Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

RC MBONI MHITA AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA KISASA LA BILIONI 5.3 USHETU,

June 17, 2026 Add Comment

 

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akiwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Mhe. Emmanuel Cherehani na viongozi mbalimbali wa Serikali, wakipanda lift ndani ya Jengo jipya la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita (kulia), akiweka jiwe la msingi wa Jengo jipya la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu lililopo Nyamilangano, wilayani Kahama.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, akifungua mlango na kuingia rasmi ndani ya Jengo jipya la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu mara baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa kimkakati uliopo Nyamilangano.

WAZIRI SANGU: MAONESHO YA AJIRA TANZANIA - CHINA YAFUNGUA FURSA ZA AJIRA KWA VIJANA

June 16, 2026 Add Comment
Na: OWM (KAM) - Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu amesema Maonesho ya Ajira kati ya Tanzania na China yameendelea kufungua fursa mbalimbali za ajira kwa vijana wa Kitanzania kupitia uwekezaji, uhamishaji wa teknolojia na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi zinazotekelezwa na kampuni za China nchini.
WADAU:AFRIKA INAPASWA KUJITEGEMEA KATIKA CHAKULA

WADAU:AFRIKA INAPASWA KUJITEGEMEA KATIKA CHAKULA

June 16, 2026 Add Comment
 

DAR ES SALAAM:

Mabadiliko yanayoendelea kufanyika katika mpango wa Marekani wa Food for Peace yameibua mjadala muhimu ambao Afrika haiwezi tena kuupuuza: utegemezi wa muda mrefu wa misaada ya chakula kutoka nje ya bara.

Kwa zaidi ya miongo saba, mpango huo umekuwa miongoni mwa vyanzo vikubwa vya msaada wa chakula kwa mataifa yanayokabiliwa na njaa, migogoro na majanga ya kibinadamu. Hata hivyo, taarifa za hivi karibuni zinaonyesha kuwa mwelekeo wa mpango huo unabadilika, huku ukihusishwa zaidi na maslahi ya kilimo na biashara ya Marekani kuliko malengo ya kibinadamu pekee.

Kwa Afrika, suala hili linapaswa kutazamwa kama tahadhari badala ya mgogoro. Linaonesha jinsi usalama wa chakula wa bara unavyoweza kuathiriwa na maamuzi yanayofanyika nje ya mipaka yake.

Kwa miaka mingi, mataifa mengi ya Afrika yamekuwa yakitegemea misaada ya chakula wakati wa ukame, migogoro au misukosuko ya kiuchumi. Ingawa misaada hiyo imeokoa maisha ya mamilioni ya watu, imeacha swali muhimu: Je, usalama wa chakula wa Afrika unaweza kuendelea kutegemea sera zinazobadilika kulingana na vipaumbele vya mataifa wafadhili?

Jibu linaonekana kuwa hapana.

Hoja hii inaendana na mjadala mpana unaoendelea kuhusu uhuru wa kiuchumi wa Afrika. Wanasiasa, wachambuzi na wanazuoni wengi wa Kiafrika wamekuwa wakisisitiza kuwa uhuru wa kisiasa hauwezi kuwa kamili bila uwezo wa bara kujitegemea kiuchumi.

Mgombea urais wa Tanzania kupitia chama cha ADC, Doyo Hassan Doyo, hivi karibuni alieleza kuwa Afrika inapaswa kuimarisha mifumo yake ya ndani badala ya kutegemea sana taasisi za kimataifa. Akizungumzia nafasi ya bara katika mfumo wa dunia, alisema lengo si kujitenga na mataifa mengine bali kuhakikisha usawa katika mahusiano ya kimataifa.

“Lengo si kujitenga, bali ni kuwa na uwiano,” alisema.

Kauli hiyo inaweza kutumika pia katika mjadala wa usalama wa chakula. Kadri nchi za wafadhili zinavyobadilisha sera zao kulingana na mahitaji ya ndani, ndivyo hatari ya Afrika kubaki katika mazingira ya kutegemea maamuzi ya wengine inavyoongezeka.

Wakati huo huo, Afrika ina rasilimali nyingi zinazoweza kuiwezesha kujitosheleza kwa chakula. Bara lina sehemu kubwa ya ardhi inayofaa kwa kilimo ambayo bado haijatumika kikamilifu, vyanzo vikubwa vya maji pamoja na nguvu kazi inayoongezeka kwa kasi.

