Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete azindua kampeni ya Urais

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete azindua kampeni ya Urais

August 23, 2015

7
8
Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizindua kampeni ya Urais katika viwanja vya Jangwani Jijini Dar es Salaam leo
(Picha zote na Freddy Maro).
umati 
Umati wa watu walifika Janwani.
9
DSC_8328
2
Umati wa watu walifika Janwani leo.
3
unnamed
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. John Magufuli akihutubia.
4 5
Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi akihutubia.
6
    Rais mstaafu, Benjamin Mkapa

BALOZI MPYA WA TANZANIA NCHINI MAREKANI MHE, WILSON MASILINGI AWASILI WASHINGTON DC

August 23, 2015

    Balozi mpya atakayeiwakilisha Tanzania nchini Marekani Mhe Wilson Masilingi akiwa amefuatana  na Mkewe  Marystella Masilingi pamoja na mwanae Nelson Masilingi wawasili kituoni kwake Washington DC, awali ya hapo Mhe Wilson Masilingi alikua Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi.
Mhe Wilson Masilingi mara baada ya kutua Washington DC akisalimiana na atakayekua dereva wake Virgilio Paz maarufu kama Bong.
Safari ya Mheshimiwa Balozi pamoja na mama ikianza kuelekea Hotelini kwake ambapo atapumzika kwa muda kabla ya kuingia nyumbani kwake Bethesda ,Maryland.
Mhe Wilson Masilingi mara baada ya kufika Hotelini kwake akisaidiwa mlango na Afisa wa Ubalozi Swahiba Habib Mndeme.

WADHAMINI WA LIGI YA BODABODA KIPUNGUNI "B" MFUKO WA PENSHENI WA PSPF WAFUNGUA RASMI MASHINDANO YA MPIRA WA MIGUU

August 23, 2015

 
  Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Delphin Richard akizungumza na madereva bodaboda wa Kipunguni 'B' kuhusu huduma zitolewazo na Mfuko wa Pensheni wa PSPF hasa katika uchangiaji wa hiari ambapo mtu yeyote anaweza kujiunga
  Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Josephat Sylvery Tirumanywa akizungumza na wananchi mbalimbali waliofanikiwa kuhudhuria ufunguzi wa mashindano ya mpira wa miguu kwa madereva bodaboda wakiume maeneo ya Kipunguni 'B' katika manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam
 Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma  akitoa maelezo ya kina kuhusu faida na huduma zitolewazo na Mfuko wa Pensheni wa PSPF hasa katika uchangiaji wa hiari, ambapo mtu yeyote anaweza kujiunga na kunufaika na huduma mbalimbali zilizo katika hifadhi ya jamii ya (PSPF), akiongea na madereva wa bodaboda wa Kipungunu 'B' wakati wa ufunguzi wa mashindano ya mpira wa miguu kwa madereva hao.
  Delphin Richard Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF,  akisalimiana na muamuzi wa mchezo wa ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Madereva wa Bodaboda wa Kipunguni 'B' ambapo mfuko wa PSPF imedhamini mashindano hayo. Katikati ni Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Josephat Sylvery Tirumanywa.

 
 Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Josephat Sylvery Tirumanywa akitambulishwa wachezaji
 Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Eliachi Remmy akisalimiana na wachezaji katika ufunguzi wa ligi ya madereva bodaboda.
Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Delphin Richard akizungumza mmoja wa wazee kuhusu Mfuko wa Pensheni wa PSPF hasa katika uchangiaji wa hiari, ambapo mtu yeyote anaweza kujiunga na kunufaika na huduma mbalimbali zilizo katika hifadhi ya jamii ya (PSPF)
  Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma akimjazia fomu ya Uchangiaji wa Hiari mmoja wa madereva wa Bodaboda wa Kipunguni B wilaya ya Ilala jijini Dar mara baaada ya kupata elimu na kuridhia na huduma za mfuko huo.

 Madereva bodaboda wawana mwitikio mkubwa wa kujiunga na mfuko wa PSPF kupitia (PSS) kwakujaza fomu za Uchangiaji wa Hiari
 Afisa wa mfuko wa pensheni, Delphin Richard(kushoto) akimuonesha sehemu ya kuweka alama ya dole gumba mmoja wa madereva wakati wa ujazaji  fomu za Uchangiaji wa Hiari
 Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Eliachi Remmy(kulia) akiwajazia fomu za Uchangiaji wa Hiari mmoja wa madereva wa Bodaboda wa Kipunguni B wakati wa mashindano ya mpira wa miguu katika eneo la Kipunguni B 

Madereva bodaboda wa mtaa wa Kipunguni 'B' kata ya Kivule manispaa ya Ilala wameanzisha ligi  ya mpira wa miguu kwaajiri ya kuendeleza kujenga afya zao kwa michezo kwani michezo ni afya kwa wote, wakati wa ufunguzi huo wa ligi hiyo ya madereva bodaboda wadhamini wa ligi hiyo ambao ni Mfuko wa pensheni wa (PSPF)nao hawakuwa mbali kwaajiri ya kuwawezesha madereva hao kwa kipindi chote cha ligi hiyo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa ligi hiyo mgeni rasmi ambaye ni mkaguzi msaidizi wa polisi kanda maalumu ya dare s salaam Josephat Sylvery Tirumanywa amewaasa madereva hao kuwa waweze kucheza kwa amani michezo yote na pia waweze kuwa ni miongoni mwa watu watakao jiunga na na mfuko wa (PSPF) ka kupitia (PSS) kwaajiri ya kuendelea kupata huduma zilizo bora na  zenye uhakika .

