UNESCO YATOA TAHADHARI ONGEZEKO LA JANGWA

UNESCO YATOA TAHADHARI ONGEZEKO LA JANGWA

June 17, 2017
Nchi yetu. Nyumba zetu. Mustakabali wetu. Hii lazima iwe kauli mbiu yetu leo - hasa katika mapambano dhidi ya kuenea kwa jangwa. Mchango wa mabadiliko ya mazingira katika uhamiaji na makazi ya watu uko wazi duniani kote. 

Idadi kubwa ya 'wakimbizi wa mazingira' sasa huwasilishwa kama moja ya matokeo makubwa ya mabadiliko ya hali ya hewa na kuenea kwa jangwa. 

Na hili hii inategemewa kundelea kuongezeka.
 Kufikia 2030, Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na Kuenea kwa Jangwa imeonya kuwa, kufikia mwaka 2030 watu wapatao milioni 135 wako katika hatari ya kuhama makazi yao kwa sababu ya kuenea kwa jangwa, na watu milioni 60 wanatarajiwa kuhama kutoka Kusini mwa jangwa la Sahara kuelekea Afrika ya Kaskazini na Ulaya.  

Utabiri huu unaonyesha kuwa sehemu zilizo kame na zile zilizo kame zaidi huathirika zaidi na kuenea kwa jangwa na kuhama kwa watu. 
Dk. Kigwangalla ahimiza ushirikiano, ashiriki iftar iliyoandaliwa na Benki ya CBA Tanzania

Dk. Kigwangalla ahimiza ushirikiano, ashiriki iftar iliyoandaliwa na Benki ya CBA Tanzania

June 17, 2017
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamisi Kigwangalla ameshiriki futari maalum iliyoandaliwa na Benki ya Biashara Afrika Tawi la Tanzania (CBA Tanzania) iliyokuwa maalum kwa ajili ya wadau na wateja wa benki hiyo, tukio lililofanyika katika Hotel ya Hyatty Regency, Kilimanjaro ijini Dar es Salaam jioni ya Juni 16.2017. Dkt. Hamisi Kigwangalla ambaye alikuwa mgeni rasmi katika tukio hilo, aliimiza ushirikiano, Umoja na upendo kwa watanzania wote hasa katika kipindi hiki cha mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Kwa upande wao CBA Tanzania walibainisha kuwa, tukio hilo ni sehemu ya kuboresha uhusiano na wateja na wadau wao. Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo Dk.Gift Shoko alisema: “Tunampongeza Naibu Waziri Dk. Kigwangalla kwa kufika na kujumuika nasi katika tukio hili maalum la Iftar. Pia tunawashukuru sana wateja wetu nchini kote kwa kuendelea kuiamini benki yetu katika kupata bidhaa na huduma za kibenki na ndio maana tunashirikiana nao sana katika maeneo maalum ambayo yanatukutanisha ili pia tuweze kujadiliana na kuboresha ushirika wetu kama tunavyokutana leo kwenye futari hii”. Alisema Dk. Shoko. Dk. Shoko aliahidi kuwa Benki itaendelea kuboresha bidhaa na huduma zake ili ziendelee kuwa na ubora wa hali ya juu kabisa ikiwa ni pamoja na kubuni huduma mbalimbali za kuwarahishia maisha wateja wanapohitaji kupata huduma za kibenki na kuboresha shughuli zao.“Benki ya CBA Tanzania tunawatakia mfungo mwema wa Ramadhani lakini pia maandalizi mema ya sikukuu hapo baadae!,” alieleza. CBA Tanzania ni sehemu ya CBA Group iliyopo katika nchi za Kenya, Uganda na Tanzania, CBA Tanzania ina matawi kumi na moja yaliyosambaa sehemu mbalimbali nchini.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamisi Kigwangalla pamoja na Mke wake wakiwasili katika Hotel ya Hyatty Kilimanjaro alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Benki ya Biashara Afrika Tawi la Tanzania (CBA Tanzania) jioni ya Juni 16.2017 Jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na Mkuu wa Idara ya Huduma Binafsi wa Benki ya Biashara Afrika Tawi la Tanzania (CBA Tanzania), Bw. Julius Ngonyani alipowasili katika Hotel ya Hyatty Regency, Kilimanjaro alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Benki hiyo Tawi la Tanzania (CBA Tanzania) jioni ya Juni 16.2017 Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa CBA Tanzania, Gift Shoko.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamisi Kigwangalla akizungumza alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Benki ya Biashara Afrika Tawi la Tanzania (CBA Tanzania) iliyofanyika katika Hotel ya Hyatty Regency, Kilimanjaro jioni ya Juni 16.2017 Jijini Dar es Salaam

