HABARI ZETU
Loading...
Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

ADO AAHIDI UFANISI, UADILIFU NA UMADHUBUTI USIMAMIZI SEKTA ZA FEDHA NA MIPANGO

June 13, 2026 Add Comment




“Nimeupokea kwa unyenyekevu na hamasa uteuzi wa kuwa Msemaji wa Sekta ya Fedha, Mipango na Hifadhi ya Jamii wa Kamati ya Wasemaji wa Kisekta ya ACT Wazalendo. Wajibu wangu ni kuzisimamia Wizara za Fedha chini ya Balozi Hamis Mussa Omar na Wizara ya Mipango na Uwekezaji chini ya Prof. Kitila Mkumbo. 

Wizara hizi zimebeba taasisi nyeti kama vile Benki Kuu ya Tanzania na Sekta ya Benki kwa Ujumla wake, Hazina, TRA, Taasisi ya Manunuzi ya Umma (PPRA), TISEZA na Taasisi nyinginezo katika tasnia ya fedha na mipango.

Ninamshukuru Kiongozi wa Chama Ndugu Dorothy Semu kwa uteuzi huu. Nitatekeleza wajibu wangu kwa ufanisi, uadilifu na umadhubuti”- Ado Shaibu Ado.

KATIBU MKUU WA CCM AKUTANA NA BALOZI WA UINGEREZA KUJADILI USHIRIKIANO WA MAENDELEO NA DIRA 2050

June 06, 2026 Add Comment

 


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Asha-Rose Migiro, leo Ijumaa Juni 5,2026 amefanya mazungumzo na Mheshimiwa Marianne Young, Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma.


Mazungumzo hayo yalihusu maeneo ya ushirikiano wa maendeleo kati ya Tanzania na Uingereza, kwa kuzingatia vipaumbele vilivyobainishwa katika Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2025–2030, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Viongozi hao walijadili fursa za kuendeleza ushirikiano kwenye maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hususan katika kuwawezesha vijana na wanawake kupitia elimu, ujuzi, ubunifu na uwekezaji.

CCM inaendelea kuthamini ushirikiano wa kimataifa unaochangia maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi wa Tanzania.

NLD YAKEMEA WANAOWINDA URAIS 2030

June 03, 2026 Add Comment






Na Oscar Assenga, Tanga

CHAMA Cha National League for Democracy (NLD),kimeonya wanasiasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kuonyesha nia ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2030 kuelekeza nguvu zao katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi badala ya kuanza harakati za kisiasa mapema.

Onyo hilo limetolewa na  Katibu Mkuu wa Chama cha NLD Doyo Hassani Doyo wakati akizungumza na wabahabari Jijini Tanga baada ya kuhitimisha ziara ya kichama katika Mkoa wa Tanga, akieleza kuwa Taifa kwa sasa linahitaji mjadala unaolenga maendeleo na ustawi wa wananchi kuliko mjadala wa urais ambao muda wake bado haujafika.

Alisema ingawa Katiba na sheria za nchi zinatoa haki kwa kila mwananchi mwenye sifa kugombea nafasi yoyote ya uongozi, ikiwemo urais, si jambo la busara kwa viongozi kuanza kujinadi kisiasa wakati wananchi bado wanakabiliwa na changamoto nyingi za maendeleo.

Aidha alisema ni haki ya  kikatiba na kisheria kugombea nafasi yoyote ya uongozi lakini kwa mtazamo wake anaona jambo hilo sio lenye afya kwa Taifa kuanza mijadala ya urais miezi michache tu baada ya uchaguzi mkuu kumalizika,.

Alidai kuwa katika siku za hivi karibuni baadhi ya wabunge wa CCM wamekuwa wakitoa kauli katika Bunge na kwenye mikutano ya hadhara ambazo, kwa tafsiri yake, zinaashiria kuanza kwa harakati za kuwania urais wa mwaka 2030.

Kwa mujibu wa Doyo, viongozi waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wanapaswa kutumia nafasi zao kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuibua hoja zenye tija na kuishauri serikali katika masuala yatakayoboresha maisha ya Watanzania.

“Wananchi waliwachagua wabunge wao kwa matarajio ya kuona changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi. Tungetarajia kuona nguvu nyingi zikielekezwa katika kujadili maendeleo, uchumi, huduma za jamii na ustawi wa wananchi kuliko kujenga mazingira ya kampeni za uchaguzi ambao bado uko mbali,” alisema.

