RAIS DK. SHEIN AFUNGUA WA MSIKITI MASJID JAAMIU ZINJIBAR -MAZIZINI
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein (katikati) akiwapungia mkono Waislamu mbali mbali alipowasili
katika ufunguzi Msikiti Massjid Jaamiu Zinjibar uliopo Mazizini Wilaya
Magharibi 'B" Mkoa wa Mjini Magharibi leo,sambamba na Kituo Kikuu cha
Sayansi na Utamaduni cha Sultan Qaboos,"Sultan Qaboos Higher Center for
Culture and Science" ambao umejengwa na Serikali ya Zanzibar kwa
kushirikiana na Serikali ya Oman.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali
Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Kituo Kikuu cha Sayansi
na Utamaduni cha Sultan Qaboos,"Sultan Qaboos Higher Center for Culture
and Science" Mhe.Habib Mohammed Al-Riyami mara alipowasili katika
ufunguzi Msikiti Massjid Jaamiu Zinjibar uliopo Mazizini Wilaya
Magharibi 'B" Mkoa wa Mjini Magharibi leo,uliojengwa na Serikali ya
Zanzibar kwa kushirikiana na Serikali ya Oman.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein (kushoto) akisalimiana na Viongozi mbali mbali mara alipowasili
katika ufunguzi Msikiti Massjid Jaamiu Zinjibar uliopo Mazizini Wilaya
Magharibi 'B" Mkoa wa Mjini Magharibi leo,ambao umejengwa na Serikali ya
Zanzibar kwa kushirikiana na Serikali ya Oman.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein alipofuatana na Viongozi mbali mbali wakiwemo Kituo Kikuu cha
Sayansi na Utamaduni cha Sultan Qaboos,"Sultan Qaboos Higher Center for
Culture and Science" wakati alipotembelea sehemu mbali mbali za Msikiti
Masjid Jaamiu Zinjibar baada ya kuufungua rasmi leo,ambao umejengwa
Mazizini Wilaya Magharibi 'B" Mkoa wa Mjini Magharibi kwa Ushirikiano wa
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Watu wa Oman.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kituo Kikuu cha
Sayansi na Utamaduni cha Sultan Qaboos,"Sultan Qaboos Higher Center for
Culture and Science" Mhe.Habib Mohammed Al-Riyami wakati alipotembelea
sehemu mbali mbali mara alipofungua Msikiti Massjid Jaamiu Zinjibar
uliopo Mazizini Wilaya Magharibi 'B" Mkoa wa Mjini Magharibi
leo,uliojengwa na Serikali ya Zanzibar kwa kushirikiana na Serikali ya
Oman.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein (kushoto) akipokea Shahada na Ufunguo kutoka kwa Mkuu wa Kituo
Kikuu cha Sayansi na Utamaduni cha Sultan Qaboos,"Sultan Qaboos Higher
Center for Culture and Science" Mhe.Habib Mohammed Al-Riyami kama ishara
ya ufunguzi rasmi wa Msikiti Masjid Jaamiu Zinjibar leo uliojengwa kwa
Ushirikiano wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Watu wa
Oman katika maeneo ya Mazizini Wilaya Magharibi 'B" Mkoa wa Mjini
Magharibi.
IMARISHENI TAKWIMU ZA UJENZI NCHINI: PROF. MBARAWA
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akihutubia
wakati wa ufunguzi wa warsha ya wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu
uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), jijini
Dar es Salaam.
Wadau
wa sekta ya ujenzi wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani), katika warsha ya
sekta hiyo kuhusu uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza la Taifa la
Ujenzi (NCC), jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto),
akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Ujenzi),
Mhandisi Joseph Nyamhanga (kulia), katika warsha ya wadau wa sekta ya
ujenzi kuhusu uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza la Taifa la Ujenzi
(NCC), jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Prof. Mayunga Nkunya (kulia),
akifafanua jambo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa
Makame Mbarawa (kushoto), jijini Dar es Salaam.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Dkt. Samson Mturi
akitoa taarifa kwa mgeni rasmi Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani), katika warsha ya wadau wa
sekta ya ujenzi kuhusu uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza hilo,
jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto),
akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Huduma za Biashara Bw. Milton Lupa
(aliyesimama), kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), wakati
alipokagua mradi wa ujenzi wa nyumba za magomeni, jijini Dar es Salaam.
