Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

NYAYO ZA LAETOLI FURSA YA VIWANDA VYA VIATU DUNIANI KUTENGENEZA VIATU VYA KIHISTORIA

March 15, 2026 Add Comment







Kuna methali isemayo “Asiyejua maana haambiwi maana “ lakini Ngorongoro leo itakuambia maana ya Nyayo za Laetoli.

Nyayo hizi ni za kihistoria na ni sehemu pekee duniani ambayo mafundi Viatu ulimwenguni wanaweza kufika na kutengeneza Viatu vya kihistoria vinavyoweza kushinda nishani ya Nobel kutokana na Nyayo za Laetoli zilivyo.

Katika eneo la Laetoli ndani ya hifadhi ya Ngorongoro, tarehe 24, Julai mwaka 1978, Mtafiti maarufu wa masuala ya Akiolojia Dr. Mary Leakey na timu yake iliyomhusisha Dkt. Paul Abell waligundua nyayo za zamadamu katika eneo la Laetoli zilizohifadhika katika mwamba wa jivu la volcano inayoaminika kuwa ililipuka katika mojawapo wa milima ya Ngorongoro miaka milion 3.6 iliyopita.

Wataalamu hawa wanaamini kuwa nyayo hizo ziliachwa na jamii ya watu wa kale wanaofahamika kama Australopithecus Afarensis.

Nyayo za Zamadamu katika eneo la Laetoli ni ushahidi wa pekee na wa bayana duniani kote usiopingika kwamba zamadamu (Hominin) kwa mara ya kwanza walianza kusimama wima na kutembea kwa miguu miwili katika eneo la Laetoli Ngorongoro Tanzania miaka milioni 3.6 iliyopita.

Binadamu hawa waliotembea wima kwa miguu miwili wametokana na babu/bibi mmoja aliyeishi miaka takribani millioni 7 iliyopita.

Mwanadamu aliyepo Tandahimba, Gamboshi kule Bariadi, Tandale kwa mtogole, Mbagala Zakiem na yule aliyepo Jerusalemu, Macca, Dubai, New York, London, Johannesburg, Tehran, Gaza, Misri hadi Sudan na Mumbai wametokana na babu na bibi mmoja.

Katika kuthibitisha uhai, Nyayo za zamadamu ndizo za kustaajabisha katika eneo la Laetoli, zipo nyayo za wanyama wengine wa kale kama vile nyayo za tembo, twiga, faru na wanyama ndogo kama sungura, kanga na aina za wadudu.

Kwa nyayo za Laetoli zilivyo, mafundi Viatu na wamiliki wa viwanda vya Viatu duniani wanaweza kufika katika Eneo hilo ili kupata ujuzi zaidi wa namna ya kutengeneza Viatu vya kihistoria.

Karibu kwetu Ngorongoro ambapo kila ukilala kuna ndoto ya maajabu inakuita



Muonekano wa Nyayo za Laetoli zilizoachwa na jamii za watu wa kale wanaofahamika kama Australopithecus Afarensis

KAMATI YA BUNGE YA SHERIA YATEMBELEA KONGANI YA BUZWAGI NA KUPONGEZA BARRICK KWA KUFUNGA MGODI KITAALAMU

March 15, 2026 Add Comment

    

Wabunge kutoka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakitembelea maeneo mbalimbali walipofanya ziara ya kikazi ya kujionea maendeleo ya Kongani Maalum la Uwekezaji (BSEZ) ya Buzwagi ambayo ipo ndani ya mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo katika hatua za mwisho za ufungaji.
Wabunge kutoka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakitembelea maeneo mbalimbali walipofanya ziara ya kikazi ya kujionea maendeleo ya Kongani Maalum la Uwekezaji (BSEZ) ya Buzwagi ambayo ipo ndani ya mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo katika hatua za mwisho za ufungaji.

