PSPTB YAFIKA CHUO KIKUU MZUMBE KUTOA ELIMU

June 05, 2023

 Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetoa mafunzo Wanafunzi wa Shahada na Shahada ya Uzamili wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo Kikuu Mzumbe hii ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu kwa umma hasa kwenye vyuo vinavyotoa masomo ya Ununuzi na Ugavi.


Akizungumza na Michuzi Blog, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi amesema Bodi hiyo imeendelea kuwapa mafunzo Wanafunzi wa Vyuo mbalimbali wanaochukua kozi hiyo ya Ununuzi na Ugavi kuhusu shughuli zinazofanywa na Bodi, Usajili kwa njia ya mtandao, mtaala mpya, pamoja na maadili na miiko ya taaluma hiyo.

Mbanyi amesema mtaala huu mpya utaanza kutumika kwenye mitihani ijayo ya mwezi wa 11 ambapo wahitimu wote watautumia hivyo wanapita vyuoni kutoa elimu ili wanapomaliza vyuo waweze kuendana na mtaala huo mpya.

Naye, Mkuu wa Idara ya Ununuzi na Usimamizi wa Vifaa Chuo Kikuu Mzumbe, Dkt. Paul M. Nsimbila ametoa shukrani kwa wafanyakazi wa PSPTB wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi kwa kuweza kufika chuoni hapo kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Bodi.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi akizungumza na Wanachuo pamoja na wafanyakazi wa Chuo Kikuu Mzumbe kuhusu namna Bodi hiyo inavyowasimamia Wataalam wa Ununuzi na Ugavi wakati wa mafunzo kwa wanafunzi wa Chuo hicho.
Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma ( PSPTB), Shamim Mdee akitoa maelezo kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo wakati wa kutoa elimu kwa wanafunzi wa Shahada na Shahada ya Uzamili wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo Kikuu Mzumbe kilichopo Mjini Morogoro.
Afisa Elimu Mkuu- Mitaala (PSPTB), Jeremiah J. Haule akitoa mada kuhusu namna ya kuongeza dhamani pamoja namna walivyobadili mtaala kwenye taaluma ya Ununuzi na Ugavi kwa wanafunzi wa Shahada na Shahada ya Uzamili wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo Kikuu Mzumbe kilichopo Mjini Morogoro ikiwa na lengo la kutoa elimu kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo.
Afisa TEHAMA kutoka PSPTB Boniface Mushi akitoa mada kuhusu namna ya mwanafunzi anavyoweza kujisajili pamoja na kufanya mitihani ya Bodi wakati wa kutoa elimu kwa wanafunzi wa Shahada na Shahada ya Uzamili wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo Kikuu Mzumbe kilichopo Mjini Morogoro ikiwa na lengo la kutoa elimu kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo.
Baadhi ya wanafunzi wa Shahada na Shahada ya Uzamili wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo Kikuu Mzumbe wakiuliza maswali mara baada ya wataalam kutoka PSPTB kuwasilisha mada mbalimbali chuoni hapo.
Mkuu wa Idara ya Ununuzi na Usimamizi wa Vifaa Chuo Kikuu Mzumbe, Dkt. Paul M. Nsimbila akitoa neno la shukrani kwa wafanyakazi wa PSPTB wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi waliofika chuoni hapo kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Bodi.
Baadhi ya wanafunzi wa Shahada na Shahada ya Uzamili wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo Kikuu Mzumbe wakifuatilia mada kutoka kwa wafanyakazi wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) waliofika chuoni hapo kwa akili ya kutoa elimu zinayohusu Bodi hiyo.
Picha ya Pamoja

DK.MWIGULU AONGOZA HARAMBEE NA KUCHANGISHA MIL.443/- UJENZI WA SHULE SEKONDARI ZA KKKT DAYOSISI YA KATI

June 05, 2023

 


Waziri wa Fedha na Mipango,Dk. Mwigulu Nchemba, akiwa amebeba kikapu chenye fedha wakati alipokuwa akiongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa shule mbili za sekondari zitakazomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kati katika changizo lililofanyika Kanisa la Emmauel Msalaba Mrefu Mjini Singida leo Juni 4, 2023. Wa pili kushoto ni Katibu Mkuu wa Kanisa hilo, Robert Kitundu.



