sharon wakiwasili na katika uwanja wa ndege wa Mwanza jioni hii.
Sebastian Ndege
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti kamati ya maandalizi ya Jembeka Festival 2016, Costantine Magavilla, Afisa Habari wa Jembe Media Group, Gsengo pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Jembe Media Group, Dr. Sebastian Ndege katika picha ya pamoja.
Neyo on Maasai Shuka
Balozi wa Umoja wa Mataifa mtoto mwanabadiliko wa mazingira, Getrude Clement akimvisha shuka la kimasai Msanii wa Kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo baada ya kuwasili jijini Mwanza leo jioni.
Getrude Clement na Neyo
Msanii wa Kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo aki-'show love' na Balozi wa Mabadiliko ya Tabianchi kutoka Umoja wa Mataifa, Getrude Clement aliyefika uwanjani hapo kumlaki na kumvisha shuka la Kimasai. Kampuni ya simu mkononi Vodacom Tanzania ndio wadhamini wakuu wa Jembeka Festival 2016 kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Fastjet, SYSCORP Cooperation, CF Hospitals, KK Security, Samsung, EF Outdoor, Lacairo Hotel, Ndege Insurance, Jembe FM.
Bujora Cultural Troup Mwanza entertain Neyo
Msanii wa kikundi cha ngoma cha Bujora Cultural Troupe cha jijini Mwanza akimshikisha nyoka aina chatu msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo alipowasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza jioni hii.
Neyo playing with a snake in Mwanza
Jembe FM Journalist Interviewing Neyo
Waandishi wa habari wa jijini Mwanza wakiwemo wa JEMBE FM wakifanya mahojiano na msanii Neyo alipowasili jijini Mwanza.
IMG_5666
Wakazi wa jijini Mwanza wakisalimana na msanii Neyo kwa shangwe na furaha waliofika kumlaki katika uwanja wandege wa jijini Mwanza.
IMG_5667
IMG_5662
IMG_5305
Msafara wa msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo ukielekea hotelini baada ya kuwasili jijini Mwanza.
Neyo at Malaika Resort
Msanii Neyo alipowasili kwenye hoteli ya Malaika Resorts ya jijini Mwanza akiwapungia wafanyakazi pamoja na wateja katika hoteli hiyo.
Justine Ndege and Neyo
Mwanasheria wa Jembe Media Group, Justine Ndege katika picha ya pamoja na Msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo katika hoteli ya Malaika Resort.
Sebastian Ndege na Neyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Jembe Media Group, Dr. Sebastian Ndege akibadilishana mawazo na msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo anayetarajiwa kutumbuiza kesho katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
NEYO APOKELEWA KAMA MFALME JIJINI MWANZA

NEYO APOKELEWA KAMA MFALME JIJINI MWANZA

May 20, 2016

Msanii wa Kimataifa kutoka nchini Marekani Neyo amewasili jijini Mwanza jioni hii akitokea Dar es Salaam na kupokelewa na umati mkubwa wa wakazi wa jiji hilo kama Mfalme katika Uwanja wa Ndege wa jijini Mwanza.
Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania ndio wadhamini wakuu wa Jembeka Festival 2016 kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Fastjet, SYSCORP Cooperation, CF Hospitals, KK Security, Samsung, EF Outdoor, Lacairo Hotel, Ndege Insurance, Jembe Media Group pamoja na Coca Cola.
Msanii huyo anatarajiwa kutumbuiza katika tamasha hilo kwa kupiga ‘Live Music’ katika uwanja wa CCM Kirumba ambapo msanii wa kimataifa kutoka nchini, Diamond Platnumz, FID Q, Stamina, Mr. Blue, Ney wa Mitego, Maua Sama, Rubby, Baraka Da Prince, Juma Nature, MO Music na wengine wengi watapanda jukwaa moja na msanii Neyo.
Neyo check out from the hotel Hyatt Regency 
Msanii wa Kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo akiondoka katika hoteli ya Hyatt Regency-The Kiliamanjaro kueelekea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa safari ya jiji Mwanza kutumbuiza kwenye Jembeka Festival 2016 ambapo wadhamini wakuu ni Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Fastjet, SYSCORP Cooperation, CF Hospitals, KK Security, Samsung, EF Outdoor, Lacairo Hotel, Ndege Insurance, Jembe FM. Kulia ni Meneja wa Hoteli hiyo, Timothy Mlay.
IMG_5465
Attu Mynah and Neyo 
Meneja Masoko wa CFAO Motors Group, Attu Mynah ambao wamedhamini usafiri uliotumika kumwendesha msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo gari aina Mercedes Benz GLE 350 D ya mwaka 2016 katika picha ya kumbukumbu na Msanii huyo kabla ya kuelekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.
Neyo ta Hyatt Regency-The Kilimanjaro
Msanii wa kimataifa Neyo aki-show love na walinzi maalum kabla ya kuelekea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere tayari kwa safari ya Mwanza.
Neyo official car Mercedes Benz GLE 350 D of 2016
Msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo akielekea kwenye gari maalum aina ya Mercedes Benz GLE 350 D ya 2016 lilitolewa na kampuni ya CFAO Motors Group.
Neyo Sorrounded by Tanzanian Bodyguard 
Msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Mwalimu JK Nyerere akiwa amezungukwa na walinzi maalum alipokuwa akielekea jijini Mwanza.
Neyo at Julius Nyerere International Airport 
Msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere akiwa na mlinzi wake wakielekea jijini Mwanza leo jioni.
Costantine Magavilla and NeyoMwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Jembeka Festival 2016, Costantine Magavilla (t-shirt ya blue) na Msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo wakijianda kupanda ndege ya Shirika la Fastjet katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kuelekea jijini Mwanza. Shirika la Ndege la Fastjet ni miongoni mwa wadhamini wa tamasha hilo.
Neyo Crew to MwanzaMkurugenzi Mtendaji wa Jembe Media Group, Dr. Sebastian Ndege akiwa na ‘crew’ iliyoambatana na msanii wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Neyo wakipanda ndani ya ndege ya Shirika la Fastjet ambao ni miongoni mwa wadhamini wa Jembeka Festival 2016 kutokea jijini Dar es Salaam kuelekea jijini Mwanza.
WAZIRI MKUU AFAFANUA KUHUSU KUTENGULIWA KWA UTEUZI WA WAZIRI KITWANGA

