BALOZI WA INDIA AAGANA NA RAIS DR.SHEIN

BALOZI WA INDIA AAGANA NA RAIS DR.SHEIN

July 17, 2015

Q1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi wa India nchini Tanzania Mhe,Debnath Shaw alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo,kumuaga Rais baada ya kumaliza muda wake wa kazi Nchini,[Picha na Ikulu.]
Q2
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na  Balozi wa India nchini Tanzania Mhe,Debnath Shaw alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo,kumuaga Rais baada ya kumaliza muda wake wa kazi Nchini, [Picha na Ikulu.]
Q3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na Balozi wa India nchini Tanzania Mhe,Debnath Shaw baada ya mazungumzo yao leo, alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais baada ya kumaliza muda wake wa kazi Nchini, [Picha na Ikulu.]
…………………………………………………..
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa hatua za India za kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuendeleza miradi mbali mbali ya maendeleo zinadhihirishwa uhusiano mwema na wa kihistoria uliopo baina ya pande mbili hizo.
Dk. Shein aliyasema hayo leo wakati mazungumzo kati yake na Balozi wa India katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaemaliza muda wake wa kazi hapa nchini Mhe. Debnath Shaw yaliyofanyika Ikulu mjini Zanzibar.
Katika mazungumzo hayo, Dk. Shein aliipongeza Serikali ya India kwa hatua yake ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha sekta zake za maendeleo.
Dk.Shein alisema kuwa Tanzania ikiwemo Zanzibar zina uhusiano na ushirikiano wa kihistoria na India ambao umeanzishwa na  waasisi wa nchi hizo akiwemo marehemu Julius Kambarage Nyerere na waasisi wa nchi hiyo akiwemo marehemu Indira Gandhi.
Dk. Shein alimueleza Balozi huyo kuwa Zanzibar inathamini sana uhusiano na ushirikiano kati yake na India hatua ambayo imesaidia kwa kiasi kikubwa kuwepo ushirikiano katika sekta mbali mbali za maendeleo ikiwemo elimu, afya, biashara, viwanda na nyenginezo.
Aidha, Dk. Shein alitoa pongezi kwa India kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta zake za maendeleo ikiwa ni pamoja na kutoa ushirikiano wake katika kuanzisha Chuo cha amali katika kijiji cha Kinyasini Mkoa wa Kaskazini Unguja ambacho wakati wowote kitazinduliwa.
Utekelezaji wa mradi huo wa ujenzi wa Chuo hicho ulidhihirishwa wakati wa ziara ya Dk. Shein nchini India mnamo Febuari mwaka 2014 alipotembelea chuo cha ‘Barefoot” kilichoko katika Jimbo la Jajasthan nchini India.
Katika mazungumzo na Balozi huyo, Dk. Shein alieleza kuwa kukamilika kwa chuo hicho kutasaidia juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutoa mafunzo ya amali na ujasiriamali sambamba na usambazaji wa umemejua na maeneo mengineyo ambapo mkazo mkubwa ni kuwawezesha wanawake wa vijijini kujikwamua na umasikini.
Sambamba na hayo, Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuipongeza Serikali ya India kwa nia yake ya kuendelea kutoa ushirikiano wake na kuunga mkono miradi ya maji, elimu na mengineyo huku akipongeza hatua zinazoendelea za kutekeleza makubaliano yaliofika katika ziara yake nchini.
Nae Balozi wa India katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Debnath Shaw alipongeza uhusiano na ushirikiano wa muda mrefu uliopo kati ya India na Zanzibar na kuadi kuuendeleza kwa lengo la manufaa kwa pande mbili hizo.
Balozi Shaw alisema kuwa India itahakikisha inakamilisha miradi yote ya maendeleo ilioanzishwa kwa mashirikiano kati yake na Zanzibar kwa kutambua kuwa kukamilika kwa miradi hiyo ndio chachu ya kuimarisha zaidi ushirikiano na uhusiano uliopo.
Aidha, Balozi Shaw alisema kuwa ziara ya Dk. Shein nchini India imeweza kupata mafanikio makubwa na kusisitiza imani yake kuwa makubaliano yote yaliofanyika baina ya India na Zanzibar yatatekelezwa kwa lengo la mafanikio kwa pande zote mbili.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Rais Kikwete azungumza na Watanzania waishio Uswisi

