RAIS KARIA KUKUTANA NA WAHARIRI WA HABARI ZA MICHEZO
Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF)
Wallace Karia atakutana na Wahariri wa Habari za Michezo Jumatano Desemba
27,2017.
Pamoja na mambo mengine Rais Karia atazungumzia
miezi minne tokea uongozi uliopo umeingia madarakani pamoja na vitu
vilivyofanyika katika muda huo.
Aidha Rais Karia ataelezea changamoto mbalimbali
zilizopo TFF pamoja na njia gani inatumika/Itatumika kuweza kupiga hatua kwa mpira
wa Tanzania.
Taarifa zaidi za mkutano huo wa Rais Karia na
Wahariri,mahali utakapofanyika pamoja na mualiko utatolewa kwa vyombo vya
habari.
Huu ni mkutano wa kwanza wa Rais Karia na Wahariri
wa habari za Michezo tokea ameingia madarakani.
Rais Karia aliingia madarakani August 12, 2017
kwenye uchaguzi uliofanyika mkoani Dodoma baada ya kushinda kwa kishindo kwenye
uchaguzi ambao pia uliwaingiza madarakani Michael Wambura kwenye nafasi ya
makamu wa Rais.
Wajumbe wa kamati ya utendaji waliongia madarakani kwenye
uchaguzi huo ni pamoja na
Kanda namba 13 Dar
es Salaam
Lameck Nyambaya
Kanda namba 12 Kilimanjaro na Tanga
Khalid Abdallah
Kanda No 11 Pwani na Morogoro
Francis Ndulane
Kanda Namba 10 Dodoma na Singida
Mohamed Aden
Kanda Namba 9 Lindi na Mtwara
Dunstan Mkundi
Kanda namba 8 Njombe na Ruvuma
James Mhagama
Kanda namba 7 Mbeya na Iringa
Elias Mwanjala
Kanda Namba 6 Katavi na Rukwa
Kenneth Pesambili
Kanda namba 5 Kigoma na Tabora
Issa Bukuku
Kanda namba 4 Arusha na Manyara
Sarah Chao
Kanda namba 3 Shinyanga, Simiyu
Mbasha Matutu
Kanda namba 2 Mara, Mwanza
Vedastus Lufano
Kanda namba 1 Kagera, Geita
Salum Chama
Imetolewa
na Idara ya Habari na Mawasiliano TFF
Desemba
22,2017
DC SENYAMULE AFUNGUA SEMINA YA KUWAJENGEA UWEZO VIONGOZI WA SERIKALI, DINI NA WASIMAMIZI MPANGO WA PETS
Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule (wa nne toka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali, dini na wasimamizi wa mpango wa "Public Expenditure Tracking System" (PETS) waliohudhuria semina iliyofanyika Same kwa kuwezeshwa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).
Na Kajunason/MMG.
Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule amewataka wasimamizi wa mpango wa Ufuatiliaji wa Matumizi ya Umma (PETS) kuwa na uadilifu katika kufiatilia matumizi ya fedha za serikali.
Hayo ameyazungumza leo wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo uliowakutanisha viongozi wa serikali, dini na wasimamizi wa mpango wa "Public Expenditure Tracking System" (PETS) uliofanyika Same kwa kuwezeshwa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).
Mhe. Senyamule alisema ni vyema watendaji hao wakafuata misingi imara itakayowezesha serikali kujua ni wapi wanamatumizi mabovu ya fedha katika halmashauli.
Aliagiza halmashauri kushirikiana kwa karibu na watu hao kwani kazi wanayoifanya ni ya halmashauri, hasa ukaguzi na mipango. "Idara ya ukaguzi ina watumishi 3 tu wanaohitaji kukagua kila kitu, sio rahisi wakidhi kwa wakati; lazima tuwashirikishe wadau wa PETS ili taarifa zao ziwe ni moja ya misingi ya ufuatiliaji kwa halmashauri," alisema Mhe. Senyamule.
Pamoja na yote Mhe. Senyamule aliomba CCT kuongeza idadi ya kata wanazofanyia kazi kutoka 11 hadi zote 34 zilizopo kwa sasa.
--
Cathbert Angelo Kajuna,
Founder and Mananging Director
Kajunason Blog,
P.O Box 6482,
Dar es Salaam.
Tel: +255 787 999 774
Alt: +255 765 253 445
www.kajunason.com
"Everything is Possible Through Peace & Stability''
SHAKA ATEMA NYONGO,ASEMA YUPO TAYARI KUWAJIBIKA IWAPO ITABAINIKA AMEFANYA UFISADI
Na Said Mwishehe,blogu ya jamii
KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM)Shaka Hamdu Shaka amesema yupo tayari kuwajibika iwapo itabainika anefanya ufisaidi wa aina yoyote katika utendaji wake kwenye nafasi aliyonayo sasa.
Shaka ametoa kauli hiyo kwenye ukumbi wa Vijana Social Hall Kinondoni jijini Dar es Salaam leo kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Umoja huo Taifa Kheir James Denis ambaye amepokelewa rasmi na kutambulishwa kwa vijana wa mkoa huo.