FCC YATOA ELIMU KWA WANANCHI WA CHALINZE

March 15, 2026 Add Comment
Maafisa wa kulinda walaji kutoka Tume ya Ushindani (FCC) wametoa elimu kwa wananchi wa Halmashauri ya Chalinze mkoani Pwani kuhusu haki na wajibu wa mlaji, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Kumlinda Mlaji duniani yanayotarajiwa kufanyika Machi 31, 2026.
Elimu hiyo imelenga kuwajengea wananchi uelewa kuhusu namna ya kutambua bidhaa na huduma zenye ubora, pamoja na hatua wanazopaswa kuchukua pale wanapokutana na udanganyifu au ukiukwaji wa haki zao kama walaji. Wananchi pia wamehimizwa kuhifadhi risiti za manunuzi na kutoa taarifa kwa mamlaka husika wanapobaini vitendo vya biashara visivyozingatia sheria.
Maafisa hao wameeleza kuwa lengo la utoaji wa elimu hiyo ni kuhakikisha walaji wanakuwa na uelewa wa kutosha ili kujilinda dhidi ya bidhaa bandia, bei zisizo halali na huduma zisizokidhi viwango. Aidha, wamesisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda maslahi yao kwa kufahamu haki na wajibu wao wanapofanya manunuzi au kutumia huduma mbalimbali.
Maadhimisho ya Siku ya Kumlinda Mlaji hufanyika kila mwaka duniani kote kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji na kuhamasisha biashara kufuata misingi ya haki, uwazi na uwajibikaji katika utoaji wa bidhaa na huduma. Serikali na taasisi mbalimbali nchini huendelea kutumia maadhimisho hayo kutoa elimu kwa jamii ili kujenga mazingira salama na yenye ushindani wa haki sokoni.
 
 
 

NAIBU WAZIRI ARDHI AITAKA NHC KUONA NAMNA YA KUANZISHA MIRADI MIKUBWA KILA WILAYA NCHINI

March 15, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga,TANGA


NAIBU Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi,Kaspar Mmuya amelitaka Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) waanze kufikiria namna ya kuanzisha miradi mikubwa ambayo inaweza kutoa huduma kwa wananchi kwenye kila mikoa na wilaya ili wajipambanue utofauti wao na mashirika mengine.

Mmuya aliyasema hayo wakati wa ziara yake ya kutembelea mradi wa Jengo la Kitega Uchumi unaosimamiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mkwakwani Plaza ambapo alisema kutokana na uwepo wa mahitaji yake kwa wananchi waliopo maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mradi huo ni moja ya miradi mingi NHC wanafanya nchini na unagharimu kiasi cha Sh.Bilioni 8.6 fedha ambazo zilizopitishwa na Bunge katika Bajeti ya Mwaka 2025/2026 ambapo ulianza mwaka jana mwezi wa sita na utakamilika kwa muda wa miezi 24 na wanategemeaJune mwakani utakamilika .

Mpaka sasa mradi huo umetekelezwa kwa asilimia 37 na fedha zilizotumika ni zaidi ya Bilioni 2 ambao utakuwa na ghorofa tatu za mwanzo za biashara za kawaida,ya pili na tatu ni kutakuwa na ofisi mbalimbali na ya nne mpaka nane hizo ni kwa ajili ya makazi watajenga nyumba 20 ambazo nyumba 10 zitakuwa na vyumba viwili pamoja na master, jiko na vitu vingine na vyumba 10 zitakuwa na vyumba vitatu.

“Kwa kweli nimetembelea mradi huu nimeridhika kwa maana nimeona thamani ya fedha iliyotumika mpaka asilimia ya utekelezaji kuna uwiano mkubwa nimeangalia ubora na umahiri wa mafundi waliokuwepo nimejiridhisha kuna unadhifu mkubwa kwenye kazi yao”Alisema Naibu Waziri huyo.

Alisema pia ujenzi wa Jengo hilo umezingatia mazingira rafiki kwa watu wote kwamba litakuwa na lifti mbili ambazo zitatoa huduma za kijamii katika ghorifa ya tatu na kuna lifti ambayo watakuwa wanatumia watu watakaokuwa wanakaa juu kwenye nyumba za makazi na nyumba hizo hazitakodishwa zitauzwa kwa mtu yoyote mwenye uwezo wa kununua na matangazo tiyari wamekwisha kuwekwa.

Alisema kuna umuhimu wa uwepo wa miradi kama hiyo katika wilaya mbalimbali ikiwezekana mradi unaofanana nao waweke kwenye majimbo yote 272 ili wakitembea wajumbe NHC wapo katika maeneo ambayo wapiga kura wa Rais,Wabunge na Madiwani wanapotokea lakini niwapongeze kwa mradi huu.

Hata hivyo alimshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu kwa kulifanya shirika hilo liwe imara kiuchumi lakini lijielewe sasa linabidi lisonge mbele katika kuwekeza zaidi katika ujenzi wa makazi.

