MKWASA AWATEMA MWADINI, BANDA NA TSHABALALA STARS KILA MMOJA NA SABABU ZAKE, WENGINE WAGONJWA

July 02, 2015

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
KOCHA wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa amewaengua wachezaji watano katika kikosi chake kinachoondoka leo jioni kwenda Kampala kumenyana na wenyeji, Uganda mwishoni mwa wiki. 
Stars itakuwa mgeni wa Korongo wa Uganda Jumamosi Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala katika mchezo wa marudiano Raundi ya Kwanza kuwania tiketi ya kucheza michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) 2016 Rwanda.
Na Mkwasa amewaengua beki Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ na kiungo Abdi Banda wote wa Simba SC kwa sababu ni majeruhi, wakati Samuel Kamuntu wa JKT Ruvu na Andrew Vincent wa Mtibwa Sugar wameachwa kwa sababu za kiufundi na Mwadini Ally wa Azam FC ni mgonjwa.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Mkwasa (kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari leo mchana ofisi za TFF, Uwanja wa Karume
Wachezaji Said Ndemla (kulia) na Simon Msuva (kushoto) wakiwa kwenye basi lao tayari kwa safari ya Uwanja wa Ndege

Mkwasa ameteua wachezaji 20 wanaoondoka jioni ya leo kwenda Kampala, ambao ni makipa; Mudathir Khamis (KMKM) na Ally Mustafa ‘Barthez’ (Yanga), mabeki ni Juma Abdul (Yanga), Shomary Kapombe (Azam), Michael Aidan (Ruvu Shooting), Mwinyi Hajji Mngwali (KMKM), Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (Yanga SC), Kevin Yondan (Yanga SC) na Hassan Isihaka (Simba SC).
Viungo ni Mudathir Yahya (Azam FC), Salum Telelea (Yanga SC), Frank Domayo (Azam FC), Simon Msuva (Yanga SC), Said Ndemla (Simba SC), Ramadhani Singano ‘Messi’ (Simba SC) na Deus Kaseke (Mbeya City).
Washambuliaji ni John Bocco (Azam FC), Atupele Green (Kagera Sugar), Rashid Mandawa (Kagera Sugar) na Ame Ali (Mtibwa Sugar).
Mara baada ya kuteuliwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kurithi mikoba ya Mholanzi, Mart Nooij aliyefukuzwa mwishoni mwa wiki kufuatia kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa Uganda katika mchezo wa kwanza na Uganda, Mkwasa alitaja kikosi wachezaji 26 na kuwa nacho kambini kwa wiki moja hoteli ya Kiromo, Bagamoyo huku mazoezi akifanya uwanja wa Boko Veterani, Dar es Salaam.
Mbali na wachezaji hao, benchi la Ufundi litaongozwa na Mkwasa, Mshauri wake wa Ufundi, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’, Msaidizi wake Hemed Morocco, kocha wa makipa, Manyika Peter, Mtunza Vifaa Hussein Swedi ‘Gaga’, Meneja Omar Kapilima pamoja na Mratibu Msafiri Mgoyi. Stars inatakiwa kushinda 4-0 Jumamosi ili kusonga mbele CHAN.
BOSS WA UN, ALVARO RODRIGUEZ ATEMBELEA SABASABA, ASEMA MAONYESHO NI FURSA YA KUJIFUNZA

