Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts
MBOLEA ZA RUZUKU ZAONGEZA UZALISHAJI, TFC YAJIPANGA ZAIDI

MBOLEA ZA RUZUKU ZAONGEZA UZALISHAJI, TFC YAJIPANGA ZAIDI

August 01, 2026 Add Comment

Na Alex Sonna– Dodoma

Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) imeanza utekelezaji wa mpango mkubwa wa kuongeza upatikanaji wa mbolea nchini kwa kuagiza tani 200,000 za mbolea kwa msimu wa kilimo wa mwaka huu, sambamba na uwekezaji katika viwanda vya kuchanganya mbolea na uchakataji wa chokaa ili kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao.

Mkurugenzi Mkuu wa TFC, Samuel Ahadi Mshote, amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha wakulima wanapata mbolea bora kwa wakati, kuongeza matumizi ya pembejeo na kuimarisha usalama wa chakula pamoja na uchumi wa kilimo nchini.

Akizungumza leo Agosti 1,2026 kwenye Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea kitaifa katika viwanja vya Dkt.John Samuel Malecela jijini Dodoma, Mshote amesema TFC ina jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa mbolea zenye ubora unaokidhi mahitaji ya wakulima, huku ikijiandaa kuanza uzalishaji wa mbolea zinazochanganywa kulingana na afya ya udongo na mahitaji ya mazao mbalimbali.

Amesema katika awamu ya kwanza kampuni imeagiza tani 70,000 za mbolea, ambapo tani 35,000 za mbolea aina ya DAP tayari zimewasili nchini na zinafungashwa katika Bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya kusambazwa kwa wakulima kupitia utaratibu wa pembejeo zenye ruzuku ya Serikali.

Aidha, amesema tani nyingine 40,000 za mbolea aina ya Urea zinatarajiwa kuwasili ndani ya muda mfupi ili kuendelea kukidhi mahitaji ya msimu wa kilimo unaoanza.

"Tunataka kuhakikisha hakuna mkulima anayekosa mbolea kwa sababu ya upungufu wa usambazaji. Ndiyo maana tumejipanga kuongeza uagizaji na kuimarisha mtandao wa usambazaji nchini kote," amesema  Mshote.

Amesema TFC imepanua mtandao wake wa huduma kwa kuongeza vituo vya mauzo kutoka nane hadi 26 vilivyopo katika mikoa 22 ya Tanzania Bara, hatua iliyorahisisha wakulima kupata mbolea karibu na maeneo yao.

Mbali na vituo hivyo, kampuni hiyo inashirikiana na zaidi ya mawakala 600 wa pembejeo za kilimo, vyama vya ushirika 29 (AMCOS) pamoja na halmashauri mbalimbali ili kuhakikisha mbolea zinawafikia wakulima hadi ngazi ya vijiji.

Kwa mujibu wa Mshote, tangu TFC ilipoanza kusambaza mbolea mwaka 2022, tayari zaidi ya tani 350,000 za mbolea za ruzuku zimesambazwa kwa wakulima wanaojihusisha na uzalishaji wa mpunga, mahindi, mboga mboga, vitunguu na mazao mengine ya biashara.

Katika hatua nyingine, amesema kampuni hiyo inakamilisha ufungaji wa mtambo wa kisasa wa kuchanganya mbolea katika jiji la Dar es Salaam, ambao utakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 300,000 za mbolea kwa mwaka kulingana na mahitaji ya udongo na mazao husika.

Amesema uwekezaji huo utapunguza utegemezi wa uagizaji wa mbolea kutoka nje ya nchi na kuongeza upatikanaji wa mbolea maalumu kwa mazao ya kimkakati kama vitunguu, ufuta, parachichi na mazao mengine yenye thamani kubwa kiuchumi.

Sambamba na hilo,amesema  TFC imeanza kutekeleza mradi wa uchimbaji na uchakataji wa chokaa mkoani Tanga baada ya kupatiwa eneo na Halmashauri ya Jiji la Tanga. Chokaa hicho kitatumika kurekebisha tindikali kwenye udongo pamoja na kuwa malighafi muhimu katika uzalishaji wa mbolea.

Mshote amesema mafanikio ya utekelezaji wa mpango wa ruzuku ya mbolea yameongeza matumizi ya pembejeo nchini kutoka tani 300,000 hadi zaidi ya tani milioni 1.2 kwa mwaka, huku takribani asilimia 80 ya wanufaika wakiwa ni wakulima wadogo.

Amesema ongezeko hilo limechangia kuimarika kwa uzalishaji wa mazao na kuiwezesha Tanzania kufikia kiwango cha zaidi ya asilimia 130 cha kujitosheleza kwa chakula.

Aidha, matumizi ya mbolea kwa hekta yameongezeka kutoka kilo 16 hadi kilo 24, huku Serikali na wadau wa sekta hiyo wakilenga kufikia kiwango cha kilo 30 kwa hekta kama kinavyoelekezwa na Azimio la Abuja kuhusu matumizi ya mbolea barani Afrika.

Amesema utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 unahitaji ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, sekta binafsi, taasisi za umma na wananchi ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa kwa wakati na kwa ufanisi.

Ameeleza kuwa dhamira ya Serikali ni kuona Tanzania inafikia uchumi shindani, wenye tija na jumuishi ifikapo mwaka 2050, huku akiahidi kuwa wataendelea kusimamia kwa dhati utekelezaji wa mipango na vipaumbele vilivyowekwa ili kuhakikisha maono hayo yanageuka kuwa matokeo yanayoonekana kwa manufaa ya Watanzania wote.

Mshote amewataka wakulima kutembelea banda la TFC katika Maonesho ya Nane Nane ili kupata elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea na kufahamu aina zinazofaa kwa mazao na mazingira yao, akisisitiza kuwa matumizi ya pembejeo bora ndiyo msingi wa kuongeza tija, kipato cha mkulima na ukuaji wa sekta ya kilimo nchini.

NGASONGWA: UCHAKATAJI WA MALIGHAFI NDANI UTAZALISHA AJIRA NA THAMANI ZAIDI

NGASONGWA: UCHAKATAJI WA MALIGHAFI NDANI UTAZALISHA AJIRA NA THAMANI ZAIDI

August 01, 2026 Add Comment

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC),Bi. Khadija Ngasongwa,akizungumza na wadau wakati wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026), inayoadhimishwa katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini. Mkutano huo unawakutanisha viongozi wa serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo kujadili mikakati ya kuharakisha maendeleo ya viwanda na biashara ya kikanda.

DURBAN - AFRIKA KUSINI

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amezishauri nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuwekeza zaidi katika maendeleo ya viwanda na miundombinu ili kuwawezesha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji.

Bi. Ngasongwa ametoa wito huo jijini Durban, Afrika Kusini, wakati akishiriki Mkutano wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC unaoendelea nchini humo.

"Ushiriki wa FCC katika wiki hii unalenga kuhakikisha sera na miongozo ya ushindani wa haki inazingatiwa katika maendeleo ya viwanda. Tunataka kuona viwanda vya ukanda wetu vinakuwa na ushindani, vinatoa fursa kwa wanawake na vijana, na vinatoa bidhaa zenye ubora kwa walaji," alisema Bi. Ngasongwa.

Ameongeza kuwa uwekezaji katika viwanda vya kuongeza thamani ya malighafi utasaidia kuwainua kiuchumi wanawake na vijana, kupanua masoko ya bidhaa za nchi za SADC na kuongeza mapato ya fedha za kigeni.

Akizungumzia ushiriki wa Tanzania, Bi. Ngasongwa amesema mkutano huo unaendana na vipaumbele vya maendeleo ya Tanzania hususan katika sekta za madini, kilimo, bidhaa za afya, miundombinu na ubunifu.

"Ushiriki wa Tanzania una umuhimu mkubwa kwa sababu unajikita katika kuimarisha mnyororo wa thamani. Ni maeneo muhimu katika safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa viwanda na kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050," alisema.

Bi. Ngasongwa pia amewataka wadau wa fedha waliopo katika mkutano huo ikiwemo TIB, Exim Bank, BADEA na Nedbank kushirikiana katika kuhamasisha upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya miradi ya maendeleo na uwekezaji nchini.

Amehitimisha kwa kusema kuwa Tanzania imebarikiwa kuwa na madini ya kimkakati na rasilimali nyingine. Hivyo ni muhimu kuyachakata ndani ya nchi badala ya kuuza malighafi ili kuongeza thamani, kuzalisha ajira na kuchochea ukuaji wa viwanda.

Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC ulifunguliwa rasmi Julai 27, 2026 na ulihitimishwa Julai 31, 2026 na umetoka na maazimio ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika biashara, uwekezaji na maendeleo ya viwanda kama sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa 46 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC utakaofanyika tarehe 17 Agosti, 2026 Jijini Durban, Afrika Kusini.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC),Bi. Khadija Ngasongwa, akizungumza na wadau wakati wa Wiki ya Tisa ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026), inayoadhimishwa katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini. Mkutano huo unawakutanisha viongozi wa serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo kujadili mikakati ya kuharakisha maendeleo ya viwanda na biashara ya kikanda.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki kutoka Tanzania wakati wa Mkutano wa 9 wa Wiki ya Viwanda wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Industrialisation Week), unaofanyika jijini Durban, Afrika Kusini.

 

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma, Bi. Roberta Feruzi akitoa maelezo kuhusu huduma zinazotolewa na FCC kwa baadhi ya wadau waliotembelea Banda la Tanzania, pembezoni mwa Mkutano wa Wiki ya Viwanda ya SADC (SADC Industrialisation Week 2026) unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (ICC), jijini Durban, Afrika Kusini.

WAKALA WA VIPIMO WAENDELEA KUTOA ELIMU YA MATUMIZI YA VIPIMO SAHIHI MKOANI NJOMBE

August 01, 2026 Add Comment

       


Njombe, Julai 31, 2026
 
Wakala wa Vipimo (WMA) wameendelea na kampeni ya utoaji elimu kuhusu matumizi ya vipimo sahihi kwa wafanyabiashara, wazalishaji na wadau mbalimbali wa biashara mkoani Njombe, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha biashara zinafanyika kwa uwazi, usawa na kwa kuzingatia sheria za vipimo.

AFISA MTENDAJI MKUU WA WMA AZUNGUMZA NA WATUMISHI ARUSHA, ASISITIZA UTOAJI HUDUMA BORA

August 01, 2026 Add Comment


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Mark Kihulla amewatembelea na kuzungumza na watumishi wa Wakala huo Mkoa wa Arusha tarehe 31 Julai 2026.

Lengo kuu la ziara hiyo lilikuwa kusikiliza changamoto za watumishi, kuwapongeza kwa utendaji wao, na kuwapa mwelekeo kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wakala.

Akizungumza na watumishi hao, Afisa Mtendaji Mkuu aliipongeza Ofisi ya Mkoa kwa kazi nzuri ya uhakiki wa vipimo wanayoendelea kufanya.

Alisema mafanikio ya WMA yanategemea uadilifu, umahiri na nidhamu ya kila mtumishi.

Aidha, aliwataka watumishi kuendelea kutoa huduma kwa ufanisi na kuzingatia maadili ya kazi. “Tuwe mabalozi wazuri wa WMA. Kila mteja tunayemhudumia ni fursa ya kujenga taswira nzuri ya Wakala,” alisisitiza.

Kwa upande wao, watumishi wa Mkoa wa Arusha walimshukuru Mtendaji Mkuu kwa uongozi wake wenye 'kuonesha njia' na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii.

Katika ziara hiyo ya Afisa Mtendaji Mkuu, watumishi walipata nafasi ya kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali ya kuboresha utoaji huduma ya vipimo katika Mkoa huo.


PSSSF YATOA ELIMU KWA MAKATIBU WA KAMATI ZA BUNGE

August 01, 2026 Add Comment

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi, akizungumza wakati wa semina maalum ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyofanyika mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.


*Mmoja atoa ushuhuda wa ‘Tunalipa Jana’


*Bunge: tunawashukuru PSSSF kwa elimu


Morogoro, Julai 31, 2026

Watumishi wa idara ya Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameridhishwa na huduma zinatolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa watumishi wa Umma (PSSSF) na wameshauri PSSSF izidishe ubunifu ili kurahisisha huduma kwa Wanachama wake.

Kauli hiyo imetolewa Julai 31, 2026 mjini Morogoro katika semina iliyoendeshwa na PSSSF maalum kwa Watumishi wa Bunge ambayo iliwashirikisha Makatibu wote wa kamati za Bunge. Semina ilikuwa ya kuwajengea uwelewa wa Kinga ya Jamii, hususani PSSSF.

“Hongereni sana matumizi ya mtandao hivi sasa mambo mmeyarahisisha sana, kwani kila kitu kinaanzwa na kumalizwa kwenye simu au kifaa kingine chochote cha kidijitali” alisema Bi. Angelina Sanga.

Mtumishi kutoka Ofisi ya Bunge, Bi. Angelina Sanga (kushoto), akiwa na Afisa Matekelezo kutoka PSSSF, Bi. Upendo Chilewa, wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bi. Sanga alipokuwa akijisajili kaaika huduma ya mifumo ya kidijitali.

Aidha, wajumbe wa semina hiyo walishauri sera ya Kinga ya Jamii ipitiwe ili iweze kwenda na wakati.

Katika semina hiyo Mtumishi Mstaafu wa Bunge Bw. Gerald Magili alithibitisha kuwa PSSSF ‘inalipa jana’ kwa kusema, “Nilitoa taarifa ya kuomba kibali cha kustaafu kwa mwajiri miezi sita kabla ya kusataafu, tarehe yangu ya kustaafu ilikuwa ni Juni 25, 2026, siku hiyo hiyo nilipokea mafao yangu ya kustaafu, hakika PSSSF mpo vizuri”.


Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto, akizungumza wakati wa semina hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge kwa ajili ya Makatibu wa Kamati za Bunge mjini Morogoro.

Akizungumza wakati wa kufunga semina hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSSSF, Bw. Hajji Moshi alishukuru ofisi ya Bunge kwa kutoa nafasi ya kufanyika semina hiyo na kusema kuwa Mfuko uko tayari wakati wowote kutoa elimu ya Kinga ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Bunge na Wanachama wengine

Mtumishi Mstaafu wa Bunge, Bw. Gerald Magili, akitoa ushuhuda wake wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bw. Magili aliipongeza PSSSF kwa kulipa mafao yake kwa wakati

“Kwa niaba ya Menejimenti ya PSSSF, tunashukuru kupokea maoni kutoka kwenu, yote tumeyachukua na tutayafanyia kazi na yale ya Kisera tutayafikisha kwa Mamlaka husika, asanteni sana” alisema Bw. Hajji Moshi.

Kwa upande wake, Bw. Michael Chikokoto, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamatii za Bunge, alisema, “Tunawashukuru PSSSF kwa kuitikia wito wetu, naamini tumejifunza mengi na tatakuwa mabalozi wenu kwa watumishi wengine wa Bunge.




Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi (kushoto), akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto (kulia), mara baada ya kuhitimishwa kwa semina ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro.

Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kwa umakini mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajj Moshi (kulia), wakati wa semina ya kujenga uelewa wa Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.

ALAMA YA UBORA YA AFRIKA YAZINDULIWA RASMI

July 31, 2026 Add Comment
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Denis Londo, amesema ubora wa bidhaa ni nguzo muhimu katika kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kwenye soko la kimataifa na kufanikisha azma ya nchi ya kujenga uchumi wenye thamani ya dola za Marekani trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO WAAHIDI KUSHIRIKIANA NA TRA KULIPA KODI KWA HIARI

July 31, 2026 Add Comment
Kariakoo, 31 Julai, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeendelea kuimarisha ushirikiano na walipakodi kupitia mikutano ya ana kwa ana (Outreach) inayolenga kusikiliza, kutatua changamoto na kutoa elimu ya kodi ili kuwawezesha walipakodi kutekeleza wajibu wao kwa hiari.

WAZIRI MKUU AZINDUA BOTI MBILI ZA DORIA NA UOKOZI

July 31, 2026 Add Comment


-Atoa siku 14 Kituo cha Kitaifa cha Oparesheni kianze kufanya kazi

RAIS DKT SAMIA SULUHU AWASILI JIJINI LUANDA NCHINI ANGOLA KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU MBILI

July 31, 2026 Add Comment
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana Waziri wa Mambo ya Nje wa Angola Mhe. Tete Antonio baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026 kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana Waziri wa Mambo ya Nje wa Angola Mhe. Tete Antonio baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026 kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.





USHIRIKIANO WA WAZAZI WAWASHA MOTO WA UFAULU NGUVUMALI

July 31, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Tanga


WAZAZI, walezi, walimu na viongozi wa Kata ya Nguvumali jijini Tanga wameanzisha mkakati wa pamoja wenye lengo la kutokomeza matokeo ya Daraja Sifuri katika mitihani ya taifa, wakiamini ushirikiano wa wadau wote wa elimu ndiyo ufunguo wa kuongeza ufaulu wa wanafunzi.


Azimio hilo lilifikiwa katika kikao cha wazazi na walezi kilichofanyika katika Shule ya Sekondari Nguvumali, ambapo wadau hao walikubaliana kuimarisha ushirikiano kati ya shule, familia na serikali za mitaa ili kuboresha matokeo ya wanafunzi wa Kidato cha Pili na Kidato cha Nne.

Akizungumza katika mkutano huo ambao uliitishwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo Ibrahim Okash, Diwani wa Kata ya Nguvumali, Mustapha Selebosi, alisema hatua hiyo inalenga kubadili taswira ya elimu katika kata hiyo kwa kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunza na kufanya vizuri katika mitihani ya taifa.


Alisema mafanikio ya wanafunzi hayawezi kupatikana bila ushiriki wa karibu wa wazazi, walezi, walimu na viongozi wa jamii.


"Siwezi kuitwa Meya wakati kata yangu inafanya vibaya katika mitihani ya taifa. Ni wajibu wetu sote kuhakikisha tunafuatilia maendeleo ya watoto wetu na kuweka mazingira yatakayowawezesha kufanya vizuri," alisema Selebosi.

Aliongeza kuwa kuboresha mfumo wa ufundishaji, kuongeza usimamizi wa wanafunzi na kuwajibisha kila mdau wa elimu ni miongoni mwa mikakati itakayosaidia kuinua kiwango cha ufaulu katika shule za kata hiyo.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Centre for Education (TCE), Yusuf Ogutu, alisema Kata ya Nguvumali ni miongoni mwa shule 10 zilizobainika kuwa na changamoto ya ufaulu, hali iliyosababisha kujumuishwa katika mpango maalumu wa mafunzo unaolenga kuongeza uwezo wa wanafunzi kujifunza kwa ufanisi na kujiandaa vizuri kwa mitihani.


Alisema mpango huo unatekelezwa na TCE kwa kushirikiana na Botnar Foundation na Inovex kupitia mradi wa Tanga Yetu, ukiwa na lengo la kuboresha ubora wa elimu katika shule za serikali.


Kwa mujibu wa Ogutu, changamoto kubwa kwa wanafunzi wengi si ukosefu wa ufundishaji, bali ni kutofahamu namna ya kujibu maswali ya umahiri, kuelewa uzito wa mada mbalimbali na kutumia mbinu sahihi za kufanya mitihani.


"Tumekuja na mafunzo haya ili kuwasaidia wanafunzi kujifunza kwa kuelewa badala ya kukariri. Tunawafundisha namna ya kuchambua muhtasari wa masomo, kutambua mada zenye uzito katika mitihani na kuelewa matumizi ya vitenzi vinavyotumika katika maswali," alisema.


Alieleza kuwa mafunzo hayo pia yanawajengea wanafunzi uwezo wa kupanga muda wa kujisomea, kujiandaa kabla ya mtihani, kufanya mitihani kwa ufanisi na kutathmini utendaji wao baada ya kumaliza mitihani.


Ogutu alisema taasisi hiyo pia imeanza kufanya utafiti katika shule zote 27 za sekondari za serikali zilizopo Jiji la Tanga ili kubaini sababu zinazosababisha kushuka kwa ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya Kidato cha Pili na Kidato cha Nne.


Alisema matokeo ya utafiti huo yatawezesha wadau wa elimu kuweka mikakati ya muda mrefu ya kuboresha ubora wa elimu na kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule hizo.


Naye Inspekta wa Polisi wa Kata ya Nguvumali, Sharifu Kiswamba, alisema pamoja na juhudi zinazoendelea kufanywa, utoro na tabia ya baadhi ya wanafunzi kuzurura mitaani wakati wa masomo bado ni changamoto kubwa inayochangia matokeo duni.


Aliwataka wazazi kuongeza usimamizi wa watoto wao na kushirikiana kwa karibu na walimu pamoja na viongozi wa kata ili kuhakikisha wanafunzi wanahudhuria masomo kikamilifu na kutumia muda wao kujifunza.


Hata hivyo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Nguvumali Ibrahim Okash alipongeza juhudi hizo akieleza kwamba vitasaidia kuwezesha kuongezeka kwa ufaulu kutokana na ushirikiano katika jambo lolote lile ni muhimu kwa ajili ya ustawi wake.


Alisema kwamba mkutano huo ni muhimu kwa sababu unawawezesha kukutana na wazazi na walezi ili kuweza kuweka nguvu za pamoja kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake ipasavyo ili kuweza kuchangia ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha nne na pili 


Mwisho

TRA KARIAKOO YAWAELIMISHA WAFANYABIASHARA KUHUSU MABADILIKO YA SHERIA ZA KODI 2026/2027

July 31, 2026 Add Comment
Kariakoo, Julai 30, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa kikodi Kariakoo imeendesha semina maalum kwa wafanyabiashara ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendelea kutoa elimu ya kodi na kuwajengea uelewa kuhusu mabadiliko ya sheria za kodi yaliyoanza kutumika kwa mwaka 2026/2027.

MD TWANGE AWATAKA WANASHERIA WA TANESCO KUENDELEA KUSIMAMIA MAADILI NA TAALUMA

July 31, 2026 Add Comment


📌 Afungua Jukwaa la Wanasheria wa TANESCO jijini Mwanza


📌 Awasisitiza kutoa ushauri wa kisheria kwa wakati na kulinda maslahi ya Shirika


Na Mwandishi Wetu, Mwanza

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, amewataka wanasheria wa shirika kuendelea kusimamia maadili ya taaluma, kutoa ushauri wa kisheria kwa wakati na kulinda maslahi ya shirika ili kuimarisha utendaji na kuhakikisha TANESCO inaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Bw. Twange ameyasema hayo wakati akifungua Jukwaa la Wanasheria wa TANESCO lililoanza Julai 28, 2026 jijini Mwanza, likiwakutanisha wanasheria kutoka Makao Makuu, Ofisi za Kanda na Kampuni Tanzu za TANESCO kwa lengo la kujengeana uwezo na kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya kisheria yanayohusu utendaji wa shirika.

Akizungumza katika ufunguzi wa jukwaa hilo, Bw. Twange amewapongeza wanasheria hao kwa mchango wao katika kulinda maslahi ya shirika na kuhakikisha shughuli zake zinafanyika kwa kuzingatia sheria na taratibu.

“Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya. Ushauri wa kisheria unaotolewa kwa wakati umekuwa ukisaidia TANESCO kufanya maamuzi sahihi na kuepusha migogoro ambayo ingeweza kuzuilika mapema,” amesema Bw. Twange.

Amewasisitiza kuendelea kuzingatia maadili ya taaluma, kutunza siri za kazi na kutoa ushauri wa kitaalamu unaolinda maslahi ya shirika.

“Kila mmoja wetu ana wajibu wa kulinda taasisi. Kwa upande wa wanasheria, hilo linaanza na kuzingatia maadili ya taaluma, kutunza siri za kazi na kuhakikisha kila ushauri unaotolewa unalinda maslahi ya TANESCO na kuimarisha utendaji wake,” amesema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa TANESCO, Wakili Sundi Mahalu, amesema idara hiyo itaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ili kuhakikisha shughuli za shirika zinaendelea kufanyika kwa kuzingatia misingi ya utawala bora na sheria.

“Jukwaa hili linatupa nafasi ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuimarisha uwezo wetu wa kitaaluma ili tuendelee kutoa huduma bora za kisheria zinazochangia mafanikio ya TANESCO,” amesema Wakili Mahalu.

Jukwaa la Wanasheria wa TANESCO linafanyika kwa siku tatu likiwa sehemu ya mkakati wa shirika wa kuendelea kuimarisha uwezo wa wataalamu wake wa sheria, hatua inayochangia ufanisi wa utendaji, usimamizi bora wa masuala ya kisheria na ulinzi wa maslahi ya shirika.


