MKINGA wakubaliana na Agizo la RC Gallawa.

MKINGA wakubaliana na Agizo la RC Gallawa.

May 02, 2013
Na Oscar Assenga,Mkinga.

MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga wamesema kimsingi wamekubaliana na agizo la Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Chiku Gallawa lakuzuia ugawaji wa eneo katika msitu wa Segoma kwa manufaa ya uhifadhiwa mazingira.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga,Andrew Ngoda alitoa taarifa hiyo jana wakati akifafanua juu ya maazimio ya kikao cha baraza la madiwani lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita juu msitu huo wa Segoma.

Alisema licha ya kuwa kulikuwa na mvutano katika kikao cha baraza hilo huku baadhi ya madiwani wakitaka eneo la msitu huo limegwe ili wanavijiji vinavyouzunguka wagawiwe lakini kimsingi mwisho wa majadiliano baraza liliamua kwa kauli moja kukubaliana na agizo la Mkuu wa Mkoa wa Tanga la kuzuia.

“Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga pamoja na kwamba lina mamlaka ya kufanya maamuzi yake lakini katika hili la msitu wa Segoma haliwezi kupingana na amri ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kwa sababu ina lengo la kuhakikisha msitu huo unadumu na uhifadhi wa mazingira unaendelea”alisema Ngoda.

Aidha maazimio katika kikao hicho walikubaliana kuwa kwa kuwa lengo la mkuu wa mkoa ni uhifadhi wa mazingira jambo ambalo ni la msingi hivyo baraza lilikubaliana kwamba msitu huo uendelee kuwa hifadhi lakini uwe chini ya wanakijiji cha Segoma.

MWISHO

Mei Day

May 02, 2013
WAFANYAKAZI wakijipanga kuvuta kamba katika sherehe za sikukuu ya Wafanyakazi Mei Day iliyofanyika jana kwenye uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga,Picha na Mwandishi Wetu.

Mei Day Oyeeeee

May 02, 2013
WAFANYAKAZI kutoka sekta mbalimbali mkoani Tanga wakiwa na mabongo wakiingia kwenye uwanja wa Mkwakwani jana katika sherehe za sikukuu ya Wafanyakazi Mei Mosi ambapo Kimkoa ilifanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga,Picha na Mwandishi Wetu.
MAAGIZO YA FIFA KUHUSU UCHAGUZI WA TFF

MAAGIZO YA FIFA KUHUSU UCHAGUZI WA TFF

May 02, 2013
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
 
Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limelitaka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuanza upya mchakato wa uchaguzi baada ya kubaini kasoro iliyotokana na ukosefu wa kutokuwepo vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadili.

FIFA ambayo ilituma ujumbe wake katikati ya mwezi uliopita kufanya utafiti kuhusu mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa TFF ambao ulisimamishwa baada ya baadhi ya wagombea kulalamika, imetaka uchaguzi ufanyike kabla ya tarehe 30 Oktoba 2013, lakini ukitanguliwa na mabadiliko ya katiba ambayo yatahusisha uundwaji wa vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadili.

Raiswa TFF, Leodegar Tenga aliwaambia waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa shirikisho hilo kuwa suala la Tanzania lilijadiliwa kwenye kikao cha Kamati ya Dharura ya FIFA kilichofanyika tarehe 28 Aprili 2013 na maamuzi yake kutumwa juzi kwa barua iliyosainiwa na KatibuMkuuwa FIFA, Jerome Valcke.

Baada ya kupokea barua hiyo, Rais wa TFF alifunga safari kwenda Dodoma jana kukutana na Mheshimiwa Waziri na Naibu wake pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

“Matarajio yetu sote yalikuwa kupokea majina ya waliopitishwa ili tufanye uchaguzi. Kinyume chake tumepokea maagizo hayo. Hata hivyo tumeona kuwa hili ni jambo la kheri kwa vile siyo tu haki itatendeka bali pia itaonekana imetendeka.” alisema Tenga, ambaye alishatangaza kuwa hatagombea tena urais baada ya kuliongoza Shirikisho kwa vipindi viwili vya miaka minne kila kimoja.

“Lengo letu ni kuhakikisha maagizo hayo yanatekelezwa na uchaguzi kufanyika mapema iwezekanvyo kabla ya tarehe iliyotolewa. Yale mambo nayoweza kufanyika kwa pamoja yatafanyika ili tuharakishe utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na FIFA.”

Uchaguzi wa TFF ulipangwa kufanyik tarehe 23 na 24 Februari 2013 na ulikuwa ukielekea ukingoni, lakini baadhi ya wagombea walienguliwa katika hatua ya mwisho na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na ndipo walipo andika barua FIFA kuomba iingilie kati.

Rais Tenga alisema kuwa ujumbe wa FIFA ulikutana na pande zote zilizoathiriwa na mchakato wa uchaguzi na kwamba baada ya kukusanya taarifa hizo, maagizohayo ya FIFA sasa yatakuwa ni suluhisho la matatizo ya muda mrefu katika uendeshaji wa mpira wa miguu nchini.

Katika barua hiyo, FIFA imeiagizaTFF:

1. Kuunda vyombo sahihi (Kamati ya Maadili itakayokuwa na vyombo viwili ambavyo ni cha kutoa maamuzi ya awali na cha rufaa) ambavyo mamlaka yake yatakuwa ni kushughulikia masuala ya ukiukwaji wa maadili;

2. Kufanya mabadiliko ya katiba kwa kuzingatia uundwaji wa vyombo hivyo;

3. Kuanza upya kwa mchakato wa uchaguzi wa Kamati ya Utendaji kwa kufungua milango kwa wagombea ambao walishachukua fomu na wagombea wapya:

4. Shughuli hiyo ikamilike ifikapo tarehe 30 Oktoba 2013.

Katika kutekeleza hayo, TFF inatakiwa iitishe Mkutano Mkuu wa Dharura kwa ajili ya kufanya mabadiliko ya Katiba kwa ajili ya kuunda kamati hizo za maadili na Kanuni za Uchaguzi kabla ya kuendelea na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Kamati Mpya ya Utendaji.

Katika maoni yake FIFA imeeleza kuwa katika mchakato, Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliwaengua au kupitisha baadhi ya wagombea kwa kubaini kuwa walikiuka Ibara ya 9 (7) ya Kanuni za Uchaguzi na pia Ibaray a 29 (7) ya Katiba ya TFF ambavyo vinahusisha suala la kufungua kesi mahakamani, kufuja fedha za shirikisho na ukosefu wa uwajibikaji wa pamoja.

Hata hivyo, FIFA ilisema kuwa watu hao walitakiwa waadhibiwe kwanza na kamati husika (kamati za maadili) kabla ya kuenguliwa na kamati za uchaguzi za TFF.

“Kutokana na ukosefu wa kamati za maadili matokeo yake, mmoja wa wagombea amekuwa akienguliwa kwenye uchaguzi kila anapombea bila ya kujua adhabu yake ni ya muda gani,” inasema barua hiyo ya FIFA.

Rais Tenga ameagiza kuitishwa kwa kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji ya TFF kupokea maagizo ya FIFA na kupanga ratiba ya utekelezaji wake kwa lengo la kuhakikisha kuwa mchakato huu unatekelezwa mapema iwezekanavyo.

      Mwisho.