MHE. AUGUSTINO MREMA AWATAKA WATANZANIA KUYAPUUZA MAANDAMANO YA CHADEMA SEPTEMBA MOSI MWAKA HUU

MHE. AUGUSTINO MREMA AWATAKA WATANZANIA KUYAPUUZA MAANDAMANO YA CHADEMA SEPTEMBA MOSI MWAKA HUU

August 28, 2016
mrema
Na Ismail Ngayonga-MAELEZO
Dar es Salaam

WAZIRI wa zamani wa mambo ya ndani ya nchi, Augustino Mrema amewataka Watanzania kuyapuuza  maandamano ya Septemba Mosi mwaka huu yaliyoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na badala waendelee na shughuli za ujenzi wa Taifa.
Mrema alisema hakuna haja ya kufanya maandamano Septemba Mosi kwani hayana faida yoyote kwa taifa badala yake wananchi wa kawaida ndio watakaoathirika.
 
Akizungumza katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hii leo Jijini Dar es Salaam, Mhe. Mrema ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Misamaha kwa Wafungwa (Parole) alisema mikutano ya hadhara na maandamano yasiyokwisha kila kukicha yatasababisha wananchi wasifanye kazi.
Nchi yetu ni maskini hivyo tunahitaji wananchi wafanye kazi kwa bidii” alisema Mrema. Alisema iwapo CHADEMA  wataona wameonewa ni vyema  watumie njia za mazungumzo au ikibidi kwenda mahakamani badala ya kufanya maandamano ambayo yanaweza kusababisha vurugu na kuharibu amani na utulivu wa nchi.
 
Aliwataka Watanzania kukumbuka maandamano ya mwaka 2001 yaliyoitishwa na Chama cha Wananchi (CUF) huko Zanzibar ambapo watu kadhaa waliuwawa na mamia kukimbilia uhamishoni nchini Kenya na Somalia.
 
Akizungumzia kuhusu utendaji kazi wa Serikali ya Awamu, Mhe. Mrema alimpogeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa hatua yake ya kurejesha maadili na miiko ya utumishi kwa watumishi wa umma nchini hali iliyosaidia kurejesha uwajibikaji wa Serikali kwa wananchi.
Mrema alisema tangu kuingia madarakani kwa Serikali ya Awamu Tano, kumekuwepo na mabadiliko kwa watendaji wa umma katika ngazi mbalimbali za kimamlaka ukitofautisha na miaka ya nyuma ambapo baadhi ya watendaji walikuwa wakifanya kazi kwa mazoea.
“Viongozi wengi wa umma walikuwa wakifanya kazi kwa mazoea bila kujali wajibu wao na wala hakukuwa na uwajibikaji cha kusikitisha mamlaka husika zilikuwa haziwachukulii hatua za kinidhamu, hivyo viongozi wa umma badala ya kuwatumikia wananchi wakawa wanatumikia matumbo yao” alisema Mrema.
Mrema alisema Rais Magufuli ameanza kutekeleza kwa vitendo ahadi yake aliyoitoa kwa wananchi ya kuwaondoa madarakani viongozi wazembe na wasiowajibika na wasiokuwa na uwezo wa kufanya kazi katika kuwatumia wananchi.
Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inastahili pongezi kwa hatua inazochukua katika mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa na ufisadi ikiwemo uanzishwaji wa Mahakama ya Mafisadi nchini, kwani hakuna maendeleo yatakayoweza kupatikana katika nchi pasipo na kupiga vita rushwa.
Mrema alisema ni wajibu wa kila mwananchi kuichukia rushwa kwa vitendo ikiwemo kuwafichua hadharani kikundi cha watu kinachojihusisha na rushwa kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia Tanzania kupiga hatua kubwa za maendeleo.
“Kama mnavyokumbuka mimi nilifukuzwa kazi serikalini kwa sababu ya kupinga ufisadi ambao kwa wakati ule ulikuwa umekithiri serikali, ivyo nilichokuwa nikikipigania mimi ndicho anachifanya Rais Magufuli” alisema Rais Magufuli.
 