Na Dotto Mwaibale, Singida

WAZIRI wa Fedha na Mipango,Dk,Mwigulu Nchemba, ameongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa shule mbili za sekondari zitakazomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kati ambapo jumla ya Sh. 443,063,800 zilipatikana na lengo lilikuwa ni kukusanya Sh.Milioni 500.

Katika fedha hizo zilizopatikana, taslimu zilikuwa ni Sh. 400,103, 800 na ahadi ikiwa ni Sh. 42,960,000. Dk.Mwigulu wakati wa harambee hiyo aliambatana na Mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima,Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu,Mbunge wa Makete, Festo Sanga, Mbunge wa Handeni Mjini, Reuben Kwagilwa na Mbunge wa Nsimbo, Anna Lupembe na viongozi mbalimbali wa kanisa hilo akiwamo Baba Askofu Dk.Alex Malasusa na Katibu Mkuu wa kanisa hilo, Robert Kitundu.

Akizungumza katika harambee hiyo iliyofanyika Kanisa la KKKT Usharika wa Emmanuel Msalaba Mrefu Mjini Singida, Dk.Nchemba ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi alisema Serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na taasisi za dini hasa katika eneo la sekta ya elimu na afya kwani shule nyingi kongwe hapa nchini zilikuwa zimeanzishwa na taasisi hizo likiwamo kanisa la KKKT.

“Kanisa la KKKT hapa nchini ni taasisi iliyochangia sana katika maendeleo ya Mtanzania na lipo katika historia ya nchi yetu na haitafutika kwani ukiondoa hizi shule za sekondari zilizopewa jina katika kila kata kabla ya hapo shule zote zilizokuwa zikitumika kwa kiwango kikubwa zilikuwa ni za kanisa,” alisema Dk. Mwigulu.

Dk.Mwigulu alisema hata katika sekta ya afya hospitali nyingi zilizokuwa zikitoa huduma zilikuwa ni za kanisa na kwamba lengo la harambee hiyo lipo kwenye malengo yaleyale ya kuhudumia jamii.

Aidha, Mwigulu alisema moja ya muundo ambao anapenda kuhusisitiza katika utekelezaji wa shughuli za miradi ya maendeleo baina ya Serikali na sekta binafsi ni ile iliyofanywa na kanisa na kuwa viongozi wengi bila ya kujali dini zao wamepitia kwenye mikono ya kanisa na kusoma katika shule za taasisi hiyo.

Askofu wa kanisa hilo Dayosisi ya Kati, Dk.Syprian Hilinti akizungumza kwenye harambee hiyo alisema Halmashauri Kuu ya kanisa hilo imeweka mpango mkakati wa miaka mitano ya kujenga shule mbili za Sekondari Kiomboi na Kititimo kuanzia mwaka 2022/ 2027 kama mradi wa kitega uchumi cha kanisa.

“Miradi hii hailengi kuuwa historia za Missioni au biblia Kiomboi balikupanua kuendana na hali halisi na mahitaji ya wakati bila kuacha au kupoteza kusudi la injili bali kulitoa kwa ubora wa kukidhi changamoto za sasa.

Alisema kuwa hawawezi kuendesha gari la kisasa kwa kutumia gia za mwaka 1926 na kuwa halmashauri hiyo imeweka mipango ya muda mrefu kujenga kitega uchumi maeneo ya nyuma ya ofisi Kuu ya Dayosisi hiyo mara baada ya kumaliza mpango wa ujenzi wa shule.

Aliongeza kuwa sambamba na mpango huo Dayosisi imeweka sera ya kuendelea kuimarisha ukarabati, maongozi, usimamizi na utendaji kwenye vituo, miradi na taasisi zake zilizopo tayari.

Alisema katika awamu ya kwanza zilikuwa zikihitajika Sh.Milioni 500 na ndio lengo la kufanya harambee hiyo.


Katika hatua nyingine Dk. Hilinti alimuomba Dk.Mwigulu kuwasilisha ombi la kanisa hilo kwa Rais Samia Suluhu Hassan la kutaka warejeshewe Shule ya Sekondari ya Luluma iliyopo wilayani Iramba Kiomboi.

Askofu wa kanisa hilo Dayosisi ya Kati, Dk.Syprian Hilinti, akiendesha harambee hiyo.

