UNESCO, TCRA YATAKA WADAU WA HABARI KATIKA MATUMIZI YA INTANETI KUZINGATIA USIRI NA MAADILI

UNESCO, TCRA YATAKA WADAU WA HABARI KATIKA MATUMIZI YA INTANETI KUZINGATIA USIRI NA MAADILI

September 14, 2015
IMG_8938
Mwenyekiti wa National Governance Internet Forum ambaye pia ni Rais wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akiwakaribisha wadau wa mitandao na watumiaji wa intaneti kwenye jukwaa hilo kabla ya kumkaribisha mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA kufungua rasmi jukwaa hilo.. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Tanzania Education and Research Network (TERNET), Amos Nungu na Kushoto ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph akifuatiwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Sunday Richard. (Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
Na Mwandishi Mwetu
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, (UNESCO), limewaomba wadau wa habari hasa wa matumizi ya intaneti kuzingatia maadili na usiri katika kazi zao ili kutovunja sheria zilizowekwa na mamlaka husika likiwemo suala la sheria ya mtandao iliyopitishwa hivi karibuni nchini Tanzania.
Hayo yameelezwa na Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliyekuwa akimwakilisha Mkurugenzi wa UNESCO, Zulmira Rodrigues katika Jukwaa la wadau wa usimamizi wa masuala ya mtandao (NIGF), lililofanyika mwishoni mwa wiki na kuandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).
UNESCO inaamini masuala ya usiri katika mitandao ni njia bora zaidi za kuepukana na suala la mmomonyoko wa maadili na usio zingatia taaluma.
Ambapo amebainisha kuwa, takribani Asilimia 84 ya Mataifa duniani wamegundua hawana sheria madhubuti ya kulinda uhuru wa usiri kwa wananchi kupitia mitandao hivyo ni muhimu kuzingatia taaluma na maadili kwenye matumizi ya intaneti hasa kwa kipindi hichi.
“UNESCO inaamini mambo muhimu ya kuzingatia juu ya matumizi ya mitandao ikiwemo kuwa na Uwazi, Upatikanaji na Ushirikishi. Kwa hayo machache, mjadala huu wa matumizi ya mtandao unaweza kufanikiwa na sie tunapenda kuungana na nyinyi katika kushirikiana katika suala hili” alieleza Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph.
IMG_9056
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Sunday Richard akifungua rasmi Jukwaa la wadau wa usimamizi wa masuala ya mtandao (NIGF) lililoandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) na kufanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano COSTECH jijini Dar. Kushoto ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliyemwakilisha Mkurugenzi wa UNESCO na kulia Mwenyekiti wa National Governance Internet Forum, Kenneth Simbaya.
Aidha, katika mkutano huo, imeelezwa kuwa, matumizi makubwa ya mtandao wa kompyuta (intaneti) yatasaidia ongezeko la pato la taifa (GDP).
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya jukwaa la mtandao wa intaneti (IGF) Kenneth Simbaya wakati wa jukwaa hilo ambapo amebainisha kuwa, katika matumizi yake ni muhimu sana kujadili kutengeneza kesho wanayoitaka watanzania katika matumizi ya mtandao.
Ameeleza chombo cha IGF kimelenga kuangalia maendeleo ya mtandao nchini usalama wake na matumizi ya mtandao yanayoelenga kubadilisha maisha ya watanzania kwani chombo hicho nchini Tanzania kimeundwa kutokana na mkutano wa kimataifa wa jamii ya wanahabari (WSIS) waliotaka kuwepo na jukwaa kuangalia matumizi ya matandao kutokana na kuongeza kwa haja ya matumizi.
Simbaya amesema Majukwaa hayo yanatakiwa kuzungumza kuhusu sera kwa lengo la kuangalia uendelevu wake , usalama, ukuaji wa mtandao wenyewe na menejimenti yake.
Kwa upande wake Mtaalamu kutoka TCRA Dk. Emmanuel Manasseh akithibitisha umuhimu wa mtandao katika maisha ya sasa na yajayo, alielza kwamba kama kutakuwepo na ongezeko la watumiaji angalau kwa asilimia 10 pato la taifa litaongezeka kwa asilimia 1.4. zaidi.
Ambapo anaendelea kubainisha kuwa, kwa sasa idadi ya watumiaji wa mtandao wameongezeka kufikia asilimia 11 na kwamba lugha ya mtandao kwa sasa inaathiri watu mbalimbali kwa namna njema na namna mbaya.
Jukwaa hilo pamoja na kuzungumza kuhusu uendelevu wake pia ulizungumzia sheria , kanuni na taratibu zinazotakiwa kuzingatiwa katika matumizi na utawala wa intaneti ili kuzifanya zitumike kwa makusudio mema zaidi.
Naye mtaalamu wa masuala ya mtandao wa intaneti, Maxence Melo kutoka Jamii Forum amesema kwamba mpaka sasa anaona kwamba matumizi ya mtandao Tanzania bado salama ingawa juhudi lazima ziendelee kufanyika kuhakikisha kwamba hali ya usalama inaendelea kuwapo.
IMG_8959
Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliyemwakilisha Mkurugenzi wa UNESCO akitoa salamu za shirika la UNESCO wakati wa mkutano wa Jukwaa la wadau wa usimamizi wa masuala ya mtandao (NIGF) ulioandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).
IMG_9012
Katibu Mtendaji wa Tanzania Education and Research Network (TERNET), Amos Nungu akitoa salamu za TERNET kwa wadau waliohudhuria jukwaa hilo.
IMG_9203
Mtaalamu kutoka TCRA Dk. Emmanuel Manasseh akiwasilisha mada iliyoelezea umuhimu wa mtandao katika maisha ya sasa na yajayo wakati wa jukwaa hilo.
IMG_9206
Pichani juu na chini ni sehemu ya washiriki waliohudhuria jukwaa hilo wakifuatilia "presentation" iliyokuwa ikitolewa na Mtaalamu kutoka TCRA Dk. Emmanuel Manasseh (hayupo pichani).
IMG_9182
IMG_9207
IMG_8974
IMG_9218
Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph kwa mtaalamu kutoka TCRA (hayupo pichani) kama wana mipango gani kuhakikisha kuwa kutakuwepo na masafa ya kutosha kwa miaka mingi ijayo kwaajili ya wananchi wa vijijini na wale wasio na uwezo.
IMG_9076
Picha ya pamoja.
IMG_9115
Maxence Melo kutoka Jamii Forum akizungumza na waandishi wa habari wakati wa jukwaa lililowakutanisha kwa pamoja wadau wa masuala ya mitandao ya intaneti.
IMG_9081
Maxence Melo kutoka Jamii Forum (katikati) akipata picha ya pamoja na wajumbe wa Tanzania Bloggers Network (TBN), Fredy Njeje wa Blog za Mikoa (kulia) na Mr. Verbs.

