WANAFUNZI WA NELSON MANDELA WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KUSAIDIA KUTATUA MATATIZO YA MAZINGIRA, MAJI

WANAFUNZI WA NELSON MANDELA WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KUSAIDIA KUTATUA MATATIZO YA MAZINGIRA, MAJI

November 03, 2016
Pichani juu na chini ni Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya EU kwa nchi za Afrika Mashariki Roeland Van De Geer akihutubia wanafunzi wa vyuo mbalimbali katika ukumbi Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela ambapo alifanya ziara ya kutembelea Chuo jijini Arusha.(Picha na Ferdinand Shayo).

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau akifafanua jambo katika ziara ya Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki, Roeland Van De Geer alipotembelea chuo hicho.
Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki Roeland Van De Geer akisalimiana na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau, wakati wa ziara ya balozi huyo chuoni hapo.
Picha ya pamoja ya washiriki wa semina ya malengo ya dunia ya Umoja wa Mataifa katika Chuo cha Nelson Mandela wakiwa na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki, Roeland Van De Geer.
Picha ya pamoja ya washiriki wa semina ya malengo ya dunia ya Umoja wa Mataifa katika Chuo cha Nelson Mandela jijini Arusha.

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau (wa pili kulia) katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu (wa pili kushoto) na Amon Manyama (kushoto).

TIGO YAJA NA VIFIRUSHI VIPYA VYA INTANETI 'MEGA MIX'

November 03, 2016
 Ofisa mkuu wa Biashara wa Tigo Shavkat Berdiev (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu Kampuni ya Simu ya Tigo kuja na vifurushi vipya vya intaneti ;Mega Mix'. Kulia ni Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga.
 Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.




 Na Dotto Mwaibale

Kampuni inayoongoza kwa mtindo wa maisha ya kidijitali Tigo Tanzania leo imetangaza kuanzishwa kwa  ofa ya MEGA MIX ambayo itakuwa inatoa vifurushi vya intaneti ambayo vitawazawadia wateja dakika za ziada kwa ajili ya kupiga simu. Ofa  hii itawapatia wateja  urahisi wa kutumia vifurushi hivi vipya kupitia kifaa chochote kinachotumia intaneti  zikiwemo simu za mkononi  na modemu. 

Akitangaza vifurushi vya Mega Mix kwa waandishi wa habari Dar es Salaam leo Ofisa mkuu wa Biashara wa Tigo Shavkat Berdiev alivielezea vifurushi hivyo  kama “hatua moja mbele ya mabadiliko katika soko  inayotoa   vifurushi sahihi zaidi: ikiwa ni suluhisho kwa watumiaji wote wa data ndani ya sekta ya mawasiliano ya simu nchini Tanzania.”

 Shavkat  aliongeza, “Wateja wetu hivi sasa  wana uhuru wa kuchagua  kutoka katika simu zao  kifurushi chochote wanachokitaka kikiwa na dakika za ziada  zitakazo wawezesha kuunganishwa na wapendwa wao  wakati tunapoukaribisha msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.”

 Aliendelea kusema, “Kwa vifurushi vipya wateja wanaweza kuhabarishwa kwa wakati katika mtiririko wa  kuunganishwa  na  wenzi wao na kuwa bega kwa bega na yanayotokea  sehemu mbalimbali duniani. Vifurushi hivi vipya vinaendelea kuonesha jinsi Tigo ilivyojikita katika kuboresha mabadiliko katika mtindo wa maisha ya kidijitali na inavyoongoza katika kutoa  teknolojia ya kisasa pamoja na ubunifu  kwa wateja wetu.

“Wateja wetu vilevile wanaweza kuzipata taarifa za kidunia, kutafuta  kupitia Google, kusikiliza muziki, kuangalia video, kupakua na hata  kutiririsha sinema. Hii ni kwa sababu  tumeunda vifurushi hivi  kwa kuzingatia mahitaji ya kipekee ya wateja  wetu  kwa kufanya uwepo urahisi katika kuchagua  kutoka  katika kifurushi kimoja  kwenda kingine kutegemeana na hali ya kifedha ya wateja.”

Aidha Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga alisema, “Kutokana na teknolojia ya 4G LTE kupatikana  kwa hivi sasa katika miji 20 vifurushi vya  Mega Mix  kunafungua enzi mpya za kufikia intaneti kusiko na ushindani, ambako kutaondoa vikwazo  na kuwawezesha watumiaji  kuona mengi, kusikia zaidi na hatimaye  kupata yaliyo mazuri katika maisha.”

Mpinga aliongeza, “Mteja anachotakiwa kukifanya ili kupata  vifurushi vya Mega Mix ni kupiga  *148*00#  halafu chagua, ‘Vifurushi vya intaneti.”