BOSS WA UN, ALVARO RODRIGUEZ ATEMBELEA SABASABA, ASEMA MAONYESHO NI FURSA YA KUJIFUNZA

July 02, 2015
IMG_5941
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Jacqueline Mneney Maleko (wa tatu kushoto) akiongozana na Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) mara baada ya kuwasili katika viwanja vya maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara 'Sabasaba', barabara ya Kilwa, jijini Dar.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).
IMG_5945
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko (wa pili kushoto) akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez wakati wakielekea katika banda la Shirika la Umoja wa Mataifa lilipo Karume Hall mara tu baada ya kuwasili.
Na Modewjiblog team, Sabasaba
Mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea banda la Umoja wa Mataifa leo katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara Sabasaba amesema Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika utekelezaji wa miradi na mikakati ya Umoja wa Mataifa miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki.
Ameongeza kuwa dunia sasa imekuwa kijiji kimoja na Umoja wa Mataifa umekuwepo Tanzania hata kabla ya uhuru, hivyo unakusudia kuendelea kuwepo kushirikiana na watanzania katika kutatua matatizo kwenye Nyanja mbalimbali.
Bw. Alvaro amewataka watanzania kusherehekea pamoja miaka 78 ya Umoja hapa nchini kwa kutoa maoni mbali mbali na kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo.
Amesema kwa pamoja tunahitaji kuzungumzia usawa wa kijinsia, masuala ya kisiasa, mabadiliko ya tabia nchi na mambo ya kiuchumi kwa ajili ya ustawi wa taifa.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko, ameushukuru Umoja wa Mataifa kwa kufanya juhudi za kusaidia vijana kuanzia ngazi za chini kabisa na kuwawezesha kuwa wajasiriamali.
Amesema kitendo cha Umoja huo kushiriki katika maonyesho ya Sabasaba sambamba na kijana Amos Mtambala waliyemuwezesha kwa kumpatia mafunzo ya sanaa za uchoraji kumeleta hamasa kubwa miongoni mwa vijana wasio na ajira nchini.
IMG_6027
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro Rodriguez akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye banda la Shirika la Umoja wa Mataifa katika viwanja vya maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara 'Sabasaba', barabara ya Kilwa, jijini Dar.
IMG_6032
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko akisaini kitabu cha wageni kwenye banda la Umoja wa Mataifa.
IMG_5959
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu, akitoa maelezo jinsi wanavyoelimisha wananchi kuhusiana shughuli mbalimbali za Umoja wa Mataifa nchini sambamba na malengo ya millenia yanayofikia kileleni kwa Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez aliyeambata na mwenyeji wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko walipotembelea banda hilo kwenye maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara 'Sabasaba', katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
IMG_5962
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akielezea maeneo ya Program mbalimbali za UNDAP yaliyofanikiwa nchini Tanzania kwa Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kulia) aliyeambata na mwenyeji wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko.
IMG_5965
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akikabidhi taarifa ya mwaka ya UNDAP kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko (katikati) aliyefuatana na Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kulia) walipotembelea banda la Shirika la Umoja wa Mataifa lililopo Karume Hall.
IMG_5973
Mkurugenzi na Meneja mradi wa TUBEGA ART ambaye ni mtaalamu wa sanaa za uchoraji, Amos Mtambala, akitoa maelezo jinsi alivyowezeshwa kupitia Shirika la Kazi Duniani (ILO) kupata elimu inayomwezesha kuwa mjasiriamali kwa kuuza michoro hiyo ndani ya banda la Umoja wa Mataifa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez alipotembelea banda la Shirika la Umoja wa Mataifa lililopo Karume Hall ndani ya viwanja vya maonyesho ya 39 ya biashara ya kimataifa maarufu kama “Sabasaba”.
IMG_5981
Afisa Mawasiliano wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) nchini, Magnus Minja akifafanua jambo kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez kuhusiana na program ya kazi njenje ya mradi wa kufundisha vijana katika shughuli za ujasiriamali inayoratibiwa na Shirika la Kazi Duniani (ILO) ambapo kijana Amos iliweze kumuinua na kujiajiri kupitia sanaa ya uchoraji.
IMG_5995
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko, akionyesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) moja ya karatasi inayotoa maelezo ya jinsi ya Watanzania wanavyoweza kushiriki kutoa maoni mbalimbali juu ya utendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kwa kutuma SMS ambayo ni bure bila malipo yoyote na moja kwa moja kumfikia Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini Alvaro Rodriguez.
Jinsi ya kutuma ujumbe mfupi wa maandishi (SMS), kwa kuandika neno UN au UMOJA WA MATAIFA ambapo kwa watumiaji wa mtandao wa Airtel watatuma ujumbe wao kwenda namba 15453, kwa watumiaji wa mtandao wa Tigo wanatuma kwenda 15055 au 15453 na kwa Vodacom ni namba 15055.
Ambapo pia njia nyingine ya kuwasilisha maoni ya moja kwa moja ni kupitia mtandao wa (Online) kwa kubofya link hii http://gpl.cc/UN2
IMG_6021
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko akizungumza na waaandishi wa habari katika banda la Shirika la Umoja wa Mataifa ambao wanashiriki maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara 'Sabasaba', katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, vilivyopo barabara ya Kilwa, jijini Dar. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro Rodriguez.
IMG_6038
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro Rodriguez akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko mfuko wenye machapisho na vijarida mbalimbali vya Umoja wa Mataifa.
IMG_6467
Afisa Utawala wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Suleiman Magoma (wa pili kushoto) akiuliza swali kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto) wakati alipotembelea banda la Umoja wa Mataifa lililopo Karume Hall katika maonyesho ya Sabasaba. Kulia ni Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama na Wa pili kulia ni Mchumi wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Vainess Molle.
IMG_6476
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro Rodriguez akijibu swali la Bw. Suleiman.
IMG_6494
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama akionyesha namna ya kutoa maoni ya utendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa Tanzania kwa njia ya SMS ambayo ni bure kwa mitandao yote ya simu za mkononi nchini kwa wadau waliotembela banda la UN Tanzania.
IMG_6435
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro Rodriguez ajibu maswali mbalimbali yalitumwa kwa njia ya mtandao na wananchi katika banda la Umoja wa Mataifa maonyesho ya Sabasaba.
IMG_5997
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Nchini, Alvaro Rodriguez na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wanaotoa huduma katika banda la Umoja wa Mataifa maonyesho ya Sabasaba.
IMG_6456
Baadhi ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa katika picha ya pamoja na Mkuu wa UN Tanzania.
ELUMELU CALLS FOR AN END TO ENERGY POVERTY