Rais Kikwete azungumza na Watanzania waishio Uswisi

July 17, 2015

 k
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na watanzania waishio  Switzerland katika hoteli ya Intercontinental jijini Geneva-Julai 16, 2015.
mail.google.com9
Watanzania waishio Switzerland.
j
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa ofisi ya mwakilishi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa  Geneva jana baada ya kuzungumza nao na kisha kupata futari katika Hoteli ya Intercontinental jijini Geneva Uswisi.
(picha na Freddy Maro)

MWANASHERIA MAKENE AREJESHA FOMU KUGOMBEA JIMBO LA KINONDONI

July 17, 2015

Mwansheria na Kada wa Chama cha Mapinduzi, Emmanuel Makene (katikati) akiwa ameambata na mkewe Dk. Sarah Makene kurejesha fomu za kuomba ridhaa ya wana CCM Kinondoni kuteuliwa kugombea Ubunge katika Jimbo la Kinondoni. Anaepokea fomu hizo ni Katibu wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe. Wengine ni wapambe wa mgombea huyo waliomsindikiza kurejesha fomu hizo leo.
Emmanuel Tamila Makene ambae ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya na Katibu wa Usalama na Maadili taifa wa Umoja wa vijana (UVCCM) akisaini kitabu cha kurejesha fomu huku mkewe Dk Sarah Makene akimwangalia kwa makini na Katibu wa CCM Wilaya akikagua fimu. Dk Sarah Makene ni Daktari katika Hospitali ya Mwananyamala anaeshughulika na wagonjwa wa Ukimwi na wWaathirika na dawa za kulevya.
Dk Sarah Makene ni Daktari katika Hospitali ya Mwananyamala anaeshughulika na wagonjwa wa Ukimwi na wWaathirika na dawa za kulevya, akipeana mkono na Katibu wa CCM Wilaya baada ya kupokea fomu za Muwewe.
Makene akiwa na Mkewe Dk Sarah pamoja na rafiki yao baada ya kurudisha fomu.
Makene akiwa na Mkewe Dk Sarah na marafiki zao baada ya kurejesha fomu.
RIDHIWANI KIKWETE KUTETEA KITI CHAKE CHA UBUNGE JIMBO LA CHALINZE, ACHUKUA FOMU LEO

RIDHIWANI KIKWETE KUTETEA KITI CHAKE CHA UBUNGE JIMBO LA CHALINZE, ACHUKUA FOMU LEO

July 17, 2015

????????????????????????????????????
Mh. Ridhiwani Kikwete mbunge wa jimbo la Chalinze akisalimiana na Diwania wa Kata ya Bwilingu Bw, Ahmed Masser wakati alipowasili katika eneo la mkutano uliofanyika mji mdogo wa Chalinze jana ukiwa na lengo la kuelezea utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM uliofanywa na Mbunge huyo kwa kipindi cha mwaka mmoja katika huduma za Afya, Elimu, Maji, Miundombinu, Uchumi, Michezo na amaendeleo mengine ya kijamii.
Mh. Ridhiwania Kikwete ametanganza rasmi jana katika mkutano huo nia yake ya kutetea jimbo la Chalinze ambapo leo mchana anatarajiwa kuchukua fomu katika ofisi za CCM wilaya ya Bagamoyo tayari kwa kuanza mchakato wa kuwania tena ubunge wa jimbo la Chalinze ili kuendeleza yale aliyokwishayaanza kutekeleza katika kipidi cha mwaka mmoja alipokuwa madarakani.
????????????????????????????????????
Mh. Ridhiwani Kikwete mbunge wa jimbo la Chalinze akisalimiana na wananchi mbalimbali wakati alipowasili katika eneo la mkutano mjini Chalinze.
????????????????????????????????????
Mh. Ridhiwani Kikwete mbunge wa jimbo la Chalinze akizungumza jambo na Katibu wake Bw. Idd Swala huku Diwani wa Kata ya Bwilingu Ahmed Nasser akisikiliza kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bw.ndugu Majid Mwanga.
????????????????????????????????????
Mh. Ridhiwani Kikwete mbunge wa jimbo la Chalinze akizungumza jambo na Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Ndugu Majid Mwanga.
????????????????????????????????????
Diwani wa Kata ya Bwilingu Ahmed Nasser akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Chalinze jana.
????????????????????????????????????
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Ndugu Majid Mwanga akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Chalinze jana.
????????????????????????????????????
Mh. Ridhiwani Kikwete mbunge wa jimbo la Chalinze akizungumza na wananchi mjini Chalinze wakati alipotangaza nia yake ya kutetea tena ubunge wa jimbo hilo.
????????????????????????????????????
Wananchi wa Chalinze wakimsikiliza Ridhiwania Kikwete mbunge wa jimbo hilo hayupo pichani wakati alipokuwa akitangaza nia yake ya kutetea tena kiti cha ubunge wa jimbo la Chalinze.
???????????????????????????????????? ???????????????????????????????????? ???????????????????????????????????? ????????????????????????????????????