Akizungumzia kuhusu hatua ya Serikali ya Awamu ya Tano kuhamishia shughuli zake Mjini Dodoma, Mrema alipongeza uamuzi huo kwani kiulinzi na kiusalama Dodoma ni pazuri zaidi kuliko Dar es Saalam kwani ni katikati ya nchi.
“Dodoma panafaa sana kiulinzi na usalama kwa kuwa ni vigumu kwa adui watoke baharini wafike hadi Dodoma kabla hawajathibitiwa” alisema Mrema.
 
“Kuhusu ubora wa miundombinu ya Mkoa wa Dodoma Mrema alisema Mkoa huo unafikika kirahisi zaidi kwa wananchi waishio mikoa ya pembezoni na mipakani kufika Dodoma kuliko ilivyo Dar es salaam ambayo iko Mashariki kabisa ya nchi”  alisema Mrema.

JAFO AFANYA ZIARA YA SIKU MBILI MKOA WA SHINYANGA NA GEITA

August 28, 2016



Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akizungumza na wananchi nje ya kiwanda cha kukamulia alizeti mjini Chato.
Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akikagua mashine za kukamulia mafuta ya alizeti mjini Chato.
Mkurugenzi wa mji wa Kahama, Andason Msumba akitoa maelezo kwa Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo kuhusu mgogoro wa soko  wanalolitaka wananchi kutumika kwa maslahi ya wananchi wa mji huo. 
Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akikagua mradi wa maji  kijiji cha Chankorongo wilayani Geita uliohujumiwa na watendaji na kumuagiza Katibu tawala wa mkoa wa Geita kuunda timu ya uchunguzi.
Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akiwa katika harambe ya kuchangia madawati mkoani Geita, kulia kwake ni Mkuu wa mkoa huo Meja jenerali mstaafu Ezekiel Kiunga pamoja na Mwenyekiti wa harambee hiyo, Ignas Inyasi.
Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akizungumza katika harambe ya kuchangia madawati mkoani Geita, ambayo alikuwa akimwakilisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na serikali za mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo amefanya ziara ya Siku mbili katika mikoa ya Shinyanga na Geita na kukagua miradi mbalimbali.

Akiwa Mkoani Shinyanga, Jafo alitembelea Hospitali ya Wilaya ya Kahama ambapo alijionea changamoto mbali mbali ikiwepo ya Jengo dogo linalotumiwa na kinamama wakati wakujifungua kutokana na hospitali hiyo kuzidiwa uwezo.

Kufuatia hali hiyo, Jafo amemuagiza Injinia wa Wilaya kuhakikisha wanaharakisha ujenzi wa Jengo kubwa la kisasa la kinamama kwani fedha zipo za Ujenzi huo ili wagonjwa wasiendelee kupata mateso kwa michakato ya Ujenzi mirefu isiyo na tija.

Kadhalika, akiwa wilayani Kahama, Naibu Waziri Jafo ametembelea Mradi wa Soko na kumuagiza Mkurugenzi wa Wilaya, Andason Msumba, kuhakikisha anakaa na timu yake ya Wataalamu ili kutatua mgogoro wa Soko hilo kwa Maslahi mapana ya wananchi wa Mji wa Kahama.

Amehitimisha Ziara yake mkoani Shinyanga kwa kuzungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama na Halmashauri ya Msalala ambapo amewataka Watumishi kufanya kazi kwa kujituma huku wakiepuka Uzembe kazini,upendeleo, kupigana majungu, na kuchukiana.

Katika mkoa wa Geita, Jafo amekagua mradi wa Maji na Kiwanda cha kukamua mafuta ya Alizeti wilayani Chato huku akimuagiza Mhandisi wa Maji wa Wilaya hiyo kuhakikisha mradi unakamilika mapema kabla ya Mwezi wa 10 ili kuweza kusaidia kutatua changamoto ya Maji.

