Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

INNOIP YAFUNGUA FURSA MPYA KWA WABUNIFU

August 22, 2026 Add Comment

 



Na OSCAR ASSENGA, Tanga


SERIKALI imezindua programu ya InnoIP Tanzania, inayolenga kuwasaidia zaidi ya wabunifu 5,000 nchini kulinda kazi zao kisheria, kuzigeuza kuwa fursa za biashara na kuchochea uundaji wa ajira.


Programu hiyo pia inalenga kukabiliana na changamoto ya wizi wa mawazo na ubunifu inayowakabili wabunifu wengi, hasa wanaoweka wazi mawazo yao kabla ya kuchukua hatua za kuyakinga kisheria.


Uzinduzi huo umefanywa Agosti 22, 2026, na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian, katika maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea katika Viwanja vya Usagara, jijini Tanga.




Akizungumza na mamia ya wadau wa sekta ya sayansi na ubunifu, Dkt. Batilda alisema Tanzania inapaswa kuhakikisha ubunifu wa ndani unalindwa kisheria na kuunganishwa na masoko makubwa ili kuongeza thamani ya bidhaa na teknolojia zinazozalishwa na Watanzania.

Alisema baadhi ya wabunifu hupoteza fursa kwa kuweka wazi mawazo yao mapema bila kuwa na makubaliano yanayoeleweka kuhusu umiliki wa ubunifu huo.


Kwa mujibu wa Dkt. Batilda, hali hiyo inaweza kumsababishia mbunifu kukosa ulinzi wa kisheria wa kazi yake na kuwafanya wawekezaji kusita kuwekeza katika kampuni changa ambazo hazina uthibitisho wa umiliki wa haki zao za miliki bunifu.


FURSA WOMEN KULENGA WANAWAKE


Sambamba na uzinduzi wa InnoIP Tanzania, Mkuu wa Mkoa alitangaza kuanza kwa programu ya Fursa Women, inayolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali kutumia teknolojia na mifumo ya kidijitali kukuza biashara zao.


Dkt. Batilda alisema matumizi ya teknolojia yanaweza kupunguza gharama za uendeshaji wa biashara na kuwawezesha wafanyabiashara kuwafikia wateja wengi kwa haraka zaidi.

Aidha, alizitaka vyuo vikuu na taasisi za utafiti kuhakikisha tafiti zinazofanyika zinageuzwa kuwa bidhaa na suluhisho halisi zinazowanufaisha wananchi, badala ya kuishia kwenye makabrasha na makabati.



Pia aliwataka wawekezaji na taasisi za fedha kushirikiana na wabunifu wa Kitanzania kwa kununua bidhaa zao, kuwekeza katika teknolojia zao na kuwawezesha kupata mitaji kwa ajili ya kukuza biashara.


Akizungumzia ushiriki wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Mkurugenzi wa Miliki, Loy Mhando, aliyemwakilisha Afisa Mtendaji Mkuu, alisema InnoIP Tanzania haimaanishi kuwa kila ubunifu lazima upatiwe hataza (Patent).


Alisema programu hiyo itawasaidia wabunifu kutambua aina sahihi ya ulinzi wa kisheria kulingana na aina ya ubunifu wao, ikiwemo hataza, alama za biashara, hakimiliki na siri za biashara.


Alifafanua kuwa InnoIP inasimamiwa na BRELA na kuratibiwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), kupitia atamizi za Dar Teknohama Business Incubator (DTBi) na Buni Innovation Hub.


Programu hiyo inalenga kuwasaidia kampuni changa, watafiti, wanafunzi wa vyuo vikuu, biashara ndogo na za kati pamoja na wajasiriamali kutambua, kulinda na kubiasharisha haki zao za miliki bunifu.


Mhando alisema katika mwaka wa kwanza wa utekelezaji, programu hiyo inalenga kufanya uchambuzi wa kina wa mahitaji ya wabunifu 120 wa awali, ambao watasaidiwa kisheria na kifedha kulinda kazi zao na baadaye kuunganishwa na wawekezaji.