Ambapo zaidi ya nyumba milioni 3 kila mwaka ni mapungufu ama mahitaji ambayo yanahitajika kwenye nchi na wanavyoelewa idadi ya watu inaongezeka kwa kiasi kikubwa na mahitaji ya nyumba yanaongezeka.

“Wito nyie wenyewe mmejionea mradi upo asilimia 37 na zaidi ya asilimia 70 ya Jengo hilo tayari watu wameanza kuchukua nafasi kununua hivyo kuna mahitaji makubwa ya nyumba hapa Tanga ushauri wangu anzeni kufikiri kuanza miradi mikubwa inayoweza kutoa huduma kwa wananchi ili kujipambanua na kujitofautisha na mashirika mengine “Alisema

Kwa upande wake Msimamizi mkuu wa Mradi huo kutoka NHC Ephahim Msigwa alisema mradi huo unatumia fedha za ndani na una ghorofa nane ambapo ghorofa tatu zitakuwa kwa ajili ya biashara na tano za makazi ya watu ambapo mpaka sasa wamekwisha kutumia Bilioni 2.1.

Mradi huo ni wa miaka miwili ambapo ulianza kutekelezwa mwezi juni mwaka 2025 na kwamba unatarajiwa kukamilika ukamilike mwezi juni 2027 ambapo mpaka sasa upo asilimia 37.9 huku wananchi zaidi ya 189 wa Mkoa wa Tanga wakinufaika na ajira kwenye mradi huo.

Mwisho

KAMATI YA BUNGE YAITAKA WMA KUHAKIKI MITA ZA UMEME KWA MUJIBU WA SHERIA

KAMATI YA BUNGE YAITAKA WMA KUHAKIKI MITA ZA UMEME KWA MUJIBU WA SHERIA

March 15, 2026 Add Comment

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeiagiza Wakala wa Vipimo (WMA) kuhakikisha mita za umeme zinahakikiwa kikamilifu kabla ya kufungwa kwa ajili ya matumizi, kwa kuzingatia sheria zilizopo ili kulinda haki za watumiaji.

Aidha, Kamati hiyo imeipongeza WMA kwa jitihada za uhakiki na ukaguzi wa vipimo mbalimbali, ikiwemo mita za maji, huku ikiitaka Wakala hiyo kuendelea kusimamia kwa ukaribu vipimo katika sekta ya ujenzi ili kupunguza malalamiko ya wananchi yanayotokana na bidhaa hizo.

Hayo yameelezwa leo Machi 14, 2026, na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika, wakati wa ziara ya kikazi katika Kituo cha WMA cha Uhakiki wa Vipimo Misugusugu mkoani Pwani kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo na kujionea shughuli za uhakiki wa vipimo zinavyotekelezwa kituoni hapo.

Akizungumza katika ziara hiyo, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, aliihakikishia Kamati kuwa wizara itatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa.

Alisisitiza kuwa azma ya Serikali ni kuhakikisha WMA inasimamia matumizi ya vipimo sahihi katika uzalishaji na uuzaji wa bidhaa mbalimbali, pamoja na Uhakiki wa mita za umeme na maji, ili kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon, akitoa salamu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, alibainisha kuwa uhakiki wa vipimo ni uti wa mgongo wa uchumi wa mkoa huo. Alieleza kuwa kwa sasa Mkoa wa Pwani una jumla ya viwanda 1,688, vikiwemo viwanda vikubwa 199 na vidogo sana 1,017, hivyo uhakiki wa usahihi wa Vipimo ni nyenzo muhimu katika kuvutia uwekezaji zaidi.

Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa WMA, Bw. Alban Kihulla, alisema kuwa ukaguzi na uhakiki wa vipimo una nafasi kubwa katika kuhakikisha haki na usawa baina ya pande mbili zinazofanya biashara.

Pia, aliwahimiza wananchi kuhakikisha wanatumia vipimo vilivyohakikiwa, huku akiwasihi watoa huduma kuzingatia uadilifu kwa kutoa huduma kupitia vipimo sahihi ili kuleta usawa na kuhakikisha bidhaa zinazonunuliwa zinaendana na thamani halisi ya fedha.

MTENDAJI MKUU ADEM AFUNGUA KIKAO KAZI CHA CHAMA CHA KUTETEA HAKI ZA WALIMU

March 14, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, amefungua kikao kazi cha Chama cha Kulinda na Kutetea Haki za Walimu (CHAKUHAWATA) kinachofanyika jijini Dodoma, akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya wadau mbalimbali wa sekta ya elimu ili kuimarisha uongozi, utawala bora na udhibiti wa ubora wa elimu nchini.

