SERIKALI MKOANI SIMIYU YAOMBA KIKUNDI CHA ULINZI CHA KIJESHI KUIMARISHA ULINZI, KUWEZESHA UFUGAJI WA SAMAKI ZIWA VICTORIA

April 17, 2017
Na Stella Kalinga, Simiyu

Serikali mkoani Simiyu imeomba kuwepo kwa kikundi cha ulinzi cha kijeshi katika Wilaya ya Busega ili kusaidia mapambano dhidi ya vitendo vya uhalifu ikiwemo uvuvi haramu na kuwezesha ufugaji wa samaki ndani ya Ziwa Victoria kufanyika kwa usalama.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka wakati wa Hafla ya kumpongeza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi hapa nchini, Jenerali Venance Mabeyo iliyoandaliwa na ndugu zake kijijini kwao Yitimwila ‘A’ katika Kata ya Kiloleri Wilayani Busega.

“Tumepata changamoto nyingi sana kwenye ziwa, matukio mengi ya kihalifu liliwemo la uvuvi haramu , sisi kama mkoa tulikuja na wazo kwamba tungehitaji tupate ‘detouch’ moja eneo la Ziwa ili ukanda huu baada ya kufanya kazi kubwa ya kuchoma makokoro ya wananchi, tuwapeleke kwenye uvuvi wa kisasa hususani ufugaji wa samaki ziwani, jambo ambalo Mheshimiwa Rais analipa kipaumbele sana; na namna pekee ya kufanya ufugaji ule wa samaki ziwani, suala la ulinzi na usalama ni muhimu sana; ” alisema Mtaka.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo (katikati) akionesha silaha alizokabidhiwa na Wazee wa Busega kama ishara ya ushujaa kwake wakati wa hafla iliyoandaliwa na ndugu zake kijijini kwao Yitimwila A wilayani Busega kumpongeza kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Magufuli.

Aidha, Mtaka amesema pamoja na kufanya ufugaji wa samaki katika Ziwa Victoria, Serikali ya Mkoa imefanya makubaliano na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF kuwawezesha wananchi wa Busega kufanya kilimo cha Umwagiliaji kwa kutumia maji ya ziwa hilo ambayo ni ya uhakika.

“Tumeongea na NSSF kwa ajili ya kuanzisha mradi ambao hautazidi bilioni moja, tutaleta mbegu za aina ya nyanya na pilipili zinazotakiwa ili wananchi wa Busega wazalishe kwa wingi. Hatutakuwa tayari kuona wananchi wanalima nyanya na kuuza ndoo moja shilingi 500, tumepanga kuanzisha mradi wa kuzalisha ‘chill sauce’ na ‘tomato source’ .”alisema Mtaka.

Ameongeza kuwa Wataalam wa Wilaya na Mkoa kwa kushirikiana na Wataalam wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji , Kituo cha Utafiti wa Kilimo Ukiriguru wanafanya upembuzi yakinifu kuona namna miundombinu ya umwagiliaji itakavyojengwa ili kuwawezesha wananchi wa Busega kulima muda wote kupitia kilimo cha Umwagiliaji badala ya kutegemea mvua.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na viongozi na waalikwa katika hafla ya kumpongeza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Salvatory Mabeyo, kijijini kwao Yitimwila A wilayani Busega, kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Magufuli kwa nafasi hiyo.

Mtaka amesema Serikali mkoani Simiyu imedhamiria kuhakikisha katika kipindi cha miaka mitatu ijayo Mkoa hauingizi bidhaa kutoka mikoa mingine na badala yake wananchi wake watazalisha na kutumia bidhaa zao wenyewe, hivyo ameomba Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kuona namna ya kuweka vituo vya kuuza zana za kilimo katika maeneo ya kanda ya Ziwa ili wananchi wapate zana bora za kisasa zitakazowasaidia kulima kisasa.

Kwa upande wake Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi hapa nchini, Jenerali Venance Mabeyo amewataka wananchi wa Busega kubadili mtazamo wao na kutumia maji ya ziwa Victoria kwa manufaa yao kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji ili wasikumbwe na tatizo la upungufu wa chakula kunapotokea ukame.

Kuhusu suala la ulinzi katika Ziwa Victoria amesema ombi la Serikali ya Mkoa la kuwa na kikundi cha Ulinzi, viongozi watalitafakari kuona namna ya kulishughulikia na akaeleza kuwa tayari Jeshi limeweka kikundi kidogo cha kiulinzi kutoka Jeshi la wanamaji, lakini kutokana na ukubwa wa Ziwa Victoria kikundi hicho hakiwezi kuhimili kufanya doria maeneo yote na akaahidi kukiimarisha zaidi.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo, akizungumza na viongozi na waalikwa mbalimbali kijijini kwao Yitimwila A wilayani Busega , katika hafla ya kumpongeza kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Magufuli kwa nafasi hiyo.

