DKT. SHEIN AFUNGUA MSIKITI WA MAKUNDUCHI,ZANZIBAR
Msikiti
mpya wa Kijiji cha Kiongoni Makunduchi wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini
Unguja ambao leo umefunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein akifungua pazia kama ishara ya ufunguzi wa Msikiti Mpya wa Kijiji
cha Kiongoni Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja (kulia) Mkuu wa
Mkoa Kusini Dk.Idriss Muslim Hijja.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein akikata utepe kuufungua Msikiti Mpya wa Kijiji cha Kiongoni
Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja na kuanza rasmi shuhuli za Ibada
(kulia) Mkuu wa Mkoa Kusini Dk.Idriss Muslim Hijja.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein (wa nne kushoto) pamoja na Mashekhe na Viongozi na Waislamu mbali
mbali wakiitikia dua iliyoombwa baada ya Swala ya Dhuhuri iliyoongozwa
na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji (kulia) baada ya ufunguzi
wa Msikiti Mpya katika Kijiji cha Kiongoni Wilaya ya Kusini Mkoa wa
Kusini Unguja.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein (wa kulia) pamoja na Mashekhe na Viongozi na Waislamu mbali mbali
wakiitikia dua iliyoombwa baada ya Swala ya Dhuhuri iliyoongozwa na
Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji (hayupo pichani) baada ya
ufunguzi wa Msikiti Mpya katika Kijiji cha Kiongoni Wilaya ya Kusini
Mkoa wa Kusini Unguja.
Mwalimu
Mkuu wa Chuo cha Kiislamu Zanzibar Dr.Sheikh Muhidin Siasa akitoa
mawaidha baada ya ufunguzi wa Msikiti mpya wa Kijiji cha Kiongoni
Makunduchi Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja na Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein.
Kadhi
Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji (kulia) alipokuwa akimkaribisha Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein azungumze na waislamu baada ya ufunguzi wa Msikiti Mpya katika
Kijiji cha Kiongoni Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja leo.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein (kushoto) akizungumza na Waislamu wa Kijiji cha Kiongoni
Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja baada ya kuufungua Msikiti mpya
kijijini hapo leo uliojengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na Mwakilishi
wa Jimbo la Makunduchi Mhe, Haroun Ali Suleiman.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein (kulia) akizungumza na Waislamu wa Kijiji cha Kiongoni Makunduchi
Wilaya ya Kusini Unguja baada ya kuufungua Msikiti mpya kijijini hapo
leo uliojengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na Mwakilishi wa Jimbo la
Makunduchi Mhe, Haroun Ali Suleiman.[Picha na Ikulu.]
WASANII WA BONGO FLAVA WAMKUMBUKA MEZ B KWENYE BONANZA LA PSPF
Msanii wa muziki wa kizazi kipya "Bongo Flava, Shilole na wacheza show
wake, wakisimama kwa dakika moja kumkumbuka msanii mwenzao wa Bongo
Flava, Mez B, mzaliwa wa Dodoma, wakati wa bonanza lililoandaliwa na
Mfuko wa Pensheni wa PSPF, kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma leo
Februari 20, 2015. Bonanza hilo lilipambwa na michezo mbalimbali kama
vile, soka, netibole, voliboli na muziki kutoka kwa wasanii mbalimbali
wakiongozwa na balozi wa PSPF, Mrisho Mpoto wa Mjomba band. Wasanii
wengine ni pamoja na Chege na Temba na Mr. Blue. Mez B, ni mzaliwa wa
mkoa wa Dodoma, ambaye alifariki leo saa tano kwenye hospitali ya mkoa
wa Dodoma, alikokuwa akipatiwa matibabu. Anatarajiwa kuzikwa Jumatatu
ijayo Februari 23.
