TAASISI YA BRIEN HOLDEN KUZINDUA HUDUMA YA UPIMAJI MACHO NA UTOAJI MIWANI KWA GHARAMA NAFUU

April 03, 2014

 
Ofisa Mkazi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Brien Holden Vision, Eden Mashayo akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam jana kuhisina na uzinduzi wa upimaji macho utakao fanyika Dar es Slaam free market mkabala na kituo cha DSTV , Kinondoni jijini Dr es Salaam. Kushoto ni Mratibu mradi huo Violet Shirima.
 Ofisa Mkazi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Brien Holden Vision, Eden Mashayo akionesha miwani itakayozinduliwa.
********
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa utoaji wa huduma ya macho bure, itakayofanyika Dar es Slaam free market mkabala na kituo cha DSTV , Kinondoni jijini Dr es Salaam.
April 03, 2014

 Mgambo wakivunja  vibanda vilivyopo eneo la posta
 Pahhh pahhh mgambo akifanya kazi yake

MCHEZAJI WA ZAMALEK AFARIKI DUNIA, RAIS CAF ASHIRIKI MSIBA

April 03, 2014

Na Salum Esry, Cairo
RAIS wa Shirikisho la Soka (CAF), Issa Hayatou ameelezea mshituko wake kufuatia kifo cha kiungo wa zamani wa Misri, Taha Basry.
Basry, gwiji wa Zamalek amefariki dunia jana Aprili 2, mwaka 2014 katika hospitali ya Cairo alikokuwa amelazwa kwa matibabu akiwa na umri wa miaka 68.
Pumzika kwa amani; Taha Basry enzi za uhai wake akiwa kocha

“Kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya CAF na mimi mwenyewe, natoa salamu zangu za rambirambi kwa Chama cha Soka Misri (EFA) na familia ya marehemu. Fikra zangu zipo nao katika wakati huu mgumu,” amesema Hayatou.
April 03, 2014

FIFA YAMUAMBIA MALINZI NA WENZAKE; TUNATAKA MCHUKUE KOMBE LA DUNIA HARAKA

Na Mwandishi Wetu, Johannesburg 
KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Jerome Valcke amezungumzia uwekezaji wa FIFA kwa CAF na majukumu ya bodi hiyo ya soka kukuza mpira barani Afrika na kusema kwamba anataka kuona bara hilo linatwaa Kombe la Dunia haraka.
“Shirikisho la Soka Afrika ni mwanachama muhimu sana wa FIFA na tutafanya kila kitu kuwasaidia wanachama wa CAF. Tunataka nchi ndani ya CAF kuzigeuza timu kuwa za kulipwa, kuweka mikakati mizuri na kuwa na mipango mizuri ya uwekezaji katika soka ya vijana,” amesema Valcke leo katika ufunguzi wa semina ya siku tatu ya CAF na FIFA kwenye ukumbi wa hoteli ya Sandton Convention Centre. 

Ufunguzi semina ya FIFA na CAF nchini Afrika Kusini leo