Amesema katika nafasi hiyo amekuwa akifanya jitihada mbalimbali za kutetea mali za umoja huo na kwa bahati mbaya hatua hiyo imemfanya apigwe vita na kumkwamisha.Amesema chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa,Dk.John Magufuli ataendelea kusimama imara kusimamia rasilimali za umoja huo na hatarudi nyuma.
Amesema amekuwa katika mazingira magumu yanayotokana na kupigwa na ikafika mahali baadhi ya watu wakaanza kumzushia mambo ambayo hayana ukweli wowote.Ametumia nafasi kueleza wazi yupo tayari kuchunguzwa na kuwa tayari kuwajibika iwapo itabainika ameshiriki kufuja mali za umoja huo."Nimeshambuliwa na kupigwa vita kwasababu tu ya kuwa na msimamo thabiti wa kusimamia mali za jumuiya na maadili.
" Naomba niseme leo hii ni siku ya historia kwangu kwani nimetoa la moyoni ambalo nimekuwa nalo muda mrefu,nimeshambuliwa na kupigwa vita bila sababu.Niseme nipo tayari kuwajibika kama nitabainika kufanya ufisadi kwa kutumia bafasi yangu,"amesema Shaka.
Amesema katika kusimamia mali za umoja huo amebaini kuliwa kwa zaidi ya Sh milioni 250 katika mabanda ya maduka ya biashara eneo la Ukumbi wa Vija a Social Hall Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Amesema kuliwa fedha hizo wakaamua kusimamisha shughuli za kibiashara na kinachoendelea kwa sasa ni kubomoa eneo hilo na kujengwa jengo la kitega uchumi ambalo litaingizia fedha umoja huo.
Ameelezea namna ambavyo amekuwa akitiwa moyo na Rais Magufuli na kufafanua hatarudi nyuma atashirikiana na mwenyekiti wa umoja huo taifa kuusimamia umoja huo.
KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM)Shaka Hamdu Shaka amesema yupo tayari kuwajibika iwapo itabainika anefanya ufisaidi wa aina yoyote katika utendaji wake kwenye nafasi aliyonayo sasa.
Shaka ametoa kauli hiyo kwenye ukumbi wa Vijana Social Hall Kinondoni jijini Dar es Salaam leo kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Umoja huo Taifa Kheir James Denis ambaye amepokelewa rasmi na kutambulishwa kwa vijana wa mkoa huo.
Amesema katika nafasi hiyo amekuwa akifanya jitihada mbalimbali za kutetea mali za umoja huo na kwa bahati mbaya hatua hiyo imemfanya apigwe vita na kumkwamisha.Amesema chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa,Dk.John Magufuli ataendelea kusimama imara kusimamia rasilimali za umoja huo na hatarudi nyuma.
Amesema amekuwa katika mazingira magumu yanayotokana na kupigwa na ikafika mahali baadhi ya watu wakaanza kumzushia mambo ambayo hayana ukweli wowote.Ametumia nafasi kueleza wazi yupo tayari kuchunguzwa na kuwa tayari kuwajibika iwapo itabainika ameshiriki kufuja mali za umoja huo."Nimeshambuliwa na kupigwa vita kwasababu tu ya kuwa na msimamo thabiti wa kusimamia mali za jumuiya na maadili.
" Naomba niseme leo hii ni siku ya historia kwangu kwani nimetoa la moyoni ambalo nimekuwa nalo muda mrefu,nimeshambuliwa na kupigwa vita bila sababu.Niseme nipo tayari kuwajibika kama nitabainika kufanya ufisadi kwa kutumia bafasi yangu,"amesema Shaka.
Amesema katika kusimamia mali za umoja huo amebaini kuliwa kwa zaidi ya Sh milioni 250 katika mabanda ya maduka ya biashara eneo la Ukumbi wa Vija a Social Hall Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Amesema kuliwa fedha hizo wakaamua kusimamisha shughuli za kibiashara na kinachoendelea kwa sasa ni kubomoa eneo hilo na kujengwa jengo la kitega uchumi ambalo litaingizia fedha umoja huo.
Ameelezea namna ambavyo amekuwa akitiwa moyo na Rais Magufuli na kufafanua hatarudi nyuma atashirikiana na mwenyekiti wa umoja huo taifa kuusimamia umoja huo.
MAKAMU WA RAIS AZINDUA KAMPENI KUIFANYA DODOMA KUWA YA KIJANI
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
ameagiza kuwa kampeni ya kupanda na ustawishaji miti isiishie Dodoma
mjini tu bali ienee katika Wilaya zote za mkoa wa huo na hatimaye nchi
nzima.
Makamu wa Rais aliyasema hayo kwenye uzinduzi wa kampeni ya kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa kijani,alisema
upandaji miti si kwa ajili ya kuhifadhi mazingira tu bali ni fursa ya
kiuchumi, kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo alitolea mfano
mti mmoja uliokomaa unaweza kunyonya hadi kiasi cha kilo 150 za gesi ya
hewa ya ukaa kwa mwaka,husaidia kupunguza joto, kusaidia kuboresha afya
zetu za mwili na akili kama tafiti zinavyoonyesha .
