Na Oscar Assenga, Lushoto.
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga,Abdi
Makange amewataka vijana wilayani Lushoto kujituma na kufikiria namna ya kubuni
ajira mbadala ikiwemo kujikita katika masuala ya ujasiriamali ili kuweza
kuendesha maisha yao
badala ya kuendelea kutegemea ajira za kuajiriwa.
Kauli hiyo aliitoa jana wakati akizungumza na wajumbe wa kamati
ya utekelezaji ya umoja huo wilaya ya Lushoto(UVCCM)wakati wa ziara yake ya
kwanza ya kukagua na kuangalia uhai wa umoja huo pamoja na kufanya mikutano ya
hadhara inayofanyika mkoa mzima wa Tanga.