Mkadiriaji
Majenzi na Msanifu Majengo Neema Kifua (wa pili kulia), akitoa taarifa
kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa
kuhusu maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za magomeni, alipotembelea
mradi huo leo, jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amewataka
wadau wa sekta ya ujenzi kuanza kuweka twakwimu takwimu zinazohusu
masuala ya ujenzi hapa nchini.
Akifungua
warsha ya wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu uboreshaji wa utendaji kazi
wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Prof. Mbarawa, amesisitiza umuhimu
wa sekta hiyo kuimarisha taarifa za aina, vifaa, viwango vinavyohitajika
kimataifa na gharama katika shughuli za ujenzi wa barabara, viwanja vya
ndege, nyumba na miundombinu mingine.
“Sekta
ya Ujenzi ina mchango mkubwa katika ujenzi wa miundombinu ya kiuchumi
na kijamii hivyo uwepo wa taarifa mbalimbali unahitajika ili kurahisisha
uelewa wa wananchi wa kawaida katika masuala ya ujenzi na gharama
zake”, amesema Prof. Mbarawa.
Aidha,
Waziri Prof. Mbarawa amewahakikishia wadau wa sekta ya ujenzi kuwa
Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ili kuhakikisha sekta hiyo
inakidhi matarajio ya watanzania wengi kwa lengo la kuwajengea
miundombinu iliyo bora na imara.
Ameongeza
kuwa mapendekezo yatakayotolewa na wadau hao yatarahisisha utekelezaji
wa miundombiu mbalimbali ambayo italeta chachu kwa sekta nyingine
zikiwemo za kilimo, nishati, utalii, viwanda, madini na uendelezaji wa
biashara na nchi nyingine za kikanda.
Kwa
upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Ujenzi) Mhandisi
Joseph Nyamhanga amesema ongezeko la miradi ya ujenzi imechangia
Serikali kutafuta wataaalm waliofanya tafiti kwa ajili ya uboreshaji wa
baraza hilo wataongeza tija na ufanisi wa sekta hii muhimu ya ujenzi kwa
wadau, wananchi na Serikali.
Naye, Mwenyekiti wa Baraza la NCC Prof.
Mayunga Nkunya amemuhakikishia Waziri Prof. Mbarawa kuwa baraza lake
litasimamia michango yote itakayotolewa na wadau hao na kuahidi
kushughulikia changamoto zinazoikabili NCC ikiwemo za takwimu ili
kuhakikisha sekta hiyo inaendelea kukua kwa kuwa ni sekta mtambuko.
Sekta
ya Ujenzi ni mojawapo ya sekta zinazokua kwa kasi hapa nchini na ina
mchango mkubwa kwa Pato la Taifa ambapo mwaka 2016 sekta hiyo ilichangia
asilimia 14 ya Pato la Taifa.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MPINA AAGIZA KIWANDA CHA UNGA WA NGANO CHA AZANIA KUFANYA VIPIMO VYA VUMBI LA LITOKALO KIWANDANI HAPO
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,
Luhaga Mpina akikagua mfereji wa maji katika kiwanda cha Chemi Cotext
kilichopo Mbezi Beach jijini Dar es salaam wakati wa ziara yake ya ukaguzi
wa mazingira.
Naibu Waziri wa Nchi Ofis ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,
Luhaga Mpina akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanya
ukaguzi wa mazingira katika eneo la kiwanda cha unga wa ngano cha Azania
kilichopo Ubungo jijini Dar Es Salaam.
NA;
EVELYN MKOKOI - DAR ES SALAAM
Akiendelea na ziara
yake ya ukaguzi na utekelezaji wa sheria ya Mazingira jijini Dar es
Saalaam, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Mazingira
Mhe. Luhaga Mpina, ameagiza Baraza la taifa la Usimizi wa Mazingira NEMC
kwa kushirikiana na uongozi wa kiwanda cha kutengeneza unga wa Ngano
wa Azania, kupima kiwango cha ubora wa hewa inayoambatana na vumbi la
unga wa ngano linalotoka kiwandani hapo baada ya shughuli za uzalishaji
na kwenda kwenye mazingira na makazi ya watu kana vinakidhi viwango
vya kimazingira.
Mpina alisema kuwa baada
ya matokeo hayo yanayotegemewa kutoka baada ya wiki mbili, serikali
ndiyo itakuwa kwenye hatua ya kusema jambo kwa wananchi pamoja na kiwanda.
