Watendaji wa vijiji waaswa kushirikisha wananchi kwenye miradi ya maendeleo

June 29, 2013
Na Amina Omari,Handeni
 
 Wenyeviti wa vijiji wametakiwa kuhakikisha wanawasomea wananchi mapato na matumizi kila baada ya miezi mitatu na kuhakikisha wanawashirikisha  kwenye miradi ya maendeleo bila kificho wala usiri.
 
Kauli hiyo imetolewa na Afisa Tarafwa kata ya Mazingara Hashi Msagati wakati wa kikao cha baraza la kata WDC kilichofanyika katika kijiji cha mazingara wilayani Handeni hapo jana alisema ni kwaida ya watendaji kutowasomea wananchi mapato na matumizi ya kijiji husika.
 
Alisema nihaki ya msingi ya mwanakijiji kujua pesa yake inayokusanya kwa ajili ya maendfeleo ya kijiji inatumika kwa mipango gani  ya maendeleo badala ya kuwafanyia kificho na kutumia fedha kwa malengo yasiyofaa.
 
“Nawaasa watendaji wa mitaa,vijiji hadi kata kuhakikisha mnawaeleza wananchi kwa uwazi bila kificho kiasi cha fedha za ruzuku za maendeleo zilizopatiwa kijiji na pesa za makusanyo ya ndani huku mkiwashirikisha katika mipango ya maendeleo ya fedha hizo”alisema Msagati.
 
 
 
Alisema kunawizi wa kalamu  hasa katika maeneo ya vijiji watendaji wanaandika kuwa wananchi wameidhinisha fedha kumbe sio kweli huku wahusika wenyewe wakiwa hawajui bali wanaona ujenzi tu unaendelea aidha wa madarasa au miundombinu yoyote .
 
Nae Diwani wa Kata ya Mazingara Kijoli aliwataka watendaji wa kata hiyo kuhamasisha wananchi kujenga nyumba za kisasa za biashara ili watendaji hao waisha ndani ya kata hiyo badala ya kuishi nje ya eneo la kazi.
 
Alisema hali hiyo imekuwa ikizorotesha shughuli za maendeleo katika kata hiyo kwani watendaji wengi hawawajibiki ipasavyo kutoka na kuishi mbali na ofisini zao hivyo huwavigumu kuwapa pale wanapohitajika na wananchi hao.
 
Mwisho

Nasi tunapenda kuwa watangazaji

June 29, 2013

MTANGAZAJI wa Kipindi cha Mimi na Mwanafunzi na muandaaji wa kipindi hicho kinachoruka kituo cha Radio Mwambao Fm kila Jumaamosi saa tatu asubuhi Seleman Kibugo mwenye shati jeusi akiwa na wanafunzi wa shule ya Shilela Academy iliyopo wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro ambao watembelea Kituo Cha Utangazaji Cha Mwambao Fm Tang leo.

NYUMBA 12 ZA WAVAMIZI WAHIFADHI YA MISITU ZATAKETEZWA KWA MOTO PANGANI

June 29, 2013


Na Amina Omari,Pangani
Jumla ya Nyumba 12 zilizokuwa zimejengwa na wahamiaji haramu jamii ya wafugaji  ndani ya hifadhi ya msitu wa Msububwe wilayani Pangani Mkoani Tanga zimeteketezwa kwa moto na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo ikiwa ni katika oparesheni ya kuondosha wavamizi wa hifadhi hiyo .
Zoezi hilo ambalo linalenga kulinga hifadhi ya msitu huo dhidi ya wavamizi hao wa  kabila la wamang”ati ambao walikuwa wamevamia hifadhi na kuanza kufanya uharibu wa kuharibu  vyanzo vya maji,  kukata miti hovyo ya kujengea nyumba , kuni pamoja na kuchunga mifugo yao.

Akiongea na gazeti hili wakati wa oparesheni hiyo Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Pilika Kasanda alisema zoezi hilo litakalo dumu kwa muda wa siku tano  la kuwamisha na kuharibu makazi ya wavamizi hao ili kulinga  hifadhi hiyo isiendelee kuharibiwa.

“Zoezi hili limeanza leo na litadumu kwa siku tano katika kukagua na kuwaondosha kwa nguvu wavamizi wote wafugaji walioko ndani ya hifadhii kwani wameanza uharibu wa vyanzo vya maji ambavyo ndio tegemeo pekee la wilaya hii”alisema Kasanda.

Alisema  wafugaji ho wamekuwa wakivamia msitu huo mara kwa mara licha ya juhudi mbalimbali walizozichukuwa za kuwapa elimu kuhusu umuhimu wa hifadhi hiyo na kuwataka warudi katika makazi yao ya awali lakini imeshindikana.