Mrisho Mpoto, a.k.a Mjomba, ambaye pia ni balozi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, akiburudisha wanachuo na watu wengine waluohudhuria bonanza hilo
Mrisho Mpoto, a.k.a Mjomba, ambaye pia ni balozi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, akiburudisha wanachuo na watu wengine waluohudhuria bonanza hilo
Mkuu wa wilaya ya Dodoma, Betty Mkwasa, (wapili kulia) akiwa na
Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, wakwanza kulia, wakati akitoa
nasaha kwa timu mbili za soka kutoka vyuo vikuu mkoani Dodoma
Maafisa wa juu wa PSPF, wakipasha misuli. Hata hivyo hawakuingian uwanjani kusakata kabumbu kutokana na muda kuwa mchache
Mchezaji wa timu ya Nertiboli ya chuo cha fedha CBE mkoani Dodoma, akiruka juu kumzuia mchezaji mwenzake kutoka UDOM
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Betty Mkwasa, (kulia), akiteta jambo na Meneja Masoko na mawasiliano wa PSPF, Constatina Martin
Nahodha wa timu ya soka ya Chuo Kikuu cha Dodoma UDOM-DIPLOMA, Abdallah
Shaaban, (kushoto, akipokea kombe la ubingwa wa soka, kutoka kwa Mkuu wa
Wilaya ya Dodoma, Betty Mkwasa, baada ya kuibuka washindi kwa upande wa
soka kwenye tamasha hilo. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam
Mayingu
MAMA SALMA KIKWETE MGENI RASMI KWENYE SHEREHE YA MAULID YA KUZALIWA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) HUKO WETE-PEMBA
Mke wa
Rais Mama Salma Kikwete akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa Karume huko
Pemba na kupokewa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Ndugu Mwanajuma Majid
Abdalla tarehe 20.2.2015. Mama Salma alialikwa Pemba kama Mgeni Rasmi
kwenye sherehe ya Maulid ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W)
iliyoandaliwa na Al-Madrasat Jabal- Hiraa.
Mke wa
Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na viongozi mbalimbali waliofika
kumpokea wakati alipowasili kwenye Uwanja wa ndege wa Karume huko Pemba
kwa ziara ya kikazi ya siku moja kisiwani humo tarehe 20.2.2015.
Mke wa
Rais Mama Salma Kikwete akipokewa rasmi kwa kuvishwa shada na wasichana
wa Almadrsat Jabal-Hiraa mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya
Shule ya Utaani huko Wete Pemba ilikofanyika sherehe ya Maulid ya
kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) ambapo Mama Salma Kikwete alikuwa mgeni
rasmi tarehe 20.2.2015.
Mamia
ya wananchi waliohudhuria sherehe ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad
(S.A.W) kwenye Shule ya Utaani huko Wete Pemba wakisikiliza hotuba ya
Mgeni Rasmi Mama Salma Kikwete (hayupo pichani) aliyokuwa akitoa wa
viongozi na wananchi waliohudhuria sherehe hizo tarehe 20.2.2015.
Mke wa
Rais Mama Salma Kikwete akitoa nasaha zake kwenye Maulid ya Kuzaliwa
Mtume Muhammad (S.A.W) iliyofanyika kwenye Shule ya Utaani huko Wete
katika Mkoa wa Kaskazini Pemba huku mamia ya watu wakimsikiliza. Mama
Salma alikuwa Mgeni rasmi kwenye sherehe hiyo iliyofanyika tarehe
20.2.2015. PICHA NA JOHN LUKUWI
FAINALI DARAJA LA KWANZA KUCHEZWA CHAMAZI .
Fainali ya kumsaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL),
inatarajiwa kufanyika kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi kuanzia
majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Awali mchezo huo wa fainali ulikuwa umepangwa kufanyika kesho kwenye
dimba la Uwanja wa Taifa, lakini kutokana na sababu zilizopo nje ya uwezo wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TTF imepelekea mchezo huo kuhamishiwa
Chamazi.
Mchezo huo wa fainali utaanza saa 10 kamili jioni, na utaonyeshwa moja
kwa moja na kituo cha Azam TV ili kuwapa nafasi wapenzi na wadau wa soka waliopo
mbali na hasa mikoani kuweza kushuhudia mchezo huo.
Bingwa wa Fainali ya Ligi Daraja la Kwanza atazawadiwa Kombe pamoja na
medali, huku mshindi wa pili akipata kikombe na medali pia.
Viingilio vya mchezo huo ni tsh.5,000 kwa jukwaa kuu na tsh. 3,000 kwa majukwaa
ya mzunguko.
Wakati huo huo, Ligi Kuu ya Vodacom inaendelea leo (Jumamosi) katika viwanja vitatu tofauti, Mgambo Shooting
watakua wenyeji wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Ndanda FC ya Mtwara watawakaribisha Wagosi wa Kaya timu ya Coastal Union
kutoka jijini Tanga katika mchezo utakaochezwa kwenye dimba la Ngwanda Sijaona.