“Baada ya matokea
hayo sasa serikali inaweza kuwa na nafasi ya moja kwamoja kuchukua hatua
kwa mwenye kiwanda ikiwa ni pamoja na kukitoza faini kwa mujibu wa sheria,
na kama matokeo ya vumbi na kelele zitokazo kiwandani hapo yatakuwa
ndani ya kiwango, sasa hatua itakayofuata ni yakuangalia mahusiano kati
ya mwenye kiwanda na wakazi majirani wa eneo hilo. Alisema Mpina.”
Aidha Mpina aliongelea
kufaanyika kwa taratibu za kujua kama suala la kiwanda hicho kuwa karibu
na makazi ya watu , ni sahihi na kwa upande wa wananchi kuwa karibu
na kiwanda hususan kuwepo kwa nyumba kila baada ya hatua moja
nalo ni sahihi.
Awali katika muendelezo
wa ziara yake ya ufuatiliaji na utekelezaji wa sheria ya mazingira jijini
Dar es Salaaam, Naibu Waziri Mpina alikitembelea kiwanda cha Chemi
cotex kilichopo Mbezi Beach.
WAZIRI CHARLES MWIJAGE AFUNGUA TAWI LA KAMPUNI YA MABATI ALAF DODOMA
WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Charles Mwijage Septemba 9, 2017 alifungua tawi la Kiwanda cha mabati ALAF katika mkoa wa Dodoma eneo la Kizota kitalu namba 148.
Kufunguliwa kwa tawi hili katika mkoa wa Dodoma ni kutokana na maamuzi ya serikali kuamia makao makuu ya nchi mkoani Dodoma kwa vitendo na kuunga mkono kauli mbiu ya Mheshimiwa Rais John Magufuli katika “ USHIRIKI KATIKA KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA KWA MAENDELEO YA TAIFA”.
Kufunguliwa kwa tawi hili kutaimarisha maendeleo ya mkoa wa Dodoma na maeneo ya jirani.
Wateja kutoka Dodoma na Singida sasa wataweza kupata suluhisho la mahitaji ya bidhaa za uezekaji kutola ALAF.
Tunauza bidhaa zilizo tayari kwa matumizi kulingana na mahitaji ya mteja hasa mabati ya rangi pamoja na kutoa ushauri wa kiufundi na kiutaalamu.
Kwa sasa kiwanda chetu cha ALAF kina matawi manne Mbeya, Mwanza, Arusha na Dodoma.
Kuhusu kampuni ya ALAF
Kampuni ya ALAF ni sehemu ya kampuni ziliyoko chini ya Kampuni ya SAFAL, kampuni inayoongoza bila mpinzani ktika utoaji wa bidhaa bora za uezekaji barani Afrika.Kampuni ya SAFAL inaendesha shughuli zake katika nchi 13 kuanzia mashariki,kati na kusini mwa bara la Afrika.
Tukiwa na uzoefu wa zaidi ya miaka 50 katika biashara, ALAF tunaongoza katika uzalishaji wa bidhaa za uezekaji za chuma.Katika kuongezea bidhaa zake za upauaji, bidhaa za kitaalamu pia zinauzwa na ALAF kama misumari (fixtite fastener), steel pipes, na Hollow section pamoja na viambatanisho muhimu kwa uezekaji.
Baadhi ya bidhaa zinazotolewa na ALAF ni Lifestile, Romantile, Versatile, Tekdek (It5), Resincot na Simba Dumu.
Wasilana nasi kwa namba hizi Dar es Salaam- O768 555 560, Arusha - 0763 707 071, Mbeya - 0765 555 560, Dodoma - 0764 131442 na Mwanza 0682 808 080.
Tunapatikana pia kuitia mitandao ya kijamii Facebook -Alaf Limited na Instagram - Alaf Limited
WAFANYAKAZI WASHAURIWA KUPIMA AFYA MARA BAADA YA KUSTAAFU
Na: Lilian Lundo – MAELEZO Dodoma.
Wafanyakazi
nchini wameshauriwa kupima afya zao mara tu wanapostaafu ili
kujihakikishia ikiwa hawajaathirika na kazi ambazo wamekuwa wakizifanya.
Hayo
yameelezwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na
Wenye Ulemavu Eric Shitindi alipokuwa akifungua semina ya viongozi wa
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) na viongozi wa
Vyama vya Wafanyakazi juu ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, leo Mjini
Dodoma.
“Kumekuwa
na mazoea kwa wafanyakazi kupima Afya pale tu wanapoajiriwa na
kutotilia maanani upimaji afya zao mara wanapostaafu ili kujua ikiwa
kazi wanazozifanya zimewaathiri kwa kiasi gani,” amesema Shitindi.
