WATUHUMIWA 16 WANAODAIWA KUJIHUSISHA NA VITENDO VYA UGAIDI WAPANDISHWA KIZIMBANI NCHINI

WATUHUMIWA 16 WANAODAIWA KUJIHUSISHA NA VITENDO VYA UGAIDI WAPANDISHWA KIZIMBANI NCHINI

July 17, 2014

001 
Baadhi ya watuhumiwa wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya ugaidi katika  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakisindikizwa na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), kuingia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Julai  17,2014 kusomewa mashitaka yao. Watuhumiwa 16 walisomewa mashitaka.
002 
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiimarisha ulinzi.
003Watuhumiwa wakiingia ndani ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
004005 006 007 008Watuhumiwa wakipelekwa maabusu baada yakusomewa mashitaka yao.
009Watuhumiwa wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya ugaidi wakiwa kwenye  ulinzi mkali.
PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE DAR ES SALAAM

MKUTANO WA KUJADILI MASUALA YA KODI AFRIKA WAFANYIKA JIJINI ARUSHA

July 17, 2014

 Waziri wa fedha Saada mkuya akijadiliana jambo na rais wa kituo cha kimataifa cha ukusanyaji kodi na uwekezaji Daniel Witt wakati wa mkutano wa siku 3 wa majadiliano ya masuala ya kodi Afrika uliofanyika jijini Arusha jana
katika hotel ya naura spring.
Mkurugenzi mkuu wa TRA Rished Bade akizungumza wakati wa ufunguzi wa  mkutano wa siku 3 wa majadiliano ya masuala ya kodi Afrika uliofanyika jijini Arusha jana
 Picha ya pamoja
 Viongozi wa kuu
 Waziri Saada Mkuya akihojiwa na wanahabari.
waziri wa fedha Saada Mkuya katikati  akiwa na mkurugenzi mkuu wa TRA kulia Rished Bade na kushoto dr.Jeffrey Owens mtaalam msahuri wa kodi na mhadhiri chuo kikuu cha uchumi na biashara Viena mara baada ya waziri kufungua mkutano wa majadiliano ya masuala ya kodi unaofanyika jijini Arusha

LORI LA MIZIGO LAGONGA KILABU CHA POMBE NA KUUA WATU WATANO PAPO HAPO

July 17, 2014

 Lori la Mizigo likiwa limepaki katikati ya kilabu hicho cha pombe ambacho kilisambalatishwa chote na chini ni mabaki ya kilabu hicho.
 Mashuhuda wakiwa wanashuhudia ajali hiyo baada ya kutokea
  Miili minne ya Marehemu ambao walifariki papo hapo baada ya Lori hilo kugonga kilabu hicho ikiwa imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Rufaa ya Iringa.
 Baadhi ya wananchi wa Eneo la Isimila wakiwa wameongezeka kushuhudia ajali hiyo mbaya iliyo uwa wata watano papo hapo.
 Hivi ndivyo Lori hilo la Mizigo lilivyo umia vibaya baada ya kugonga kirabu hicho na kukisambalatisha usiku wa kuamkia jana na kusababisha vifo vya watu watano papo hapo.
 Baadhi ya Ndugu wa Marehemu wakipata taarifa za Ajali hiyo katika eneo la tukio isimila
Ndugu wa Marehemu wakiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa kwa ajili ya kuwaona Marehem hao.
 
Picha zote na Iringa Yetu Blog

HIVI NDIVYO RAIS KIKWETE ALIVYOZINDUA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA MKINGA

July 17, 2014

Mhe. DktJakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa na viongozi wa kitaifa, Mkoa  na Wilaya ya Minga mwishoni mwa wiki wakati akizindua rasmi nyumba mpya za gharama nafuu  ambazo zimejengwa na Shirika la nyumba (NHC) kwa ajili ya  watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga   zinalenga kupunguza kero ya makazi kwa watumishi hao .

 Mhe. Kikwete amekuwa kwenye ziara ya siku moja katika Wilaya hiyo ambapo amepata fursa ya kuongea na wananchi katika mkutano wa hadhara  na kisha kuwafuturisha eneo la malamba jeshini.
 Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Benedick Kilimba  akimuonyesha Rais Jakaya Kikwete michoro ya nyumba ambazo Shirika hilo imezijenga Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga wakati wa uzinduzi  wa mradi wa nyumba za gharama nafuu kwa watumishi wa Wilaya hiyo jana
 Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi wa nyumba mpya za watumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Mkinga  Mkoani Tanga zilizojengwa na Shirika la nyumba la Taifa (NHC), kulia ni  Naibu Waziri wa Ardhi, nyumba na Maendeleo na Makazi, George Simbachawene  na kushoto ni Mwakilishi wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba  na  watatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa.



Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuashiria kupokea  mashine mpya na za kisasa 40  za kufyatulia  matofali (Hydraform) ambazo Shirika la nyumba la Taifa (NHC)  imezipa Halmashauri zote za Mkoa wa Tanga ili kuwapatia vikundi vya vijana  kuanzisha mradi wa ufyatuaji wa matofali na kuweza kujikwamua kimaisha. Picha na Salim Mohamed-Mwananchi

HIVI NDIVYO RAIS JAKAYA KIKWETE AKUTANA NA MGOMBEA WA URAIS WA MSUMBIJI MKOANI TANGA JULAI 12

July 17, 2014



 Mgombea wa Urais wa Msumbiji kwa tiketi ya Chama cha FRELIMO Mheshimiwa Filipe Nyusi pamoja na mwenyeji wake Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakivishwa skafu baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege mkoani Tanga ambapo alikutana na Mwenyekiti wa CCM Taifa,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete.
  Mgombea wa Urais wa Msumbiji kwa tiketi ya Chama cha FRELIMO Mheshimiwa Filipe Nyusi akishiriki kucheza ngoma na wenyeji wa Tanga waliojitokeza wakati wa mapokezi.
  Mgombea wa Urais wa Msumbiji kwa tiketi ya Chama cha FRELIMO Mheshimiwa Filipe Nyusi akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mheshimiwa Chiku Galawa mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Tanga.
Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Mgombea wa Urais wa Msumbiji kwa tiketi ya chama cha FRELIMO Mheshimiwa Filipe Nyusi katika Ikulu ya Tanga ambapo walifanya mazungumzo.
Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia Chama cha FRELIMO Mheshimiwa Filipe Nyusi akimsalimia Mzee Said Mbaruku wa Tanga wakati alipomtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akiwa kwenye mazungumzo na Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia Chama cha FRELIMO Mheshimiwa Filipe Nyusi,Ikulu mjini Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kwenye mazungumzo na Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia Chama cha FRELIMO Mheshimiwa Filipe Nyusi pamoja na Mbunge wa Tanga Mjini Mheshimiwa Omar Nundu nje ya Ikulu mjini Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete na Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia Chama cha FRELIMO Mheshimiwa Filipe Nyusi wakiwa kwenye picha ya pamoja Ikulu Ndogo mjini Tanga,wengine katika picha ni Komredi Oscar Monteiro,Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ,Mbunge wa tanga mjini Mh.Omar Nundu ,WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Kapteni Mstaafu George Mkuchika na Viongozi wengine kutoka Msumbiji
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia Chama cha FRELIMO Mheshimiwa Filipe Nyusi mara baada ya kumaliza mazungumzo Ikulu mkoani Tanga.(Picha na Adam Mzee).

ZIARA YA RAIS KUFUNGUA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU MKUZO, SONGEA

July 17, 2014


 
Rais Jakaya Kikwete na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mh. Saidi Mwambungu kulia , Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa shirika la Nyumba NHC Bw. David Shambwe wakikata utepe kwa pamoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi huo.

 Rais Dr. Jakaya Kikwete akipata taarifa ya mradi huo wa nyumba za gharama nafuu kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa shirika la Nyumba NHC Bw  David Shambwe

  Rais Dr. Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo 

 Rais Dr. Jakaya Kikwete akiwasili  katika eneo la mradi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na Shirika la Nyumba  (NHC) na kupokelewa na Ndg. David Shambwe Kaimu Mkurungenzi Mkuu NHC na Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara wakati alipokagua mradi huo uliopo katika wilaya ya Songea mkoani Ruvuma  akiwa katika ziara yake ya kikazi leo, Rais Dr. Jakaya Kikwete anaendelea na ziara mkoani  humo leo. (PICHA ZOTE KWA HISANI YA KITENGO CHA MAWASILIANO NA HUDUMA KWA JAMII CHA NHC)

 Rais jakaya Kikwete akipata maelezo ya kuhusu Mashine za kufyatulia matofali  ambazo zimegawiwa kwa kila wilaya za mkoa wa  Ruvuma

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka akizungumza katika hafla hiyo mchana huu