Kajala aendesha droo ya kwanza ya Ijue Nguvu ya Buku ya Biko

April 17, 2017
Msanii nyota wa filamu Tanzania, Kajala Masanja, kulia akishiriki katika droo ya kwanza ya bahati nasibu ya Ijue Nguvu ya Buku inayoendeshwa na Kampuni ya Biko ambapo ilimpata mshindi wake wa kwanza wa Sh Milioni 10 ambaye ni Christopher Mgaya, Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, Juhudi Ngolo.



‘Nguvu ya Buku’ yampatia Sh Milioni 10 Christopher Mgaya

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
DROO ya kwanza ya kuwania Sh Milioni 10 iliyochezeshwa mwishoni mwa wiki imempatia donge nono mkazi wa Temeke, Christopher Mgaya na kuweka historia ya kuwa mtu wa kwanza kujinyakulia kitita hicho kutoka kwa mchezo wa bahati nasibu wa Biko.

Droo hiyo ilichezeshwa na msanii nyota wa filamu nchini Tanzania, Kajala Masanja akishirikiana na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Juhudi Ngolo.

Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Juhudi Ngolo kushoto akichezesha droo kumtafuta mshindi wa Sh Milioni 10, ambapo mkazi wa Temeke, Christopher Mgaya aliibuka na kitita hicho. Kulia ni msanii wa filamu, Kajala Masanja, akishuhudia.

Akizungumza katika droo hiyo, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema kwamba jumla ya washindi 2000 walipatikana katika zawadi mbalimbali, huku Mgaya yeye akiibuka kinara wa Sh Milioni 10.

Heaven alisema kwamba baada ya kupatikana kwa mteja huyo, taratibu za kumkabidhi hundi yake ya Sh Milioni 10 unaweka ili mteja huyo apate fedha zake haraka iwezekanavyo.

“Tumeanza vizuri kwa kufanikiwa kumpata mshindi wetu wa kwanza wa Sh Milioni 10 ambapo alicheza bahati nasibu yetu, huku yeye akifanikiwa kuibuka mshindi.
Droo hiyo ya kutafuta mshindi wa Sh Milioni 10 inaendelea
Droo inaendelea kutafuta mtu wa kunyakua Sh Milioni 10
Msanii Kajala Masanja akimpigia simu mshindi wa Sh Milioni 10, Christopher Mgaya jana jijini Dar es Salaam.

“Utaratibu ni ule ule kwasababu kila mtu anaweza kushinda kwa kuinguza muamala kwa Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money ambapo ataingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 kwenye kipengele cha lipa bili, huku pia akiingiza namba ya 2456 kama namba ya kumbukumbu ambapo Sh 1000 atakayocheza itampatia tiketi mbili za kushinda hapo hapo au tiketi ya kumuingiza kwenye droo ya kuwania Sh Milioni 10”, Alisema Heaven.

Naye Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Juhudi Ngolo alisema kwamba wameikagua kampuni ya Biko na kuvutiwa na utaratbu wa mchezo wao, hali inayoonyesha kwamba Watanzania wapo salama katika kucheza mchezo huo.

“Nimekuwa mwakilishi wa kwanza kutoka Bodi kusimamia wakati wa kumtafuta mshindi wa Sh Milioni 10 ambapo naamini Watanzania wataamua kucheza zaidi,” Alisema Ngolo.

Naye Mgaya mshindi wa bahati nasibu hiyo ya Sh Milioni 10 alisema haamini kwamba ameshinda Sh Milioni 10 hadi hapo atakapokabidhiwa kitita chake ingawa kimemfanya avuje jasho wakati anatangazwa yeye ndio mshindi.

“Nimefurahishwa kushinda kwangu mshiko wa Biko wa Sh Milioni 10 ambapo siamini kama nimeshinda zawadi hiyo kubwa kutoka kwenye Kampuni ya biko,” Alisema Mgaya.

Kwa mujibu wa Biko, mbali na ushindi wa Sh 5000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni Moja zinazolipwa kila siku na papo kwa hapo kwenye simu za wateja, ushindi wa Sh Milioni 10 utapatikana kila mwisho wa wiki kwa kuchezesha droo inayokutanisha washiriki wote wa siku za wiki.