Burudani za Vodacom zaleta furaha Pasaka Dar
Mshinda
wa kitita cha shilingi milioni 10/- kupitia promosheni ya Jaymillions
inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Shamila Ramadhani(kushoto)akikabidhiwa
hundi yake na Balozi wa promosheni hiyo Hillary Daud ‘JayMillions’
baada ya kuipuka mshindi wa kitita hicho kupitia promosheni hiyo
katikati ni mume wa mshindi huyo Abdallah Mahoka.Makabidhiano hayo
yalifanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Dar Live wakati wa
Tamasha la Mwana Dar Live lililofanyika Mbagala jijini Dar es Salaam.Ili
mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno JAY au AUTO kwenda
namba 15544.
Balozi
wa promosheni ya Jaymillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hillary
Daud ‘Jaymillions’akiwasomea tarakimu kwenye hundi iliyokuwa na thamani
ya shilingi milioni 10/-wakazi wa mbagala waliofika katika tamasha la
Mwana Dar live lililofanyaika katika ukumbi wa Dar live mbagala jijini
Dar es Salaam katika kuadhimisha sikukuu ya pasaka,Hundi hiyo
ilikabidhiwa kwa mshindi wa promosheni hiyo Shamila
Ramadhani(kusho)akiambatana na mumewe Abdallah Mahoka(katikati) Ili
mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno JAY au AUTO kwenda
namba 15544.
Mshinda
wa kitita cha shilingi milioni 10/- kupitia promosheni ya Jaymillions
inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Shamila Ramadhani(kushoto)pamoja na
mumewe Abdallah Mahoka wakiinua hundi yao juu ili wakazi wa mbagala
waliohudhuria tamasha la Mwana Dar Live waione baada ya kukabidhiwa
rasmi na Balozi wa promosheni hiyo Hillary Daud(hayupo pichani) baada ya
kuipuka mshindi wa kitita hicho kupitia promosheni hiyo.Makabidhiano
hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Dar Live wakati wa
Tamasha hilo lililofanyika Mbagala jijini Dar es Salaam.Ili mteja kujua
kama ameshinda anatakiwa kutuma neno JAY au AUTO kwenda namba 15544.
Msanii
wa muziki wa kizazi kipya Ali Kiba akiwapagawisha washabiki wa muziki
wake waliofurika katika Tamasha la Mwana Dar Live lililodhamini na
Vodacom Tanzania, Katika kuadhimisha sikukuu ya pasaka na kufanyika
katika ukumbi wa Dar Live Mbagala jijini Dar es Salaam.
Mamaa
Aisha Mashauzi akitumbuza muziki wa Taarabu katika Tamasha la Mwana Dar
Live lililodhamini na Vodacom Tanzania, Katika kuadhimisha sikukuu ya
pasaka na kufanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala jijini Dar es
Salaam.
Msanii
wa nyimbo za mchiriku Sueleman Jabiri”Msaga Sumu”akisaga sumu ipasavyo
kwa washabiki wa muziki wake wakati wa Tamasha la Mwana Dar Live
lililodhamini na Vodacom Tanzania, Katika kuadhimisha sikukuu ya pasaka
na kufanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala jijini Dar es Salaam.
Wapenzi
wa burudani ya muziki wa kizazi kipya na muziki wa taarabu wamepata
burudani ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka kutoka kwa magwiji wa muziki
wa kizazi kipya na taarabu katika matamasha ya burudani yaliyoandaliwa
na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania yaliyofanyika Coco Beach na Dar
Live ,Mbagala jijini Dar es Salaam.
Tamasha
la wazi lililofanyika Coco beach liliwavutia wakazi wengi wa jiji
hususani vijana pia kuhakikisha watoto hawaachwi nyuma nao waliandaliwa
burudani zao ambapo waliweza kucheza na kufurahia sikukuu ya Pasaka.
Wasanii
wa kizazi kipya Bob Junior na Shilole waliacha historia ya aina yake
kwa mamia ya washabiki wa muziki wa kizazi kipya waliofika katika fukwe
ya Coco kwa jinsi walivyoweza kukonga nyoyo zao na kudhihirisha kuwa
muziki wao ni wa kiwango cha juu pia walikuwepo wasanii mbalimbali
chipukizi ambao pia walimwaga burudani kwa mashabiki.
Funga
kazi ilikuwa Dar live Mbagala ambapo msanii mahiri wa Bongofleva Ali
Kiba kwa kushirikiana na mwanamama anayetamba katika muziki wa taarabu
nchini Aisha Mashauzi walimwaga burudani za aina yake na kupagawisha
washabiki waliofika katika tamasha la Mwana Dar Live ukumbini hapo
kusherehekea sikuu ya Pasaka.
Meneja
Uhusiano wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu amesema kuwa kampuni yao
imeamua kuandaa na kudhamini matamasha haya kwa ajili ya kuwapatia
furaha na burudani wateja wake na wananchi kwa ujumla katika msimu huu
wa sikukuu ya Pasaka na kuweza kuwakutanisha washabiki na wanamuziki
wawapendao na itaendelea kufanya hivyo kupitia promosheni ya Ishi Kistaa
na aliwakumbusha wateja kutuma neno STAR kwenda namba 15670 ili wapate
fursa ya kuwakutanisha na wasanii wawapendao.