WAZIRI MKUU AFAFANUA KUHUSU KUTENGULIWA KWA UTEUZI WA WAZIRI KITWANGA

May 20, 2016

JIL 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema uamuzi wa Rais Dk. John Pombe Magufuli kutengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Charles Kitwanga umefuata kanuni za utumishi wa umma ambao unakataza mtumishi kulewa akiwa kazini.
“Zipo sheria za utumishi ambazo mtumishi hatakiwi kunywa pombe na wala hapaswi kulewa akiwa kazini… mtumishi anapaswa kuwa na akili timamu inayokuwezesha kufanya kazi za Serikali,” alisema.
Ametoa ufafanuzi leo usiku (Ijumaa, Mei 20, 2016) wakati akijibu swali la mwandishi wa TBC1 aliyetaka kujua kama taarifa zilizoenea kuhusu kutenguliwa kwa Waziri huyo ni za kweli.
“Ni kweli Mheshimiwa Rais, Dk. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Charles Kitwanga kuanzia leo tarehe 20 Mei, 2016 baada ya kuonekana amelewa wakati wa kazi. Na hili lilibainika pale alipokuwa akijibu maswali ya wizara yake leo asubuhi,” alisema Waziri Mkuu.
Waziri Mkuu amesema kuna swali aliloulizwa ambalo hakulijibu vizuri na kwamba swali hilo litapaswa kurudiwa kuulizwa baada ya wabunge kuomba muongozo wa swali hilo.
IMETOLEWA NA: OFISI YA WAZIRI MKUU,
  1. L. P. 980,
DODOMA.
IJUMAA, MEI 20, 2016.

WAUGUZI MUHIMBILI WAADHIMISHA SIKU YAO LEO.

May 20, 2016


  Mkurugenzi wa Uuguzi na Ukunga wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Agness Mtawa akisoma kiapo kwa wauguzi katika maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani. Maadhimisho hayo yamefanyika leo katika hospitali hiyo. 
 Wauguzi wa hospitali hiyo wakila kiapo katika maazimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani.
 Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Laurence Museru akifuatilia maazimisho ya Siku ya Waaguzi Duniani yaliofanyika leo ukumbi wa CPL kwenye hospitali hiyo.
 Mwenyekiti wa Chama Cha Wauguzi Tawi la Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Sabastian Luziga akisoma risala ya wauguzi mbele ya Kaimu Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Profesa Laurence Museru.
 Wauguzi, Cleopatra Mtei (kushoto) na Nasra Said (kulia) wa hospitali hiyo wakifuatilia risala iliyosomwa leo na mwenyekiti huyo.

Baadhi ya wauguzi wa hospitali hiyo wakifuatilia risala iliyosomwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Wauguzi Tawi la Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Sabastian Luziga. 
PICHA NA JOHN STEPHEN, HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI (MNH)

KAIMU  Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru amewakumbusha wauguzi kufanya kazi kwa kufuata maadili na misingi ya taaluma yao na kuwafichua wachache ambao wanaenda kinyume na maadili kazi ili hatua stahiki zichukuliwe.

Profesa Museru ametoa wito huo leo katika maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duaniani , ambapo wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili leo wameadhimisha siku hiyo.

