MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA UELIMISHAJI UMMA KUHUSU UALBINO

MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA UELIMISHAJI UMMA KUHUSU UALBINO

June 13, 2015

1
Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Dkt. Kevin Mandopi akizungumza na wadau mbalimbali wa masuala ya haki za binadamu katika mkutano wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelimishaji Umma Kuhusu Ualbino uliofanyika kwenye ofisi za Tume hiyo leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali Bibi. Neema Ringo na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bibi. Nkasori Sarakikya.
2
Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bibi. Mary Massay akitoa ufafanuzi kuhusu haki za watu wenye ualbino katika mkutano wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelimishaji Umma Kuhusu Ualbino uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bibi. Nkasori Sarakikya.
3
Mwakilishi wa UNESCO Bi. Zulmira Rodrigues akizungumza kwenye mkutano wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelimishaji Umma Kuhusu Ualbino leo jijini Dar es Salaam ambapo ameishauri Serikali kuweka mikakati ya muda mrefu ili kukomesha ukatili na unyanyapaa dhidi ya watu wenye ualbino.
4
Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali Bibi. Neema Ringo (kushoto) akitoa rai kwa watanzania kutoa taarifa mapema za vitendo vya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino katika mkutano wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelimishaji Umma Kuhusu Ualbino uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Dkt. Kevin Mandopi na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bibi. Nkasori Sarakikya.
5
Baadhi ya waandishi wa habari na wadau wa masuala ya haki za binadamu wakifuatilia mkutano wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelimishaji Umma Kuhusu Ualbino uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Fatma Salum – Maelezo
ZIARA YA RAIS DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE NCHINI UHOLANZI JUNI 08, 2015

ZIARA YA RAIS DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE NCHINI UHOLANZI JUNI 08, 2015

June 13, 2015
1

2

3
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Watanzania waishio Uholanzi waliojitokeza kumlaki wakati akiwasili jijini The Hague, Uholanzi,  Juni 8, 2015   4
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo na muhtasari wa ziara yake toka kwa Balozi wa Tanzania nchini Uholani Mhe Wilson  Masilingi baada ya kuwasili The Hague Juni 8, 2015    5
Rais Jakaya Kikwete akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uholanzi Mhe. Bert Koenders  jijini The Hague   Juni 8, 2015   6gfdhdh
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katikati wakati Waziri wa Zanzibar Mhe Ramadhani akigonganisha glasi na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uholanzi Mhe. Mark Rutte jijini The Hague   Juni 8, 2015.  Kushoto ni  Balozi wa Tanzania nchini Uholani Mhe Wilson  Masilingi 
8
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mfalme Willem Alexander katika kasri la Kifalme la Noordeinde jijini The Hague   Juni 8, 2015.  
9

10 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai ICC Jaji Silvia Alejandra Fernandes de Gurmendi alipotembelea makao makuu ya mahakama hiyo jijini The Hague  Juni 8, 2015 
11

12

14

15
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakiwa  na Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai ICC Jaji Silvia Alejandra Fernandes de Gurmendi alipotembelea makao makuu ya mahakama hiyo jijini The Hague  Juni 8, 2015. 16
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikutana na kuongea na Mabalozi wa nchi mbalimbali za Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Uholanzi  jijini The Hague   Juni 8, 2015.   
17
picha ya pamoja na mabalozi wa nchi mbalimbali za Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Uholanzi  jijini The Hague   Juni 8, 2015.   
18 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Waziri Mkuu wa Uholanzi Mhe Mark Rutte  jijini The Hague  Juni 8, 2015.

WAGOMBEA URAIS CCM NA HADITHI YA LIGI KUU BARA

June 13, 2015



Harakati za kutangaza nia kwa wagombe nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) limeshika kasi, hata hivyo wale wanaodhaniwa kuwa nguvu hakuna hata mmoja ambaye mkoa wake una timu katika Ligi Kuu Bara.


Ni kama wagombea hao wameikwepa ligi kuu ambayo ingeweza kutumika kama mtaji wa kisiasa kwao kwa kupata kura za wanamichezo.