Hata hivyo, changamoto zinaendelea kujitokeza katika maeneo ya umwagiliaji, uhifadhi wa mazao, usafirishaji na uchakataji wa bidhaa za kilimo. Kiasi kikubwa cha mazao hupotea baada ya kuvunwa huku baadhi ya nchi zikiendelea kuagiza chakula kutoka nje.

Hali hii inaonesha kuwa tatizo si ukosefu wa rasilimali, bali ni namna ya kuzitumia kwa ufanisi.

Eneo la Biashara Huria la Afrika (AfCFTA) linaweza kuwa sehemu ya suluhisho. Kupitia ushirikiano wa kikanda, nchi za Afrika zinaweza kurahisisha biashara ya mazao ya kilimo na kuhakikisha maeneo yenye ziada ya chakula yanasaidia yale yanayokabiliwa na upungufu.

Lakini mafanikio hayo hayawezi kupatikana bila taasisi imara za ndani.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Lupa Ramadhani, anaamini kuwa uimara wa mifumo ya utawala ni msingi muhimu wa kujenga uhuru wa kweli wa Afrika.

“Kushindwa kuchukua hatua ndani ya nchi kunakaribisha uangalizi kutoka nje,” amesema.

Kauli hiyo inaakisi hali ilivyo katika sekta ya chakula. Pale ambapo sera za kilimo hazitekelezwi ipasavyo, uwekezaji ni mdogo au taasisi zinashindwa kutimiza wajibu wake, utegemezi wa misaada kutoka nje huongezeka.

Katika kipindi ambacho dunia inashuhudia mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi, pamoja na kuongezeka kwa ushindani wa kijiografia kati ya mataifa makubwa, Afrika inalazimika kufikiria upya mkakati wake wa maendeleo.

Hii haimaanishi kukataa ushirikiano wa kimataifa. Misaada ya kibinadamu itaendelea kuwa muhimu wakati wa majanga na dharura. Hata hivyo, ushirikiano huo unapaswa kuimarisha vipaumbele vya Afrika badala ya kuvibadilisha.

Mustakabali wa usalama wa chakula wa bara hautaamuliwa Washington, Brussels au katika miji mingine ya dunia. Utaamuliwa na maamuzi yatakayofanywa katika miji mikuu ya Afrika kuhusu uwekezaji katika kilimo, miundombinu, biashara ya kikanda na taasisi za umma.

Mjadala kuhusu Food for Peace ni zaidi ya mjadala wa misaada. Ni ukumbusho kwamba uhuru wa kweli unahitaji uwezo wa kulisha wananchi wako mwenyewe. Kwa Afrika, huo si uchaguzi wa kisera pekee, bali ni hitaji la kimkakati kwa mustakabali wa bara.

TAASISI ZA UMMA NA BINAFSI ZAHIMIZWA KUWAJIBIKA KWA JAMII

TAASISI ZA UMMA NA BINAFSI ZAHIMIZWA KUWAJIBIKA KWA JAMII

June 16, 2026 Add Comment

Mwenza wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Neema Mwigulu Nchemba, amehimiza Taasisi za umma na binafsi kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za kijamii kupitia utekelezaji wa programu za uwajibikaji kwa jamii (CSR).

Ameyasema hayo, Juni 16, 2026 katika hafla ya kukabidhi vifaa vya hospitali vilivyotolewa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) katika Hospitali ya Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Shirika hill.

Aisha, Mama Neema ameishukuru, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya hususani katika ujenzi wa Hospitali, utoaji wa ajira kwa wataalamu wa atya, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na kuimarisha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi ziliOrahisisha upatikanaji wa huduma bora za afya nchini.

Amesema vifaa hivyo vilivyotolewa vinajumuisha vitimwendo 20, vitanda vya kujifungulia vitano, vitanda vya kufanyia uchunguzi vitano, vitanda vitano vya kulaza wagonjwa, machela moja ya kisasa, makabati matatu ya kuhitadhia vitaa tiba pamoja na mabeseni yenye vifaa mbalimbali kwa ajili ya akinamama 30 waliojifungua vitasaidia vitasaidia kuboresha utoaji wa huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Chamwino na kuongeza ustawi wa mama na mtoto.