Amesema wananchi hawawezi kuwa na Upungufu wa Maji wakati kuna maji mengi ya Ziwa Victoria. Akikagua Mradi wa kiwanda cha kukamua Mafuta ya Alizeti, Jafo alimwagiza Mkurugenzi kuhakikisha anashirikiana na Sido ili kuweza kuukamilisha mradi huo haraka.

Akiwa njiani kuelekea Geita mjini, Jafo alipita Jimbo la Busanda wilaya ya Geita Vijijini na Kukagua Mradi wa Maji uliokamilika Kijijini Makondeko kisha Safari ikaelekea Kijiji cha Chankorongo ambapo kuna Mradi wa Maji wa muda mrefu usio kamilika ambapo mpaka sasa umetumia zaidi ya Bilioni moja na dalili za kukamilika bado.

Kufuatia hali hiyo, Naibu Waziri huyo amemwagiza Katibu tawala wa Mkoa wa Geita Selestine Gesimba kuunda tume maalum ya kuchunguza sakata la mradi huo wa maji wa Chankorongo ambapo wamepewa mwezi mmoja kukamilisha uchunguzi huo.

Alimwagiza Katibu Tawala Mkoa akishirikiana na Wakurugenzi wote kuhakikisha suara la Oprass linapewa kipaumbele kwa watumishi na linafanyika kwa wakati na ipasavyo. Naibu Waziri aliwahakikishia watumishi kuwa serikali inafuatilia changamoto mbalimbali zinazowakabili na kuwataka wawe na Subra.


Wakati huo huo, akiwa Mkoani Geita Jafo alimwakilisha Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa katika Harambee ya ya kuchangia Madawati.

Katika harambe hiyo Jafo alihamasisha na kuweza kukusanywa kiasi cha Shilingi Bilioni Moja, mia saba arobaini Milioni , laki tano na elfu tisini na saba (1,740,597,000) Kiasi ambacho kilimfanya Mkuu wa Mkoa huo Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga kumshukuru sana Naibu waziri huyo kwani  hakutegemea kiasi hicho kikubwa cha Fedha kuweza kupatikana.

KIFAHAMU KIPINDI KIPYA CHA 'CHUKUA HATUA' KINACHOHUSU VIJANA MKOANI DODOMA

August 28, 2016
 Watangazaji wa kipindi kipya cha CHUKUA HATUA Happy Balisidya na Mohammed Hammie, siku ya kwanza walipokutana wakati wa maandalizi ya kutengeneza kipindi hicho.
Mohammed Hammie na Happy Balisidya wakiwa katika nyuso za furaha baada ya kufahamu watakuwa wakiendesha kipindi cha CHUKUA HATUA.