Huku wakata miwa wa Kagera Sugar wanaoutimia Uwanja wa Kambarage mjini
Shinyanga wakiwakaribisha Maafande wa Jeshi la Polisi kutoka mjini Morogoro
timu ya Polisi.
Ligi hiyo ya Vodacom itaendelea tena kesho jumapili katika viwanja vitatu
tofauti, Uwanja wa Chamazi wenyeji Azam
FC wataikaribisha timu ya maafande wa Jeshi la Magereza nchini Tanzania
Prisons, mchezo utakaonza majira ya saa 2 kamili usiku.
Mjini Shinyanga wenyeji timu ya Stand United wataikaribisha Simba SC kwenye
Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku wagonga nyundo wa jiji la Mbeya, timu
ya Mbeya City wakicheza na timu ya Young Africans kwenye Uwanja wa Sokoine
jijini Mbeya.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU
TANZANIA (TFF)
Best Regards,
Baraka Kizuguto
MEDIA & COMMUNICATION OFFICER
T: +255 22-2861815 I F: +255 22-2861815 I C: +255 713 455970
E: b.kizuguto@tff.or.tz, or bafmaks@gmail.com I W: www.tff.or.tz
A:I P.O.BOX 1574 Karume Memorial Stadium /Shaurimoyo/Uhuru Street I Dar es salaam I Tanzania
LOGA AULA AFC LEOPARDS YA KENYA
KOCHA wa
zamani wa Simba SC, Zdravko Logarusic ameteuliwa kuifundisha, AFC Leopards ya Kenya
na tayari ameshatua kuanza kibarua hicho.
Logarusic ambaye
ni raia wa Crotia ametua Kenya, juzi jioni saa 12:30 kwa madaha kwenye Uwanja wa
Kimataifa wa Jomo Kenyatta huku akiwa mawani mazito ya jua.
Akizungumza
na gazeti hili kwa njia ya mtandao wa kijamii wa facebook, Zdravko Logarusic
alisema amekwenda Kenya baada ya mapumziko baada ya Simba ya Dar es Salaam
kumtupia virago
“Nafurahi
kurejea Kenya kwani naamini kazi niliyoifanya nikiwa na Gor-Mahia wengi
walivutiwa nayo naamini hata Tanzania kipindi nilichokuwa na Simba mashabiki
walivutiwa na kiwango changu cha ufundishaji ila siasa za mpira ndo zinafanya
kocha waondoke kwenye vilabu na kujikuta wanakurudi tena”, alisema Loga
Logarusic
kocha mwenye kujiamini alipokelewa na Mwenyekiti wa klabu hiyo, Allan Kasavuli
na Katibu msaidizi, Asava Kadima na ameshajiunga na timu kambini Mumias,
magharibi mwa Kenya ambapo ilikuwa na kocha msaidizi, Yusuf Chippo
Logarusic anakuwa
na kibarua cha kwanza leo baada ya AFC Leopards itakapokuwa ikicheza dhidi ya Chemelil Sugar nyumbani kwao, ambapo pazia la Ligi Kuu ya
Kenya litakuwa likifunguliwa rasmi licha ya mgogoro unaoendelea na Shirikisho
la Soka Kenya, FKF, kuhusu idadi ya timu zitakazoshiriki ligi hiyo.
‘Loga’, ambaye amewahi kuzifundisha klabu za Ashanti Gold na King Faisal FC za Ghana pamoja Gor Mahia ambao wapinzani wa Leopards ya Kenya na Simba ya Dar es Salaam amefurahi kurejea Kenya ujio ambao mashabiki wameupokea kwa furaha
‘Loga’, ambaye amewahi kuzifundisha klabu za Ashanti Gold na King Faisal FC za Ghana pamoja Gor Mahia ambao wapinzani wa Leopards ya Kenya na Simba ya Dar es Salaam amefurahi kurejea Kenya ujio ambao mashabiki wameupokea kwa furaha
TASWIRA KUTOKA NYUMBANI KWA WAZAZI WA MAREHEMU MEZ B
Asubuhi ya February 20, 2015 Tanzania
zilianza kusambaa taarifa za msiba wa aliyewahi kuwa member wa kundi la
Chamber Squad Mez B, taarifa hizo zilithibitishwa kwenye vyombo vya
habari na dada wa marehemu Rachel.Msiba upo eneo la Kisa Dodoma,
endelea kuwa karibu ili kujua taratibu za msiba huu zikoje ikiwa ni
pamoja na siku ya Mazishi.