Awali, akimkaribisha mgeni rasmi kuzungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Viwanda na Blashara, Judith Kapinga amesema Serikali itaendelea kuhimiza taasisi zake kutekeleza kwa vitendo sera ya uwajibikaji kwa jamii ili kuchangia kuboresha huduma za kijamii na maisha ya wananchi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, amesema Mkoa wake uko tayari katika kushirikiana na Wizara Pamoja na TBS kwa ujumla katika kuendeleza Sekta ya Viwanda na Biashara na jitihada za uwajibikaji kwa Jamii katika Mkoa wake.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya (TBS) Profesa Othman Chande na Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi wamesema TBS itaendelea kutekeleza sera yake ya kuwajibika kwa jamii (CSR Policy) ili kuendelea kuwa karibu na jamii katika kuleta tija na maendeleo.

WAFANYABIASHARA WATAKIWA KUHAKIKI MIZANI KABLA YA KUIUZA SOKONI

June 16, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Wadau wa sekta ya mizani nchini wameiomba Serikali kuangalia upya gharama za uhakiki wa mizani pamoja na kuboresha mazingira ya biashara ili kuwawezesha wazalishaji wa ndani kushindana kwa usawa na bidhaa zinazoingia nchini kwa njia zisizo rasmi.
EWURA YAFIKIA WANANCHI,MAONESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2026

EWURA YAFIKIA WANANCHI,MAONESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2026

June 16, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeanza kushiriki katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yaliyoanza rasmi leo, tarehe 16 mpaka 23 Juni, yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma
Akizungumza kuhusu ushiriki wa EWURA katika maonesho hayo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa EWURA, Bi. Hawa Ramadhan Mniga, amesema maonesho hayo ni fursa muhimu kwa Mamlaka hiyo kuwafikia Watanzania na kuwapatia uelewa kuhusu majukumu yake katika usimamizi wa sekta za nishati na maji.
“Wananchi watakaotembelea banda la EWURA watapata fursa ya kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo mifumo mbalimbali ya kidijitali inayotumiwa na Mamlaka katika utoaji wa huduma kwa wateja, pamoja na maboresho yanayoendelea kufanyika kwa lengo la kuongeza ufanisi, kasi na ubora wa utoaji wa huduma,” amesema Bi. Mniga.
Ameongeza kuwa eneo lingine lililopatiwa kipaumbele ni uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kufanikisha lengo la Taifa la kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.
Aidha, ametoa rai kwa wananchi, wadau wa sekta mbalimbali na washiriki wa maonesho hayo kutembelea banda la EWURA ili kupata elimu, kuuliza maswali na kufahamu kwa undani huduma zinazotolewa na Mamlaka hiyo.

TRAMEPRO: TUTAENDELEA KUWA SAUTI YA WATU WENYE UALBINO

Kajunason June 16, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu.

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO),imetoa mwito kwa wananchi wote kuendelea kuwa mabalozi wa haki, upendo na mshikamano kwa watu wenye ualbino na makundi mengine yaliyo katika mazingira magumu.

Aidha limewataka ndugu wote wenye ualbino nchini Tanzania na duniani kote, wasikate tamaa na kuwakumbusha waendelee kuamini katika uwezo wao,kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii na kutimiza ndoto zao na kwamba Dunia inahitaji mchango, vipaji na uwezo wenu.

Hayo yamesemwa na Boniventura Mwalongo ambaye ni Katibu Mkuu wa Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO)

na Mjumbe wa Kamati Maalumu ya Pamoja ya Kushughulikia Changamoto za Watu Wenye Ualbino nchini alipokuwa akitoa salamu katika Maadhimisho ya kimataifa ya kuongeza uelewa kuhusu Ualbino yaliyofanyika Juni 13,2026.

“TRAMEPRO inapenda kuwahakikishia watu wote wenye ualbino kwamba itaendelea kuwa sauti yao na mshirika wao katika kutetea haki, usawa, heshima na maendeleo yao. Ahadi yetu ni kwamba kamwe hatutawasaliti katika kusimamia haki zenu na haki za binadamu kwa ujumla. 