KAMATI YA BUNGE YAKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA KAMPASI YA CHUO KIKUU MZUMBE TANGA

March 14, 2026 Add Comment
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe. Husna Juma Sekiboko (Mb) akiongoza Wajumbe wa Kamati hiyo kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya Tanga, unaotekelezwa kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET).

VIJIJI VINNE MBULU VYAANZA KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI WA BILIONI 41

March 13, 2026 Add Comment

Wananchi na wakazi wa Hydom wilayani Mbulu mkoa wa Manyara wamemshukuru Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kufuatia Wizara ya Maji kupitia RUWASA kutekeleza mradi mkubwa wa Majisafi ya bomba wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 41 na tayari vijiji vinne vimeshaanza kunufaika na mradi huo.

Wametoa pongezi hizo wakati wa ziara ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira alipotembelea na kukagua mradi huo ikiongozwa na Mwemyekiti wake Mhe. Jackson Kiswaga (Mb) katika eneo la Hydom lilipo tangi kubwa la ujazo wa lita 2,000,000 la mradi huo.

Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA Mha. Wolta Kirita aliieleza Kamati hiyo kuwa tayari wananchi zaidi 800 wameshasajiliwa na kupatiwa kadi za malipo kabla ya matumizi kwani mradi huo unaenda sambamba na ufungaji wa dira za maji za malipo ya kabla, ambapo mwananchi anaweza kuchota maji kwenye kituo muda wowote anapokuwa anahitaji huduma hiyo.

Mkurugenzi Mkuu Kirita alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika Novemba 2027.

Kwa mujibu wa Meneja wa RUWASA mkoa wa Manyara Mha. James Kionaumela alisema mradi huo umeshaanza kutoa huduma katika vijiji vinne na ukikamilika utahudumia zaidi ya wakazi 100,000 wa eneo hilo.

Naye Mkuu wa wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semindu akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga alisema kwa sasa wananchi wa wilaya hiyo wanapata maji kwa saa 12 kwa siku huku akiipongeza RUWASA kwa kazi nzuri katika kutekeleza mradi huo.








KAIMU KAMISHNA WA UHIFADHI TAWA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAANDALIZI YA BAJETI YA TAWA

KAIMU KAMISHNA WA UHIFADHI TAWA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAANDALIZI YA BAJETI YA TAWA

March 13, 2026 Add Comment

Na. Joyce Ndunguru, Dodoma.

Kaimu Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Mlage Yussuf Kabange amefungua rasmi kikao kazi cha maandalizi ya bajeti ya TAWA kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kilichofanyika Machi 13,2026, Jijini Dodoma, Kamishna Kabange amesema Bajeti ya mwaka 2026/27 ni ya kipekee kwa kuzingatia kuwa ni bajeti ya kwanza katika kuchangia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2025 pamoja na Dira ya maendeleo ya Taifa 2050.

“Pia bajeti hii imezingatia kutafsiri Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan wakati wa kuzindua Bunge la 13, Mkakati wa kuongeza mapato wa TAWA na ni bajeti ya kwanza tangu Bodi ya Nne ya Wakurugenzi ya TAWA iteuliwe”, amesema Kamishna Kabange.

Kamishna Kabange ameongeza kuwa katika bajeti hii TAWA itajielekeza katika vipaumbele mbalimbali ikiwemo kuimarisha ulinzi na usimamizi wa Rasilimali wanyamapori na malikale.

Pia, Kuimarisha shughuli za utalii pamoja na kuongeza idadi ya watalii kwa kuboresha miundombinu ya utalii pamoja na kuongeza vyanzo vipya vya mapato.

Kadhalika, Utatuzi wa migogoro ya mipaka na udhibiti wa wanyamapori wakali na waharibifu pamoja na Kuimarisha mazingira ya utendaji kazi kwa watumishi na uwezo wa Mamlaka katika kutoa huduma.

Vilevile , Kamishna Kabange amewapongeza Makamanda na Askari ambao wamekuwa mstari wa mbele kusimamia utekelezaji wa malengo ya Mamlaka. Aidha, amewaelekeza Makamanda wa vituo kuhakikisha Usimamizi madhubuti wa vitendea kazi yakiwemo magari.