WATANZANIA KUDUCHU WALIOJITOKEZA HARAMBEE YA CSI UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON, DC JUMLA YA $2,696 ZAPATIKANA

September 14, 2015
Ivan Matovu akisherehesha harambee ya Childbirth Survival International iliyofanywa kwa ushirikiano wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani siku ya Jumamosi Septemba 12, 2015 katika chumba cha mkutano cha Nyerere ndani ya jengo la Ubalozi huo na jumla ya $2,696 zilikusanywa siku hiyo kwa ajili ya kusaidia kuokoa maisha ya wazazi wanaotarajia kujifungua katika Hospitali ya Wilaya ya Biharamuro. CSI walishawahi toa msaada wa namna hiyo hospitali ya Amana iliyopo Wilaya ya Ilala jijini Dar na nchini Uganda kwa lengo hilo la kuokoa maisha ya wazazi watarajiwa wa kujifungua. Takribani ya wazazi 35 hufa kila siku aidha kwa sababu ya kukosekana vifaa au kwa uzembe na kutokuwepo kwa elimu ya kutosha itakayosaidia kuokoa maisha ya mzazi hao. Na kama ingekua daladala kila siku inatokea ajali na kuua wa 35 nadhani nchi ingacha shughuli zake na kulitazama swala hilo kwa upana zaidi lakini mtizamo wa akina mama hao 35 wanaopoteza maisha kila siku kwa ajili ya kujifungua bado wananchi na serikali haijalichukulia swala hili uzito unaostahili ya kuokoa maisha ya akina mama hao. PICHA NA VIJIMAMBO NA KWANZA PRODUCTION
 Tausi Swedi mmoja ya waanzilishi wa CSI akielezea kazi kubwa inayofanywa na Childbirth Survival International kujaribu kuokoa maisha ya akina mama wanaojifungua.
 Mkurugenzi na mmoja ya waanzilishi wa CSI nchini Tanzania Mama Stella Mpanda akielezea kazi ya Childbith Survival International nchini Tanzania.
Sandra Kiyonga mmoja wa CSI akielezea jambo.

Jessica Mushala akiipongeza CSI kwa kazi kubwa na nzuri ya kuwasaidia akina mama wanaojifungua Duniani kote kwa kutoa elimu ya uzazi na vifaa kwa wazazi na wakunga kujaribu kuokoa maisha ya wazazi wanaojifungua kutokana na uzembe au kutokua na vifaa ikiwemo elimu ya uzazi.

Kikundi cha utamaduni cha ngoma ya asili aina ya mbuutu ya Uganda ikitumbuiza kwenye harambee hiyo.