“Tutaendelea kushirikiana na Serikali, Bunge, taasisi mbalimbali, wadau wa maendeleo na jamii kwa ujumla katika kuhakikisha kuwa watu wenye ualbino wanapata ulinzi, heshima, fursa na haki zote wanazostahili kama raia wengine,”amesema na kuongeza "Utu, usawa, upendo na uhifadhi wa mazingira ni msingi wa maendeleo endelevu na jamii yenye amani kwa wote."

Akieleza zaidi kuhusu maadhimisho hayo amesema TRAMEPRO inaamini siku hiyo ni fursa muhimu ya kuendelea kuelimisha jamii kuhusu haki, usawa, usalama, afya na ustawi wa watu wenye ualbino, pamoja na kupinga ubaguzi, unyanyapaa na vitendo vyote vya ukatili vinavyokiuka haki zao za msingi. 

Pia maadhimisho hayo yanakumbusha wajibu wa pamoja wa kujenga jamii inayoheshimu utu, usawa na haki za kila mwanadamu bila kujali tofauti zake za kimaumbile.

“TRAMEPRO inatoa pongezi kwa Chama cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS), Albinism Sports Club, Serikali, Bunge, wataalamu wa tiba asili, wadau wa afya, elimu, michezo na mazingira pamoja na wanachama wote wa TRAMEPRO kwa mchango wao katika kuimarisha ustawi, usalama na maendeleo ya watu wenye ualbino nchini.”

Wakati huo huo Mwalongo ametumia maadhimisho hayo kueleza wanatambua na kupongeza mechi ya kirafiki iliyochezwa Juni 6,2026 kati ya Bunge Sports Club na Albinism Sports Club, ambayo imeendelea kuwa mfano bora wa matumizi ya michezo katika kuhamasisha ushirikishwaji, mshikamano, uelewa na mapambano dhidi ya ubaguzi kwa watu wenye ualbino. 

Tukio hilo limeonesha michezo ni nyenzo muhimu ya kuunganisha jamii na kuimarisha mshikamano wa kitaifa.Tunatoa shukrani za dhati kwa viongozi wa Bunge Sports Club, Waheshimiwa Wabunge na wadau wote walioshiriki kufanikisha tukio hilo muhimu. 

Aidha, wanaguswa na moyo wa upendo, utu na kujali uliooneshwa na Salma Kikwete, ambaye baada ya kuguswa na hali halisi ya baadhi ya wachezaji wa Albinism Sports Club alionesha moyo wa kuwafariji na kuwasaidia. Kitendo hicho ni mfano wa kuigwa katika kujenga jamii yenye huruma, mshikamano na usawa.

“Pia tunatoa shukrani kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS)kwa kuwezesha upatikanaji wa miche iliyotumika katika zoezi hilo. Mchango huo unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za Serikali, mashirika ya kiraia na wananchi katika kulinda mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.”

NEMC YAVIFUNGIA VIWANDA VIWILI MKURANGA KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA

June 15, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekifungia kiwanda cha SAN SHAN na BAI-LY PAPER CO. LTD kwa kukiuka sheria na taratibu za mazingira, hatua iliyochukuliwa baada ya timu ya ukaguzi wa mazingira uliofanyika katika Wilaya ya Mkuranga ukiongozwa na Meneja wa Utekelezaji wa Sheria wa NEMC, Mhandisi Luhuvilo Mwamila.

TANGA KUPOKEA MWENGE WA UHURU JUNI 17, MIRADI YA BIL. 27.7 KUKAGULIWA

June 15, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga, Tanga

Mkoa wa Tanga unatarajia kuupokea Mwenge wa Uhuru Juni 17, mwaka huu, ambapo utakimbizwa katika halmashauri zote 11 za mkoa huo na kukagua, kuzindua pamoja na kuweka mawe ya msingi katika miradi 73 yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 27.7.

Hayo yalisemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk. Batilda Burian, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026.

Dk. Burian alisema Mwenge wa Uhuru utapokelewa katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mpya, Kijiji cha Mtoro, Kata ya Tunguli wilayani Kilindi ukitokea Mkoa wa Morogoro, kabla ya kukimbizwa kwa umbali wa kilometa 1,340 katika halmashauri zote za mkoa huo.