RAIS KIKWETE AKABIDHIWA RASMI UENYEKITI WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI
Tanzania inaunga mkono kwa dhati Ushirikiano wa Kikanda na
muumini mkubwa wa Umoja wa Africa na Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC).
muumini mkubwa wa Umoja wa Africa na Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC).
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema hayo jijini
Nairobi mara baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa EAC na Rais Uhuru
Kenyatta wa Kenya ambaye amekua mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa kipindi
cha mwaka mmoja uliopita
Nairobi mara baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa EAC na Rais Uhuru
Kenyatta wa Kenya ambaye amekua mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa kipindi
cha mwaka mmoja uliopita
“Tunaamini kwamba Jumuiya ya Afrika Mashariki
iliyogawanyika, haitaweza kuchukua nafasi yake kamili na heshima
katika familia ya Mataifa ya Afrika na dunia kwa ujumla” Rais amesema
na kuongeza kuwa Tanzania inakua kuwa masoko yaliyogawanyika,
miundombinu hafifu baina ya nchi, havina nafasi katika dunia ya leo
wala ya baadaye.
iliyogawanyika, haitaweza kuchukua nafasi yake kamili na heshima
katika familia ya Mataifa ya Afrika na dunia kwa ujumla” Rais amesema
na kuongeza kuwa Tanzania inakua kuwa masoko yaliyogawanyika,
miundombinu hafifu baina ya nchi, havina nafasi katika dunia ya leo
wala ya baadaye.
Rais
Kikwete amesema na kumpongeza Rais Kenyatta kwa kusimamia
utekelezwaji wa maazimio na miradi ya pamoja ya Jumuiya wakati wa
kipindi chake cha uenyekiti na kuahidi kuwa Tanzania haitawaangusha
wana Afrika Mashariki katika kutekeleza azma yao ya pamoja ya
kuendeleza Jumuiya ambayo inaundwa na nchi za Burundi, Kenya, Rwanda,
Tanzania na Uganda.
Kikwete amesema na kumpongeza Rais Kenyatta kwa kusimamia
utekelezwaji wa maazimio na miradi ya pamoja ya Jumuiya wakati wa
kipindi chake cha uenyekiti na kuahidi kuwa Tanzania haitawaangusha
wana Afrika Mashariki katika kutekeleza azma yao ya pamoja ya
kuendeleza Jumuiya ambayo inaundwa na nchi za Burundi, Kenya, Rwanda,
Tanzania na Uganda.
Rais
Kikwete amesema katika utekelezaji wa ajenda ya EAC, biashara
imeongezeka kwa kiasi kikubwa na kwamba nchi zote wanachama zinayaona
matunda hayo.
Katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2013 biashara katika nchi za EAC
imeongezeka kutoka dola za kimarekani 3, 722.9 hadi dola 5,805.6
ambapo kati ya mwaka 2012 hadi 2013 kumekua na ongezeko la asilimia
6.
Kikwete amesema katika utekelezaji wa ajenda ya EAC, biashara
imeongezeka kwa kiasi kikubwa na kwamba nchi zote wanachama zinayaona
matunda hayo.
Katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2013 biashara katika nchi za EAC
imeongezeka kutoka dola za kimarekani 3, 722.9 hadi dola 5,805.6
ambapo kati ya mwaka 2012 hadi 2013 kumekua na ongezeko la asilimia
6.
“Kama biashara isiyo rasmi ingerasimishwa, kwa hakika,
ongezeko hili la biashara lingekua juu zaidi ya hapa, hivyo imefikia
wakati muafaka kurasimisha biashara isiyo rasmi katika ushirikiano
wetu” Rais amesema na kuongeza kuwa ” kwa njia hii serikali
zitakusanya kodi na hivyo kuna umuhimu wa kuelekeza nguvu katika
kusaidia biashara ndogo ndogo na zile zisizo rasmi kwa kuziwekea
mazingira mazuri”.
ongezeko hili la biashara lingekua juu zaidi ya hapa, hivyo imefikia
wakati muafaka kurasimisha biashara isiyo rasmi katika ushirikiano
wetu” Rais amesema na kuongeza kuwa ” kwa njia hii serikali
zitakusanya kodi na hivyo kuna umuhimu wa kuelekeza nguvu katika
kusaidia biashara ndogo ndogo na zile zisizo rasmi kwa kuziwekea
mazingira mazuri”.