Pia Afisa masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Ismail Juma amesema wameamua kuungana na madeeva boda boda hao ili kuweza kuwapa elimu katika suala la kuwekeza na kufaidika na mafao mbalimbali yanayo tolewa na PSPF kwani Pindi watakapo jiunga na mfuko huo wataona matunda mengi hasa kutokana na kuwa ni watu ambao wanategemewa na familia zao hivyo kama Pspf wana mafao ambayo wataweza kujikwamua kama mafao ambayo wanaweza kuwasomesha watoto,vilevile fao la uzazi hata fau la nyumba pia ujiungapo na mfuko huu utafaidika na wala hauto jutia 

Naye Bw.Delphin Richard ambaye pia ni Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa (PSPF) amewasisitiza madereva kutii sheria za barabarani na pia kuweza kucheza ligi hiyo kwa amani maana wamepewa dhamana ya kuwasafirisha abiria kwa amani na upendo ,hivyo kati ya jeshi la polisi na madereva husaidiana kufanya kazi kwa umoja na hivyo kuweka mahusiano mazuri katika kufanikisha nchi yetu inajengwa na sisi watanzania kwa kuendeleza upendo na amani pindi tuwapo barabarani,aliongeza kwa kuwapa shukrani madereva ya kuweza kuchagua mfuko wa pensheni wa Pspf kuwa wadhamini wa michuano hiyo kwani PSPF ipo kwaajiri ya kila mmoja  na kuweza kuwaasa  waweze kuwahamasisha watu mbalimbali kuweza kujiunga na mfuko huo ili kuhakikisha mabadiliko ya wananchi mbalimbali yanatokea kimaisha ,elimu,afya na mengine mengi.

Mfuko wa pensheni wa PSPF unafuraha ya kuwa kwa sasa wananchi wanajua kile kilicho sahihi nakuongeza kuwa wananchi mbalimbali waweze kufika maeneo ya kipunguni B ilikuweza kushirikiana na madereva hao kwa kuwashangilia wakati ligi ikiwa inaendelea na ligi hiyo itakayo dumu kwa takibani wiki moja.


NI ZAIDI YA MAFURIKO JANGWANI LEO

August 23, 2015

 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwa wingi kwenye uzinduzi wa kampeni kwenye viwanja vya Jangwani.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha
 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 -2020
 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mgombea mwenza Samia Suluhu Hassan ilani ya uchaguzi ya CCM kwenye uzinduzi wa kampeni uliofanyika viwanja vya Jangwani.
 Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli pamoja na mgombea mwenza Mhe. Samia Suluhu Hassan wakionyesha Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015-2020  katikati ni Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ndiye aliwakabidhi ilani hiyo kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM Jangwani.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikweteakizungumza baada ya kukabidhi ilani kwa mgombea wa CCM
 Umati wa wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakiwa wamefurika kwa wingi kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM Jangwani.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa jiji la Dar es salaam waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam.


 Hii ndio CCM
 TOT wakitoa burudani kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM jijini Dar es Salaam.

 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(kulia) akiwa pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM jijini Dar es Salaam.
 Wasanii wa bongo wakiwa jukwaani.