BANDA LA MAONESHO LA TANZANIA LANG'ARA KWENYE MKUTANO WA TICAD VI

August 28, 2016


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akipokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa TanTrade, Bw. Edwin Rutageruka mara baada ya kuwasili kwenye Banda la Maonesho la Tanzania yanayofanyika wakati wa Mkutano wa TICAD VI Jijini, Nairobi. Makampuni na Taasisi mbalimbali kutoka nchi za Afrika ikiwemo Tanzania na Japan yanashiriki maonesho hayo yanayolenga kuvutia wawekezaji na wafanyabishara. 
Mhe. Naibu Waziri akipata maelezo kuhusu bidhaa mbalimbali zinazozalishwa Tanzania zilizokuwepo kwenye Banda hilo. Bidhaa hizo ni pamoja na Kahawa, Majani ya Chai na Viungo vya chakula.
Banda la Tanzania kama linavyoonekana.
Mhe. Waziri akipata maelezo ya namna watu wa makampuni mbalimbali walivyovutiwa na kahawa ya Tanzania.
Mhe. Naibu Waziri akikaribishwa na Bi. Latifa Kigoda, Afisa Mwandamizi kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) alipotembelea banda la Tanzania.
Mhe. Naibu Waziri akisaini kitabu cha wageni bandani hapo.
Mhe. Naibu Waziri akisikiliza maelezo kutoka kwa Bi. Kigoda kuhusu namna TIC ilivyojipanga kutangaza fursa za uwekezaji kwa wawekezaji mbalimbali wanaohudhuria mkutano wa TICAD VI.
Bi. Kigoda akimpatia Jarida Maalum lililoandaliwa na TIC kwa ajili ya kuvutia wawekezaji waliohudhuria mkutano wa TICAD VI.
Bi. Kigoda akimpatia maelezo Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Bi. Talha Waziri ambaye alikuwa amefuatana na Mhe. Naibu Waziri.
Mmoja wa wageni aliyetembelea bandani hapo akipata maelezo ya fursa za uwekezaji zilizopo nchini kutoka kwa Bi. Kigoda.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Dkt. Susan Kolimba akipata maelezo kutoka kwa Bw. Lameck Borega, Meneja wa Uwekezaji wa EPZA. 
Mhe. Dkt. Kolimba akimpatia ushauri wa namna ya kuwashawishi wawekezaji kuja nchini kuwekeza kupitia EPZA.
Mhe. Naibu Waziri akiwa amewasili kwenye Banda la Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na kupatiwa maelezo na Bi. Alistidia Karaze, Afisa Utafiti Mkuu kwenye Bodi hiyo.
Mhe. Naibu Waziri akimpatia ushauri Bi. Karaze wa namna ya kuboresha huduma za utalii nchini ikiwemo maonesho ili kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea nchini.

Mafundi wa TEMESA washauriwa kutumia mafunzo waliyoyapata kuendana na mabadiliko ya teknolojia

August 28, 2016


Mjumbe wa Bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri(katikati aliyesimama) akizungumza na mafundi wa TEMESA wakati akifunga mafunzo ya mafundi wa Wakala hao iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Agosti 26,2016.
Kaimu Mtendaji TEMESA Mhandisi Manase Ole Kujan(kulia) akitoa neno kwa mafundi wa TEMESA wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo kwa mafundi hao iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Agosti 26,2016 kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri .
Mjumbe wa Bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri akionesha moja ya vifaa vilivyokabidhiwa na mafundi wa TEMESA kwa ajili ya karakana zao wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo kwa mafundi hao iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Agosti 26,2016.
Mjumbe wa Bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri akikabidhi cheti kwa mmoja wa mafundi Bw.Saidi Waziri kutoka Arusha wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo kwa mafundi hao iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Agosti 26,2016.
Mjumbe wa Bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri akikabidhi moja ya vifaa vilivyotolewa kwa ajili ya karakana za TEMESA kwa Bw. Japhet Mwita mmoja wa washiriki wa mafunzo yaliyofanyika hivi karibuni katika hafla ya kuhitimisha mafunzo hayo iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Agosti 26,2016.
Mjumbe wa Bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri akikabidhi moja ya vifaa vilivyotolewa kwa ajili ya karakana za TEMESA kwa Bw. Japhet Mwita mmoja wa washiriki wa mafunzo yaliyofanyika hivi karibuni katika hafla ya kuhitimisha mafunzo hayo iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Agosti 26,2016.

RAIS DKT MAGUFULI AHUDHURIA MISA YA JUBILEI YA DHAHABU (MIAKA 50) YA NDOA YA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA NA ANNA MKAPA

August 28, 2016
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe wakati akiwasili kuhudhuria  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 "Maharusi"  Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakiingia kanisani  tayari kwa  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 "Maharusi"  Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakiingia kanisani  tayari kwa  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa  wakiwa tayari kwa  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa  na wageni waalikwa akiwemo Rais Dkt John Pombe Magufuli na mkewe mama Janeth Magufuli  katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Sehemu ya wanafamilia wa Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa    katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 MC Mavunde akipiga kinanda wakati wa  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016

  Sehemu ya wanafamilia wa Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa    katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Sehemu ya waumini na wageni waalikwa   katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Sehemu ya waumini na wageni waalikwa   katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Sehemu ya waumini na wageni waalikwa   katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Sehemu ya waumini na wageni waalikwa   katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Sehemu ya waumini na wageni waalikwa   katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Sehemu ya waumini na wageni waalikwa   katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016