Rais
Kikwete amerejea nyumbani mara baada ya mkutano huo ambao umehudhuriwa
na Marais wa nchi zote tano za Jumuiya na Rais Salva Kiir wa Sudan
Kusini ambaye amehudhuria kama mualikwa maalum katika kipindi hiki
ambapo mazungumzo ya awali ya kuijadili nchi yake kama inaweza kupata
uanachama katika EAC yanaendelea.
Kikwete amerejea nyumbani mara baada ya mkutano huo ambao umehudhuriwa
na Marais wa nchi zote tano za Jumuiya na Rais Salva Kiir wa Sudan
Kusini ambaye amehudhuria kama mualikwa maalum katika kipindi hiki
ambapo mazungumzo ya awali ya kuijadili nchi yake kama inaweza kupata
uanachama katika EAC yanaendelea.
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete na mwenyeji wao Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya pamoja na
Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais
Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakizungumza chemba kabla ya kuingia
kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Kenyatta International
Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya katika mkutano wa kawaida
wa 16 wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari
20, 2015
Mrisho Kikwete na mwenyeji wao Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya pamoja na
Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais
Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakizungumza chemba kabla ya kuingia
kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Kenyatta International
Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya katika mkutano wa kawaida
wa 16 wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari
20, 2015
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete na mwenyeji wao Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya pamoja na
Rais Paul Kagame wa Rwanda kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa
Kenyatta International Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya
katika mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa nchi za Afrika
Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari 20,
2015
Mrisho Kikwete na mwenyeji wao Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya pamoja na
Rais Paul Kagame wa Rwanda kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa
Kenyatta International Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya
katika mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa nchi za Afrika
Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari 20,
2015
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete, Naibu Rais wa Kenya, Mhe. William Rutto na maafisa
wengine wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa
Kenyatta International Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya
wakati wimbo wa Taifa wa Tanzania katika mkutano wa kawaida wa 16 wa
Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari 20,
2015
Mrisho Kikwete, Naibu Rais wa Kenya, Mhe. William Rutto na maafisa
wengine wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa
Kenyatta International Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya
wakati wimbo wa Taifa wa Tanzania katika mkutano wa kawaida wa 16 wa
Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari 20,
2015
Kutoka kushoto ni
mgeni mwalikwa, Rais wa Sudani Kusini, Mhe Salva Kiir, Rais wa
Burundi, Mhe Pierre Nkurunziza, Rais Jakaya Mrisho
Kikwete(Tanzania),Rais Uhuru Kenyatta(Kenya)Rais Yoweri Museveni
(Uganda) Rais Paul Kagame (Rwanda) na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC) Balozi Dk Richard Sezibera wakiwa kwenye ukumbi wa
mikutano kwenye mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa nchi za
Afrika Mashariki
mgeni mwalikwa, Rais wa Sudani Kusini, Mhe Salva Kiir, Rais wa
Burundi, Mhe Pierre Nkurunziza, Rais Jakaya Mrisho
Kikwete(Tanzania),Rais Uhuru Kenyatta(Kenya)Rais Yoweri Museveni
(Uganda) Rais Paul Kagame (Rwanda) na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC) Balozi Dk Richard Sezibera wakiwa kwenye ukumbi wa
mikutano kwenye mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa nchi za
Afrika Mashariki
Rais Jakaya Mrisho
Kikwete(kushoto)akipokea bendera ya Afrika Mashariki(EAC)kutoka kwa
Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta ikiwa ni ishara ya kumkabidhi rasmi
Uenyekiti wa EAC kwenye mkutano wa kawaida wa 16 wa
Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika leo Ijumaa Februari 20,
2015 katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini
Nairobi. Picha na IKULU
Kikwete(kushoto)akipokea bendera ya Afrika Mashariki(EAC)kutoka kwa
Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta ikiwa ni ishara ya kumkabidhi rasmi
Uenyekiti wa EAC kwenye mkutano wa kawaida wa 16 wa
Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika leo Ijumaa Februari 20,
2015 katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini
Nairobi. Picha na IKULU
Subscribe to:
Posts (Atom)