BUNGE LAPITISHA SHERIA YA KUANZISHWA BARAZA LA VIJANA
Na Anitha Jonas – MAELEZO,Dodoma.
…………………………………………………….
Serikali inatarajia kuanzisha Baraza la Vijana litakalo kuwa chombo cha vijana kitakacho waunganisha Kitaifa bila kujali itikadi zao za Kisiasa,Imani zao za Kidini wala tofauti zao za Rangi,hayo yamesemwa na Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Mhe.Fenella Mukangara alipokuwa akisoma Muswada wa Sheria ya Baraza la Vijana Tanzania Bungeni Mjini Dodoma.
Mheshimiwa Mukangara aliendelea kusema Baraza hilo litaisaidia Serikali kuweza kuwafikia vijana kwa urahisi na kusikiliza shida zao pamoja na kutoa ufumbuzi wa hoja mbalimbali za vijana.Hata hivyo chimbuko la Muswada huo ni katika kutekeleza Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya 2007,Ibara ya 3 Sehemu ndogo ya 11 inayosema kwa uwazi Serikali itawezesha kuundwa kwa Baraza Baraza la Vijana na kuanzisha mfumo wa kisheria ili kuliwezesha kufanya kazi.
“Madhumuni ya Muswada huu ni Kutunga Sheria ya Baraza la Vijana Tanzania(The Youth Council of Tanzania 2015) ili kuwa na chombo cha Kitaifa cha kuwewezesha vijana kujadili masuala yao,kutambua majukumu yao,kukuza maadili mema,kukuza moyo wa umoja ,uzalendo,uwajibikaji na kujitolea kwa malengo chanya miongoni mwao katika nchi yetu,”alisema Mhe.Mukangara.
Mbali na hayo katika sehemu ya pili kifungu cha 4-15 cha Muswada huo unaeleza juu ya masharti mbalimbali kuhusu Uanzishwaji,Uanachama,Muundo na kazi za Baraza.Pia sehemu hii imefafanua Mamlaka ya Baraza na vyombo vya utendaji katika ngazi ya Taifa,Mkoa na Wilaya.
Aidha,kwa upande wa maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii yaliyosomwa na Mwenyekiti wake Said Mtanda aliishauri Serikali katika kifungu cha 4(3)Kisomeke Uanachama utakuwa na uwazi na hiari kwa kijana yeyote mwenye umri wa kuanzia miaka 15 mpaka 35.Pia kifungu cha 4(4) imeeleza kuwa baraza halitakuwa kisiasa liongezwe neno halitakuwa na Itikadi za Kidini.
Katika kipindi cha majadiliao ya Muswada huo naye Mhe.Kuluthum Mchuchuri (Mb) Viti Maalum CUF aliipongeza Serikali kwa mchakato wake mzuri wa kuandaa Baraza la Vijana litakalo saidia vijana kujadili matatizo yao na kuyawasilisha Serikali kwa kupatiwa ufumbuzi kwa urahisi,pia ameishauri Serikali katika suala la wajumbe uwawakilishi waanze kuanzia ngazi ya Kata na Serikali pia iweke wazi ni kwa utaratibu gani wawakilishi hao watapatikana.
Naye Mhe.Magret Sitta Mbunge wa Viti Maalum CCM aliiomba Serikali kuandaa ziara kwenda kuangalia mabaraza ya Vijana katika nchi za wenzetu yanafanyaje kazi na kujifunza,pia aliendelea kuiomba Serikali itoe mafunzo mbalimbali ya ufundi kwa kushirikia na taasisi ya Veta na Vyuo vya Wananchi ilikuwapatia elimu itakayo wasaidia vijana kujikwamua kiuchumi na kupunguza idadi ya vijana wa vijiweni.
Pamoja na hayo naye Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR) Mhe.Moses Machali alishauri Serikali Kuanzisha asasi moja ambayo vijana watakayo jiunga huko ili kudhibiti uanzishwaji wa asasi bandia kwa watu wenye nia ya kujinufaisha,pia aliipongeza Serikali kwa kuleta Muswada huo kwani unamanufaa Makubwa kwa vijana.
Aidha,mbali ya kuwepo na marekebisho mbalimbali ya Muswada huo Serikali iliyapokea maombi ya Suala la Baraza hilo kuanzia katika ngazi ya Kata ilikupata uwakilishi uliyowa uhakika na baraza likalete manufaa kwa kuanzia ngazi ya chini ambapo ndipo vijana wengi wanapatikana na jamii inawafahamu kwa usahihi zaidi.
Halikadhalika Serikali iliridhia kuanzishwa kwa uwakilishi wa vijana watano kutoka kundi maalum kwa maana ya wenye ulemavu na ili kuweka uwianao wa vijana hawa kuweza kuwasilisha maombi yao kwa Serikali kwa urahisi huku ikizingatia mahitaji yao maalum.