Alisema uteuzi wa wabunifu hao utazingatia vigezo mbalimbali, ikiwemo umuhimu wa ubunifu husika kwa jamii pamoja na uwezo wake wa kuzalisha faida.


Kwa mujibu wa Mhando, programu hiyo itawasaidia wabunifu kupitia hatua saba: utambuzi na uhamasishaji; mafunzo na warsha za vitendo; uchambuzi wa mahitaji; maandalizi ya ramani ya ulinzi; uwasilishaji wa maombi ya usajili; ubiasharishaji kwa kuwaunganisha na wawekezaji; pamoja na ufuatiliaji endelevu.


Aliwataka wabunifu na kampuni changa kutumia fursa hiyo mapema badala ya kusubiri hadi mgogoro wa umiliki unapotokea, mawazo yao yanaponakiliwa au mwekezaji anapohitaji uthibitisho wa kisheria kuhusu umiliki wa biashara.

 

Naye Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu, alisema miliki bunifu si suala la kisheria pekee, bali ni rasilimali muhimu ya kiuchumi inayoweza kuwa msingi wa kuvutia uwekezaji, utoaji wa leseni kwa viwanda vingine, uhamishaji wa teknolojia na ujenzi wa biashara zinazoweza kukua hadi masoko ya kimataifa.


“Changamoto yetu kuu kwa sasa nchini si ukosefu wa mawazo; ni kuhakikisha kuwa mawazo mazuri ya vijana, watafiti na wabunifu wetu yanalindwa kisheria, yanaendelezwa na hatimaye yanafikishwa sokoni,” alisema Dkt. Nungu.


Alisema mafanikio ya InnoIP hayatapimwa kwa idadi ya watu watakaohudhuria mafunzo na semina pekee, bali kwa matokeo, ikiwemo kuongezeka kwa idadi ya ubunifu unaolindwa kisheria, teknolojia mpya kuingia sokoni, biashara kukua, uwekezaji kuvutiwa na ajira mpya kuzalishwa.



Akizungumzia programu ya Fursa Women, Dkt. Nungu aliishukuru Airtel Tanzania kwa kushirikiana na COSTECH katika kufadhili programu hiyo.


Alisema ushirikiano huo unaonesha umuhimu wa sekta ya umma na binafsi kufanya kazi kwa pamoja katika kujenga jamii yenye ujuzi wa kidijitali.


Alifafanua kuwa kupitia Fursa Women, wanawake watajengewa uelewa kuhusu matumizi sahihi na salama ya mifumo ya kidijitali katika kutangaza bidhaa, kuwafikia wateja, kufanya na kupokea malipo mtandaoni pamoja na kuhifadhi kumbukumbu za biashara zao.


Dkt. Nungu alitoa wito kwa wawekezaji na sekta binafsi kutambua kuwa ubunifu wa Kitanzania ni fursa ya uwekezaji ambayo bado haijatumika kikamilifu.


Aliwaalika kushirikiana na Serikali katika kujaribu, kununua na kupanua matumizi ya teknolojia pamoja na suluhisho mbalimbali zinazozalishwa na Watanzania.


Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanatarajiwa kufungwa Jumatatu na Waziri Mkuu, Mhe. Mwigulu Nchemba.

BALOZI SALUM AZITAKA FCC, TBS NA WMA KUPAMBANA NA BIDHAA BANDIA NA DUNI

August 21, 2026 Add Comment
Mameneja wa Kanda na Mikoa wa Taasisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Tume ya Ushindani (FCC) pamoja na Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) wameagizwa kuhakikisha hakuna bidhaa bandia na duni katika maeneo yao wanayoyasimamia kiutendaji.