Hata hivyo Meneja hifadhi msitu huo John Mkenda alisema kabla ya zoezi hilo walianza kutoa elimu kwa jamii  inayozunguka hifadhi kuhusu umuhimu wa hifadhi hiyo na madhara ya uharibufu unaofanyika ili kuhakikisha wanalinda hifadhi na viumbe vilivyoko.

“Tulianza kutembelea vijiji vinavyozunguka hifadhi ili kutoa elimu ya mazingira kisha tukawatembelea na wavamizi ambao ni jamii ya wamasai na kuwashauri watoke kwa amani kabla ya hatua za kisheria kuanza kufuatwa ,tunashukuru walitii ili wengine walikaidi”alisema Mkenda.

Aliongeza kuwa nyumba nne hawakuzichoma moto kutoka na kutowakuwa wazazi bali wapo watoto pekee lakini nao wamewapa siku mbili kuondoka kwa hiari kabla ya kuanza kuchoma moto nyumba hizo pamoja na vitu vyao.
MWISHO

Mkutano mkuu Coastal Union kufanyika kesho.

June 29, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
MKUTANO Mkuu wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga unatarajiwa kufanyika kesho  katika makao makuu yake yaliyopo katika barabara ya kumi na moja jijini Tanga ambapo agenda mbalimbali zitazungumzwa.

Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Hemed Aurora “Mpiganaji”aliliwaambia waandishi wa habari kuwa agenda kuu itakuwa ni kuwajulisha wanachama wao mafanikio yaliyopatikana katika msimu wa ligi kuu uliomalizika na malengo yao katika msimu ujao.

Aurora alisema suala lengine ambalo litazungumza katika mkutano huo ni Katibu Mkuu wao, Kassim El Siagi kusoma taarifa ya mapato na matumizi kwa wanachama wao ambao watahudhuria lengo likiwa ni kuwapa ufahamu kuhusu mambo hayo.

Aliongeza kuwa agenda nyengine ni kuzungumzia maendeleo ya wachezaji wao pamoja na kuweka mikakati ya ya msimu mpya wa ligi katika mwaka 2013-2014 ambapo lengo lao ni kushiriki ligi hiyo kwa mafanikio makubwa zaidi ya ligi iliyopita.

Mwenyekiti huyo alisema wachezaji waliosajiliwa na klabu hiyo wanatarajiwa kuwasili mkoani hapa kuanzia leo na mpaka Julai 3 mwaka huu wachezaji wote waliosajiliwa watakuwa wamekwisha kuwasili kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.


Akizungumzia usajili wao msimu huu, Aurora alisema walichokifanya ni kuziba mapungufu yaliyijitokeza katika mzunguko wa pili wa ligi ili kuweza kukiimarisha lengo likiwa kuleta upinzani na mafanikio msimu ujao.

Mwisho.

WIZARA ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo yapewa changamoto.

June 29, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.

SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo imeshauriwa kuweka utaratibu wa kukaa na makocha wa kigeni wanaofundisha timu za Taifa muda mrefu ili kuweza kupata mafanikio badala ya kuwabadilisha kila wakati kitendo ambacho kinadumaza soka badala ya kupiga hatua kwenda mbele.



Ushauri huo ulitolewa na Golikipa wa zamani wa timu ya Coastal Union ya Tanga, Nyendi Mpangala wakati akizungumza na mwandishi wa blog hii hivi karibuni ambapo alisema kitendo cha ubadilishwaji wa makocha hao kunawafanya hata wachezaji wenyewe kutokuelewa kile wanachofundishwa kutokana na kila kocha mpya anakuwa na mbinu zake.



Nyendi aliwahi kuichezea Costal Union ya Tanga kati ya mwaka 2000-2003 alipoamua kuacha kujishughulisha na mambo ya soka hapa nchini na kueleza mpira wa sasa hivi ni tofauti na zamani kutokana na enzi hizo wachezaji wengi walikuwa na vipaji vyao binafsi kuliko ilivyokuwa wakati huu .



Alisema ili soka letu hapa nchini liweze kupiga hatua ni lazima serikali ihakikishe wanahamasisha wadau kuanzisha vituo vya mafunzo ya soka (Academy) ambazo zitakuwa imara kwa ajili ya maendeleo ya soka hapa nchini ikiwemo kuvilinda vipaji hivyo pamoja na kulinda viwanja vya michezo vilivyopo maeneno mbalimbali na kuwapa fuksa wachezaji kucheza.



Akizungumzia nafasi ya mlinda mlango alisema ni ngumu lakini ni rahisi endapo wachezaji wenyewe wataipenda kutokana na kuwa nafasi ambayo mara moja unaweza kupata nafasi ya kwenda kucheza kwenye timu nyengine ikiwemo timu ya Taifa kwa sababu ni mahali ambapo mtu anaonekana.



Mwisho.