Serikali inatarajia kuanzisha Baraza la Vijana litakalo kuwa chombo cha vijana kitakacho waunganisha Kitaifa bila kujali itikadi zao za Kisiasa,Imani zao za Kidini wala tofauti zao za Rangi,hayo yamesemwa na Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Mhe.Fenella Mukangara alipokuwa akisoma Muswada wa Sheria ya Baraza la Vijana Tanzania Bungeni Mjini Dodoma.
Mheshimiwa Mukangara aliendelea kusema Baraza hilo litaisaidia Serikali kuweza kuwafikia vijana kwa urahisi na kusikiliza shida zao pamoja na kutoa ufumbuzi wa hoja mbalimbali za vijana.Hata hivyo chimbuko la Muswada huo ni katika kutekeleza Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya 2007,Ibara ya 3 Sehemu ndogo ya 11 inayosema kwa uwazi Serikali itawezesha kuundwa kwa Baraza Baraza la Vijana na kuanzisha mfumo wa kisheria ili kuliwezesha kufanya kazi.
“Madhumuni ya Muswada huu ni Kutunga Sheria ya Baraza la Vijana Tanzania(The Youth Council of Tanzania 2015) ili kuwa na chombo cha Kitaifa cha kuwewezesha vijana kujadili masuala yao,kutambua majukumu yao,kukuza maadili mema,kukuza moyo wa umoja ,uzalendo,uwajibikaji na kujitolea kwa malengo chanya miongoni mwao katika nchi yetu,”alisema Mhe.Mukangara.
Mbali na hayo katika sehemu ya pili kifungu cha 4-15 cha Muswada huo unaeleza juu ya masharti mbalimbali kuhusu Uanzishwaji,Uanachama,Muundo na kazi za Baraza.Pia sehemu hii imefafanua Mamlaka ya Baraza na vyombo vya utendaji katika ngazi ya Taifa,Mkoa na Wilaya.
Aidha,kwa upande wa maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii yaliyosomwa na Mwenyekiti wake Said Mtanda aliishauri Serikali katika kifungu cha 4(3)Kisomeke Uanachama utakuwa na uwazi na hiari kwa kijana yeyote mwenye umri wa kuanzia miaka 15 mpaka 35.Pia kifungu cha 4(4) imeeleza kuwa baraza halitakuwa kisiasa liongezwe neno halitakuwa na Itikadi za Kidini.
Katika kipindi cha majadiliao ya Muswada huo naye Mhe.Kuluthum Mchuchuri (Mb) Viti Maalum CUF aliipongeza Serikali kwa mchakato wake mzuri wa kuandaa Baraza la Vijana litakalo saidia vijana kujadili matatizo yao na kuyawasilisha Serikali kwa kupatiwa ufumbuzi kwa urahisi,pia ameishauri Serikali katika suala la wajumbe uwawakilishi waanze kuanzia ngazi ya Kata na Serikali pia iweke wazi ni kwa utaratibu gani wawakilishi hao watapatikana.
Naye Mhe.Magret Sitta Mbunge wa Viti Maalum CCM aliiomba Serikali kuandaa ziara kwenda kuangalia mabaraza ya Vijana katika nchi za wenzetu yanafanyaje kazi na kujifunza,pia aliendelea kuiomba Serikali itoe mafunzo mbalimbali ya ufundi kwa kushirikia na taasisi ya Veta na Vyuo vya Wananchi ilikuwapatia elimu itakayo wasaidia vijana kujikwamua kiuchumi na kupunguza idadi ya vijana wa vijiweni.
Pamoja na hayo naye Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR) Mhe.Moses Machali alishauri Serikali Kuanzisha asasi moja ambayo vijana watakayo jiunga huko ili kudhibiti uanzishwaji wa asasi bandia kwa watu wenye nia ya kujinufaisha,pia aliipongeza Serikali kwa kuleta Muswada huo kwani unamanufaa Makubwa kwa vijana.
Aidha,mbali ya kuwepo na marekebisho mbalimbali ya Muswada huo Serikali iliyapokea maombi ya Suala la Baraza hilo kuanzia katika ngazi ya Kata ilikupata uwakilishi uliyowa uhakika na baraza likalete manufaa kwa kuanzia ngazi ya chini ambapo ndipo vijana wengi wanapatikana na jamii inawafahamu kwa usahihi zaidi.
Halikadhalika Serikali iliridhia kuanzishwa kwa uwakilishi wa vijana watano kutoka kundi maalum kwa maana ya wenye ulemavu na ili kuweka uwianao wa vijana hawa kuweza kuwasilisha maombi yao kwa Serikali kwa urahisi huku ikizingatia mahitaji yao maalum.