Championi Jumamosi limewatazama baadhi ya wagombea hao CCM na hakuna hata mmoja ambaye jimbo au mkoa wake una timu ya ligi kuu au ambayo imepanda kucheza michuano hiyo msimu ujao.
Bernald Membe
Membe ni Mbunge wa Jimbo la Mtama lililopo mkoani Lindi pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Lindi haina timu katika ligi kuu na klabu yake ya mwisho kushiriki michuano hiyo ni Kariakoo Lindi ambayo ilishuka daraja miaka 12 iliyopita.

Stephen Wassira
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira ambaye pia ni Mbunge wa Bunda mkoani Mara ametangaza nia ya kuwani nafasi ya urais. Polisi Mara ilishiriki ligi kuu mara ya mwisho miaka ya mwanzoni ya 2000, tangu hapo Mara haina katika ligi hiyo hadi leo.

Samuel Sitta
Mbunge wa Jimbo la Urambo Mashariki, Tabora, ambaye pia ni Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta ametangaza nia ya kutaka kuwa rais wa Tanzania, hata hivyo mkoa wake hauna timu ligi kuu. Rhino Rangers ndiyo timu ya mwisho ya Tabora kucheza ligi hiyo msimu wa 2013/14.

Edward Lowassa

Waziri Mkuu aliyejiuzulu na Mbunge wa Jimbo la Monduli mkoani Arusha, Edward Lowassa ni miongini mwa watangaza nia wenye nguvu nchini lakini mkoa wake hauna timu ligi kuu. Mara ya mwisho watu wa Arusha kutazama mechi za ligi kuu pale kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid ilikuwa msimu wa 2013/14 ambapo JKT Oljoro ilishuka daraja.

SERIKALI YATOA MANENO YAKE KUHUSIANA NA SUALA LA SIMBA NA SINGANO

June 13, 2015



Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, imewataka wachezaji wa Ligi Kuu Bara kuwa na wanasheria wao wa kusimamia wakati wa kusaini mikataba yao.


Kauli hiyo ya serikali imekuja baada ya kiungo mshambuliaji Ramadhan Singano ‘Messi’ kuwa katika mgogoro wa kisheria na Klabu ya Simba kuhusu mkataba wake na timu hiyo.

Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia, ameliambia Championi Jumamosi kuwa, kupitia mgogoro huo ni vizuri wachezaji wakatumia wanasheria katika kutazama mikataba yao ili kuzuia migogoro inayoweza kujitokeza siku za mbele.

“Hili sakata la Messi na Simba nalisikia juu juu tu, lakini ukitazama vizuri utagundua mchezaji hakuwa na msimamizi wa maana katika kusaini mkataba ule, ndiyo maana sasa wanapingana.

“Hivyo kuanzia sasa wachezaji wanapaswa kuwa na wanasheria wao binafsi ili wawasimamie katika mambo ya mikataba kwani wengi wanasaini mikataba bila kujua kilichomo ndani yake,” alisema Nkamia ambaye amewahi kuwa katibu mwenezi wa Simba.

“Siyo jambo jema kwa mchezaji kukimbilia fedha tu bila kujali kilichomo katika mkataba na kusaini akiwa haelewi kilichoandikwa au kukisoma na kukubaliana nacho.”

Katika madai ya msingi, Messi anasisitiza mkataba wake unaisha Julai Mosi, mwaka huu wakati Simba wanasema mkataba huo unaisha Julai Mosi, mwakani, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limewataka wawili hao kuketi upya kuzungumzia mkataba mpya huku likivunja mikataba ya awali kwa kuwa ina dosari.