Ameendelea
kwa kusema kuwa, upimaji wa afya mara baada ya kustaafu utasaidia
watumishi kujua afya zao na ikiwa watakuwa wameathirika upitia kazi
walizokuwa wakizifanya basi mwajiri atawajibika mkulipa fidia mtumishi
huyo.
Aidha
amesema kuwa licha ya juhudi za Serikali katika kusimamia Usalama na
Afya maeneo mengi ya kazi sio ya kuridhisha kutokana na waajiri wengi
kutokuzingatia sheria na kanuni mbalimbaliza Usalama na Afya.
Hivyo
basi kutokana na waajiri hao kutofuata sheria na kanuni hizo
kumesababisha maeneo mengi ya kazi kulalamikiwa kutokana na ukiukwaji wa
sheria hizo.
Vile
vile amesema kuwa baadhi ya waajiri na wafanyakazi wana uelewa mdogo
kuhusu kuzingatia maelekezo ya Usalama na Afya Mahali pa kazi ikiwemo
matumizi sahihi ya vifaa kinga.
Kwa
upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa
Kazi (OSHA) Khadija Mwenda amesema kuwa, wameamua kuandaa semina hiyo
kwa viongozi wa vyama vya wafanyakazi hapa nchini ili na wao wakatoe
elimu hiyo kwa wafanyakazi wote nchini kutokana na wafanyakazi hao
kutokuwa na uelewa mzuri juu ya masuala ya Usalama na Afya Mahali pa
Kazi.
Kaimu
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Bi.
Khadija Mwenda akiongea na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya
Wafanyakazi Tanzania(TUCTA) na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakati
wa Ufunguzi wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi
Leo Mjini Dodoma.Kulia ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya
Wafanyakazi (TUCTA) Bw.Qambos Sule
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw.
Eric Shitindi akiongea na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya
Wafanyakazi Tanzania(TUCTA) na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakati
wa Ufunguzi wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi
ambapo aliwashauri wafanyakazi nchini kupima afya mara wanapostaafu ili
kujihakikishia kama hawajaathirika na kazi walizokuwa wanafanya.Katikati
ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA)
Bw.Qambos Sule na Kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na
Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Bi. Khadija Mwenda
Makamu
wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw.Qambos Sule
akiongea naViongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi
Tanzania(TUCTA) na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakati wa Ufunguzi
wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi, kulia ni
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu
Bw. Eric Shitindi na kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama
na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Bi. Khadija Mwenda
Makamu
wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw.Qambos Sule
(KUSHOTO) na Katibu Mkuu Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw.
Jones Majura(KULIA) wakiteta jambo na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri
Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw. Eric Shitindi baada ya
ufunguzi wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi leo
Mjini Dodoma
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw.
Eric Shitindi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Semina kuhusu
masuala ya usalama na afya mahala pa kazi Leo Mjini Dodoma. PICHA NA
IDARA YA HABARI-MAELEZO,DODOMA
CRC yazinduwa mradi wa utoaji huduma za msaada wa kisheria
Mwenyekiti wa Kituo cha Usuluhishi wa masuala ya kijamii na kijinsia, CRC, Saida Mukhi akizungumza na washiriki wa warsha kwa wadau wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria na ushauri nasihi kwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye wilaya mbili za mkoa wa Dar es Salaam, Kinondoni na Ubungo. Kulia ni Mratibu wa Kituo cha Usuluhishi cha CRC, Bi. Gladness Munuo.
Mwenyekiti wa Kituo cha Usuluhishi wa masuala ya kijamii na kijinsia, CRC, Saida Mukhi (kulia) akizungumza na washiriki wa warsha kwa wadau wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria na ushauri nasihi kwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Ofisa Mradi wa Kituo cha Usuluhishi wa masuala ya kijamii na kijinsia, CRC, Suzan Charles akitoa ufafanua juu ya mradi wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria na ushauri nasihi kwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye wilaya mbili za mkoa wa Dar es Salaam.
Mmoja wa washiriki wa warsha hiyo kwa wadau wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria na ushauri nasihi akichangia mada.
KITUO cha Usuluhishi wa masuala ya kijamii na kijinsia, CRC kimezinduwa mradi wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria na ushauri nasihi kwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye wilaya mbili za mkoa wa Dar es Salaam, yaani Kinondoni na Ubungo.