“Ni
dhahiri, kampeni hii ya kuifanya mji wa Dodoma kuwa wa kijani ni kuunga
mkono uamuzi wa Rais wetu, Dkt. John Pombe Magufuli wa kuhamishia
Makamo Makuu ya Nchi kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma kwa vitendo.”
Alisema Makamu wa Rais.Makamu
wa Rais amewataka Viongozi na Wana Dodoma kuipokea kampeni hii kwa
mikono miwili na kutoa kila aina ya ushirikiano ili kufikia lengo zuri
lililokusudiwa.
Makamu
wa Rais ambaye alihamia rasmi mjini Dodoma siku ya ijumaa tarehe 15
Desemba, 2017 alitoa pongezi kwa Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais
Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba na Ofisi yake kwa kuja na
wazo zuri .
Makamu
wa Rais alisisitiza kuwa hategemei kuona zoezi la upandaji miti lianze
na kuisha leo, na badala yake liwe la kudumu, pia alizitaka manisapaa
zitunge sheria ndogo zitakazoelekeza shule, chuo, taasisi na familia
kuanzisha bustani ndogo za miti zitakayomudu mazingira husika,Makamu wa
Rais aliendelea kusema kuwa ni vyema kupunguza ukataji wa miti kiholela
ambapo alizitaka sheria, kanuni na taratibu zizingatiwe kabla ya kukata
miti na kusema tupande miti kabla ya kukata mti.
Makamu
wa Rais alimalizia kwa kutoa shukrani kwa kampuni ya TATU Mzuka kwa
kujitoa na kuhakikisha kampeni hii inatekelezwa na kutoa wito kwa Bodi
ya Bahati Nasibu ya Taifa ya Tanzania iige mfano na kuelekeza makampuni
mengine ya bahati nasibu yaweze kutoa mchango wake katika shughuli za
kijamii hususan kwenye suala la hifadhi ya mazingira.
Pia
Makamu wa Rais alitoa shukrani kwa Jeshi la Kujenga Taifa Makotopora,
DUWASA, Magereza na Tanzania Forest Services (TFS) kwa kujitoa na
kushiriki kikamilifu kwenye zoezi hili.Mwisho, Makamu wa Rais aliwataka Wanawake wa mkoa wa Dodoma kuanzisha vikundi mbali mbali vya upandaji .
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akiandaa mti wake kabla ya kuupanda mara baada ya kuzinduzi kampeni ya
kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa Kijani iliyofanyika kwenye chanzo cha
maji bonde la Makutupora, Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akipanda mti mara baada ya kuzinduzi kampeni ya kuufanya mji wa Dodoma
kuwa wa Kijani iliyofanyika kwenye chanzo cha maji bonde la Makutupora,
Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akihutubia wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuufanya mji wa Dodoma kuwa
wa Kijani iliyofanyika kwenye chanzo cha maji bonde la Makutupora,
Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Waziri
wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January
Makamba akitoa maelezo ya kampeni ya kupanda miti wakati wa uzinduzi wa
kampeni ya kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa Kijani iliyofanyika kwenye
chanzo cha maji bonde la Makutupora, Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu
wa Rais)
WANAFUNZI SHULE ZA SEKONDARI IRINGA KUNUFAIKA NA ELIMU YA MASOMO YA SAYANSI
Wanafunzi
wa shule za sekondari manispaa ya iringa kunufaika na elimu ya masomo ya
sayansi kutokana na kuandaliwa kambi maalumu kwa ajili ya kuwafindisha kutoka
kwa walimu waliobobea katika masomo hayo kwa wanafunzi wa watakao kuwa tayari
kupata elimu hiyo.
Ofisi
ya mbunge wa viti maalum Ritta Kabati imeandaa mpango wa kuwaongezea elimua
wanafunzi wa shule za sekondari manispaa ya Iringa kwa kuanzisha kambi ya
masomo ya sanyasi itakayo kuwa inafanyika bure kwa wanafunzi wa watakao kuwa
tayari kupata elimu hiyo.
Akizungumza
na Nuru fm Dicksoni Kawovela ambaye ni mratibu wa miradi ya jamii kutoka ofisi
ya mbunge RITTA KABATI amesema kuwa wameamua kuja na mpango huo kwa lengo la
kuinua elimu ya sayansi kwa wanafunzzi wa shule za sekondari hapa manispaa.
Aidha
Kawovela amesema kuwa mafunzo hayo yatakuwa na manufaa kwa walimu na wanafunzi
watakaokuwa wanahudhuria masomo haya ambayo yatakuwa yanatolewa bure.
Kawovela
amewaka wazazi wa wanafunzi kuwaruhusu watoto wao kwenda kwenye makambi hayo
ili waongezewe uwezo katika masomo ya sayansi.
Hata
hiyo Kawovela alisema kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo atakuwa mama Salma
Kikwete ambaye ni mbunge wa kuteuliwa na Rais katika Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania
Subscribe to:
Posts (Atom)