Aliongeza kuwa kuanza kwa siasa za urais mapema kunaweza kuathiri umakini wa viongozi katika utekelezaji wa majukumu yao na hata kupunguza kasi ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya wananchi.

Doyo pia aligusia kauli mbalimbali zilizowahi kutolewa na baadhi ya viongozi wa serikali kuhusu watu wanaotamani nafasi ya urais mapema, akisema hali hiyo inaonyesha dalili za kuanza kujitokeza kwa makundi ya kisiasa ndani ya chama tawala kabla ya wakati wake.

Hata hivyo, alisisitiza kuwa viongozi wa vyama vyote vya siasa wanapaswa kuweka mbele maslahi ya taifa kwa kushirikiana kutafuta suluhisho la changamoto zinazowagusa wananchi katika maisha yao ya kila siku.

Katika hatua nyingine, Doyo aliwataka Watanzania kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan katika juhudi zake za kusimamia maendeleo ya nchi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Sasa ni wakati wa kushughulikia changamoto za wananchi, kuimarisha huduma za kijamii na kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya taifa. Wakati wa siasa za urais ukifika, kila mwenye sifa na nia atapata nafasi ya kujitokeza,” alisema.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa NLD Wilaya ya Tanga amesema bado kuna changamoto nyingi zinazohitaji ufumbuzi wa haraka mkoani humo, hususan katika sekta ya maji na miundombinu ya barabara.

Alisema viongozi wa chama hicho walijionea hali halisi ya baadhi ya maeneo wakati wa ziara yao, ambapo wananchi wengi bado wanakabiliwa na uhaba wa maji safi na salama pamoja na miundombinu duni inayokwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii.

Alitaja baadhi ya barabara zinazounganisha maeneo ya Maramba, Mashewa, Korogwe, Mwakijembe na Lushoto kuwa miongoni mwa miundombinu inayohitaji maboresho ya haraka kutokana na hali yake kuwa mbaya.

“Tulipita katika maeneo mbalimbali na kujionea changamoto wanazokabiliana nazo wananchi. Bado kuna maeneo mengi yenye matatizo ya maji na miundombinu ambayo yanahitaji kipaumbele kutoka kwa mamlaka husika,” alisema.

Viongozi hao wa NLD walihitimisha kwa kuitaka serikali, viongozi wa kisiasa na wadau wa maendeleo kuelekeza nguvu katika kutatua kero za wananchi na kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo, wakisisitiza kuwa wananchi wanahitaji kuona matokeo ya maendeleo kuliko kushuhudia mijadala ya uchaguzi ambao bado uko miaka kadhaa mbele.

MWISHO

MWENYEKITI WA CCM TANGA YAKABIDHI MILIONI 500 KUKAMILISHA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI WAKE

June 01, 2026 Add Comment

 


>Yalenga Kuimarisha Ufanisi wa Chama

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimeongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wake wa ujenzi wa nyumba 36 za watumishi baada ya Mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo, Rajab Abdulrahman, kukabidhi shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo unaotekelezwa katika wilaya tisa za mkoa huo.

Fedha hizo zilikabidhiwa  kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, katika hatua inayodhihirisha dhamira ya chama ya kuboresha mazingira ya kazi na makazi kwa viongozi wake wa ngazi za wilaya.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Rajab alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba mwaka huu na kwamba utakuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha utendaji wa watumishi pamoja na shughuli za chama katika maeneo mbalimbali ya mkoa.

Alieleza kuwa mradi huo una thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.5, huku fedha zote zinazohitajika kwa ajili ya utekelezaji wake zikiwa tayari zimepatikana kupitia michango ya wanachama, viongozi na wadau mbalimbali wa chama.

"Mradi huu unagharimu jumla ya shilingi bilioni 2, milioni 500 na laki 250. Fedha hizi zimepatikana kupitia michango mbalimbali ikiwemo milioni 56 zilizotolewa awali, milioni 10 kutoka kwa MNEC pamoja na michango iliyokusanywa kutoka wilaya zote za mkoa," alisema Rajab.

Mwenyekiti huyo alibainisha kuwa kukamilika kwa nyumba hizo kutasaidia kutatua changamoto za makazi kwa baadhi ya viongozi wa chama katika ngazi ya wilaya, jambo litakaloongeza utulivu wa kazi, uwajibikaji na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Alisema nyumba hizo si tu kwamba zitakuwa makazi ya viongozi, bali pia ni uwekezaji wa muda mrefu wa chama katika kujenga taasisi imara yenye uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuendelea kuwahudumia wanachama wake.