Alisema Juni 28, mwaka huu, Mwenge huo utakabidhiwa Mkoa wa Kilimanjaro katika Uwanja wa Shule ya Msingi Hedaru.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa, kati ya miradi 73 itakayofanyiwa kazi na Mwenge wa Uhuru, miradi 34 itawekewa mawe ya msingi, 26 itafunguliwa na kuzinduliwa, huku miradi 11 ya vijana na miradi miwili ya sekta ya maji ikikaguliwa.

Alifafanua kuwa miradi hiyo ina thamani ya Sh bilioni 27.76, ambapo Sh milioni 300.6 ni nguvu za wananchi, Sh bilioni 1.27 ni michango ya halmashauri, Sh bilioni 10.7 ni fedha za Serikali Kuu na Sh bilioni 15.47 ni kutoka kwa wahisani.

Akizungumzia kaulimbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema, “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo,” Dk. Burian alisema mkoa umejipanga kuhakikisha wananchi wa makundi mbalimbali wanashiriki kikamilifu katika shughuli zote za Mwenge.

“Tumewaandaa viongozi wa serikali, watumishi wa umma, viongozi wa dini, wanawake, vijana, watu wenye mahitaji maalumu pamoja na makundi mengine kushiriki kikamilifu kuanzia mapokezi hadi makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru,” alisema.

Aliongeza kuwa wananchi watapata fursa ya kuushika na kuukimbiza Mwenge huo kama sehemu ya kuimarisha mshikamano na umoja wa kitaifa unaosisitizwa katika kaulimbiu ya mwaka huu.

Mbali na kuhamasisha maendeleo, alisema Mwenge wa Uhuru utaendelea kutoa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, malaria, VVU/UKIMWI, matumizi ya dawa za kulevya na umuhimu wa lishe bora.

Dk. Burian aliwataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi katika maeneo ya mapokezi, miradi na mikesha mbalimbali ili kushiriki shughuli za Mwenge wa Uhuru.

“Mkoa umejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanapata burudani na hamasa kupitia ushiriki wa wasanii na vikundi mbalimbali vya sanaa katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utakesha,” alisema.

Alisema kwa ujumla maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2026 yamekamilika kwa kiwango cha kuridhisha na mkoa uko tayari kwa shughuli zote za mbio hizo.




ORYX YAZINDUA KITUO KIPYA CHA MAFUTA WAZO, YAAHIDI KUSOGEZA HUDUMA ZA NISHATI KARIBU NA WANANCHI

June 15, 2026 Add Comment
KAMPUNI ya Oryx Energies Tanzania imezindua kituo kipya cha mafuta eneo la Wazo jijini Dar es Salaam huku mkakati wa kampuni hiyo ukiwa ni kuendelea kusogeza huduma za nishati za mafuta na gesi karibu na wananchi.

SERIKALI YAHAKIKISHA MAZINGIRA BORA KWA SHULE BINAFSI

June 15, 2026 Add Comment
SERIKALI imezitaka taasisi binafsi za elimu kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa mageuzi ya elimu yanayolenga kuimarisha ujuzi, sayansi na teknolojia, huku ikiipongeza Shule ya Kimataifa ya Luminous kwa mchango wake katika kukuza ubora wa elimu nchini.

CBE YAONGEZA KOZI ZENYE MAHITAJI MAKUBWA KATIKA SOKO LA AJIRA

June 15, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

CHUO Cha Elimu ya Biashara (CBE) kimepanua wigo wa fursa za elimu ya juu nchini baada ya kupata ithibati kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) kwa ajili ya kuendesha programu sita mpya zitakazoanza kupokea wanafunzi katika mwaka wa masomo 2026/2027.

PHD YA DKT. NSEKELA YAFICHUA SIRI YA MAGEUZI NA MAFANIKIO YA CRDB

Kajunason June 15, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Pretoria

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Abdulmajid Mussa Nsekela, ametunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) kutoka Chuo Kikuu cha Afrika Kusini (UNISA), hatua inayotafsiriwa kama ushahidi wa namna taaluma, utawala bora na uongozi wa kimkakati vinavyoweza kuibadilisha taasisi ya kifedha na kuleta matokeo chanya ya biashara.

Dkt. Nsekela alihitimu shahada hiyo Juni 12, 2026, baada ya kukamilisha utafiti uliochambua uhusiano kati ya utawala wa makampuni na ufanisi wa kifedha wa benki za Afrika Mashariki, huku ukitathmini athari za uvujaji wa taarifa katika utendaji wa taasisi za fedha.