Akizungumza na wadau wa mradi huo yaani baadhi ya wasaidizi wa sheria, maofisa ustawi wa jamii, wanasheria, mahakimu, Askari Polisi Dawati la Jinsia, maofisa watendaji wa mitaa kutoka wilaya za Kinondoni na Ubungo, Mwenyekiti wa CRC, Saida Mukhi aliwataka wadau hao kushirikiana ili kuhakikisha vitendo vya ukatili wa kijinsia vinakomeshwa na kupungua.
Alisema lengo la mradi huo unaofadhiliwa na shirika la Legal Service Facilities (LSF) ni kuhimarisha zaidi upatikanaji wa msaada wa kisheria na ushauri nasihi kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia.
Aliongeza kuwa mradi huo utajikita zaidi katika utoaji wa msaada wa kisheria na ushauri nasihi kwa waathirika na kuhakikisha mfumo wa upatikanaji wa haki unafanya kazi vizuri.
"...wadau katika maeneo hayo mnatakiwa kuhakikisha tunapinga vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo vinaweza kusababisha madhara ya mwili, kingono au kisaikolojia au mateso kwa wanajamii, ikiwa ni pamoja na wahusika kunyimwa uhuru," alisema Bi. Saida Mukhi akifungua warsha ya wadau hao.
Kwa upande wake, Mratibu wa Kituo cha Usuluhishi cha CRC, Bi. Gladness Munuo akifafanua zaidi kwa washiriki wa semina hiyo alisema mradi huo utaendeshwa katika Kata za Makumbusho na Kawe kwa Wilaya ya Kinondoni huku kwa Wilaya ya Ubungo utajikita kwenye Kata ya Saranga.
Alisema CRC itashirikiana na wadau katika maeneo hayo kuhakikisha inapiga vita vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo mara nyingi vimekuwa na madhara ya mwili, kingono au kisaikolojia au mateso kwa wanajamii na mara nyingine kuwanyima uhuru.
Sehemu ya washiriki wa warsha kwa wadau wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria na ushauri nasihi kwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye wilaya mbili za mkoa wa Dar es Salaam, Kinondoni (Kata za Makumbusho na Kawe) na Ubungo (Kata ya Saranga).
Sehemu ya washiriki wa warsha kwa wadau wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria na ushauri nasihi kwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye wilaya mbili za mkoa wa Dar es Salaam, Kinondoni (Kata za Makumbusho na Kawe) na Ubungo (Kata ya Saranga).
Picha ya pamoja ya washiriki wa warsha kwa wadau wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria na ushauri nasihi kwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia wakiwa na mgeni rasmi Bi. Saida Mukhi.
--
___________________________________________________________________________________
Joachim Mushi, Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mhariri Mkuu wa Thehabari.com.
Mail address:- mushi@thehabari.com/ jomushi79@yahoo.com/ info@thehabari.com
Mobile:- 0717 030066 / 0756 469470
Web:- www.thehabari.com
http://joemushi.blogspot.com
TCRA WAENDESHA WARSHA YA VYOMBO VYA HABARI MTANDAONI NA KUZINDUA KAMPENI YA KUSISITIZA MATUMIZI BORA YA MITANNDAO YA KIJAMII-AWAMU YA PILI
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jones Kilimbe akifungua rasmi warsha ya vyombo vya Habari Mtandaoni iliyo wahusisha Blogu na 'Online Tv' katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa J.K Nyerere Jijini Dar es salaam.
Bw. Thadeus Lingo kutoka TCRA akiendesha mada kuhusu Matumizi Salama ya Mitandao ya Kijamii
Mwakilishi wa Chama cha wamiliki wa Blogu Tanzania(TBN) Bw. Maxence Melo akiwasilisha mada juu ya Maudhui ya Mtandaoni na Changamoto zake.