KAMBI MBWANA AJITOSA UBUNGE HANDENI VIJIJINI

July 17, 2015
Mwandishi wa Habari za Michezo na mdau wa maendeleo ya wilaya ya Handeni, Kambi Mbwana, mwenye fulana ya CCM, akikabidhiwa fomu ya kuwania Ubunge, Jimbo la Handeni Vijijini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Katibu Msaidizi wa CCM wilayani Handeni, Asha Muya, wilayani Handeni, mkoani Tanga. Kulia kwa Mbwana ni Jerome Mhando, mmoja wa wadau waliomsindikiza katika tukio la uchukuaji fomu ya kuwania nafasi ya kuwatumikia wana Handeni. Picha na Mpiga Picha Wetu.

Na Mwandishi Wetu, Handeni
MWANDISHI wa habari za michezo na mdau wa maendeleo wilayani Handeni, mkoani Tanga, amejitokeza rasmi katika mbio za kuwania ubunge jimbo la Handeni Vijijini kwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Makabidhiano hayo ya fomu yalifanyika mbele ya Katibu Msaidizi wa CCM wilayani Handeni, Asha Muya, ikiwa ni siku chache baada ya milango ya uchukuaji fomu za kuwania nafasi za Ubunge na udiwani kufunguliwa rasmi. Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo, Mbwana alisema kwamba ameamua kujitokeza katika mbio hizo za ubunge ili afanyie kwa vitendo yale aliyokuwa anayapenda, hususan katika suala zima la maendeleo, huku wachache wao wakishindwa kuelewa faida ya harakati zake, zikiwapo zile za kuitangaza Handeni kwa njia mbalimbali.

Alisema wilaya yao imekuwa na changamoto kadhaa zinazohitaji nguvu za pamoja katika suala zima la shida ya kubwa ya maji, migogoro ya ardhi, ukosefu wa huduma bora za kijamii, hivyo kunahitajika jitihada na mipango ya pamoja kufanikishaji mambo hayo.
“Nilikuwa kimya kwa siku kadhaa nikiangalia akina nani wapo katika mchakato wa kuhitaji nafasi ya kuwatumikia wananchi wa Handeni Vijijini na kusikitishwa na watu wasioishi huku na wasiokuwa na uchungu wala dhamira ya kuwakwamua wananchi wakijitokeza kwa wingi kuwania nafasi ya ubunge, inaonyesha wapo kwa maslahi yao zaidi.

“Hii haiwezi kukubalika, ukizingatia kwamba wananchi wameendelea kuishi maisha ya mashaka kwa kukosa maji safi, elimu, afya, michezo, utamaduni na mambo mengine yanayopaswa kufanyiwa kazi kwa kushirikiana na watu wote, wakiwamo viongozi wa kisiasa, watendaji wa serikali na Watanzania kwa ujumla,” alisema Mbwana.
Licha ya kuonekana mpya katika ulingo wa kisiasa hususan kwa nafasi ya ubunge, Mbwana anakumbukwa na kushukuriwa na wengi kutokana na mradi wake wa Tamasha la Handeni Kwetu linalofanyika kila mwisho wa mwaka, kuasisi Taasisi ya Handeni Kwetu Foundation, bila kusahau kuandika kitabu kinachojulikana kama Dira na Tumaini Jipya Handeni kilichopokewa kwa hisia tofauti, haswa kutokana na kilichoandikwa kwenye kitabu hicho.