"NEXT EINSTEIN" YAZINDUA WIKI YA SAYANSI AFRIKA TANZANIA

June 17, 2017
Mtaalamu wa masomo ya Sayansi, Fadhil Leonard akiwaelekeza wanafunzi wa Shule ya Msingi namna ya kutengeneza gari linalojiendesha bila ya kuwa na dereva wakati wa hafla ya uzinduzi wa Wiki ya Sayansi Afrika Tanzania iliyofanyika  katika viwanja vya Shule ya Al-Murtaza Upanga jijini Dar es Salaam leo. 
VIDEO: BUNGE LA WATOTO LAVUTIA WENGI MKOANI MWANZA

VIDEO: BUNGE LA WATOTO LAVUTIA WENGI MKOANI MWANZA

June 17, 2017
Jana juni 16,2017 mataifa mbalimbali barani Afrika yaliungana pamoja kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika. Mkoani Mwanza, maadhimisho hayo yalifanyika uwanja wa Furahisha kwa kujumuisha matukio mbalimbali ya watoto. Wengi walivutiwa na kipengere cha bunge la Watoto mkoani Mwanza kwenye maadhimisho hayo yaliyokuwa na kaulimbiu ya "Maendeleo Endelevu 2030: Imarisha Ulinzi na Fursa Sawa kwa Watoto.
Tazama video

MAKAMU WA RAIS SAMIA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA DAR

June 17, 2017
 Watoto wakikimbia walipokuwa wakiandamana kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kinyerezi, ambapo yalifanyika kimkoa wilayani Ilala, Dar es Salaam leo.Maadhimisho hayo yaliongozwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan. PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Maandamano yalielekea kwenye viwanja hivyo
 Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan akiwashukuru na kuwapatia vyeti wauguzi wa kujitolea  walioshiriki kampeni kupima magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwa watoto na vijana  wakati wa T
 WATOTO WAKIPIMWA UREFU
 Maandamano
 Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan akiwasalimia watoto pacha Brighton na Bright Shirima alipokuwa akikagua mabanda ya tiba kwenye Tamasha la Uelimishaji na Upimaji Afya na Kinga dhidi ya Magonjwa yasiyoambukiza kwa watoto na vijana wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika
 Kikundi cha hamasa cha Ilala kikihamasisha wakati wa maadhimisho hayo
 Brass Band ya Polisi ikiongoza maandamano 
 Makamu wa Rais Samia akisalimiana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kigwangala
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akihutubia 

 Kikundi cha ngoma cha Shule ya Msingi Umoja kikitumbuiza kwa ngoma ya kibati wakati wa maadhimisho hayo

 Kikundi cha Umoja kikitumbuiza kwa ngoma ya Makhirikhiri


 Makamu wa Rais, Samia akimkabidhi cheti cha shukrani DkNg'wege aliyekuwa mmoja wa madaktari walioshiriki kupma afya za watoto na vijana wakati wa maadhimisho hayo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akihutubia katika maadhimisho hayo.Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigangwala na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema.

Mtoto wa miaka sita, darasa la kwanza azindua kitabu katika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika

June 17, 2017
Mtoto Ethan Thedore Yona akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kitabu chake kwa njia ya mtandao(App) kijulikanacho kama Ethan Man, hafla hiyo imefanyika leo kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika viwanja vya JKY Park Jijini Dar Es Salaam.

Mtoto Ethan Thedore Yona akitoa maelezo kwa watoto wenzie jinsi ya kutumia App yake ya Ethan Man kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika viwanja vya JKY Park Jijini Dar Es Salaam leo.

Mtoto Ethan Thedore Yona akitoa maelezo kwa watoto wenzie jinsi ya kutumia App yake ya Ethan Man kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika viwanja vya JKY Park Jijini Dar Es Salaam leo.

Kampuni ya Tigo Yaadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika kwa kushirikiana na wadau kwenye viwanja vya JKY Park Jijini Dar Es Salaam

June 17, 2017

Meneja mauzo na masoko wa taasisi ya Shule Direct Shaweji Steven (kushoto) akimuonesha Meneja Mawasiliano ya Umma kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Woinde Shisael (kulia) kifaa cha kusoma vitabu kwa njia ya mtandao kwa ajili ya wanafunzi wa elimu ya sekondari wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam mapema leo.

Mtaalamu wa kutengeneza roboti inayotumika kwa kuchezea watoto,Mkufu Tindi (aliyekaa) akitoa maelezo kwa Meneja Mawasiliano ya Umma wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Woinde Shisael (katikati) wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam mapema leo.


Meneja Mawasiliano ya Umma wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Woinde Shisael akizungumza na waandishi wa habari wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam mapema leo.
Watoto mbalimbali waliofika kwenye maadhimisho  maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam mapema leo.
Watoto wakiwa katika picha ya pamoja katika  maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam mapema jana.