"Tunajenga misingi ya chama kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Viongozi wanaweza kubadilika, lakini miundombinu tunayojenga leo itaendelea kulitumikia chama kwa miaka mingi ijayo," alisisitiza.

Rajab aliongeza kuwa ujenzi wa chama ni jukumu endelevu linalohitaji mshikamano wa wanachama wote, akisisitiza kuwa maendeleo ya chama hayawezi kupatikana bila ushiriki wa pamoja wa wanachama wake.

Kutokana na hilo, aliwataka wana-CCM wa Mkoa wa Tanga kuendelea kuchangia kwa hali na mali, kutumia elimu na uzoefu wao pamoja na nguvu kazi katika kukiimarisha chama.

Kwa upande wake, Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, alisema mradi huo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa chama wa kuimarisha utendaji wake katika ngazi za wilaya kwa kuhakikisha viongozi wanapata mazingira bora ya kazi na makazi.

Alifafanua kuwa kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo zitatumika na viongozi muhimu wa chama na jumuiya zake.

"Kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo ni nyumba ya Katibu wa CCM wa Wilaya, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Vijana, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi pamoja na nyumba ya Katibu wa UWT," alisema Kizigo.

Alieleza kuwa uwepo wa nyumba hizo utasaidia kupunguza gharama za upangaji wa makazi, kuimarisha upatikanaji wa viongozi katika maeneo yao ya kazi na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za chama na jumuiya zake.

Kwa mujibu wa Kizigo, kukamilika kwa mradi huo kutakuwa hatua muhimu katika kuijengea CCM Mkoa wa Tanga miundombinu imara itakayosaidia kuendeleza shughuli zake za kisiasa, kiutawala na kijamii kwa ufanisi zaidi katika miaka ijayo.

NLD YATETEA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI

May 24, 2026 Add Comment

 



>Sheria Isichague Chama

NA OSCAR ASSENGA, TANGA

Katibu Mkuu wa Chama cha NLD, Doyo Hassan Doyo, amesema mjadala unaoendelea kuhusu hatua zinazochukuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa umeonyesha jinsi baadhi ya Watanzania wanavyotoa hukumu za haraka bila kutafakari misingi ya sheria.

Doyo alisema kumekuwa na mtazamo kwamba Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inalenga zaidi vyama vya upinzani, huku ukweli ukiwa ni kwamba taasisi hiyo inasimamia sheria bila kuangalia itikadi ya chama husika.

Akizungumza wakati wa ziara ya chama hicho mkoani Tanga, alisema hatua zilizochukuliwa hivi karibuni dhidi ya baadhi ya viongozi wa kisiasa zinatokana na matamshi yaliyotafsiriwa kuwa na viashiria vya uvunjifu wa sheria za vyama vya siasa.

“Sheria iko wazi. Chama au kiongozi anayekiuka taratibu anaweza kupewa adhabu ya faini, kusimamishwa shughuli au hata kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria. Hii siyo kwa chama fulani pekee,” alisema.



Alieleza kuwa baada ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutoa kauli zilizozua mjadala, Ofisi ya Msajili iliwaandikia barua ya kutaka maelezo. Hatua hiyo, kwa mujibu wa Doyo, ilitafsiriwa vibaya na baadhi ya wananchi pamoja na wanaharakati waliodai kuwa upinzani unaonewa.

Hata hivyo alisema hali hiyo imebadilika baada ya mmoja wa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) naye kuandikiwa barua kufuatia matamshi yake ya kisiasa.

“Watu walidhani sheria inafanya kazi kwa upande mmoja, lakini sasa imeonekana wazi kuwa anayevunja sheria ndiye anayechukuliwa hatua, bila kujali anatoka chama gani,” alisema.

Doyo alisema vyama vya siasa vinapaswa kutambua kuwa vimesajiliwa kwa mujibu wa sheria na hivyo vina wajibu wa kuendesha shughuli zake ndani ya mipaka ya kisheria.

Alionya kuwa siasa zisizo na nidhamu zinaweza kupelekea uvunjifu wa amani na kuhatarisha usalama wa Taifa.

“Ukianza kufanya siasa nje ya sheria, maana yake unaondoka kwenye misingi ya kisiasa na kinachofuata ni migogoro na vurugu. Taifa haliwezi kujengwa kwa misingi ya shinikizo na vitisho,” alisema.



Aidha, aliitaka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuendelea kusimamia sheria kwa uthabiti bila kuogopa presha za kisiasa kutoka kwa wanasiasa au wanaharakati.

