Na Nestory Ngwega,Tanga
MKUU wa wilaya ya Tanga Halima Dendego amesema,serikali itaendelea kuunga mkono mikutano ya dini inayohubiri amani na upendo ili kujenga maadili mema ya ndani ya jamii na kudumisha amani.
Aliyasema hayo jana wakati alipokuwa akifungua mkutano wa neno la Mungu katika viwana vya Usagara jijini Tanga uliondaliwa na umoa wa makanisa ya kipentekoste.
Alisema kuwa amani ni kipaumbele cha kwanza katika nchi na kwamba serikali itashirikiana na wapenda amani wote.
Aliwapongeza waumini wa kikristo kwa kuonyesha mshikamano na kutunza amani iliyopo hivyo akawataka wananchi wote kwa ujumla waishi kwa upendo ili kudumisha amani.
Kwa upande wake muhubiri wa kimataifa Johannes Amritzer aliishukuru serikali na wananchi wa Tanga kwa ujumla kwa ushirikino na kuwapokea kwa upendo.
Alisema upendo aliouona ni ishara ya wazi kuwa wananchi wa Tanzania wanaishi kwa umoja na upendo na kwamba yeye ataendelea kuhubiri amani ya rohoni ambayo ndiyo inayozaa amani ya nje kwa kila mwanadamu.
Akimkaribisha mkuu wa wilaya,Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mkutano huo Askofu Agostino Dedu alisema kuwa mkutano huo umekuwa wa baraka kubwa kiroho na kiuchumi pia ikizingatiwa kuwa wageni wapatao 150 kutoka Ulaya na Marekani wapo Jiini Tanga kuhudhuria mkutano huo na hivyo uongeza pato kwa wafanyabishara wa mahoteli,vyakula na bidhaa zingine.
Mwisho.
MKUU wa wilaya ya Tanga Halima Dendego amesema,serikali itaendelea kuunga mkono mikutano ya dini inayohubiri amani na upendo ili kujenga maadili mema ya ndani ya jamii na kudumisha amani.
Aliyasema hayo jana wakati alipokuwa akifungua mkutano wa neno la Mungu katika viwana vya Usagara jijini Tanga uliondaliwa na umoa wa makanisa ya kipentekoste.
Alisema kuwa amani ni kipaumbele cha kwanza katika nchi na kwamba serikali itashirikiana na wapenda amani wote.
Aliwapongeza waumini wa kikristo kwa kuonyesha mshikamano na kutunza amani iliyopo hivyo akawataka wananchi wote kwa ujumla waishi kwa upendo ili kudumisha amani.
Kwa upande wake muhubiri wa kimataifa Johannes Amritzer aliishukuru serikali na wananchi wa Tanga kwa ujumla kwa ushirikino na kuwapokea kwa upendo.
Alisema upendo aliouona ni ishara ya wazi kuwa wananchi wa Tanzania wanaishi kwa umoja na upendo na kwamba yeye ataendelea kuhubiri amani ya rohoni ambayo ndiyo inayozaa amani ya nje kwa kila mwanadamu.
Akimkaribisha mkuu wa wilaya,Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mkutano huo Askofu Agostino Dedu alisema kuwa mkutano huo umekuwa wa baraka kubwa kiroho na kiuchumi pia ikizingatiwa kuwa wageni wapatao 150 kutoka Ulaya na Marekani wapo Jiini Tanga kuhudhuria mkutano huo na hivyo uongeza pato kwa wafanyabishara wa mahoteli,vyakula na bidhaa zingine.
Mwisho.