“Kama
ilivyo kauli mbiu yetu kuwa “ukiwa na Vodacom maisha ni
murua”tunahakikisha mbali na kutoa huduma bora kwa wateja wetu pia
tunajua kuwa kuna muda wanahitaji kufurahi kwa burudani hivyo ndio maana
tunaandaa na kudhamini matamasha ya aina hii na tutaendelea kufanya
hivyo siku zote ikiwa ni moja ya njia ya kusema ahsante kwa wateja wetu
kwa kutuunga mkono”Alisema.
HITMA YA MAREHEMU MZEE KARUME YASOMWA LEO ZANZIBAR
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Vuai Ali Vuai maara
alipowasili katika viwanja vya Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja
kubhudhuria katika Hitma ya Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee
Abeid Amani Karume Iliyofanyika leo asubuhi.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein(katikati) akiwaongoza Viongozi mbali mbali pamoja na Wananchi
katika Kisomo cha hitma ya aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu
Mzee Abeid Amani Karume katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui
Mjini Unguja Iliyofanyika leo asubuhi.
Baadhi
ya Viongozo wakisoma hitma akiwemo aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar
Marehemu Mzee Abeid Amani Karume(kushoto) Balozi Ali Karume katika
ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja Iliyofanyika leo
asubuhi.
Waislamu
na wananchi mbali mbali wakiwa katika kisomo cha hitma ya aliyekuwa
Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume katika
ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja Iliyofanyika leo
asubuhi.
Akinamama
wa Mitaa mbali mbali ya Mji wa Unguja wakiwa katika kisomo cha Hitma ya
aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume
katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja Iliyofanyika
leo asubuhi.
Mke wa
Rais Zanzibar Mama Mwanamwema Shein(katikati) akiwa na Mama Shadya
Karume Mke wa Rais Mstaafu wa Zanzibar(wa tatu kulia) Mama Fatma Karume
(wa pili kulia) Mke wa Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mama Zakia
Bilali (kushoto) Bi Khadija Aboud (wa pili kushoto)Mjumbe wa Kamati Kuu
wa CCM,katika hitma ya kumuombea dua Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu
Mzee Abeid Amani Karume,iliyosomwa leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM
Kisiwandui Mjini Unguja.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein akiweka shada la mauwa katika kaburi la Marehemu Rais wa kwanza wa
Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume,baada ya kisomo cha hitma na dua
iliyoombwa na wananchi wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini
Zanzibar leo asubuhi.
Makamo
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilali
akiweka shada la mauwa katika kaburi la Marehemu Rais wa kwanza wa
Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume,baada ya kisomo cha hitma na dua
iliyoombwa na wananchi wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini
Zanzibar leo asubuhi.
Muasisi
wa Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Hamid Ameir akiweka shada la mauwa katika
kaburi la Marehemu Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani
Karume,baada ya kisomo cha hitma na dua iliyoombwa na wananchi wa
Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar leo asubuhi.
Balozi
Ali Karume (Mtototo) kwa niaba ya familia akiweka shada la mauwa katika
kaburi la Marehemu Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani
Karume,baada ya kisomo cha hitma na dua iliyoombwa na wananchi wa
Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar leo asubuhi.
Wake
wa Viongozi wakiitikia dua iliyoombwa katika kaburi la Marehemu
MzeeAbeid Amani Karume baada ya hitma iliyosomwa leo katika ukumbi wa
Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja na kuhudhuriwa na waislamu mbali
mbali Mjni na Vijijini.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein pamoja na Viongizi wengine wakiitikia Dua iliyoombwa na Mufti Mkuu
wa zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi (kulia) baada ya kisomo cha hitma
iliyosomwa leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja.
Baba
Askofu wa Anglikan wa Kanisa la Mkunazini Michael Hafidh akiomba dua
wakati Viongozi mbali mbali waliofika katika kaburi la aliyekua Rais wa
Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,baada ya kisomo cha
hitma iliyosomwa leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini
Unguja.(Picha na Ikulu, Zanzibar.)
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed
Shein leo ameongoza hitma ya kumuombea dua Rais wa Kwanza wa Zanzibar
Marehemu mzee Abeid Amani Karume, iliyofanyika Afisi Kuu ya CCM
Kisiwandui mjini Zanzibar.
Hitma
hiyo, ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohammed Kharib Bilal, Rais mstaafu
wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Awamu ya Sita, Mhe. Amani Abeid
Karume, Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad na
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd.
Viongozi
wengine walihudhuria katika hitma hiyo ni Mufti Mkuu wa Zanzibar
Sheikh Saleh Omar Kabhi, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji,
Sheikh wa Mkoa wa Dar-es- Salam Sheikh Mussa Salum na viongozi wengineo.