Mratibu Msaidizi wa Polisi Joshua Mwangasa akitoa mada juu ya Hali ya Usalama Mtandaoni
Mzee Abdul Ngarawa Mjumbe wa Kamati ya Maudhui kutoka TCRA akitoa neno la Busara wakati wa warsha hiyo ambapo alisisitiza kuzingatia uzalendo umuhimu wa kutazama utu na staha ya mtu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi James Kilaba (Kushoto) akiongoza majadiliano kwa ujumla ambapo wadau walichangia mawazo na kuuliza maswali mbalimbali
Bwana Daniel Mbega Mmiliki wa Blogu ya Maendeleo Vijijini akichangia mawazo yake wakati wa warsha hiyo
Bw. William Malecela Maarufu kwa jina la Le Mutuz mmiliki Blogu ya Wananchi na Le Mutuz Tv Onine akichangia mambo mbalimbali na kutoa maoni yake wakati wa Warsha hiyo Mwenyekiti wa Chama cha wamiliki wa Blogu Tanzania(TBN) Bw. Joachim Mushi (kulia) akitoa neno la Shukurani kwa niaba ya waendesha wote wa mitandao kwa TCRA kuendesha warsha hiyo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi James Kilaba pamoja na wadau wengine wakizindua Rasmi Kampeni ya kusisitiza matumizi bora ya Mitandao ya Kijamii awamu ya Pili ambapo Kauli mbiu inasema "Usinitumie Sitaki na Simtumii Mwengine Nitakuripoti" Baada ya uzinduzi wa Kampeni hiyo. Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya TCRA Bi. ValerieNdeneingo-Sia Msoka akitoa neno la kufunga wakati wa Warsha hiyo. Wadau mbalimbali wakiwa katika warsha hiyo
Picha zote na Fredy Njeje/ Blogs za Mikoa Tanzania
Na.
Paschal Dotto-MAELEZO.
Serikali ya Awamu ya Tano
kupitia Mamlaka ya Mawasiliano nchini(TCRA) imetia nia kuboresha mawasiliano
kwa umma hasa katika matumizi ya mitandao ya kijamii ili kuwawezesha watanzania
kupata elimu bora ya maendeleo na kujenga uchumi uliobora.
Haya
yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka hiyo Dkt. Jonas
Kilimbe alipokua akihutubia hadhara ya
wamiliki wa vyombo vya habari mtandaoni (blogu na Online TV) katika uzinduzi wa
kampeni ya awamu ya pili ya “kusisitiza matumizi bora ya mitandao ya kijamii” iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha
Kimataifa cha Julius Nyerere.
Katika hafla hiyo, Dkt.
Kilimbe alisema kuwa kwa sasa teknolojia ya mtandao inakua kwa kasi kwa hiyo huduma
za habari zinapatikana kila sehemu kwa njia ya mtandao na kufanya matumizi ya
mitandao kuwa makubwa.
“Sekta ya mawasiliano
kwa umma imepiga hatua kubwa sana duniani kwa sasa, kwa kiasi kikubwa mtandao
unachangia kuwepo kwa habari nyingi. Tanzania inajumla ya televisheni za mitadaoni
zipatazo 50 pamoja na blogu 150 ambazo zote zinatoa taarifa kwa wananchi, hii
inaashiria kuwa mawasiliano kwa umma yamehamia zaidi kwenye mtandao”, alisema
Dkt.Kilimbe.
Aidha Dkt.Kilimbe alisema
kuwa sekta hii inapaswa kuangaliwa zaidi kwani ni sekta muhimu kwa ujenzi wa
Taifa na kuwaasa vijana kutumia vizuri teknolojia hiyo kwa kujielimisha
kuhusiana na masuala ya maendeleo kuliko kutumia vibaya mitandao hiyo.
“Tuna jukumu zito na ni
kubwa kwa sababu sekta hii ya mawasiliano imeshikiria kila kitu na tasnia ya
habari ina nguvu kubwa sana kwa kuleta elimu ya maendeleo kwa wananchi kwa hiyo
waandishi mitandaoni tumieni weledi
mkubwa kwa habari za maendeleo.”, alisisitiza Dkt. Kilimbe.
Dkt.Kilimbe alisema
kuwa katika matumizi ya teknolojia hii mpya yanapaswa kuzingatiwa kwa ajili ya ujenzi wa taifa hasa kwa wale
wanaotumia vizuri mitandao ya kijamii inawapa elimu kubwa ya maendeleo.
Aidha Dkt. Kilimbe
amekishukuru chama cha wamiliki wa blogu na televisheni mtandaoni(TBN) kwa
kuleta umoja na kuzingatia maadili na weledi wa umilikajia wa vyombo hivyo kwa
kuwahabarisha wananchi.
Naye mtoa mada na
mwakilishi kutoka TCRA Bw. Thadeus Lingo alisisitiza usalama wa matumizi ya
mtandao akisema kuwa idadi ya watumiaji wa mitandao imeongezeka duniani kuanzia
Julai 1, 2017 na kufikia bilioni 3.8 huku kati ya hao bilioni 3.4 ambayo ni
sawa na asilimia 92 ni watumiajia wa mitandao ya kijamii hali iliyosababisha
kuongezeka kwa vyombo vya habari kuhamia mtandaoni, kwa hiyo weledi unahitajika
katika kuhabarisha umma kwa njia hii.
Subscribe to:
Posts (Atom)