Katika maadhimisho hayo Profesa Museru amewasisitiza wauguzi hao kutambua kwamba muuguzi ni mtu muhimu katika kutoa huduma, hivyo hawana budi kuwahudumia wagonjwa kwa moyo ili kuondoa malalamiko.

“ Nawaomba muwafichue wale wachache ambao wanatoa lugha zisizofaa kwa wagonjwa kwani mkifanya hivyo mtatusaidia sana kuondoa kero na malalamiko yanayotolewa dhidi yenu,” amesema Profesa Museru.

Mipango ya Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Akielezea mipango ya MNH Profesa Museru amesema Hospitali hiyo ina mpango wa kuwaendeleza kitaaluma watumishi wake wakiwemo wauguzi ili watoe huduma yenye kiwango cha juu zaidi.
Mpango mwingine ni kuboresha sehemu za kufanyia kazi, kununua vifaa tiba kadiri fedha zinavyopatikana pamoja na kutafuta kibali kwa lengo la kuajiri wauguzi wengine ili wasaidie kutoa huduma kwani wauguzi waliopo sasa hawatoshelezi mahitaji.

Kutekeleza agizo la Rais
Kwa mujibu wa Profesa Museru Hospitali ya Taifa Muhimbili imefanya mabadiliko makubwa katika kutekeleza agizo la Rais Dk John Magufuli na kuhakikisha kwamba wagonjwa wanaokuja kutibiwa MNH wanapata dawa na kupata vipimo kwa wakati. 

Hivyo ametoa wito kwa wauguzi kushiriki katika jitihada zote zinazofanywa na Hospitali katika kuongeza mapato ya hospitali hiyo.

Akisoma risala ya wauguzi, Mwenyekeiti wa chama cha wauguzi Tawi la MNH, Sebastian Luziga amesema changamoto inayowakabili ni kuwapo kwa idadi ndogo ya wauguzi hali inayoathiri utendaji kazi.


“Idadi ya wauguzi ni ndogo ukilinganisha na idadi ya wagonjwa kwani kwa siku muuguzi anahudumia wagonjwa kati ya 20 hadi 30 tofauti na uwiano ambao muuguzi mmoja anatakiwa kuhudumia wagonjwa 6 hadi 8 kwa siku.” Amesema Sebastian.

Kauli mbiu ya siku ya wauguzi Duniani mwaka huu ni “Wauguzi Nguvu ya Mabadiliko, Uboreshaji wa uthabiti wa mifumo ya afya”

Mei 12 wauguzi wote Duniani wanamkumbuka muasisi wa uuguzi mama Florence Ningtngale.

YANGA YAWASILI NCHINI,YAPOKELEWA KWA KISHINDO NA MASHABIKI WAKE.

May 20, 2016


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
MABINGWA wa soka Ligi Kuu ya Bara wamewasili jijni wakitokea Angola katika mechi ya narudiano dhdi ya Espirance Sagdrada ya Angola.

Yanga ambayo imefuzu hatua makundi wamewasili mida ya saa nane na dakika 45 na mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa kocha wa timu hiyo Hans Van Pluijim amesema timu imefanya vizuri pamoja na figisu figisu ambazo wamefanyiwa.

Amesema anawapongeza viongozi wa Yanga kwa kupambana na hujuma lakini wamefanikiwa kuingia hatua ya makundi na wamejifunza mengi Angola ambapo watayafanyiwa kazi huku akiwapongeza wachezaji wake kwa juhudi walizoonyesha uwanjani kuhakikisha wanafuzu.

"Wachezaji wamefanya vizuri na wamejituma na kuhahakikisha wanavuka hatua hiyo na wamejituma sana nawapongeza na tumejifunza mengi sana Angola,"amesema Pluijm

Amesema  kikosi kwa sasa hakina cha kupoteza kitaendeea na kambi kuhakikisha wanasonga mbele katika mashindano hayo lengo lao ni kuona wanafika hatua ya fainali.
Golikipa wa timu ya Yanga Deogratius Munish Dida akizungumza na waandishi wa habari baada y kuwasili kutoka Angola.
 Kocha Mkuu wa Yanga Hans Van De Pluijm akiwasabahi mashabiki wa timu ya Yanga waliofika kuwalaki uwanja hapo mapema leo mchana.
 Wachezaji wa Yanga wakitoka  nje ya uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakitokea nchini Angola
 Wachezaji wa Yanga wakitoka  nje ya uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakitokea nchini Angola
 Kocha Mkuu wa Yanga Hans Van De Pluijm akiwasabahi mashabiki wa timu ya Yanga
  Wachezaji wa Yanga wakitoka  nje ya uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakitokea nchini Angola.Picha na Zaynab Nyamka,Globu ya Jamii.