RC BURIAN ATOA MWELEKEO KWA WANANCHI 66 WA MSAKANGOTO

August 21, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga, MUHEZA

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, amewataka wananchi 66 wa Kitongoji cha Bago Maisha Plus ,Kijiji cha Msakangoto, Kata ya Kigombe wilayani Muheza, kuondoka katika eneo walilokuwa wakiishi na kuhamia eneo jipya lililotengwa na Serikali ya Kijiji, huku akiahidi kuwa Serikali itaendelea kuwasaidia katika kipindi cha mpito.

Wananchi hao wamekumbwa na changamoto hiyo baada ya nyumba zao kubomolewa kufuatia utekelezaji wa amri ya mahakama iliyotokana na mgogoro wa umiliki wa eneo hilo.

Balozi Burian alitoa kauli hiyo leo alipofanya ziara katika eneo hilo na kukutana na wananchi hao, ambapo alisema Serikali haina mamlaka ya kuzuia utekelezaji wa amri ya mahakama.

Alisema baada ya kubaini kuwa eneo hilo lilikuwa ndani ya hati ya umiliki ya mwekezaji wa Mashamba ya Mkonge ambaye tayari alikuwa amefungua kesi mahakamani na kupata amri ya kuwaondoa wananchi, Serikali ililazimika kuheshimu uamuzi huo.

“Serikali haiwezi kupingana na sheria ya mahakama. Aliyekuja kubomoa alikuwa anatekeleza maelekezo ya mahakama. Hata hivyo, sisi kama Serikali tuliona ni lazima tuzungumze na wananchi na mwekezaji ili kutafuta suluhisho la kibinadamu,” alisema.

Alisema awali wananchi hao walipelekwa katika eneo hilo na Serikali ya Kijiji, huku wakiwa na vielelezo vilivyoonyesha kuwa waliruhusiwa kuishi katika eneo hilo, jambo lililopelekea Serikali ya Mkoa kuingilia kati baada ya mgogoro kujitokeza.

Balozi Burian alisema Serikali ya Mkoa imefanya mazungumzo na mwekezaji kupitia Wizara inayohusika na Uwekezaji, hatua iliyosaidia kuwezesha kupatikana kwa eneo jingine kwa ajili ya kuwahamishia wananchi hao.

Alisema eneo lililotengwa awali kwa ajili ya makazi mapya lilibainika kuwa halifai kutokana na kuwa na maji, hivyo Serikali ililazimika kutafuta eneo jingine.

“Wawakilishi wenu wamekuja ofisini kwangu mara tatu. Hatua ya kwanza ilikuwa kwenda kuzungumza na mwekezaji, hatua ya pili mwekezaji akakubali kutoa Sh200,000 na hatua nyingine ni kuhakikisha hakuna mtu anayewasumbua wakati taratibu za kuwahamisha zikikamilishwa,” alisema.


Balozi Burian alisema maturubai  ambayo  wanayatumia kwa  muda wakati wakijiandaa kujenga makazi yao mapya.

“Kesho asubuhi tutahamisha maturubai hayo kwenda kwenye eneo ambalo mtaenda kuhamia. Mtayatumia kwa mwezi mmoja wakati mkiendelea kujipanga kujenga makazi yenu,” alisema.

Alisema Serikali itaendelea kutafuta wadau na wasamaria wema watakaoweza kusaidia katika ujenzi wa makazi mapya kwa wananchi hao.

Aidha, aliwataka wananchi hao kutokata tamaa na kuacha kuchukua hatua zinazoweza kuwaingiza katika mgogoro mwingine wa kisheria.

“Ndugu zangu, mchakato mzima nimewaeleza. Sina mamlaka ya juu zaidi ya hapa. Kila mhimili una kiwango chake cha kushughulikia jambo. Likishafika mahakamani, Serikali haiingilii tena,” alisema.