  Sehemu ya waumini na wageni waalikwa   katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Sehemu ya waumini na wageni waalikwa   katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Wanakwaya katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Kiongozi wa kwaya  katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Sehemu ya wanafamilia wa Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa    katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Bw. Nicholaus Mkapa, mtoto wa Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa  akisoma somo la kwanza   katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
  Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha Josephat Lebulu akiongea na wana familia, waumini na wageni waalikwa katika  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa hiyo katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe akiongoza Ibada ya ukumbusho wa ahadi za ndoa wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe akiongoza Ibada ya ukumbusho wa ahadi za ndoa wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe akiongoza Ibada ya ukumbusho wa ahadi za ndoa wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Rais Dkt Magufuli, mkewe Mama Janeth Magufuli, Mama Maria Nyerere, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa na waumini na wageni waalikwa  wakiwa katika Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe akiongoza Ibada ya ukumbusho wa ahadi za ndoa wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa akimvisha pete Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa akivishwa pete na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakifurahia jambo baada ya zoezi hilo
 Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe akitoa neno kwa "maharusi" hao wenye furaha 
  Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe akitoa neno kwa "maharusi" . Kulia ni  Balozi Anthony Nyaki aliyesimamia harusi yao siku kama ya leo miaka 50 iliyopita. Matron alikuwa Marehemu Lucy Lameck.
  "Maharusi"  Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wanaketi baada ya ukumbusho wa viapo vya ndoa yao katika  kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016

 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa akiongea na kadamnasi 

  Rais Dkt Magufuli, mkewe Mama Janeth Magufuli, Mama Maria Nyerere, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa na waumini na wageni wakiendelea na misa
 Mawaziri wakuu wastaafu walikuwepo. Kutoka kushoto ni Jaji Joseph Sinde Warioba na mkewe Evelyn Warioba. Mzee Cleopa Msuya, Mama Amne Salim na mumewe Dkt. Salim Ahmed Salim na Mhe Edward Lowasssa na mkewe mama Regina Lowassa
 Sir Andy Chande akiungana na waalikwa katika misa hiyo
 Mohamed Dewji na mkewe wakiwa katika misa hiyo
 Mstari wa mbele
 Makamu Mwenyekiti wa CCM Ndg Philip Mangula na mkewe pamoja na wageni wengine
 Mawaziri wakuu wastaafu walikuwepo. Kutoka kushoto ni Jaji Joseph Sinde Warioba na mkewe Evelyn Warioba. Mzee Cleopa Msuya, Mama Amne Salim na mumewe Dkt. Salim Ahmed Salim na Mhe Edward Lowasssa na mkewe mama Regina Lowassa
 Katibu Mkuu Kiongozi Eng. John Kijazi, Maspika wastafu Mzee Pius Msekwa na Mama Anne makinda na Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Balozi Ombeni Sefue
 Sehemu ya waalikwa
 Jaji Mkuu mstaafu Mhe. Barnabas Samatta na mkewe pamoja na waalikwa wengine
 Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Mhe. Marten Lumbanga na mkewe pamoja na Waziri mstaafu Profesa Philemon Sarungi na mkewe Mama Sarungi
 Waalikwa
 Wageni waalikwa 
 Waalikwa
 Sehemu ya waalikwa
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakiongoza wana familia kupeleka matolea altereni
 Kwaya 
 Sehemu ya waalikwa
 Waalikwa
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha Josephat Lebulu akiongoza misa 
 Misa ikiendelea
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha Josephat Lebulu akiongoza misa 
 Misa ikendelea
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akimtakia amani Mama Anna Mkapa
Mama Janeth Magufuli na Mama Maria Nyerere wakiwatakia amani Mzee Mkapa na Mama Anna Mkapa
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akimtakia amani Mhe. Edward Lowassa

 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakipokea hati malumu ya ndoa kutoka Vatican kwa Baba Mtakatifu Papa Francis kutoka kwa Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakipongezwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo