Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

REA YAPELEKA NEEMA NANYAMBA

October 28, 2025 Add Comment
-Umeme waibua fursa za kiuchumi

BIL 860 ZINATUMIKA UJENZI MIRADI YA DHARURA NCHINI -ENG MOHAMED BESTA

October 28, 2025 Add Comment
Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan inaendelea na ujenzi wa mpango wa dharura uliaoanzishwa chini ya TANROADS kufuatia maafa ya mafuriko makubwa yaliyosababishwa na mvua za El Nino na Kimbunga Hidaya kuanzia mwezi Oktoba 2023 hadi Mei 2024.
 MAKUBALIANO YA  NM-AIST NA  ECSA  KUKUZA TEKNOLOJIA BUNIFU ZA KIAFYA

MAKUBALIANO YA NM-AIST NA ECSA KUKUZA TEKNOLOJIA BUNIFU ZA KIAFYA

October 28, 2025 Add Comment
   

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) Prof. Maulilio Kipanyula (kushoto) na Mkurugenzi wa Jumuiya ya Afya Afrika Mashariki, Kati na Kusini( ECSA) Dkt. Ntuli Kapologwe (kulia,) wakisaini hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika Afya leo Oktoba 28,2025.

.....

TAASISI  ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imesaini hati ya makubaliano na Jumuiya ya Afya ya Afrika Mashariki, Kati na Kusini (ECSA) yenye lengo la kushirikiana katika tafiti, ubunifu na uenezaji wa teknolojia bunifu katika sekta ya afya.

Akizungumza wakati wa hafla ya kusaini makubaliano hayo Oktoba 28,2025, Makamu Mkuu wa Taasisi, Prof. Maulilio Kipanyula, alisema NM-AIST imejikita katika kuzalisha teknolojia bunifu na kufanya tafiti zenye matokeo chanya katika jamii.

Makubaliano hayo yameainisha maeneo kumi ya ushirikiano, yakiwemo tafiti za pamoja, matumizi ya teknolojia za kidijitali katika mifumo ya afya, na kuimarisha ubunifu unaolenga kuzalisha majawabu ya changamoto za kiafya barani Afrika.

“Sisi kama taasisi ya sayansi, teknolojia na ubunifu, tumejidhatiti kuzalisha teknolojia na majawabu yatakayosaidia kuimarisha mifumo ya afya nchini na barani Afrika. ESCAC ipo katika nchi nyingi, hivyo kwa NM-AIST hii ni fursa ya kushirikiana, kujenga mifumo ya afya, na kupeleka majawabu ya kidijitali katika sekta ya afya,” alisema Prof. Kipanyula.

Kwa mujibu wa Prof. Kipanyula, NM-AIST ni taasisi yenye idadi kubwa ya hati miliki (patents) nchini zipatazo 33 ambapo baadhi zinahusiana moja kwa moja na masuala ya afya, ikiwemo teknolojia ya lishe kupitia uji chapchap, mfumo wa kutambua picha za X-ray kwa kutumia akili unde, gauni maalum la theatre, na dripu bunifu inayochanganya mchanganyiko wa dawa kwa wakati mmoja.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa ESCAC, Dkt. Ntuli Kapologwe, alisema makubaliano hayo ni ya kimkakati na yanatarajiwa kuleta matokeo chanya katika muda mfupi, ikiwemo kuanzishwa kwa kituo cha umahiri wa sayansi, teknolojia, ubunifu na utafiti.

“Tumeweka mkazo katika diplomasia ya sayansi na afya, ili nchi wanachama tisa zinufaike na ubunifu wa NM-AIST. Hali ya udumavu katika ukanda wetu ni asilimia 30 hadi 35, hivyo tunahitaji teknolojia za lishe kukabiliana na changamoto hiyo,” alisema Dkt. Ntuli.

Aliongeza kuwa ushirikiano huo utahusisha pia matumizi ya teknolojia za kidijitali na akili uunde katika utoaji wa huduma za afya, ustawi wa jamii na lishe, sambamba na kuimarisha dhana ya Afya Moja (One Health) kwa nchi zaidi ya 55 barani Afrika.

Kwa sasa, NM-AIST inahudumia wanafunzi kutoka nchi 17 za Afrika, huku ECSA ikijumuisha wanachama kutoka nchi 12, jambo linalotarajiwa kuongeza wigo wa ushirikiano na athari chanya kwa afya ya jamii katika bara zima.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) Prof. Maulilio Kipanyula (kushoto) na Mkurugenzi wa Jumuiya ya Afya Afrika Mashariki, Kati na Kusini( ECSA) Dkt. Ntuli Kapologwe (kulia,) wakisaini hati ya Makubaliano ya ushirikiano katika Afya leo Oktoba 28,2025.

Makamu Mkuu wa NM-AIST, Prof. Maulilio Kipanyula (kushoto), akimkabidhi zawadi Mkurugenzi wa Jumuiya ya Afya Afrika Mashariki, Kati na Kusini, Dkt. Ntuli Kapologwe (kulia), ikiwa ishara ya kumbukumbu mara baada ya hafla ya kusaini hati ya makubaliano, Oktoba 28, 2025, Arusha.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Maulilio Kipanyula (kushoto), na Mkurugenzi wa Jumuiya ya Afya Afrika Mashariki, Kati na Kusini, Dkt. Ntuli Kapologwe (kulia), wakionyesha hati ya makubaliano baada ya kuiweka saini, Oktoba 28, 2025, Arusha.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi naTeknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Maulilio Kipanyula (kushoto) akiongea wakati wa hafla ya kusaini hati ya makubaliano, Oktoba 28, 2025, Arusha.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya Afya Afrika Mashariki, Kati na Kusini, Dkt. Ntuli Kapologwe (kulia), akiongea wakati wa hafla ya kusaini hati ya makubaliano, Oktoba 28, 2025, Arusha, kushoto ni Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof. Maulilio Kipanyula.

Makamu Mkuu wa NM-AIST, Prof. Maulilio Kipanyula (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Jumuiya ya Afya Afrika Mashariki, Kati na Kusini, Dkt. Ntuli Kapologwe (kulia),pamoja na wajumbe wa Menejimenti ya NM-AIST na ECSA mara baada ya hafla ya kusaini hati ya makubaliano, Oktoba 28, 2025, Arusha.

Mradi wa WLER wabadilisha mitazamo ya kijamii Kitunda

October 28, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KITUO Cha Taarifa na Maarifa katika kata ya Kitunda kimefanikiwa kuibua ajenda za kijamii na kuhamasisha usalama wa watoto wa kike pamoja na ushiriki wa wanawake katika uongozi, kufuatia kufanya tathimini ya mradi wa Women’s Leadership and Economic Rights (WLER).

MIAKA 4 YA RAIS SAMIA, BIL 712 ZATEKELEZA MIRADI YA TANROADS MOROGORO-ENG MKUMBO

October 28, 2025 Add Comment
Mkoa wa Morogoro una mtandao wa Barabara wa kilometa 2,071.23, katika mtandao huo, Barabara kuu ni kilometa 849.43 na Barabara za mkoa ni kilometa 1,221.81.Aidha jumla ya Kilomita 510.37 za Barabara kuu ni za kiwango cha lami na kilomita 339.06 ni za changarawe, kwa Barabara za mkoa kilomita 190.32 ni za lami na kilomita 1,031.49 ni za changarawe.

Mkoa wa Morogoro umepokea kiasi cha shilingi bilioni 712 Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuhudumia miradi ya miundombinu ya Barabara Pamoja na madaraja katika mkoa wa Morogoro huku miradi 7 ya Dharula ya Ujenzi wa Madaraja (CERC) inayofadhiliwa na Benki ya Dunia yenye thamani ya Shilingi bilioni 37.840 ikiwa inaendelea kwa kasi kuboresha miundombinu ya barabara zilizoharibiwa na mvua za El-nino pamoja na Kimbunga hidaya

Hayo yamebainishwa na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Morogoro Mhandisi John Mkumbo ofisini kwake leo tarehe 25 Octoba 2025 wakati akizungumzia kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan tangu aingie madarakani ambaye ametoa shilingi bilioni 712 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya Barabara na madaraja.

Mhandisi Mkumbo ameitaja miradi hiyo kuwa ni Pamoja na Ujenzi Daraja la Chakwale katika Barabara ya Iyogwe – Chakwale - Ngiloli unaojengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 6.438, Ujenzi Daraja la Nguyami Barabara ya Iyogwe – Chakwale - Ngiloli kwa gharama ya shilingi Bilioni 7.166, Ujenzi Daraja la Kihonda katika Barabara kuu ya Morogoro – Dodoma kwa gharama ya shilingi bilioni 5.311, Ujenzi Daraja la Bwage katika barabara Mziha – Turiani na Daraja la Mjonga barabara ya Mvomero – Ndole Kibati kwa gharama ya shilingi bilioni 10.038, Ujenzi Daraja la Doma katika Barabara kuu ya Tanzam kwa gharama ya shilingi bilioni 4.146 na Ujenzi Daraja la Ngerengere katika Barabara kuu ya Morogoro – Dodoma kwa gharama ya shilingi Bilioni 4.737

Amesema kuwa serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi mikubwa ya Maendeleo ya kimkakati ya Ujenzi wa barabara na madaraja katika Mkoa wa Morogoro yenye thamani ya shilingi bilioni 670.820 ikiwemo Mradi wa ujenzi wa barabara ya Ubena Zomozi – Ngerengere (Kizuka Army Camp) yenye urefu wa kilomita 11.6 kwa gharama ya shilingi bilioni 20.540, na Mradi wa Ujenzi wa barabara ya Bigwa – Kisaki (sehemu ya Bigwa –Mvuha yenye urefu wa kilomita 78 kwa gharama ya shilingi bilioni 132.015

Mhandiisi Mkumbo ameitaja miradi mingine kuwa ni ujenzi wa barabara ya Ifakara – Kihansi – Mlimba – Taweta – Madeke, Sehemu ya Ifakara – Mbingu yenye urefu wa kilomita 62.5 kwa gharama ya shilingi bilioni 97.178, Mradi wa ujenzi wa barabara ya Ifakara – Kihansi, Sehemu ya Mbingu – Chita JKT kilomita 37.5 kwa gharama ya shilingi bilioni 70.824, Ujenzi wa barabara zinazo elekea katika stesheni za reli ya SGR: (Kihonda kilomita 10 na Rudewa – kilosa kilomita 3) kwa gharama ya shilingi bilioni 27.016 na ujenzi wa barabara kuu ya Ifakara - Lupiro - Malinyi - Londo - Lumecha/Songwe (Forest - Londo -Kitanda); Sehemu ya 1: Ifakara - Lupiro – Malinyi (kilomita 112) kwa gharama ya shilingi bilioni 323.246

Katika mkoa wa Morogoro serikali imekalisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo ya kimkakati ya ujenzi wa barabara na madaraja yenye thamani ya shilingi bilioni 205.873, miradi hiyo ni Ujenzi wa Barabara ya Mikumi - Kidatu – Ifakara (Sehemu ya Kidatu – Ifakara, (Kilomita 66.9) kwa kiwango cha Lami pamoja na daraja la Ruaha Mkuu (Mita 133) kwa gharama ya shilingi Bilioni 164.756 na Ujenzi wa Barabara ya Dumila – Kilosa – Mikumi (Kilomita 142) Kwa Kiwango cha Lami, Sehemu ya Rudewa – Kilosa, Kilomita 24 pamoja na ujenzi wa Madaraja matatu ya Kobe (Mita 16), Wailonga (Wailonga mita 20) na Mazinyungu (Mita 20) kwa gharama ya shilingi bilioni 41.116

Mhandisi Mkumbo amebainisha kuwa TANROADS mkoa wa Morogoro inaendelea na hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi Sita (6) ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara zenye thamani ya Shilingi bilioni 3.602 ikiwemo barabara ya Msamvu (Round About) – Morogoro mjini – Bigwa JCT, barabara ya Kizuka Army Camp – Ngerengere - Ngerengere SGR Station Pamoja na Daraja la Ngerengere, Barabara ya Ubenazomozi (Ngerengere SGR station Jct) – Mvuha – Kisaki - Mtemere JCt (159km) Access road kwenda Julius Nyerere Hydropower Project, barabara ya Gairo - Nongwe, kilomita 54, barabara ya Miyombo - Lumuma - Kidete, kilomita 72, Daraja Mkondoa katika barabara ya Dumila - Kilosa – Mikumi na Barabara ya kutoka ya kutoka Geti SUA – Kupitia Mzinga hadi Mzumbe yenye urefu wa kilomita 13 pamoja na madaraja ya Mzinga na Kauzeni.

Aidha Mhandisi Mkumbo ameleza kuwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 22.734 kwa ajili ya kazi za matengenezo ya barabara na madaraja ambapo kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 3.390 ni kwa ajili ya matengenezo ya kawaida ya barabara kuu za lami, bilioni 1.285 ni kwa ajili ya matengenezo ya kawaida ya barabara kuu za Changarawe, bilioni 7.100 ni kwa ajili ya Matengenezo ya Muda maalum Barabara Kuu za lami, bilioni 1.000 ni kwa ajili ya Matengenezo ya Muda maalum Barabara Kuu za Changarawe, milioni 645.373 ni kwa ajili Matengenezo ya kawaida Barabara za Mkoa za lami za Mkoa, bilioni 4.656 ni kwa ajili Matengenezo ya kawaida Barabara za Mkoa za Changarawe, bilioni 1.677 ni kwa ajili ya Matengenezo ya Muda maalum Barabara za Mkoa za Changarawe, milioni 6.000 ni kwa ajili ya Matengenezo ya maeneo korofi, bilioni 1.320 ni kwa ajili ya Matengenezo makubwa ya madaraja (Bridge Major Repair) na bilioni 1.654 ni kwa ajili ya Matengenezo ya kawaida ya Madaraja.

MCHENGERWA AFUNGA KAMPENI KWA KUTOA WITO KWA WANANCHI KUZINGATIA AMANI

October 28, 2025 Add Comment

Na Yohana Kidaga- Utete, Rufiji

Mgombea wa Ubunge jimbo la Rufiji, Mhe. Mohamed Mchengerwa amefunga kampeni yake huku akitoa wito wananchi kushiriki kwenye uchaguzi wa kesho kwa amani na kurejea majumbani huku akimwombea kura Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika mkutano wa kufunga kampeni jana kwa jimbo la Rufiji kukiombea kura Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika kesho Oktoba 29, 2025 kwa ngazi ya Urais, Ubunge na Udiwani katika eneo la Utete Mhe. Mchengerwa ambaye pia ni Waziri wa TAMISEMI ametoa wito kwa wananchi wote nchini kutumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura wakizingatia amani na utulivu katika kipindi cha uchaguzi.
Aidha, amefafanua kuwa wananchi wawaepuke baadhi ya watu wenye nia mbaya ya kuleta fujo kwa kuwa amani ikitoweka watakaopata shida ni watoto, wazee na akina mama ambao hawana hatia.

"Ndugu zangu naomba ieleweke kuwa watanzania hatuna Tanzania nyingine hivyo ni muhimu kuelewa kuwa nchi yetu imejengwa katika misingi ya amani aliyotuachia baba wa taifa Mwalimu Nyerere hivyo hatuna budi kuendelea kutunza amani yetu katika kipindi hiki cha uchaguzi". Amesisitiza Mhe Mchengerwa 
Aidha, ameeleza kuwa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeleta mapinduzi makubwa nchini ambapo Jimbo la Rufiji limekuwa ni miongoni mwa wanufaika wakubwa.

Ametaja baadhi ya maeneo ambayo Serikali imeboresha kwa jimbo la Rufiji ni kwenye kuleta huduma ya umeme kwenye vijiji vyote na ujenzi madaraja na barabara za kiwango cha lami, huduma ya maji safi na salama, ujenzi wa zahanati na vituo vya afya pia madarasa ya shule za msingi na Sekondari.
Amesema endapo wananchi watampa ridhaa tena ya kuliongoza jimbo hilo atahakikisha anaiomba Serikali kukamilisha kazi kubwa iliyofanyika hususan ya ujenzi wa barabara ya Utete- Nyamwage na ahadi zote zilizo ndani ya Ilani ya CCM.

Mkutano wa kufunga kampeni ulikuwa na vibe Babkubwa kutoka kwa wasanii mbalimbali wa muziki wakiongozwa na msanii anayetamba nchini Mboso, na msanii chipukizi Dogo Pattern aliyechana mistari na kuwaacha wapenzi wa Singeli kuserebuka vilivyo.
Mhe. Mchengerwa ni Mbunge wa tisa wa kuchaguliwa katika jimbo hilo la Rufiji toka lianzishwe na kuongozwa na wabunge kadhaa kuanzia Mhe. Bibi Titi Mohamed ambapo anaelezewa kuwa ni miongoni mwa wabunge walioliletea maendeleo makubwa Jimbo hilo ukilinganisha na wabunge waliotangulia.

Licha ya kuwa Mbunge wa tisa wa Jimbo hilo, Mhe. Mchengerwa ni miongoni mwa wanasiasa wachache nchini ambao wamehudumu kwenye mihimili yote katika nafasi za juu za uandamizi.


Akiwa kwenye mkutano wa kampeni zake alioufanya Ikwiriri, Mgombea wa Urais, mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alimwelezea Mhe Mchengerwa kuwa amefanya kazi nzuri katika Wizara zote nne alizomteua kuhudumu kwenye kipindi chake cha uongozi.

VIONGOZI WA DINI WAENDELEA KUHIMIZA AMANI UCHAGUZI MKUU

October 27, 2025 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha amani, umoja na uzalendo kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, wakisisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa ustawi wa taifa na ibada halisi kwa Mungu.

WACHAMBUZI WA SIASA NA DIPLOMASIA WATOA WITO KWA VIJANA NA WANANCHI KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMIU KWA UZALENDO NA BUSARA

October 27, 2025 Add Comment

 


Na Rahel Pallangyo


Wachambuzi wa masuala ya siasa, diplomasia, na maendeleo wametoa wito kwa vijana na wananchi kwa ujumla kutumia mitandao ya kijamii kwa busara na uzalendo, huku wakisisitiza umuhimu wa kufanya tathmini ya kina kuhusu ukweli wa taarifa wanazopokea na kusambaza, hususan katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi.


Wito huo umetolewa Oktoba 26, 2025, jijini Dar es Salaam, wakati wa mdahalo wa 'Wajibu wa Kidijitali kwa Amani ya Nchi Kabla, Wakati na Baada ya Uchaguzi” uliofanyika katika Ukumbi wa American Corner, Makumbusho ya Taifa 

Mchambuzi wa masuala ya diplomasia na siasa, Abdulkarim Atik, amewataka vijana nchini kufanya tathmini ya kina kuhusu ukweli wa taarifa wanazopokea na kusambaza kupitia majukwaa ya kidijitali. Amesema lengo ni kuepusha taharuki na migawanyiko katika jamii inayosababishwa na habari za uwongo na propaganda zenye lengo baya.

"Ikiwa vijana watatambua ukweli wa taarifa wanazopata, itawasaidia kufanya maamuzi sahihi na kuchangia katika kulinda amani ya nchi hususan kipindi cha uchaguzi," alisisitiza Atik.

Naye Mwandishi wa habari wa Crown Televisheni, Imani Luvanga, amesisitiza kuwa mitandao ya kidijitali ni nyenzo muhimu ya mawasiliano na taarifa, na kwamba siyo mibaya kama inavyodhaniwa. Alifafanua kuwa changamoto kubwa ipo kwa watumiaji, ambao mara nyingi hueneza taarifa zisizo sahihi na zenye kuchochea migogoro.

Luvanga alieleza kuwa matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii yanaweza kuleta mabadiliko chanya, yakiwemo maendeleo ya kiuchumi. Alisisitiza umuhimu wa watu kujitambua wanapotumia mitandao hiyo, kwa kuelewa sababu za kuitumia, aina ya taarifa wanazohitaji, na faida wanazotarajia kunufaika nazo.

Kwa upande wake, mdau wa siasa na maendeleo, Reeves Ngalemwa, alisisitiza umuhimu wa kuweka msingi imara wa uzalendo tangu utotoni.


"Ni muhimu kuweka mazingira ya kuwaandaa watoto kujifunza uzalendo tangu wakiwa shule za msingi ili wakue wakiwa na mapenzi ya kweli kwa nchi yao," alisema Ngalemwa.

Aliongeza kuwa lengo la kuanza kuwajenga watoto katika hatua za awali ni kuandaa kizazi chenye uelewa mpana wa masuala ya kitaifa, kinachotambua lipi ni sahihi na lipi si sahihi, hususan katika zama hizi za kidijitali. Ngalemwa alihitimisha kwa kusema kuwa msingi huu imara utasaidia kujenga Taifa lenye vijana wanaopenda na kulinda maslahi ya nchi yao.

Mchambuzi wa masuala ya vyombo vya habari na mpiga picha maarufu, Isa Michuzi, amesisitiza kwamba wananchi wanatakiwa kujua na kuyachunguza kwa kina mambo mengi yaliyomo katiukja mitandao kwani mengine ni propaganda za chuki.

"Watu wanastahili kuangalia kwa umakini sana. Propaganda inaweza kuwa nzuri au mbaya. Tumefika hapa si kwa bahati mbaya, ni matokeo ya kuruka hatua. Kila mtu awe mlinzi wa taifa," alieleza Michuzi.


Alionya kuwa kutokuwa na uangalifu katika kusambaza taarifa hufanya jamii iingie katika migogoro isiyo ya lazima.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TBN , Beda Msimbe alizungumzia haja ya vijana wa sasa kuwa na ndoto zilizojengwa imara katika muktadha wa kitaifa na uzalendo huku wakiangalia mambo katika upana wake na si kuchukua tukio moja tu.


Alisema vijana wanahitaji msingi  imara ili maamuzi yao yawe ya kusonga mbele badala ya kuumiza taifa. Lengo ni kuweka maslahi ya Taifa mbele katika matumizi yao ya mitandao ya kijamii na katika kufanya maamuzi ya kisiasa.


Mdahalo huo uliokuwa chini ya Mwenyekiti Jukwaa la Wachambuzi, Magid Mjengwa ulihudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wahariri wa mawasiliano ya kidijitali, wanabloga kutoka Taasisi ya Tanzania Bloggers Network (TBN), wanafunzi wa Chuo cha Diplomasia, wadau wa amani, na waandishi wa habari.

REA YAWASHA UMEME KWENYE SHULE YA MSINGI NA SEKONDARI MTWARA

October 27, 2025 Add Comment
Watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa nyakati tofauti wamewasha umeme katika Shule ya Msingi Julia Wilayani Newala na Shule ya Sekondari Mbawala ya Wilayani Mtwara Mkoani Mtwara kupitia Mradi wa Ujazilizi 2C unaotekelezwa katika Wilaya zote mkoani humo.
TANZANIA YAING’ARA KIKANDA MASHINDANO YA UANDISHI WA INSHA ZA EAC NA SADC

TANZANIA YAING’ARA KIKANDA MASHINDANO YA UANDISHI WA INSHA ZA EAC NA SADC

October 26, 2025 Add Comment
 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar,akikabidhi vyeti  mbalimbali kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetoa tuzo kwa wanafunzi ambao ni washindi wa uandishi wa insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 huku ikiwasisitiza  kutumia uwezo wao binafsi katika kuandika insha badala ya kutegemea matumizi ya teknolojia ya Akili Mnemba.

Akizungumza katika hafla ya utoaji tuzo hizo leo Oktoba 26,2025 jijini Dodoma Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt.Hussein Omar  amesema kuwa uandishi wa insha ni sehemu ya mafunzo na inawajengea wigo mpana wa kujifunza masuala muhimu yanayohusu jumuiya hizo.

“Nawaomba wanafunzi kujiepusha na matumizi ya Akili Mnemba katika kuandika insha zenu kwa sababu kwanza itakuwa sio uhalisia wa uandishi wenu, lakini pia ni aina ya udanganyifu ambao utawatoa kwenye kinyang’anyiro cha ushindani,” amesema Dkt.Omar

Aidha, amewataka wanafunzi kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kwa ufasaha katika kufanya tafiti ili kuongeza maarifa kuhusu shughuli, malengo na mipango ya jumuiya hizo mbili.

Aidha amesema kuwa  ushindi huo ni ishara ya ubora wa elimu nchini na juhudi za pamoja za walimu, wakuu wa shule, na wizara husika katika kuandaa wanafunzi wenye uwezo mkubwa wa kufikiri na kujenga hoja.

“Ninafarijika kuona wanafunzi wetu wanaongoza katika ngazi za kikanda, jambo linaloonyesha kuwa Tanzania inaendelea kufanya vizuri katika kukuza elimu bora na ubunifu kwa vijana wake,” amesema

Pia ametoa wito kwa wakuu wa shule na waratibu wa insha kuhakikisha wanafunzi wote wanashiriki kikamilifu katika mashindano hayo kwa kufuata miongozo iliyowekwa, huku akisisitiza umuhimu wa kuhamasisha wanafunzi wenye mahitaji maalumu kushiriki.

“Wakuu wa shule ni wasimamizi wakuu wa mashindano hayo, hivyo wanapaswa kuhakikisha wanafunzi wanashiriki kikamilifu na kufuata taratibu za uandishi ili kuepuka kuondolewa katika hatua za usahihishaji,” ameongeza Dkt.Omar

Kwa upande wake Kamishna wa Elimu, Dkt. Lyabwene  Mtahabwa,amesema mashindano hayo yamekuwa kichocheo kikubwa cha kukuza umahiri wa wanafunzi katika uandishi, utafiti, na ufahamu mpana wa masuala ya kijamii, kiuchumi na kisiasa katika jumuiya hizo mbili za kikanda.

“Mashindano hayo yamekuwa chachu kwa vijana kufanya utafiti, kujifunza na kuelewa vyema hatua za uimarishaji mahusiano baina ya nchi wanachama na umuhimu wa muunganiko huu wa kikanda,” amesema  Dkt. Mtahabwa.

Dkt. Mtahabwa amewapongeza washindi wote wa kitaifa na kikanda, akiwemo Hollo Alice Kadala kutoka Shule ya Sekondari Msalato, aliyeshika nafasi ya tatu kitaifa na ya tatu kikanda katika mashindano ya SADC mwaka 2023, pamoja na Blandina Kabalemesa wa Shule ya Sekondari Anwarite, aliyeshika nafasi ya kwanza kitaifa na ya nne kikanda katika mashindano ya EAC mwaka 2024.

“Hawa wanafunzi ni mfano bora wa kuigwa. Ushindi wao unaonyesha juhudi na ubora wa elimu yetu. Tunawapongeza walimu, wazazi na waratibu wote kwa malezi bora na mwongozo uliowezesha mafanikio haya,” amesema 

Awali, Mratibu wa Insha kutoka Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Bi.Matuha Masati,ameipongeza Sekretarieti ya  Afrika Mashariki na Jumuiya ya Nchi za SADC Kwa kuendesha Mashindano ya Uandishi wa Insha kwani yamekuwa chachu Kwa vijana kufanya utafiti,kujifunza na kufahamu vizuri mchakato na hatua mbalimbali za uimarishaji Kwa nchi wanachama.

Amesema kuwa mashindano hayo husimamiwa na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) kwa insha za nchi za Afrika Mashariki (EAC) na za SADC husimamiwa na Wizara ya Elimu kwa upande wa Tanzania bara na Zanzibar.

Amesema kuwa  jumla ya wanafunzi 1,096 walishiriki katika mashindano ya uandishi wa insha za EAC na SADC mwaka 2023, wakiwemo wanafunzi 557 wa EAC na 539 wa SADC, huku mwaka 2024 ukishirikisha wanafunzi 892, kati yao 243 wa SADC na 649 wa EAC.

“Kwa sasa, Wizara inatoa tuzo kwa washindi 10 bora wa kitaifa kwa kila shindano, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo walipewa tu washindi watatu wa juu. Hatua hii imeongeza hamasa kubwa kwa wanafunzi kushiriki,” amesema 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar,akizungumza wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar,akizungumza wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Kamishna wa Elimu, Dkt. Lyabwene M. Mtahabwa,akizungumza wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Mratibu wa Insha wa kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bi. Matuha Massati, akitoa maelezo wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Hollo Alice Kadala kutoka Shule ya Sekondari Msalato, aliyeshika nafasi ya tatu kitaifa na ya tatu kikanda katika mashindano ya SADC mwaka 2023,akizungumza  wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar, (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar, (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar, (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar, (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kutunuku zawadi kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar,akikabidhi vyeti  mbalimbali kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar,akikabidhi vyeti  mbalimbali kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Hussein Omar,akikabidhi vyeti  mbalimbali kwa washindi wa Kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha kwa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa mwaka 2023 na 2024 hafla iliyofanyika leo Oktoba 26,2025  jijini Dodoma.