Messi amejitangaza kuwa mchezaji huru na Simba inasisitiza kuwa kiungo huyo bado ni mali yao na hapaswi kuzungumzia mkataba wake kwenye vyombo ya habari.
Rais Kikwete aongoza maadhimisho ya watu wenye Albism Duniani

Rais Kikwete aongoza maadhimisho ya watu wenye Albism Duniani

June 13, 2015

1
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na baadhi ya watoto wenye albinism mara baada ya kuwasili katika uwanja wa michezo wa Sheikh amri Abeid mjini Arusha leo ambapo aliongoza maadhimisho ya siku ya watu wenye Albinism Duniani.
2
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa na baadhi ya watoto wenye albism katika uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha wakati wa maadhimisho ya siku ya watu wenye albinism Duniani.
picha na Freddy Maro
TAARIFA ZA KIMICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

TAARIFA ZA KIMICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

June 13, 2015


index 
Msafara wa timu ya Taifa ya Tanzania (taifa Stars) inayodhaminiwa na kampuni ya bia ya Kilimanjaro Premium Lager tayari umewasili salama katika eneo la Borg El Arab jijini Alexandria na kufikia katika hoteli ya Panacea tayari kwa mchezo wake wa kesho.
Taifa Stars ambayo ilikuwa kambini nchini Ethiopia kwa takribani wiki moja, iliondoka jana usiku Addis Ababa  na kuwasili uwanja wa ndege wa Cairo majira ya saa 8 usiku, kisha kuunganisha kwa usafiri wa basi mpaka Borg El Arab takribani masaa matatu.
Kocha mkuu wa Taifa Stars Mart Nooij, atakiongoza kikosi chake katika mazoezi ya mwisho leo saa 1 usiku katika uwanja wa Borg El Arab kwa saa za Misri, sawa na saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Akiongelea mchezo wa kesho, Nooij amesema anashukuru kikosi kimefika salama nchini Misri na kipo katika hali nzuri, vijana wana ari na morali ya hali ya juu, anaamini kesho timu itfanya vizuri katika mchezo huo dhidi ya wenyeji Misri.
Nooij amesema mchezo wa kesho ni muhimu kwake, na kikosi chake kitacheza mpira wa kasi na pasi za haraka haraka, huku safu ya ushambuliaji ikihakikisha inatumia vizuri nafasi itakazozipata.
Aidha kuelekea katika mchezo huo wa kesho, kiungo Amri Kiemba ameungana na wachezaji wengine waliokuwa kambini Addis Ababa kuchukua nafasi ya Mrisho Ngasa ambaye alishindwa kuungana na timu kutokana na sababu zilizopo nje ya uwezo wake.
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia tayari amewasili jijini Alexandria kwa ajili ya kuipa sapoti Taifa Stars katika mchezo huo wa kesho.
Mchezo kati ya Misri na Tanzania utachezwa kesho saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki na kati katika uwanja wa jeshi la Misri (Borg El Arab) uliopo takribani kilometa 70 kutoka jijini Alexandria na kilometa 200 kutoka jiji la Cairo.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

MWENGE ULIVYOKIMBIZWA KIMBIZWA KOROGWE, TANGA

June 13, 2015



Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Tanga, Hafsa Mtassiwa  (kushoto) akipikea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Mariam Juma na makabidhiano kufanyika kijiji cha Kweshemshi Korogwe Vijijini  leo.




 Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa, Juma Khatib Chumu na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Tanga, Hafsa Mtassiwa (kulia) wakisoma maandishi mara baada ya kuzindua kituo cha upashanaji habari za kilimo na mifugo  kata ya Magoma Wilaya ya Korogwe  Vijijini leo.
Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa, Juma Khatib Chumu akipanda mti katika kituo cha mradi wa upandaji na utunzaji wa mazingira shule ya Sekondari ya Kwagunda kata ya Magoma  Korogwe  Vijijini Tanga  wakati wa mbio za mwenge Wilayani humo. Alieshika jembe ni  Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Hafsa Mtassiwa.
Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa, Juma Khatib Chumu, akimtishwa ndoo ya maji, Zubeda Abeid mkazi wa kijiji cha Nyuzi kata ya Magoma Wilaya ya Korogwe Vijijini wakati wa mbio za Mwenge uliokimbizwa Wilayani humo.
.Kiongozi wa mbia za mwenge wa uhuru ,Juma Chumu na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Tanga wakisoma maandishi mara baada ya kuzindua mradi wa maji kijiji cha Mnyuzi kata ya Magoma Tanga.
Rais Kikwete awasili Arusha kuongoza maadhimisho ya Siku ya Albino