Aidha, Kamishna Kabange amewaelekeza Makamanda kuendelea na utangazaji wa vivutio vya utalii pamoja na kubuni mazao mapya ya utalii.

“Nitoe rai kwenu kuendelea kuwa wabunifu na kutangaza maeneo mnayoyasimamia,” amesema Kamishna Kabange 

Sambamba na hilo, Kamishna Kabange amewaelekeza Makamanda kuendelea kusimamia askari kutekeleza majukumu yao kwa weledi na kwa kuzingatia haki, sheria na miongozo iliyowekwa.

Kikao kazi cha maandalizi ya bajeti kimehudhuriwa na viongozi wa TAWA kwa ngazi ya Makao Makuu, Kanda na Vituo.

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA MABORESHO YA BANDARI YA TANGA

March 13, 2026 Add Comment





Na Oscar Assenga,TANGA

Kamati ya kudumu ya Bunge ya miundombinu leo imefanya ziara ya kutembelea Bandari ya Tanga huku ikiridhinshwa na uboreshaji wa miundombinu katika Bandari ya Tanga hatua inayoonesha mabadiliko ya kiutendaji ikiwemo ongezeko la shehena za mizigo.

Hayo yalisemwa leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Profesa Joyce Ndalichako wakati wa ziara hiyo katika Bandari ya Tanga ambapo alisema maono ya Serikali yameleta mapinduzi katika Bandari ya Tanga na wao kama wasimamizi wataendelea kuisimamia Serikali katika utekelezaji wa mradi huo



Uboresho huo wa Bandari ya Tanga umepelekea kuvuka lengo la upokeaji wa shehena za mizigo kutoka mataifa mbalimbali kutoka tani 137,000 mwezi Oktoba hadi kufikia tani zaidi ya 200,000 mwezi Novemba mwaka 2025.



Alisema kutokana na maboresho hayo wana kila sababu ya kuipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uboreshaji wa Bandari ya Tanga hatua inayochagiza kuinua uchumi wa mkoa wa Tanga kwa kiasi kikubwa.




Profesa Ndalichako alisema kwamba uwekezaji huo wa shilingi bilioni 429.1 uliofanywa na Serikali katika Bandari ya Tanga umewezesha uchimbwaji wa kina na ujenzi wa gati hatua iliyoiongezea ufanisi wa utendaji na hivyo kuwezesha meli kubwa kutia nanga na kurahisisha shughuli za upakiaji na upakuaji wa mizigo.

Aliongeza Serikali ina maono ya kuunganisha Bandari na reli ambapo mpango uliopo ni kujenga reli ya kisasa ya SGR kutoka Tanga hadi Musoma hatua itakayochochea maendeleo ya mkoa wa Tanga na kuzalisha ajira kwa vijana.



Kamati ya kudumu ya Bunge ya miundombinu imeipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uboreshaji wa Bandari ya Tanga hatua inayochagiza kuinua uchumi wa mkoa wa Tanga kwa kiasi kikubwa.

Uwekezaji wa shilingi bilioni 429.1 uliofanywa na Serikali katika Bandari ya Tanga zimewezesha uchimbwaji wa kina na ujenzi wa gati na hatimaye kuleta ufanisi wa utendaji katika Bandari hiyo hatua inayowezesha Meli kubwa kutia nanga na kurahisusha shughuli za upakiaji na upakuaji wa mizigo.



Aidha katika hatua nyengine Profesa Ndalichako amesema Serikali ina maono ya kuunganisha Bandari na reli ambapo mpango uliopo ni kujenga reli ya kisasa ya SGR kutoka Tanga hadi Musoma hatua itakayochagiza maendeleo ya mkoa wa Tanga hususani kwa vijana kupata ajira.



Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, alisema Serikali inaendelea na mpango wa kuunganisha bandari hiyo na mtandao wa reli wa kilomita 248 (Tanga–Mruazi–Ruvu) na hatimaye kufika Arusha.



Alisema pamoja na kuwa na reli ya SGR kupitia Minjingu na Engaruka hadi Musoma itakuwa kiunganishi muhimu cha kiuchumi.

Naye kwa upande wake ,Meneja wa Bandari ya Tanga, Salehe Mbega alisema maboresho hayo yameongeza kina cha maji kufikia mita 12 hali inayoruhusu meli kubwa zenye urefu wa hadi mita 200 kutia nanga gatini tofauti na hapo awali.