Utafiti huo umebainisha kuwa mifumo imara ya utawala, uwazi katika utoaji wa taarifa na udhibiti wa taarifa nyeti huongeza imani ya wawekezaji, kuimarisha utendaji wa kifedha na kuweka msingi wa ukuaji endelevu wa taasisi.
Akizungumza baada ya kutunukiwa shahada hiyo, Dkt. Nsekela alisema kujifunza ni safari endelevu inayowasaidia viongozi kufanya maamuzi bora na kuimarisha utendaji wa taasisi wanazoongoza.

"Usimamizi makini wa makampuni si suala la nadharia pekee, bali ni msingi wa utendaji bora na mafanikio endelevu katika sekta ya fedha. Safari hii imeniongezea maarifa yatakayochangia zaidi katika kuendeleza taasisi na sekta yetu," alisema.

Mafanikio hayo ya kitaaluma yanakuja wakati Benki ya CRDB ikiendelea kushuhudia ukuaji mkubwa chini ya uongozi wake tangu alipoteuliwa mwaka 2018. Katika kipindi hicho, bei ya hisa za benki imeongezeka kutoka Sh95 hadi kufikia takribani Sh3,000 kwa hisa, huku faida baada ya kodi ikiongezeka kutoka Sh bilioni 64.1 hadi Sh bilioni 728.6 mwaka 2025.
Benki hiyo pia imefanikiwa kuharakisha mageuzi ya kidijitali, ambapo zaidi ya asilimia 98 ya miamala yake hufanyika kupitia majukwaa ya kidijitali. Idadi ya wateja imeongezeka na kufikia zaidi ya milioni 7.2 wanaohudumiwa kupitia matawi, mawakala, ATM, SimBanking na huduma za intaneti.

Katika kipindi hicho, CRDB imepanua shughuli zake nje ya mipaka ya Tanzania kwa kuimarisha uwepo wake Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, sambamba na kufungua ofisi ya uwakilishi Dubai ili kuvutia mitaji na kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika masoko ya kimataifa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Profesa Neema Mori, alisema mafanikio ya Dkt. Nsekela yanaonesha namna taaluma na uongozi makini vinavyoweza kuleta mageuzi makubwa ndani ya taasisi za biashara.

Alisema Benki ya CRDB imeendelea kuwa mfano wa mafanikio yanayojengwa katika misingi ya utawala bora, ubunifu na maamuzi yanayotokana na matumizi sahihi ya taarifa.

Mafanikio ya Dkt. Nsekela yanatoa funzo kwa viongozi wa biashara barani Afrika kuhusu umuhimu wa kuwekeza katika maarifa na kujifunza kila wakati ili kujenga taasisi imara, zenye ushindani na uwezo wa kuhimili mabadiliko ya mazingira ya biashara duniani

RAIS DKT. MWINYI AJUMUIKA KATIKA MAZISHI YA MSANII MKONGWE, MAREHEMU MZEE ONYANGO

June 15, 2026 Add Comment








RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, leo tarehe 13 Juni 2026, amejumuika na wanafamilia, ndugu, jamaa, wasanii, na mamia ya waombolezaji katika mazishi ya msanii mkongwe, marehemu Issa Joseph Mohamed, maarufu kwa jina la Mzee Onyango, yaliyofanyika Kawe , Wilaya ya Kinondoni, Jijini Dar es Salaam.



Mazishi hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwemo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, pamoja na wasanii wa fani mbalimbali na wananchi waliofika kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu.


Mara baada ya kuwasili, Rais Dkt. Mwinyi alisaini kitabu cha maombolezo na kutoa mkono wa pole kwa wanafamilia.


Marehemu Issa Joseph Mohamed alizaliwa tarehe 14 Aprili 1950 na kufariki dunia tarehe 11 Juni 2026, akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Jijini Dar es Salaam.


Wakati wa uhai wake, marehemu alipata umaarufu mkubwa kupitia kazi zake za filamu na maigizo na kujizolea heshima kubwa miongoni mwa Watanzania kwa jina la Mzee Onyango.


Marehemu amezikwa katika Makaburi ya Kondo, Ununio, Wilaya ya Kinondoni, Jijini Dar es Salaam.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa; jina la Bwana lihimidiwe. Amina.