Wahudhuriaji kwenye harambee hiyo. Kwa picha zaidi bofya HAPA
Geofrey Adroph BLOGGER P.O.BOX 24793, Mob: +255 755 274953 /+255 713 363965, Email: pamojapure@gmail.com. Blog: http://www.pamoja.co.tz/ DAR ES SALAAM, TANZANIA

MCHANGANYIKO WA ASALI NA MDALASINI KATIKA KUTIBU CHUNUSI SUGU

September 14, 2015
Asali ikiwa imechanganywa na mdalasini tayari kwa matumizi



Wadau wetu wale ambao wanasumbuliwa sana na CHUNUSI iwe USONI, KIFUANI, MGONGONI n.k wanaweza tumia mchanganyiko mzuri wa ASALI na MDALASINI WA UNGA kwa kupaka angalau mara moja kwa siku.
ASALI na MDALASINI zinasaidia kuponyesha kwasababu zina tabia za ANTI-BACTERIAL( zinaua na kuzuia mazalia ya bacteria)
Jinsi ya kufanya:-
1. Chukua vijiko vitatu(3) vya chai vya ASALI
2. Chukua nusu kijiko cha chai cha MDALASINI WA UNGA safi
3. Changanya pamoja kupata uji uji mzuri
4. Paka sehemu yenye chunusi na kisha kaa nayo kwa angalau dakika 10-30 kisha osha kwa maji ya uvuguvugu.
ANGALIZO: MDALASINI unaweza kuwasha kwenye ngozi hivyo unashauriwa ujaribu kupaka kidogo kwenye kiganja cha mkono kwanza ili kupata uhakika kua haitakusumbua.

(Imeandaliwa na Honey Spring na Jamiimojablog)



 0683370065 au 0769129351

Gharika ya watu yashuhudia uzinduzi rasmi wa kampeni za CCM za kugombea urais wa Zanzibar

September 14, 2015
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja kwa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mama Fatma Karume  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Amani Abeid Karume  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  na Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Amani Abeid Karume  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
Sehemu ya gharika ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Sehemu ya gharika ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Ndege ndogo ikipita juu ya  Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiwasili katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
  Rais Kikwete akimlaki Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiwasili katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Gharika ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 gharika ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Mama akisaidiwa kwenda kupata huduma ya kwanza baada ya kuhemewa na gharika ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
Nyomi  ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015

Utenzi ukisomwa  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Sehemu ya gharika ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
  Sehemu ya gharika ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
  Sehemu ya gharika ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Kikwete, mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahman Kinana wakiwa na furaha katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
  Rais Kikwete, mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahman Kinana wakiwa na furaha katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Kada mashuhuri wa CCM Visiwani Zanzibar Mzee Borafia akiongea katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Umati ukishangilia katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 CCM OYEEEEEE....anasema kada huyu katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Kikwete akimpongeza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. Mohamed Gharib Bilali baada ya kuhutubia katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Amani Abeid Karume  akihutubia kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
Viongozi wakiwa jukwaa kuu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Wanahabari wakirekodi tukio hilo la kihistoria kw kila aina ya vifaa vya kisasa ikiwemo drone ya kupigia picha kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Msanii Diamond na kundi lake la Wasafi wakitumbuiza kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
  Msanii Diamond na kundi lake la Wasafi wakitumbuiza kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg. Vuai Ali Vuai akisoma ratiba ya mkutano   kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akihutubia umati kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi akiwa amehemewa kwa gharika ya watu  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Rais Kikwete akihutubia kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Rais Kikwete akisisitiza jambo wakati akihutubia kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Rais Kikwete akifafanua jambo wakati akihutubia kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Diamond na kundi lake wakitumbuiza  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Jukwaa kuu likifurahia onesho la Diamon na kundi lake  wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Rais Kikwete akirejea tena mbele kumtambulisha mgombea wa Urais wa CCM Dkt Ali Mohamed Shein  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
Rais Kikwete na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahmana Kinana wakijiandaa kumtambulisha mgombea wa Urais wa CCM Dkt Ali Mohamed Shein  kwenye Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015.
 Msaada unatolewa kwa mama aliyepoteza fahamu  kutokana na wingi wa wananchi wakati wa mkutano huo
 Nyomi mkutanoni hapo
  Rais Kikwete na Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein wakionesha Ilani ya Uchaguzi ya CCM katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akihutubia gharika hiyo ya watu katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Sehemu ya wananchi, wanaCCM  na viongozi uwanjani hapo
 Dua ikisomwa  baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Kikwete na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa Rais Kikwete wakipongezana kwa   furaha baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Gharika ya watu ikiondoka kwa furaha na amani baada ya mkutano uliofana wa uzinduzi wa  kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Kikwete akiaga wakati akiondoka Unguja kurejea Dar es salaam  baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Kikwete akiaga wakati akiondoka Unguja kurejea Dar es salaam  baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Kikwete akimnyakua mtoto wakati  akiondoka baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Kikwete akimbeba  mtoto huyo  baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
  Rais Kikwete akipata picha na watoto  baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
  Rais Kikwete akiaga baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Kikwete akiagana kwa furaha na wananchi  baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Kikwete akiagana kwa furaha na wananchi  baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
  Rais Kikwete akiaga wakati akiondoka Unguja kurejea Dar es salaam  baada ya  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
 Rais Mstaafu Benjamin Mkapa akiagana na viongozi wa CCM wa Visiwani wakati akiondoka Unguja kurejea Dar es salaam  baada ya kuunguruma katika  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
"....CCM JUU!" anasema Rais Mstaafu Benjamin Mkapa wakati akipanda ndege kuondoka baada ya kuhudhuria kuunguruma katika  uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015. PICHA NA IKULU