Sunday, January 5, 2014
AZAM YAFUZU ROBO FAINALI BAADA YA KUIFUNGA TUSKER 1-0
Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
MABINGWA watetezi, Azam FC wamefanikiwa kuwa timu ya kwanza kufuzu Robo Fainali za Kombe la Mapinduzi, baada ya usiku huu kuifunga Tusker ya Kenya bao 1-0, katika mchezo wa Kundi B, Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
MABINGWA watetezi, Azam FC wamefanikiwa kuwa timu ya kwanza kufuzu Robo Fainali za Kombe la Mapinduzi, baada ya usiku huu kuifunga Tusker ya Kenya bao 1-0, katika mchezo wa Kundi B, Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Hadi
mapumziko, tayari Azam walikuwa mbele kwa bao hilo 1-0 lililotiwa
kimiani na mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche baada
ya kuchukua pasi ya Waziri Salum.
Mfungaji wa bao pekee la Azam leo, Kipre Tchetche akimtoka beki wa Tusker anayejaribu kulala kuokoa mpira |
Wachezaji wa Azam wakimpongeza Kipre Tchetche kulia baada ya kufunga bao muhimu leo Amaan |
Tusker ndiyo waliouanza mchezo huo kwa kasi na kupeleka mashambulizi langoni mwa Azam kwa takriban dakika 10, lakini baada ya hapo vijana wa Joseph Marius Omog wakazinduka na kuanza kuwapeleka Wakenya.