Alisema wananchi wanapaswa kuanza maisha katika eneo jipya huku wakiamini kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao katika kutafuta suluhisho la changamoto zinazowakabili.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao, Ally Mohamed, mkazi wa Maisha Plus, alisema suala la fidia limekuwa miongoni mwa changamoto kubwa zilizowafanya kuwa na wasiwasi kuhusu kuhamia eneo jipya.

Alisema baadhi yao walitumia mafao waliyopata kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kujenga nyumba zao, hivyo kubomolewa kwa nyumba hizo kumewasababishia hasara kubwa.

“Baadhi yetu tulitumia mafao yetu ya NSSF kujenga nyumba. Sasa nyumba zimebomolewa na tunajiuliza tutaanzaje maisha upya,” alisema.

Akijibu suala hilo, Balozi Burian alisema wananchi waliokuwa na madai ya fidia wakati shauri likiendelea walikuwa na nafasi ya kuyawasilisha mahakamani.

Hata hivyo, alisema Serikali ya Mkoa imeendelea kufanya mazungumzo na mwekezaji kwa lengo la kutafuta namna ya kuwasaidia wananchi hao katika kipindi hiki cha mpito.


Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Kigombe (CCM) Shahongwe Mgandi aliishukuru Serikali ya Mkoa kwa hatua iliyochukua, akisema viongozi wa kata watahakikisha wananchi hao wanapata usalama na huduma muhimu katika eneo jipya.

Alisema Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limeanza maandalizi ya kufikisha huduma ya umeme katika eneo hilo, ikiwa ni pamoja na kusimika nguzo.

Alisema pia maeneo ambayo wananchi hao watahamia yatatambuliwa kisheria na kutambuliwa kama kitongoji, huku Serikali ikiendelea kuboresha barabara na huduma nyingine muhimu.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Maisha Plus alishukuru Serikali ya Mkoa kwa hatua hiyo na kuiomba iruhusu wananchi hao, inapowezekana, kuhamisha baadhi ya miti waliyokwishaipanda katika eneo la awali ili kuitumia katika mazingira ya makazi mapya.

Hatua hiyo, alisema, itawasaidia wananchi hao kuanza maisha mapya huku wakitunza mazingira katika eneo watakalohamia.

TRA KARIAKOO NA MABALOZI JENGO WAIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA KUTOA ELIMU YA KODI KWA WALIPAKODI

August 21, 2026 Add Comment
Kariakoo, 20 Agosti, 2026

‎ Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeimarisha ushirikiano na uongozi wa Mabalozi Jengo kwa lengo la kuwafikia walipakodi na wadau mbalimbali kwa ufanisi zaidi.

AIRTEL AFRICA YAANDIKA HISTORIA KWA KUZINDUA INTANETI YA SATELAITI KWA SIMU DRC

August 21, 2026 Add Comment

Kinshasa, 17 Agosti 2026: Airtel Africa imeandika historia baada ya kuwa kampuni ya kwanza ya mawasiliano barani Afrika kuzindua kibiashara intaneti ya satelaiti kwa simu nchini Jamhuriya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ikifungua ukurasa mpya katika upatikanaji wa mawasilianokatika maeneo yasiyofikiwa na minara ya kawaida ya simu.

HII NDIO TOFAUTI KATI YA WAONGOZAJI WA NDEGE NA WAEGESHAJI WA NDEGE

August 21, 2026 Add Comment

 

Katika sekta ya usafiri wa anga, kuna wataalamu mbalimbali wanaoshiriki kuhakikisha ndege zinafanya safari kwa usalama na ufanisi. Miongoni mwa wataalamu ambao mara nyingi huchanganywa ni Waongozaji wa Ndege, wanaojulikana kama Air Traffic Controllers, na Waegeshaji wa Ndege, wanaojulikana kitaalamu kama Aircraft Marshallers.

Waegeshaji wa ndege ni wataalamu wanaofanya kazi katika maeneo ya maegesho ya ndege viwanjani. Mara nyingi huonekana wakiwa wamevaa mavazi maalum ya usalama na kutumia vijiti vya mwanga au ishara za mikono kumwelekeza rubani wakati ndege inapokaribia sehemu ya maegesho au inapojiandaa kuondoka.