Kwa mujibu wa Doyo, uwepo wa taasisi imara zinazotekeleza sheria kwa haki ndiyo msingi wa kulinda amani na utulivu wa nchi.

Katika ziara hiyo ya NLD iliyoanzia Pangani na kuelekea Lushoto, chama hicho kimesema kinaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuheshimu sheria, taratibu na kanuni za kisiasa ili kuimarisha demokrasia na mshikamano wa Taifa.

TUME YATEUA WAGOMBEA 17 UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA ISMANI

May 11, 2026 Add Comment



Na. Mwandishi Wetu, Ismani

Wagombea 17 wameteuliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kugombea ubunge Jimbo la Ismani lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Mkoani Iringa.

Uteuzi huo umefanywa kwa niaba ya Tume na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Ismani, Ndugu. Caroline Angwen Otieno leo tarehe 10 Mei, 2026.

Wagombea walioteuliwa na vyama vyao kwenye mabano ni Ndugu. Emmanuela Kaganda Mtatifikolo (CCM), Ndugu. Farida Issa Mwapungu (MAKINI), Ndugu. Asha Athumani Chuma (UPDP), Ndugu. Protas Shaibu Mgimbila (CCK), Ndugu. Fidelis Daud Mtikile (SAU), Ndugu. Hadija Husen Makawa (ADA-TADEA) Ndugu. Zavely Raurent Seleleka (UDP) na Ndugu. Subira Majuto Kalolo (NLD).

Wengine ni Ndugu. Bernard George Mwingira (DP), Ndugu. Burton Emilyo Chetenge (NCCR-Mageuzi), Ndugu. Mbalinga Christian Thomas (N.R.A), Ndugu. Mark Isdory Mhemela (AAFP), Ndugu. Nassim Yahaya Upete (CUF), Ndugu. Mwaka Lameck Mgimwa (TLP), Ndugu. Asma Abdallah Othman (UMD), Ndugu. Maimuna Martin Lumato (ADC) na Ndugu. Daudi Issa Masasi (CHAUMMA).

Akizungumza baada ya uteuzi huo, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo, Ndugu. Caroline Angwen Otieno amesema kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Tume,

Kampeni kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Ismani pamoja na kata 12 za Tanzania Bara zitaanza kesho tarehe 11 hadi 31 Mei, 2026 na uchaguzi utafanyika siku ya Jumatatu tarehe 01 Juni, 2026.

Baada ya hatua hii ya uteuzi, kinachofuata ni kubandika fomu za uteuzi eneo la wazi kwa ajili ya kuwapa fursa ya kuweka pingamizi wale wanaoruhusiwa kuweka pingamizi kwa mujibu wa sheria.

Baada ya saa 24 kupita na endapo hakutakuwa na pingamizi wagombea hao 17 wataendelea na kampeni kuanzia kesho tarehe 11 hadi 31 Mei, 2026 na uchaguzi utafanyika tarehe 01 Juni, 2026, amesema.

Kata 12 za Tanzania Bara zitakazofanya uchaguzi mdogo wa Udiwani ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.


















TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAMKABIDHI RASMI MGOMBEA UBUNGE WA CCM JIMBO LA ISIMANI FOMU ZA KUGOMBEA UBUNGE

May 05, 2026 Add Comment

 

TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imemkabidhi rasmi fomu za kugombea ubunge wa jimbo la Isimani kwa Emanuela Mtatifikolo Kaganda, kwa ajili ya Uchaguzi Mdogo unaotarajiwa kufanyika Juni 1 mwaka huu.


Zoezi hilo limefanyika katika ofisi za tume zilizopo Ihemi chini ya usimamizi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi jimbo la Isimani, Caroline Ang’weni Otieno.

Emanuela alikabidhiwa fomu hizo akisindikizwa na viongozi mbalimbali wa wilaya akiwemo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Iringa Vijijini, Costantino Kihwele ambapo baada ya kupokea fomu, Emanuela aliwashukuru viongozi na wanachama wote kwa kujitokeza, akisisitiza kuwa ana dhamira ya kutoa mchango chanya kwa maendeleo ya jimbo la Isimani.

Katika hotuba yake, aliwatambua viongozi wa jumuiya zote za chama ikiwemo jumuiya ya wazazi, vijana na UWT, pamoja na madiwani na viongozi wa ngazi mbalimbali.