MOROCCO YAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI NA TANZANIA

July 31, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mahusiano ya kidiplomasia kati ya Ufalme wa Morocco na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yameendelea kuimarika kwa kasi tangu ziara ya kihistoria ya Kiserikali ya Mfalme Mtukufu Mohammed VI nchini Tanzania mwaka 2016, huku ushirikiano katika sekta mbalimbali ukizidi kupanuka na kuleta manufaa kwa mataifa yote mawili.

LRCT YAFANYA WARSHA YA NAFASI YA SHERIA YA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA UTEKELEZAJI WA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

July 31, 2026 Add Comment

 



Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Kurekebisha sheria Tanzania  Bw. Burhan Kishenyi, akizungumza Julai 30, 2026 wakati akifungua warsha ya uelimishaji kuhusu Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, Sura ya 183, inayolenga kuimarisha uelewa wa wadau katika kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa kwa ufanisi sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
...........................................
Na Mwandishi Wetu Dodoma


Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Kurekebisha sheria Tanzania  Bw. Burhan Kishenyi, leo tarehe 30.07.2026 amefungua warsha ya uelimishaji kuhusu Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, Sura ya 183, inayolenga kuimarisha uelewa wa wadau katika kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa kwa ufanisi sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Warsha hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, jijini Dodoma, na imewakutanisha washiriki kutoka taasisi mbalimbali za umma na wadau wanaoshughulika na masuala ya haki na ustawi wa watu wenye ulemavu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Bw. Kishenyi amesema kuwa utekelezaji wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ni msingi muhimu katika kujenga jamii jumuishi inayotoa fursa sawa kwa wananchi wote bila ubaguzi. 

Amesisitiza kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inaweka msisitizo katika ushirikishwaji wa makundi yote ya jamii, ikiwemo watu wenye ulemavu, ili kuchangia kikamilifu maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Aidha, amewataka washiriki kutumia warsha hiyo kujadili kwa kina wajibu wa kila taasisi katika kutekeleza matakwa ya sheria, kubadilishana uzoefu na kuibua mapendekezo yatakayosaidia kuondoa vikwazo vinavyokwamisha upatikanaji wa haki na huduma kwa watu wenye ulemavu.

Washiriki wa warsha hiyo wanatarajiwa kujengewa uwezo kuhusu tafsiri na utekelezaji wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, pamoja na namna ya kuoanisha utekelezaji wake na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambayo inalenga kujenga Tanzania jumuishi, yenye usawa, haki na maendeleo endelevu kwa wananchi wote.

Kwa upande wake , Bw. Harold Sungusia, Rais Mstaafu wa TLS ambaye pia ni wakili wa kujitegemea  alisisitiza umuhimu wa kuwashirikisha watu wenye ulemavu katika mchakato wa maboresho ya sheria ili kuhakikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatekelezwa kwa misingi ya usawa, haki na ushirikishwaji.

Akizungumza katika mkutano uliojadili mwelekeo wa maboresho ya sheria na maendeleo ya taifa, Bw. Sungusia alisema kuwa sheria bora zinapaswa kuzingatia mahitaji ya makundi yote ya jamii, ikiwemo watu wenye ulemavu, ili wasibaki nyuma katika safari ya maendeleo.

Alieleza kuwa ushiriki wa watu wenye ulemavu katika utoaji wa maoni na maamuzi kuhusu sheria ni muhimu kwa sababu unasaidia kutunga na kuboresha sheria zinazolinda haki zao na kuondoa vikwazo vinavyowazuia kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii, kiuchumi na kisiasa.

Aidha, alibainisha kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 unahitaji mfumo wa sheria unaohakikisha fursa sawa kwa wananchi wote bila ubaguzi wa aina yoyote.

Bw. Sungusia alisema kuwa kujenga taifa lenye maendeleo endelevu kunategemea uwepo wa sheria jumuishi zinazolinda haki za kila mwananchi na kuweka mazingira yanayowawezesha watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Washiriki wa mkutano huo walikubaliana kuwa ushirikishwaji wa makundi maalumu katika mchakato wa maboresho ya sheria ni nguzo muhimu ya kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kujenga jamii yenye usawa na haki kwa wote.
Wadau mbalimbali wakishiriki warsha hiyo.

Wadau wakichangia mada katika warsha hiyo.
Michango mbalimbali ikitolewa katika warsha hiyo.
Warsha hiyo ikiendelea
Michango ikiendelea kutolewa.
Taswira ya warsha hiyo.