MKUU WA MKOA MH.JOEL BENDERA AZINDUA MFUKO WA AFYA YA JAMII ULIYOBORESHWA ( CHF ) MKOANI MANYARA

MKUU WA MKOA MH.JOEL BENDERA AZINDUA MFUKO WA AFYA YA JAMII ULIYOBORESHWA ( CHF ) MKOANI MANYARA

August 23, 2015

New Picture
Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa CHF ILIYOBORESHWA mkoani Manyara,Mkuu wa Mkoa Mh.Joel Bendera akiwasili katika viwanja vya Halmshauri ya Mji wa Mbulu akiongozana toka kulia ni Mganga Mkuu wa Mkoa –Bw.Ally Uledi,Mkurugenzi wa CHF Bw.Eugene Mikongoti na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Dr.Michael Kadeghe.
New Picture (1)
Waziri katika ofisi ya Raisi Mauhusiano na Uratibu na Mbunge wa Hanang, Mary Nagu akawaelimisha wananchi umuhimu wa kujiunga na CHF ILIYOBORESHWA katika siku ya uzinduzi .Kulia kwake ni Mkurugenzi wa shirika la Pharm Access kutoka Uholanzi Bw.Sicco Van Gelder ambao ndio wafadhili wa mradi huu wakishirikiana na NHIF.
New Picture (2)
Mkurugenzi wa CHF Bw.Eugene Mikongoti akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Manyara katika moja ya banda la maonyesho ambapo wananchi walipata fursa ya kupimwa afya zao, kuchangia damu pamoja na kupata taarifa mbalimbali zihusuzo CHF iliyoboreshwa na NHIF.Wengine toka kushoto ni Bw.Isaya Shekifu Kaimu Meneja wa NHIF – Manyara, Bw. Ally Uledi- Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara na Dr.Heri Marwa Mkurugenzi wa Mradi wa Health Insurance – PharmAcess Tanzania
New Picture (3)
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mh.Joel Bendera akimkabidhi kadi ya CHF iliyoboreshwa mwanachama mpya aliyejiunga katika siku ya uzinduzi wa kimkoa wilayani Mbulu mkoani Manyara.
New Picture (4)
Mgeni rasmi wa siku ya uzinduzi wa CHF ILIYOBORESHWA mkuu wa Mkoa wa Manyara Mh.Joel Bendera akiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Mbulu Dr.Michael Kadeghe kukabidhi moja ya pikipiki tano zilizotolewa kwa maafisa wa CHF iliyoboreshwa ili kuwarahisishia kazi ya uandikishaji na uhamasishaji kwa wananchi wa tarafa tano za wilaya ya Mbulu.
New Picture (5)
Mkuu wa mkoa wa Manyara Mh.Joel Bendera akiwasha moja ya pikipiki tano alizokabidhi kwa maafisa wanaoshughulika na CHF ILIYOBORESHWA mbele ya umati wa wananchi wa wilaya ya Mbulu katika siku ya uzinduzi wa mradi huu kimkoa.
……………………………………………………………………………
Mkuu wa mkoa wa Manyara, Mh.Joel Bendera amezindua rasmi Mfuko wa Afya
ya Jamii Uliboreshwa (iCHF) mkoani Manyara.Uzinduzi huo uliohudhuriwa
na wageni mbalimbali akiwemo Mh.Mary Nagu(Mbunge-Hanang) na Waziri
katika ofisi ya Raisi Mahusiano na Uratibu, Wakuu wa wilaya za Hanang
na Mbulu pamoja Wawakilishi wa wizara ya afya na Ustawi wa Jamii,
ulifanyika katika viwanja vya halmashauri ya mji wa Mbulu.
Mkuu wa Mkoa alitoa maagizo kwa viongozi wa mkoa na wilaya kuhakikisha
kuwa wanasimamia vizuri mradi huu na kuhamasisha wananchi wajiunge kwa
wingi ili kufanikisha sera ya serikali ya kuboresha huduma za afya kwa
wananchi wote.
Pia halmshauri  za wilaya mkoani Manyara zimetakiwa kuweka bajeti maalum
itakayowezesha utekelezaji wa mpango endelevu wa kuziingiza kaya
maskini katika Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kila mwaka ili
kuwahakikishia huduma bora za matibabu.
Mradi huo wa iCHF mkoani Manyara unaendeshwa kwa ushirikiano baina
shirika la Pharm Access International (PIA) la Uholanzi, Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) na Halmashauri za wilaya za Mbulu, Babati
na Hanang kwa lengo la kuboresha huduma na kuhamasisha idadi kubwa ya
wananchi kujiunga na mfumo wa kulipia kabla gharama za matibabu ili
kuzuia vifo visivyo vya lazima katika jamii.
Bendera alisema ili kuiwezesha serikali kufikia lengo lake la
kufikisha huduma bora za afya kwa kila mtanzania kuna umuhimu wa
kipekee kwa halmashauri zinazounda mkoa huo kuhakikisha wananchi wote
wanajisajili katika iCHF wakiwemo maskini ili nao waweze kuhakikishiwa
upatikanaji wa matibabu.
“Kwa kutambua changamoto ya kutokuwepo rasilimali za kutosha katika
vituo vya kutolea huduma ndio maana serikali iliamua kuanzisha mfumo
huu wa kuchangia kidogo kila mwaka gharama za matibabu kabla ili
kumwezesha kila mwananchi kupata matibabu kwa nia ya kuchangia fedha
kidogo.”, alisema.
Aidha aliongeza, “Wito wangu kwenu wananchi ni jiandikisheni kwa wingi
kwasababu ugonjwa haupigi hodi… kwa upande wa halmashauri hebu anzeni
kuweka fedha kwa mpango mtakaokubaliana ili wale maskini nao waweze
kusaidiwa kupata matibabu kama wenzao wengine wenye uwezo wa
kuchangia”, alisema.
Awali Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya
(NHIF) Eugine Mikongoti akizungumza katika uzinduzi huo aliwataka
watoa huduma za afya kupitia iCHF kumaliza malalamiko ya wagonjwa kwa
kuhakikisha michango yote ya wananchi inatumika ipasavyo kwa ajili ya
kununulia dawa na vifaa tiba ili kuwawezesha kuona thamani halisi ya
fedha zao.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mradi wa PIA alisema katika miezi sita
kuanza kwa utekelezaji wa iCHF humo idadi ya wananchi wanaojiunga
inaongezeka kwa kasi kutokana na kuongezwa kwa idadi ya vituo vya
kutolea huduma, maduka ya dawa, ushirikihswaji jamii na uhamasishsaji