 Akiwasalimia wananchi waliofika kushuhudia


Vikundi vya nguma na burudani ikiburudisha katika tukio hilo mchana wa leo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, alipofungua leo hii nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC katika eneo la Mkuzo, Mkoani Ruvuma.
Kwa ujumla Mh. Rais alisema yafuatayo:-
      Amerejea kauli yake aliyoitoa Kasera , Mkinga Tanga kwa kulipongeza Shirika kwa kazi nzuri linayofanya hususan ya uamuzi wake wa  kizalendo wa kujenga nyumba za watu wa kipato cha kati na chini katika Halmashauri za Miji na Wilaya hapa nchini.
      Alizitaka Halmashauri za Miji na Wilaya kulipatia Shirika pamoja na mashirika na mifuko mingine ya jamii kama NSSF, PPF, LAPF, GEPF na mengineyo ardhi yenye masharti nafuu ili kuwezesha ujenzi wa nyumba na hatimaye kuweza kuipanga miji ipasavyo.
      Aliziagiza Halmashauri hasa ya Songea kutumia fursa za mikopo kutoka benki washirika na NHC kuweza kununua nyumba za gharama nafuu zilizojengwa badala ya kuendelea na mtindo wa kutaka kupanga nyumba hizo..
     Alilipongeza Shirika kwa kuwezesha vijana mashine za kufyatulia matofali jambo ambalo litatoa ajira kwa vijana. Alifurahishwa na mpango huo na kuzitaka Halmashauri nchini kuusaidia mpango huo ili uwe endelevu na wenye manufaa kwa vijana.
Rais Kikwete afungua ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma

Rais Kikwete afungua ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma

July 17, 2014


1 (1) 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipanda mti wa kumbukumbu wakati wa ufunguzi  rasmi wa ofisi za taasisi ya kuzuia rushwa TAKUKURU mkoa mjini Songea leo.Kushoto ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bibi Mary Mosha.
2 (1) 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi jingo la ofisi ya TAKUKURU mkoa wa Ruvuma leo mjini Songea.
3 (1) 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na kaimu Mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU Bibi Mary Mosha wakifunua kitambaa katika jiwe la msingi wakati wa ufunguzi wa jingo la ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma leo.Rais Kikwete yupo katika ziara ya kikazi  ya wiki moja mkoani Ruvuma(picha na Freddy Maro)
MBUNGE MACHALI ATUHUMIWA KUMPIGA BABA YAKE MZAZI

MBUNGE MACHALI ATUHUMIWA KUMPIGA BABA YAKE MZAZI

July 17, 2014

Moses Machali Kasulu MjiniNa Mwandishi wetu,Kigoma
MBUNGE wa Jimbo la Kasulu mjini Moses Machali anatuhumiwa kumtwanga baba yake mzazi  Mzee Machali  sambamba na kumfukuza nyumbani kwake,kutokana na kitendo chake cha kulewa kupindukia ambayo imekuwa adha kwa mbunge huyo na kupelekea mgogoro mkubwa baina yake na mzazi  huyo .
Mbunge huyo amefikia hatua hiyo baada ya kuchoshwa na ulevi huo na kupelekea kumpa kichapo kilichosababisha kuteguka kwa mkono  sanjari na kumtupia nguo zake nje na hatimaye mzee huyo kukimbilia kwa Balozi wa nyumba kumi  Dickson Joaqim kwa msaada wa kisheria.
Awali Julai ,15, 2014 usiku mzee alichelewa kurudi nyumbani na alipomgongea mwanae afungue mlango ndipo akapata kichapo kutoka kwa mbunge huyo baada ya kuona adha hiyo ni sugu kwa mzee wake.
 
Akiongea kwa njia ya simu na mtandao huu mbunge huyo  alisema mzazi wake  anapenda kunywa pombe kupindukia hali inayomfanya kila wakati wagombane juu ya tabia hiyo ambapo kwa upande wa pili kisiasa inamuathiri katika uwajibikaji wake kwa wananchi.
Alisema baba yake anatumiwa na chama  cha ccm  kwa lengo la kumdhoofisha kisiasa hasa katika kipindi hiki cha majeruhi cha kuelekea uchaguzi mkuu mwakani na kumtaja balozi wa mtaa wa mwilavya  Dickson Joaqim ni miongoni mwa watu wanaomshawishi mzee wake  kituo cha polisi kumshtaki.
“sijafikia hatua ya kumpiga mzee wangu,najitambua ndio maana namsihi baba achane na pombe ambapo mimi najiskia vibaya kuona  analewa sasa tukiwekana sawa baadhi ya watu wanadai nampangia sheria na ndo hivyo wanazusha ya kuzusha” alibainisha Machali.
Alisema kwa  kuthibitisha  hilo umma kuwa hajampiga mzee wake  na kwenye mkutano wa hadhara wilayani hapo, atakuwa sambamba na mzee huyo na kukiri mzee wake amefuta kesi dhidi yake na kusisitiza ccm  watumie mbinu za ziada na kudai hawana jipya.
Shuhuda mmoja jina kapuni akiri kumuona  mzee huyo akiwa na `PF3′ akitembea kwa shida huku mkono wake ukiwa umevimba akipatiwa matibabu katika moja ya zahanati ya wilayani hapo
 
Akithibitisha  hilo Kamanda wa Polisi Mkoa Frasser Kashai alisema ni kweli mzee wake amefungua jalada la kumshataki mbunge huyo  na wao wanaendelea na uchunguzi zaidi ili kukamilisha taratibu za mashataka.