Jukumu lao ni kuhakikisha ndege inaelekezwa kwa usahihi katika eneo lililotengwa bila kuhatarisha usalama wa ndege, vifaa vya uwanja, majengo au watu waliopo katika mazingira ya karibu. Ishara wanazotumia hutambulika kimataifa na humsaidia rubani kufanya maamuzi sahihi hasa katika maeneo ambayo mwonekano kutoka ndani ya ndege unaweza kuwa na mipaka.

Historia ya kazi ya uegeshaji wa ndege inaanzia katika miaka ya mwanzo ya maendeleo ya usafiri wa anga, ambapo mawasiliano kati ya marubani na wahudumu wa ardhini yalitegemea zaidi ishara za mikono. Pamoja na maendeleo ya teknolojia katika viwanja vya ndege, kazi ya Aircraft Marshaller bado inaendelea kuwa sehemu muhimu ya shughuli salama za ndege ardhini.

Kwa upande mwingine, Waongozaji wa Ndege, au Air Traffic Controllers, wana jukumu la kusimamia na kuratibu mwendo wa ndege angani na katika maeneo maalum ya viwanja vya ndege. Hutumia mifumo ya mawasiliano, ufuatiliaji na taratibu za uongozaji wa ndege kuhakikisha ndege zinatenganishwa kwa umbali salama na kupewa maelekezo wakati wa kuruka, kutua na kujiendesha katika maeneo wanayoyasimamia.

Tofauti kubwa kati ya wataalamu hawa ni kwamba Air Traffic Controllers huongoza na kuratibu mwendo wa ndege kupitia mawasiliano ya redio na mifumo ya uongozaji, wakati Aircraft Marshallers humwelekeza rubani kwa ishara za kuona katika eneo la maegesho ya ndege.

Pamoja na tofauti hiyo ya majukumu, wataalamu hawa wote ni sehemu muhimu ya mfumo wa usalama wa usafiri wa anga na huchangia kuhakikisha shughuli za ndege zinafanyika kwa mpangilio, usalama na ufanisi.

Nchini Tanzania, Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) ina jukumu la kusimamia na kudhibiti usalama wa usafiri wa anga kwa kuzingatia sheria, kanuni na viwango vinavyotambuliwa kitaifa na kimataifa, ikiwemo miongozo ya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga, ICAO.

 Chanzo- TCAA

MENEJA MKUU: HUDUMA BORA KWA MTEJA NDIO KIPAUMBELE CHA SHIRIKA

August 21, 2026 Add Comment

Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA. Ashraph Abdulkarim amewataka watumishi kuhakikisha kuwa wanakuwa suluhu ya changamoto za wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo kwa kusikiliza, kutoa majawabu ya uhakika kwa wakati na kutoa mrejesho kwa wafanyabiashara hao kwa wakati na kuzingatia mkataba wa huduma kwa mteja.
WRS KUONGEZA TIJA KWA WAKULIMA WA PARACHICHI, WRRB YATAKIWA KUHARAKISHA

WRS KUONGEZA TIJA KWA WAKULIMA WA PARACHICHI, WRRB YATAKIWA KUHARAKISHA

August 20, 2026 Add Comment

Na.Mwandishi Wetu- Dodoma

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake na kuitaka kuharakisha matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRS) katika zao la parachichi ili kuongeza tija kwa wakulima.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika, ametoa pongezi hizo leo Agosti 20, 2026 jijini Dodoma baada ya Kamati hiyo kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya WRRB kwa mwaka 2025/26.

Mhe. Mwanyika amesema Kamati imeridhishwa na utendaji kazi wa WRRB, hasa katika kushughulikia changamoto za wananchi, na kuitaka Bodi hiyo iongeze kasi katika utoaji elimu ili kuchochea matumizi ya mfumo huo katika maeneo mengine.

