WAKURUGENZI WATENDAJI WA HALMASHAURI, MIJI, MANISPAA NA MAJIJI 185 WALA VIAPO VYA MAADILI LEO IKULU

July 12, 2016


Sehemu ya Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, Miji, Manidpaa na Majiji 185 wakipata maelezo ya awali kabla ya kula kiapo cha maadili ya viongozi leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, Miji, Manidpaa na Majiji 185 kabla ya hawajakula kiapo cha maadili ya viongozi leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Mkutano ulioitishwa  na Rais John Magufuli kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote za wilaya na baadhi ya Wakuu wa  wilaya  ikulu jijini Dar es salaam Julai 12, 2016.

PROF. JUMANNE MAGHEMBE AKUTANA NA BALOZI WA UJERUMANI HAPA LEO

July 12, 2016


Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akimkaribisha Balozi wa Ujerumani hapa nchini, Mhe. Egon Konchanke alipomtembelea jana tarehe 11 Julai, 2016 ofisini kwake, Mpingo House, Jijini Dar es Salaam kujadili mambo mbalimbali yanayohusu sekta ya Maliasili nchini.
Waziri Maghembe (kulia) akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Balozi Konchanke (kushoto).
Balozi Konchanke (kushoto) akimueleza jambo Prof. Maghembe (kulia) katika mazungumzo hayo.
Balozi Konchanke (kushoto) akimuonesha Waziri Maghembe (kulia) ramani ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi ambayo Balozi huyo ameahidi kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza utalii wake kwa pamoja na ule wa Mkoa wa Kigoma (Hifadhi ya Mahale)
Waziri Maghembe (kulia) akizungumza katika kikao hicho.

KIWANDA CHA TWIGA CEMENT CHA WAZO CHAPEWA MWEZI MMOJA KUREKEBISHA MFUMO WA UTOAJI TAKA ILI KUNUSURU MAZINGIRA.

July 12, 2016

              
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina akizungumza na Uongozi wa kiwanda cha twiga cement,pamoja na Maafisa kutoka Baraza la Usimamizi wa Mazingira(NEMC)alipofanya ziara mapema hii leo.           



Naibu waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh,luhaga Mpina (katikati)na Meneja mazingira kiwandani hapo bw. Richard Magoda akitembezwa ndani ya kiwanda  baada ya kupata malalamiko ya uchafuzi wa mazingira  kutoka kwa wananchi.          

Baadhi ya Sehemu za Uzalishaji ndani kiwanda hicho ambayo yanalalamikiwa na Wanachi kwa Uzalishji vumbi linalowaathiri wananchi.
EVELYN MKOKOI DAR ES SALAAM

Kiwanda cha kutengeneza cement cha Twiga cement cha wazo jijini Dar  Es Saalaam kimepewa muda wa mwezi mmoja kurekebisha mfumo wao wa utoaji taka ili kunusuru uharibifu wa mazingira na maisha viumbe hai.

Hayo yamesemwa Leo jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina katika ziara yake ya kutembelea kiwanda hicho.

Mhe. Mpina amekitaka kiwanda hicho  kushirikiana na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC kupima vumbi litokanalo na uzalishaji kiwandani.. ili kuona kama ni la kiwango ambacho si hatarishi kwa mazingira na viumbe hai vinavyozunguka maeneo hayo.

Maagizo hayo ya Naibu waziri Mpina yametokana na malalamiko ya wananchi wa maeneo jirani na kiwanda hicho yanayoeleza kuwa kiwanda hakina mahusiano mazuri na wakazi au majirani wa maeneo hayo.

Aidha amemtaka muwekezaji huyo kuimarisha mahusiano baina ya kiwanda hicho na wananchi na kufanyia marekebisho kasoro zilizoonekana kujitokeza kiwandani hapo na kuwaasa wawekezaji wa kiwanda hicho kufanya kazi pamoja na kuheshimu sheria hususan za mazingira.

Kwa upande wa Baraza la Taifa na Usimamizi wa Mazingira Nemc kumeonekana kuwa na uzembe katika ufuatiliazi wa utekelezaji wa sheria za mazingira hasa kiwandani hapo, baada ya mkurugenzi wa uzingatiaji na utekelezaji wa baraza hilo Bi Ruth Lugwisha kushindwa kujibu swali aliloulizwa na Naibu waziri Mpina kuwa ni lini Mara ya mwisho baraza hilo lilijiridhisha kwa kuchukua vumbi kiwandani hapo na kulipima ili kujua lina athari kwa kiasi gani kwa mazingira na viumbe hai.

Kwa upande wake Meneja wa Mazingira wa kiwanda hicho Bw. Bw. Richard Magoda amejitetea kuwa kiwanda kina mahusiano mazuri na wanachi kwani kimeweza kutoa misaada katika baadhi ya maeneo ikiwa ni pamoja na vyandarua na kuchonga barabara za baadhi ya mitaa.

Wakati huo huo viongozi wa serikali za  mitaa Bw. Gration Mbelwa ambaye ni mwenyekiti wa kata ya madale na  Atilio Maginga mwenyetiki wa serikali ya mtaa wa mivumoni..wametofatofautiana kwa  kusema kwamba kiwanda kina mashirikiano mazuri na wananchi, wakati mwenyekiti wa kata ya madale akiwakilisha wanachi kwa kulalamika kuwa kiwanda hakina mahusiano mazuri na wananchi..

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, ANGELINE MABULA AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA UENDELEZAJI MILKI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

July 12, 2016
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabula (kushoto), akihutubia wakati akifungua mkutano wa wadau wa uendelezaji milki uliofanyika Makao Makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Upanga jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Usimamizi Milki, Hamad Abdallah, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu, Mkurugenzi wa Nyumba wa wizara hiyo, Charles Mafuru na Mkurugenzi wa Fedha wa NHC, Felix Maaly. Mkutano huo uliandaliwa na NHC.
 Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu, akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabula kuufungua.
 Mwonekano wa meza kuu wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.
Wadau wa uendelezaji milki wakiwa kwenye mkutano huo.

Wadau wa uendelezaji milki wakiwa kwenye mkutano huo.


Taswira ya chumba cha mkutano huo.
Mwonekano wa chumba cha mkutano katika ufunguzi wa mkutano huo.