Na Oscar Assenga,Tanga.
UONGOZI wa Klabu ya African Sports "Wanakimanumanu"umeishukuru uongozi wa Dar es Salaam Young African kwa kuwapokea vema walipokuwa jijini Dar es Salaam pamoja na kuwaandalia malazi mazuri ambayo yaliifanya timu hiyo kujisikia kama wapo nyumbani wakati timu hiyo ilipokwenda kucheza na Friends Rangers ya Kinondoni kwenye uwanja wa Chamazi.
UONGOZI wa Klabu ya African Sports "Wanakimanumanu"umeishukuru uongozi wa Dar es Salaam Young African kwa kuwapokea vema walipokuwa jijini Dar es Salaam pamoja na kuwaandalia malazi mazuri ambayo yaliifanya timu hiyo kujisikia kama wapo nyumbani wakati timu hiyo ilipokwenda kucheza na Friends Rangers ya Kinondoni kwenye uwanja wa Chamazi.
Shukrani hiyo zilitolewa jana na Katibu wa Klabu
hiyo,Khatib Enzi ambapo alisema mapokezi waliyoyapata wakati wakiwa
jijini humo yalikuwa ya aina yake na hivyo kuamini hali ambayo inaonyesha mapenzi walionayo baina ya timu hizo mbili.
'Hawa ndio ndugu zetu ukarimu wao na ushirikiano
wao wakati tukiwa jijini Dar es Salaam ulidhihirisha kuwa mapenzi yao
kwetu ni makubwa zaidi hivyo tunahaidi kuendelea kuudumisha undugu huo "Alisema Enzi.
Mchezo huo ulimalizika kwa African Sports kukubali
kichapo cha mabao 2-1 na hivyo watalazimika kushinda bao 2-0 kwenye
mechi yao ya marudinao itakayochezwa kwenye uwanja
wa Mkwakwani mjini hapa Jumapili wiki hii ili timu hiyo iweze kujiweka
katika mazingira mazuri ya kusonga mbele kwenye mashindano hayo.
Akizungumzia maandalizi ya mechi hiyo,Enzi alisema
wachezaji wao wanaendelea vizuri na mazoezi yao kila siku katika uwanja
wa shule ya sekondari Usagara chini ya kocha wao
Edmund Nyoni ambaye kazi yake ni kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri
katika michezo yao mbalimbali kwenye mashindano hayo.
Alisema licha ya mandalizi hayo kuendelea vizuri
lakini wana mchezaji mmoja majeruhi,Rashid Mbu ambaye huenda akaikosa
mechi hiyo ambayo ni muhimu kwao kushinda ili kuweza kusonga mbele kwenye mechi zao zijazo na kuweza kutimiza azma yao ya kushiriki ligi daraja la kwanza msimu ujao.
Aidha waliomba wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza
kuisaidia timu hiyo ambayo imedhamiri kurudi ilipotokea na hivyo kuleta
hamasa na ushindani kwenye soka mkoani hapa na Tanzania kwa ujumla.
Mwisho.