NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
MABAO mawili yaliyofungwa na Mohamed Mtindi yalitosha kuipa
ushindi timu ya Coastal Union kwenye mechi yao ya Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya Mbeya City
mchezo uliochezwa leo kwenye dimba la CCM Mkwakwani.
Bao hizo zilifungwa kwenye dakika za 82 na 89 ziliweza kuinua shangwe na nderemo kwa wapenzi na mashabiki wa soka mkoani Tanga ambao walijitokeza kushuhudia mchezo huo.
Mchezo huo ambao ulianza kwa kasi kwa timu zote
kushambuliana kwa zamu ambapo mpaka timu zote zinakwenda mnapumziko hakuna timu
iliyoweza kuona lango la mwenzie.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa timu zote kuingia
uwanjani hapo zikiwa zimefanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake ambapo
kwa upande wa Coastal Union waliwatoa Ally Iddy,Crispian Odulla na Ayoub Yahaya
ambao nafasi zao zilichukuliwa na Suleimani Selembe,Mohamed Mtindi,Yayo Lutimba
na Keneth Masumbuko.
Kwa upande wa Mbeya
City waliwatoa Mwegane
Yeya,Jeremia John nafasi zao zilichukuliwa na Fransisi Casto na Richard Peter
ambao waliweza kucheza vema licha ya kushindwa kuibuka na ushindi kwenye mechi
hiyo.
Vikosi vilivyozeshwa leo kwa upande wa Coastal Union
iliwachezesha Shabani Kado,mbwana hamisi,abdi banda,juma nyoso,yusuph
chuma,jerry santo,Daniel lyanga,ally iddi,haruna moshi,crispian odulla na ayoub
yahya.
Kwa upande wa Mbeya City iliwachezesha Davidi buruani,azizi
sibo,hasan mwasapili,deogratis Julius,yusuph abdallah,Anthony matogolo,mwagane
yeya,steven mazand,paul nonga,jeremia john na peter mapunda.
Picha na matukio mengine ya mechi hii yatakujia muda sio mrefu.