Rais Kikwete awasili Arusha kuongoza maadhimisho ya Siku ya Albino

June 13, 2015

mail.google.comMwenyekiti wa Chama Cha Albino Tanzania,  Ernest Kimaya akimkaribisha Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA) muda mfupi baada ya kuwasili leo jioni. Rais Kikwete atakuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya kimataifa wa Albino itakayofanyika katika uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid.kushoto no Bwana Godson Molel mwenyekiti wa Chama cha Albino Mkoa wa Arusha.
(picha na Freddy Maro)

KINANA AMTEMBELEA MKULIMA WA SHAMBA LA KISASA LA NDIZI KIJIJI CHA KIKUKURU WILAYANI KYERWA KAGERA

June 13, 2015

????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa mkulima wa Kahawa na Ndizi Ndugu Eustace Kubalienda Kishunji ambaye ni mmiliki wa shamba la Ndizi,, Amesema shamba hilo  lina  miche 345 ambayo huvuna magunia 25 na ana shamba la migomba ambalo humpatia mavuno ya  mikungu  kwa mwezi 45.
Mzee Kishunji ambaye anaishi katika kijiji cha Kikukuru kata ya Mabira ameweza kusomesha watoto wawili katika vyuo vikuu vya Dar es salaam na Dodoma na amejenga nyumba ya kisasa yenye thamani kubwa ya fedha kutokana na kilimo bora cha kisasa.
Katibu Mkuu Kinana yuko ziarani katika mikoa ya Kagera , Geita na Mwanza akikagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Umeamka pamema leo.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitembelea shamba la ndizi akiongozana na Mkuu wa mkoa wa Kagera na  wakiongozwa na mzee 
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Baadhi ywa wananchi wakiwa katika mkutano huko Kikukuru
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua zahanati ya kata ya Kongorogo.
????????????????????????????????????
Wananchi wakimshangilia Kinana wakati ailpowasili katika kijiji cha Kongorogo
????????????????????????????????????
Wananchi wakimshangilia Kinana wakati ailpowasili katika kijiji cha Kongorogo
????????????????????????????????????
Hili ndilo Jengo lenyewe  linalojengwa mpakani hapo.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi hawapo pichani wakati alipotembelea soko la biashara la Kimataifa linalojengwa Kigorogoro Mpakani mwa Tanzania na Uganda 
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM akifungua maji katika bomba wakati alipotembelea mradi wa maji wa Kibingo
????????????????????????????????????
Wananchi wakimpokea kwa shangwe Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana  alipowasili kwenye uwanja wa Kibindo
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika kijiji cha Kibingo.
????????????????????????????????????
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Kibingo wilayani Kyerwa.
????????????????????????????????????
 Mkuu wa Mkoa wa Kagera akiwasalimu wananchi wa Isingiro, wilaya ya Kyerwa.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano wa hadhara.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kijiji cha Isingiro, wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimia wakazi wa kijiji cha Isingiro, wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimia wananchi wakati alipowasili kwenye mkutano  mjini Isingiro.
????????????????????????????????????
Baadhi ya akina mama waliokuwepo kwenye mkutano wakimshangilia Kianan.
????????????????????????????????????
Baadhi ya migomba katika shamba la mzee Ndugu Eustace Kubalienda Kishunji
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Isingiro
????????????????????????????????????
 Mbunge wa Kyerwa Bw.Eustace Katagira akihutubia wananchi wa Isingiro kwenye mkutano wa hadhara ambao Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alikuwa mgeni rasmi.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchikatika mkutano wa hadhara Isigiro
????????????????????????????????????
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Kagera Mh. John Mongela, kulia ni Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Kagera.