ELUMELU CALLS FOR AN END TO ENERGY POVERTY

July 02, 2015
Pix 1
L-R: Former president of Ghana John Kufuor; President of Cote D'Ivoire Alassane Ouattara, Co-Chair of the Africa Energy Leaders Group (AELG); Tony O. Elumelu, Chairman of Heirs Holdings and Co-Chair of the AELG; Vice President of Nigeria Yemi Osinbajo during the inaugural meeting of the AELG held in Abidjan yesterday to discuss regional solutions to the electricity deficit in Africa.
Pix 2
L-R: Former presidents of Nigeria and Ghana Olusegun Obasanjo; John Kufuor; President of Cote D'Ivoire Alassane Ouattara, Co-Chair of the Africa Energy Leaders Group (AELG); Tony O. Elumelu, Chairman of Heirs Holdings and Co-Chair of the AELG); Vice President of Nigeria Yemi Osinbajo during the inaugural meeting of the AELG held in Abidjan yesterday to discuss regional solutions to the electricity deficit in Africa.
Pix 3
Energy For ALL: l-r. Vice President of Nigeria Yemi Osinbajo and Tony O. Elumelu, Chairman of Heirs Holdings and Co-Chair of the Africa Energy Leaders Group (AELG) during the inaugural meeting of the AELG held in Abidjan, Cote D'Ivoire to discuss regional solutions to addressing the electricity deficit in Africa
Pix 4
Energy For ALL: l-r. Vice President of Nigeria Yemi Osinbajo and Tony O. Elumelu, Chairman of Heirs Holdings and Co-Chair of the Africa Energy Leaders Group (AELG) during the inaugural meeting of the AELG held in Abidjan, Cote D'Ivoire to discuss regional solutions to addressing the electricity deficit in Africa.
Pix 5
L-R: Co-Chair of the Africa Energy Leaders Group (AELG) and Chairman Heirs Holdings, Tony Elumelu, Former presidents of Nigeria and Ghana Olusegun Obasanjo; John Kufuor; President of Cote D'Ivoire Alassane Ouattara, Co-Chair of the AELG; Vice President of Nigeria Yemi Osinbajo and other African leaders during the inaugural meeting of the AELG held in Abidjan yesterday to discuss regional solutions to the electricity deficit in Africa.
“Providing access to electricity for schools, hospitals, businesses and industries is the single most impactful intervention that can be made to transform the continent. It has tremendous implications for job creation, health, food security, education, technological advancement and overall economic development.” Mr. Tony Elumelu said today in Abidjan.
African businessman and philanthropist Tony Elumelu who is the Chairman of Heirs Holdings and Founder of the Tony Elumelu Foundation joined African economic and political leaders today in Abidjan to call for an end to energy poverty on the continent. The leaders came together in Abidjan under the umbrella of the African Energy Leaders Group (AELG).
The AELG was launched during the 2015 World Economic Forum in Davos, Switzerland. The group brings together political and business leaders at the highest level to drive the reforms and investment needed to end energy poverty and to ensure sustainable fuel supplies on the continent.
Mr. Elumelu is a founding partner and Co-chair of the AELG. Other founding partners of AELG include Ivoirian President Allasane Ouattara; Ghanaian President John Mahama; President, African Development Bank Dr Donald Kaberuka; President & CEO, The Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote; President ECOWAS Commission, Kadre Desire Ouedraogo; and President UEMOA Cheikhe Hadjibou Soumare.
Providing access for all Africans to reliable, affordable energy services and efficient appliances by 2030 is a key goal of AELG. The AELG objective of ensuring universal access to modern energy is in line with those of the United Nations Sustainable Energy for All (SE4All) initiative run by the UN Secretary General's Special Representative Kandeh Yumkella, one of the champions of the AELG. Mr. Elumelu pledged to support the work of AELG.
“I am making a pledge to provide $150,000 over the next three years to support the operations of the AELG secretariat,” he said. “I want to call on the governments of the member states of the ECOWAS region, and AELG members and partners to also step up with significant multi-year commitments to sustain the organization.” Following Mr Elumelu's lead, pop superstar, Akon, who was also in attendance at the event to promote his Lighting Africa Initiative, pledged $200,000 to support the work of the AELG secretariat.
On the closing panel for the AELG meeting where Elumelu was joined by Akon, former presidents Obasanjo and Kufuor, Vice President Osinbajo, and the Prime Ministers of Cote D'Ivoire, Mali, Benin, Togo, and Niger, he challenged the public sector leaders to follow the lessons learned from the democratization of the telecoms sector to unlock growth in the power sector.
In 2013, Tony Elumelu committed to investing $2.5 billion in the power sector in Africa through President Obama's Power Africa Initiative. Transcorp Plc, Chaired by Elumelu, acquired the largest gas powered generating plant in Nigeria, located in Ughelli, Delta State in late 2013. By the end of this year, the Transcorp Ughelli plant will be generating 1,000 MW and the company is in discussions with GE to add an additional 1,000 MW soon after.
MRATIBU MKAZI WA UMOJA WA MATAIFA TANZANIA ATEMBELEA BANDA LA MODEWJIBLOG MAONYESHO YA SABASABA LEO