Viongozi wakuu wa kanisa hilo wakiombea mchango uliotolewa na mgeni rasmi katika harambee hiyo, Dk.Mwigulu Nchemba.

Maaskofu wastaafu wa Kanisa hilo, Dk. Alex Malasusa (kushoto) na Eliuphoo Sima wakiwa kwenye harambee hiyo.

Mgeni rasmi katika harambee hiyo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk.Mwigulu Nchemba (kulia) akiwaelekeza jambo wabunge alioongozana nao kwenye shughuli hiyo, Mbunge wa Singida, Mashariki, Miraji Mtaturu 9kushoto) na Mbunge wa Singida Mjini Musa Sima.

Baba Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kati, akipeana mkono na Mbunge wa Singida, Mjini Musa Sima baada ya kuchangia katika harambee hiyo.

Viongozi hawa wakiwa kwenye harambee hiyo. Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Kanisa hilo, Mhandisi Robert Kitundu, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk.Mwigulu Nchemba, Mbunge wa Singida Mjini, Musa Sima na Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu.

Dk. Mwigulu Nchemba (wa pili kulia) akiwatambulisha wabunge alioongozana nao katika harambee hiyo. Kutoka kulia ni Mbunge wa Singida, Mashariki Miraji Mtaturu, Mbunge wa Singida Mjini, Musa Sima, Mbune wa Handeni Mjini, Reuben Kwagilwa, Mbunge wa Makete, Festo Sanga, Mbunge wa Jimbo la Nsimbo, Anna Lupembe na Katibu Mkuu wa kanisa hilo, Robert Kitundu

Waumini wa kanisa hilo wakiwa kwenye harambee hiyo

Harambee ikiendelea.

Wachungaji wakiwa katika foleni ya kwenda kuchangia harambee hiyo

Viongozi wa kanisa hilo wakiwa kwenye harambee hiyo.

Wapiga matarumbeta wakitoa burudani

Mwimbaji wa nyimbo za injili Ambwene Mwasongwe akitoa burudani safi la nyimbo za kumtukuza Mungu.

Afisa Maendeleo wa Wilaya ya Ikungi, Haika Masawe alikuwa ni miongoni mwa watu waliokuwepo kwenye harambee hiyo.

Mwimbaji Ambwene Mwasongwe akiendelea kuzikonga nyoyo za waumini wa kanisa hilo katika harambee hiyo

Burudani za nyimbo za kumtukuza Mungu ambazo zilikuwa zikihamasisha utoaji wa sadaka zikiendelea kuimbwa

Kwaya ya Waadzabe kutoka Wilaya ya Mkalama ikitoa burudani kwenye harambee hiyo.

Wachungaji wa kanisa hilo wakiwa kwenye harambee hiyo

Harambee ikiendelea.

Taswira ya harambee hiyo.

Kwaya Kuu ya kanisa hilo ikitumbuiza.

Changizo likifanyika.

Burudani zikiendelea kufanyika.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba akionesha furaha yake wakati wa harambee hiyo.

Dk. Mwigulu Nchemba (katikati) Mbunge wa Singida Mjini Musa Sima kulia na Katibu Mkuu wa kanisa hilo, Robert Kitundu (kushoto) wakionesha umahiri wa kusakata muziki wa nyimbo za injili wakati wa harambee hiyo.

Katibu Mkuu wa kanisa hilo, Robert Kitundu, akizungumza kwenye harambee hiyo.

Mbunge wa Singida Mjini Musa Sima akiwa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Singida, Shabani Hamisi kwenye harambee hiyo.

Askofu Dk. Alex Malasusa akiteta jambo na Dk. Mwigulu Nchemba wakati wa harambee hiyo.

Mwimbaji wa nyimbo za injili Ambwene Mwasongwe (kulia) akiendelea kuwapagawisha waumini wa kanisa hilo kwa nyimbo za kumtukuza Mungu. Katikati ni Katibu Muhutasi Bodi ya Maji Bonde la Kati, Happiness Mlingi,akifurahia nyimbo hizo.

Harambee hiyo ikiendelea.

Wachungaji na wageni waalikwa wakiwa kwenye harambee hiyo.

Kwaya ikiwa kwenye harambee hiyo.
Kwayaikitoa burudani katika harambee hiyo.

Burudani ikiendelea.