Wengine
ni viongozi wa serikali zote mbili na viongozi wastaafu, viongozi wa
vyama vya siasa, Masheikh kutoka Zanzibar na Tanzania Bara, Wabunge na
Wawakilishi, wananchi kutoka sehemu mbali mbali pamoja na Mabalozi
wadogo waliopo hapa Zanzibar.
Hitma
hiyo ya kumuombea dua Marehemu Mzee Abeid Amani Karume pia ni miongoni
mwa maadhimisho ya Siku ya Mashujaa ilitanguliwa na Qur-an tukufu,
iliyosomwa na Ustadh Sharif Muhidin na kuongozwa na Sheikh Jafar kutoka
Masjid Noor Mohammad,iliopo Kwa Mchina Mwanzo.
Mara
baada ya hitma hiyo, Sheikh Mkoa wa Dar-es-Salaam, Sheikh Mussa Salum
alitoa mawaidha na kumuelezea marehemu mzee Abeid Amani Karume kuwa ni
kiongozi aliyepigania maendeleo ya wananchi wa Zanzibar na kumuombea
MwenyeziMungu ampe makaazi mema Peponi.
Akieleza
kuhuhu umuhimu wa siku hii, Sheikh Mussa alisema kuwa siku ya leo ni
muhimu sana kwa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kwa lengo la kumuombea
dua Marehemu Karume pamoja na mashujaa wengine.
Aidha,
Sheikh Mussa alitumia fursa hiyo kukumbusha juu ya umauti na kusisitiza
kuwa ni jambo ambalo litafika kwa kila kiumbe alichokiumba
MwenyeziMungu na kusisitiza kuwa ni vizuri mwanaadamu akakumbuka asili
yake na hatma yake.
“Kifo
ni onyo, kifo ni mawaidha na kifo ni mazingatio...kutokana na hali hiyo
kuna kila sababu ya kutenda mema, kuwa na mahaba, kuwa na udugu wa
kiimani.. huku tukiendelea kumuombea dua mzee wetu huyu kwani yeye
ameonja umauti kama ilivyoeleza Qur-an ikiwa na maana kuwa roho yake
bado iko hai” alisema Sheikh Mussa.
Pamoja
na hayo, Sheikh Mussa katika kutilia mkazo suala zima la udugu wa
kiimani alitoa pongezi kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein kwa kuendelea kusimamia Serikali ya
Mapindui ya Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa ambayo imewafanya
Wazanzibari kuimarisha udugu wao na kuwa kitu kimoja kama Uislamu
unavyotaka.
Alisema
kuwa hatua hiyo imezidisha umoja sambamba na kuimarisha amani na
utulivu uliopo na kuifanya Zanzibar kuwa tulivu na kusisitiza kuwa huo
ndio udugu wa kiimani.
Baada
ya kisomo hicho cha hitma ambacho hufanyika kila mwaka inapofika tarehe
7, Aprili, viongozi hao na wananchi waliohudhuria katika hitma hiyo
walimuombea dua, marehemu mzee Abeid Karume katika kaburi lake lililopo
pembezoni mwa afisi hiyo ya CCM Kisiwandui dua iliyoongozwa na viongozi
wa dini tofauti akiwemo Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Kabhi, Askofu
Michael Hafidh kutoka Kanisa la Anglikana Zanzibar na Bhaguan Suria
(Mshamba) aliyesoma kwa niaba ya Wahindu.
Viongozi
na wanafamilia waliweka mashada ya maua katika kaburi la marehemu mzee
Abeid Amani Karume akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Mohammed Kharib Bilal, Mzee Hamid Ameir
aliyeweka shada la maua akiwakilisha wazee walioshiriki Mapinduzi ya
Januari 12, 1964.
Mwakilishi
wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Luteni Jeneral
S.A. Ndomba, Balozi Ali Karume aliyewakilisha familia ya Marehemu Sheikh
Abeid Amani Karume na Balozi mdogo wa China anayefanya kazi zake hapa
Zanzibar Mhe. Xie Yualing aliyewawakilisha Mabalozi wenzake wa hapa
nchini.
Aidha,
Mama Mwanamwema Shein aliungana na akina mama wengine katika hitma hiyo
katika Afisi hiyo ya CCM Kisiwandui, akiwemo mjane wa marehemu mzee
Abeid Karume, Mama Fatma Karume, Mama Asha Bilali,Mama Zakia Bilal, Mama
Asha Balozi na Mama Pili Balozi, Mama Shadya Karume na viongozi wengine
wanawake wa kitaifa wakiwemo Mawaziri, Wabunge, Wawakilishini na
wananchi kutoka sehemu mbali mbali ya Zanzibar na Tanzania Bara.
April
7, 1972 ndiyo siku aliyouawa Rais wa Kwanza wa Zanzibar marehemu Mzee
Abeid Amani Karume na wapinga maendeleo nchini ambapo hivi leo imetimia
miaka 43 tokea utokee msiba huo.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Subscribe to:
Posts (Atom)