George Simbachawene akizungumzia kuhusu Ugunduzi wa nane wa gesi asilia
Waziri wa Nishati na Madini (wa pili Kulia) Mhe.George Simbachawene akizungumza na waandishi wa Habari Mjini Dodoma kuhusu Ugunduzi wa nane wa gesi asilia uliyofanywa na Kampuni ya Statoil katika eneo la Bahari Kuu,(wa kwanza kulia) ni Naibu Waziri Nishati na Madini Dkt Charles Mwijage,na (wa kwanza kushoto) ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu Nishati na Madini Mhe.Richard Ndassa (Mb) wa Sumve CCM.
Picha na Anitha Jonas – MAELEZO,Dodoma.
ZIARA YA KINANA MOSHI MJINI
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia vijana wa boda boda
,Stendi Kuu kata ya Mawenzi ambapo aliwaambia kuwa boda boda ni sehemu
ya kupata kipato hivyo inabidi wafanye shughuli yao hiyo kwa umakini
mkubwa ,ikiwa kudumisha umoja, kufuata sheria, kujisajili na kutambulika
na mamlaka husika ,kuaminika ili waweze kukopesheka.
Katibu
wa Umoja wa Boda Boda Moshi mjini akisoma risala kwa Katibu Mkuu wa CCM
Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye mkutano uliofanyika ,Stendi Kuu kata ya
Mawenzi Moshi mjini.
Wafanyabiashara
wa soko la kati,Moshi mjini wakiwa wamefunga njia kuzuia msafara wa
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana usipite mpaka wawasilishe
kero yao ya kufungiwa soko kwa mwaka mzima na uongozi wa halmashauri ya
mji kwa maelezo ya kupisha ukarabati ambao haujafanyika.
Katibu
wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisoma ujumbe ulioandikwa kwenye
mabango na wafanyabiashara wa soko la kati,Moshi mjini.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma risala ya wafanyabiashara wa soko la kati,Moshi mjini.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wafanya biashara
ambao soko lao limefungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Katibu wa NEC
Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kuingia kwenye soko la kati, Moshi mjini
mkoani Kilimanjaro ambalo lilifungwa kupisha ukarabati ambao mpaka sasa
ni mwaka 1 hakuna kilichofanyika na wafanyabiashara wanaishi maisha
magumu.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wafanyabiashara wa
soko la kati ambalo limefungwa kwa mwaka mzima sasa.
Ukuta wa soko la kati Moshi mjini ukiwa na matangazo yanayozuia kufanya biashara
Katibu
wa Vikoba kata ya Kongoroni Mariam Chawapoma akisoma risala ya kikundi
chao kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana .
Wanachama wa Vikoba wakishangilia jambo wakati wa mkutano na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wanachama wa Vikoba
kata ya Makongoroni ambapo alishiriki kuzindua vikoba 11 vyenye
wanachama 330,Kata ya Makongoroni,Moshi mjini.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua matofali baada
ya kutembelea kikundi Vijana cha Kata ya Miembeni
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na umati wa akina mama Lishe wa Njoro,Moshi mjini.
Wajasiriamali na mama lishe wakishangilia ujio wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika kata yao ya Njoro.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wajasiriamali pamoja na mama lishe.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Katibu wa NEC
Itikadi na Uenezi Nape Nnauye pamoja na Mwenyekiti wa CCM mkoa Ndugu Idd
Juma
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikatiza kwenye maji wakati
akielekea kwenye eneo la mkutano wa hadhara Bomambuzi viwanja vya shule
ya msingi Mandela.
Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka wilaya ya Moshi mjini Ndugu
Aggrey Marealle akihutubia wananchi wa Moshi mjini ambapo aliwaambia
kuwa wakati umefika wa kufanya mabadiliko ya kweli kwa kuchagua CCM
kuongoza mji wa Moshi.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Moshi mjini
mkutano wa hadhara Bomambuzi viwanja vya shule ya msingi Mandela na
kuwaambie wastuke sasa wasiendelee kukandamizwa na viongozi wasiojali
maendeleo yao.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Moshi mjini
kwenye mkutano wa hadhara Bomambuzi viwanja vya shule ya msingi Mandela
na kuwaambia kuwa wamekuwa na ushabiki kwa miaka 20 imefika wakati sasa
kuamua kuchagua maendeleo kwa manufaa ya maisha yao
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia picha ya gari
alilotumia Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kabala halijafanyiwa
ukarabati na Chuo cha Ufundi Veta, Moshi mjini.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijaribu kuendesha gari
alilotumia Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakati wa harakati za
kutafuta uhuru,kulia ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiteremka kwenye gari
alilotumia Baba wa Taifa wakati wa harakati za kutafuta uhuru.
Wananchi
wakiuaga msfara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara
baada ya mkutano kumalizika kwenye viwanja vya shule ya msingi
Mandela,Bomambuzi, Moshi Mjini.
