COASTAL UNION YAWAFUNDISHA SOKA NDANDA,YAWAFUNGA BAO 2-1 MKWAKWANI LEO

October 04, 2014
KIKOSI CHA COASTAL UNION KILICHOIPIGA NDANDA SC MABAO 2-1 UWANJA WA CCM MKWAKWANI.




TIMU ya Coastal Union ya Tanga leo imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ndanda SC ya Mtwara katika pambano la Ligi kuu soka Tanzania bara .

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani ambap ulikuwa na kasi kutokana na timu zote ksuhambuliana kwa zamu.

Mabao ya Coastal yalifungwa na Joseph Mahundi akimaliza pasi ya Hamisi Mbwana "Kibacha" na bao la pili likifungwa na Hussein Sued aliyemaliza krosi ya Razack Khafani.
  
Bao la kufutia machozi la Ndanda FC lilifungwa dakika ya 57 kupitia Nassoro Kapamba kwa njia ya penati iliyotokana na mchezaji wa Coastal Union Sabri Rashid kuunawa mpira eneo la hatari na mwamuzi wa mchezo huo Amoni Paul kutoka Mara kuamuru ipigwe penati hiyo.