Akitoa ufafanuzi wa hoja za wajumbe, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, ameahidi kufanyia kazi maelekezo ya Kamati hiyo na kuihakikishia kuwa ataendelea kulinda majukumu ya taasisi zilizo chini yake kwa mujibu wa sheria.

Awali, akiwasilisha taarifa kwa Kamati hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema kwa mwaka 2025/26, WRRB imetoa leseni kwa waendesha ghala 235, kusajili ghala 951, wanunuzi 390, waweka mali 2,667 na kutoa stakabadhi za ghala 214,170.

KAMATI YA BUNGE YAIPONGEZA WIZARA YA VIWANDA NA TAASISI ZAKE KWA UFANISI

August 20, 2026 Add Comment
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, kupitia Mwenyekiti wake Mhe.Deodatus Mwanyika, ameipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na taasisi zake kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake ya udhibiti ubora kwa ufanisi .
TBS YAPONGEZWA KWA KUIMARISHA UDHIBITI  WA UBORA WA BIDHAA

TBS YAPONGEZWA KWA KUIMARISHA UDHIBITI WA UBORA WA BIDHAA

August 20, 2026 Add Comment

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo imeipongeza TBS kwa kutekeleza majukumu yake ya udhibiti ubora kwa ufanisi.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.Deogratias Mwanyika kwaniaba ya kamati wakati wa kikao cha Kamati cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu,katika, ofisi za Bunge Jijini Dodoma mapema leo.

Mhe.Mwanyika amesema juhudi zinazofanywa na TBS katika kuhakikisha usalama na ubora wa bidhaa zinazotumiwa na Watanzania zinaonekana hata hivyo ametoa rai kwa TBS kuendelea kutoa elimu na kuongeza jitihada sambambana na kuwa na programu maalum za kushughulikia bidhaa zinazoingizwa nchini kwa njia zisizo rasmi.

Naye Mhe. Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga(Mb) ameishukuru kamati hiyo na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo na ushauri uliotolewa na kamati hiyo ili kuendelea kurahisisha utendaji kazi wa TBS.

Vile vile Mhe.Kapinga amesema lengo la Wizara kupitia TBS ni kuhakikisha kunakuwa na bidhaa zenye ubora na usalama katika soko zinazozalishwa ndani na zinazotoka nje ya nchi.

KAMATI YA KUDUMU YA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR YAZURU NEMC

August 20, 2026 Add Comment
-Yafurahishwa na Mradi wa Kituo cha Gesi Asilia kwa matumizi ya Nishati Safi

MWENGE WA UHURU WAZINDUA TAWI LA CRDB TINDE

August 20, 2026 Add Comment

    

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wakifurahia wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga wakati wa uzinduzi rasmi wa tawi hilo.
Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga wakati wa uzinduzi rasmi wa tawi hilo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akitembelea Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga wakati wa uzinduzi rasmi wa tawi hilo.
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya CRDB, Xavery Makwi, akiimba shairi wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya CRDB, Xavery Makwi, akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Meneja wa CRDB Kanda ya Magharibi, Jumanne Wagana, akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Mbunge wa Jimbo la Itwangi, Azza Hillal Hamad, akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru wakati wa uzinduzi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Mwenge wa Uhuru ukiondoka katika Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga baada ya kukamilika kwa shughuli za uzinduzi wa tawi hilo.


Mwenge wa Uhuru ukiondoka katika Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga baada ya kukamilika kwa shughuli za uzinduzi wa tawi hilo.
Wafanyakazi wa Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga.

Na Elizabeth Cosmas na Kadama Malunde - Shinyanga

Mwenge wa Uhuru umezindua rasmi Tawi la Benki ya CRDB Tinde mkoani Shinyanga, huku Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akiipongeza benki hiyo kwa kuendelea kupanua wigo wa huduma za kifedha na kuzisogeza karibu na wananchi.