TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Aprili 2, 2014
WACHEZAJI NGORONGORO HEROES WAAHIDI USHINDI
Nahodha
wa timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro
Heroes), Aishi Manula amesema wamejipanga kwa ajili ya kupata ushindi
kwenye mechi dhidi ya Kenya itakayochezwa Jumapili (Aprili 6 mwaka huu)
katika mji wa Machakos.
Akizungumza leo (Aprili 2 mwaka huu)
kwenye hafla ya kukabidhiwa bendera kwa timu hiyo kwenye ofisi za
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Manula ambaye pia anaidakia
timu ya Azam alisema lengo lao ni kufanya vizuri kwenye mechi hiyo.