WABUNGE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI WATEMBELEA IDARA YA UHAMIAJI

WABUNGE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI WATEMBELEA IDARA YA UHAMIAJI

November 03, 2016
uv
Mwenyekiti wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki Tawi la Tanzania, Makongoro Nyerere(kulia) akizungumza wakati wa mkutano na Wakuu wa Idara ya Uhamiaji(hawapo pichani).Wabunge hao walitembelea idara hiyo kujifunza  shughuli zinazofanywa na idara  hiyo . Wengine ni Wabunge  Shyrose Bhanji(kulia) na   Angela Kizigha(kushoto). Mkutano huo umefanyika   jijini Dar es Salaam.( Picha na Abubakari Akida)
uv5
 
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji akizungumza wakati wa mkutano na Wakuu wa Idara ya Uhamiaji(hawapo pichani).Wabunge hao walitembelea idara hiyo kujifunza  shughuli zinazofanywa na idara .Kulia ni Mbunge Makongoro Nyerere  na Kushoto ni  Angela Kizigha.Mkutano huo umefanyika   jijini Dar es Salaam.( Picha na Abubakari Akida)
uv1
Kaimu Kamishna  Jenerali   wa  Uhamiaji, Victoria Lembeli  akizungumza wakati wa mkutano na Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki waliotembelea idara  hiyo, ikiwa ni ziara yao ya kujifunza shughuli  mbalimbali zinazofanywa  na idara  hiyo ikiwemo suala la pasi za kusafiria katika nchi hizo.Ziara hiyo imefanyika  jijini Dar es Salaam.(Picha na Abubakari Akida
uv2
Kaimu Kamishna  Utawala  na  Fedha  wa Idara ya Uhamiaji, Naibu Kamishna Abbas Irovya,  akizungumza wakati wa mkutano na Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki waliotembelea idara ya Uhamiaji kujadili shughuli zinazofanywa na idara hiyo, ikiwa ni ziara yao ya kujifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na nchi za Afrika Mashariki ikiwemo  suala la pasi za kusafiria katika nchi hizo.Ziara hiyo imefanyika  jijini Dar es Salaam.( Picha na Abubakari Akida)
uv3
 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Abdullah Mwinyi akizungumza wakati wa mkutano na Wakuu wa Idara ya Uhamiaji(hawapo pichani).Wabunge hao walitembelea idara hiyo kujifunza  shughuli mbalimbali zinazofanywa  ikiwemo utoaji wa pasi za kusafiria katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kushoto ni  Katibu wa Wabunge wa Afrika Mashariki Twaha Taslima. Mkutano huo umefanyika  jijini Dar es Salaam. (Picha na Abubakari Akida)
uv4
Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Victoria Lembeli(wanne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wabunge  wa Bunge la Afrika Mashariki Tawi la Tanzania baada ya kutembelea Makao Makuu ya Idara hiyo katika kujifunza mambo mbalimbali yanayofanywa na idara .Watatu kulia ni Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania katika Bunge hilo, Makongoro Nyerere.Ziara hiyo imefanyika   jijini Dar es Salaam.(Picha na Abubakari Akida)
MUSWADA WA HABARI WAELEZEWA KUWA MUAROBANI DHIDI YA KASHFA NA UCHOCHEZI.

MUSWADA WA HABARI WAELEZEWA KUWA MUAROBANI DHIDI YA KASHFA NA UCHOCHEZI.

November 03, 2016
ber
Mkurugenzi wa Kurgenzi ya Mawasiliano wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Bernard James
……………………………………………………….
Na: Mwandishi Wetu.
MUSWADA wa huduma za Habari wa mwaka 2016 umeelezewa kuwa muarubani wa uandishi wa habari za kughushi na uchochezi kutokana na kuwa na vifungu vyenye kumlinda mwandishi na kumuweka hatiani pindi anapoenda kinyume na matakwa ya sheria.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Kurgenzi ya Mawasiliano wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Bernard James wakati wa  mahojiano maalum na mwandishi wa habari hii leo Jijini Dar es Salaam.
“Baadhi ya waandishi wa habari wamekuwa na tabia za kandika habari za kughushi na mara nyingine zenye lengo la kumkashfu mtu, ni imani yangu kwamba muswada huu ni muafaka kwa watu kama hao”. Alisema Bernard.
Bernard alivitaja vifungu hivyo kuwa ni Sehemu ya Tano ya muswada huo kuanzia kifungu cha 32 hadi 39 ambavyo vinahusu mambo ya kashfa ambapo mwandishi ana anayo haki yake,  hali kadharika anao wajibu wa kuzingatia misingi ya sheria na mipaka yake.
Huku sehemu ya saba ikihusisha makosa mbalimbali yakiwemo uchochezi,habari za kuchochea uasi, makosa yanayohusu utangazaji, vyombo vya habari na kosa la habari za kutia hofu kwa jamii.
Alisema kuwa ni vyema wanahabari wakatambua kwamba Serikali imeleta muswada huo si kwa nia ya kukandamiza uhuru wa habari bali ni nia yake yakutaka kuona kunakuwa na maboresho katika tasnia  ya hii na siyo kama ambavyo wengi wao wamekuwa wakipotosha.
Aidha Bernard aliongeza kuwa muswada huo ukipitishwa utapelekea kuanzishwa kwa chombo kitakachosimamia waandishi wa habari kwa kuwapa Vitambulisho, kusimamia  maadili na mienendo ya taaluma za waandishi wa habari na kuongeza kuwa tasni itaheshimika kwani wale makanjanja hawatakuwa na nafasi tena.
“Binafsi naunga mkono muswada huu upitishwe ili tasnia ya habari iheshimike kama taaluma nyingine zinavyoheshimika”.Aliongeza.
Amewaomba wanahabari wenzake kuunga mkono Muswada huu unaotarajiwa kusomwa Bungeni kwa mara ya pili siku ya Ijumaa ya tarehe 4 Novemba ambapo utajadiliwa na kupitihwa.