MRATIBU MKAZI WA UMOJA WA MATAIFA TANZANIA ATEMBELEA BANDA LA MODEWJIBLOG MAONYESHO YA SABASABA LEO

July 02, 2015
IMG_6278
Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akisalimiana na Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale alipotembelea katika banda la mtandao huo ambao mwaka huu mwezi Septemba unatimiza miaka 7 tangu kuanzishwa ambapo wametumia fursa ya maonyesho ya saba saba kukutana na wadau mbalimbali wanaotumia mtandao huo kupata habari mbalimbali sambamba na kubadilishana mawazo na ushauri wa maboresho ya kazi. Kushoto aliyefuatana naye ni Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu. Kulia ni mdau wa karibu na mshauri wa mtandao wa habari Modewjiblog, Lemmy Hipolite.
IMG_6282
Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, aliyeambatana na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akiangalia moja ya documentary ya TV katika banda hilo minayoonyesha wadau mbalimbali wanaotumia mtandao huu ambao walipata kuhojiwa.
DSC_0646
Mmoja wa wadau wa Modewjiblog, Rehema Pascal akiuzungumzia mtandao wa habari wa Modewjiblog alipotembelewa ofisini kwake wakati wa kurekodi 'documentary' hiyo.
IMG_6284
Pichani juu na chini ni Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akiangalia kazi mbalimbali zinazofanywa kwenye mtandao wa habari wa Modewjiblog alipotembelea banda hilo katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara Sabasaba yanaoendelea kurindima katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
IMG_6297 IMG_6304
Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akiondoka mara baada ya kutembelea banda la Modewjiblog, lililopo katika banda la MeTL Group.
IMG_5671
Meneja mwendeshaji wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Zainul Mzige akitoa maelezo juu ya mtandao huo unavyofanya kazi zake ambapo aliwataka vijana hao kutembelea mara kwa mara ikiwemo kufaidika na nafasi za ajira zinazotolewa kwenye mtandao huo zikiwemo habari za kitaifa na kimataifa, burudani, michezo, utamaduni n.k.
IMG_5688
Meneja mwendeshaji wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Zainul Mzige (kulia) na Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale wakikabidhi zawadi za fulana maalum kwa wadau waliotembelea katika banda la mtandao huo katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara Sabasaba yanaoendelea kurindima katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
IMG_5508
Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale akikabidhi zawadi ya kofia na fulana kwa Mmiliki wa blog ya Kajunason blog, Cathbert Kajuna (kulia) aliyetembelea banda la mtandao huo.
DSC_1164
Wadau wakiendelea kumiminika kwenye banda la Modewjiblog katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara Sabasaba yanaoendelea kurindima katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
DSC_0795
Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale akikabidhi zawadi ya fulana na kofia kwa Mwandishi wa Michuzi blog, Chalila Kibuda aliyembelea banda hilo.
DSC_1277
Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale (kulia) akitoa maelezo ya utofauti wa habari za kwenye magazeti na blog kwa mmoja wa wadau anayesoma habari mbalimbali katika mtandao huo, Peter Chilumba.