MSHINDI WA MWISHO WA”MTOKO WA MBUGANI” WA KAMPENI YA TUTOKE NA SERENGETI AFURAHIA MTOKO WAKE WA SIKU TATU NDANI YA HIFADHI YA SERENGETI
Mshindi wa mwisho wa shindano la
“Tutoke na Serengeti” Bw.Gabriel Robert Moriale (Kulia) akiwa na kaka
yake Bw.Joshua Robert Moriale (Kushoto) walipowasili mamlaka ya hifadhi
ya Ngorongoro jijini Arusha tayari kwa kuanza safari ya kwenda Hifadhi
ya Taifa ya Serengeti kukamilisha mtoko wao wa siku tatu ndani ya
hifadhi hiyo. Robert aliibuka mshindi wa mwisho wa “Mtoko wa mbugani”
baada ya kushiriki kwenye kampeni ya “Tutoke na Serengeti” iliyoendeshwa
na kampuni ya bia ya Serengeti kwa ushirikiano na BPESA kwa takriban
miezi(4) ambapo washindi walijinyakulia zawadi nyingine kama Limo Bajaj,
fedha taslim, Bia za bure sambamba na punguzo la Tsh.300 kwenye bia ya
Serengeti Premium.
Mshindi wa mwisho wa shindano la “Tutoke
na Serengeti” Bw. Robert Gabriel Moriale wa pili (Kushoto) aliyeongozana
na mdogo wake Bw. Joshua Robert (Wa kwanza kulia) wakitalii ndani ya
Ngorongoro na kupata maelekezo kutoka kwa mwelekezi (Tour guide) kabla
ya kuanza safari ya kwenda Serengeti national park. Bw. Robert aliibuka
mshindi wa mwisho wa “Mtoko wa mbugani” baada ya kushiriki kwenye
kampeni ya “Tutoke na Serengeti” iliyokua ikiendeshwa na kampuni ya bia
ya Serengeti kwa ushirikiano na BPESA kwa takriban miezi(4) ambapo
washindi walijinyakulia zawadi nyingine kama Limo Bajaj, fedha taslim,
Bia za bure sambamba na punguzo la Tsh.300 kwenye bia ya Serengeti
Premium.
Ndugu wa mshindi wa “Mtoko wa
Mbugani” ajulikanaye kwa jina la Joshua Robert akimpiga picha simba
ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwenye mtoko wao wa siku tatu
ndani ya hifadhi hiyo.Joshua alimsindikiza kaka yake Bw.Gabriel Robert
aliyeibuka mshindi wa mwisho wa mwisho wa “Mtoko wa mbugani” baada ya
kushiriki kwenye kampeni ya “Tutoke na Serengeti” iliyokua ikiendeshwa
na kampuni ya bia ya Serengeti kwa ushirikiano na BPESA kwa takriban
miezi(4) ambapo washindi walijinyakulia zawadi nyingine kama Limo Bajaj,
fedha taslim, Bia za bure sambamba na punguzo la Tsh.300 kwenye bia ya
Serengeti Premium.
Mshindi wa mwisho wa shindano la
“Tutoke na Serengeti” Bw.Gabriel Robert Moriale akiangalia kundi kubwa
la wanyama aina ya pundamilia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti
wakati wa kukamilisha mtoko wao wa siku tatu ndani ya hifadhi hiyo.
Robert aliibuka mshindi wa mwisho wa “Mtoko wa mbugani” baada ya
kushiriki kwenye kampeni ya “Tutoke na Serengeti” iliyokua ikiendeshwa
na kampuni ya bia ya Serengeti kwa ushirikiano na BPESA kwa takriban
miezi(4) ambapo washindi walijinyakulia zawadi nyingine kama Limo Bajaj,
fedha taslim, Bia za bure sambamba na punguzo la Tsh.300 kwenye bia ya
Serengeti Premium.
Mshindi wa mwisho wa shindano la
“Tutoke na Serengeti” Bw. Robert Gabriel Moriale (Kulia) aliyeongozana
na mdogo wake Bw. Joshua Robert (Kushoto) wakifuruahia bia ya Serengeti
Premium wakati wakitalii ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakati
wa kukamilisha mtoko wa siku tatu ndani ya hifadhi hiyo. Bw. Robert
aliibuka mshindi wa mwisho wa “Mtoko wa mbugani” baada ya kushiriki
kwenye kampeni ya “Tutoke na Serengeti” iliyokua ikiendeshwa na kampuni
ya bia ya Serengeti kwa ushirikiano na BPESA kwa takriban miezi(4)
ambapo washindi walijinyakulia zawadi nyingine kama Limo Bajaj, fedha
taslim, Bia za bure sambamba na punguzo la Tsh.300 kwenye bia ya
Serengeti Premium.
Subscribe to:
Posts (Atom)