Aliweka wazi kuwa, licha ya jimbo hilo kupitia kipindi kigumu kutokana na msiba wa aliyekuwa mbunge, wananchi wamethibitisha umoja na mshikamano mkubwa.

Emanuela alitoa shukurani za pekee kwa uongozi wa chama kuanzia ngazi ya shina hadi taifa, kwa kusimamia mchakato wa uteuzi kwa haki na uwazi na alipongeza pia wagombea wenzake walioshiriki mchakato huo na kuonyesha umoja baada ya kukamilika kwa uteuzi.

Aidha, alisisitiza kuwa jimbo la Isimani tangu kuanzishwa kwake limeongozwa na kiongozi mmoja, marehemu William Vangimembe Lukuvi, ambaye alifanya kazi kubwa ya kuliletea maendeleo.

Aliahidi kuendeleza misingi ya maendeleo iliyoachwa na kiongozi huyo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Vijijini, Costantino Kihwele, alimpongeza Emanuela kwa kuteuliwa na kamati kuu kuiwakilisha CCM kwenye uchaguzi huo mdogo.

Aliwahimiza wanachama kuendelea na umoja na maandalizi ya kampeni, akieleza kuwa chama kitafanya kampeni za kidiplomasia na za ushahidi wa kazi zilizofanyika.

Kihwele pia aliwapongeza wagombea wengine waliokuwa kwenye mchakato wa awali kwa kuonyesha uzalendo na kukubali matokeo, akiahidi kuwa watashirikishwa kikamilifu katika kampeni zitakapoanza rasmi.

Viongozi na washiriki wa mkutano huo walionyesha hamasa ya pamoja, huku wakiahidi kumpa mgombea wao ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa Juni 1.






CCM YAMNG’OA KIGOGO UWANJA WA MKWAKWANI

March 11, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga,TANGA

KAMATI ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga imeagiza kusimamishwa kazi Meneja wa Uwanja wa Mkwakwani Akida Machai kutokana na mapungufu mbalimbali yaliyobainika wakati wa ziara ya kamati hiyo kwa ajili ya kujionekana maendeleo yake.

Akizungumza kuhusu maamuzi hayo ,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman ambapo alisema kwamba ukiangalia mapato yanayopatikana na gharama ambazo zinatumika zikitolewa sawasawa na CCM hakuna chochote kinachopatikana lakini maji yanalipwa na CCM ,Umeme unalipwa na CCM.

Alisema wanafanya hivyo kuhakikisha wananchi waendelee kupata burudani ya michezo sasa wanapotoa fedha na kuona mambo bado hawaendi kama wanavyotarajia ni jambo ambalo limekuwa likiwaumiza.


“Mimi Binafsi nilitoa milioni 50 inawezekana fedha hamtafiti nyie ndio maana hamuoni uchungu wake mimi natayetafutaa fedha kwa wadau anawawaomba anajua uchungu wake lakini wao kwa sababu hawajui uchungu wake na walimuweka yeye kama meneja wakiamini angeweza kutusaidia kuhakikisha uwanja huo muda wote unaweza kuwa bora unatumika”Alisema

“Lakini ukija wakati wote uwanja umekuwa kama Mbuga za Wanyama haiwezekani sio sawa mpaka leo viti vimeletwa havijafungwa na mmeviacha mpaka vimeota majani”Alisema

Aidha alisema kwamba wao wamekaa kama viongozi waliochaguliwa ili uwanja uweze kufikia vigezo lakini mpaka kufikia wakati uwanja kufungiwa na TFF hivyo hawawezi kukubali.

“Nilisema kwa hali ilivyo muda wowote TFF wangeweza kuja kutufungia uwanja hivyo nitoe maelekezo kwa Kamati ya Siasa mkoa kaeni Mtafute Meneja mwengine ili changamoto hizo ziweze kuondoka”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba kwa mpangaji Yule mwenye baa pale nje ambayo haijakidhi vigezo na Shirikisho la Soka nchini (TFF) walishasema ile baa inazuia washabiki kuingia uwanjani wakati wa mpira na inatakiwa kuondoka lakini mpaka leo haijaondoka.

“Maanake huyo mtu ana mapembe kiasi gani yeye ni mpangaji kwenye eneo letu lakini anakigomea CCM hivyo nahitaji hii baa leo iondoke ili maelekezo na maagizo ya TFF tuweze kuyatimiza na apatikane Meneja mwengine haraka ili aweze kushirikina na vongozi wa CCM kufungwa viti hivyo na nanatoa mwezi mmoja”Alisema

Awali akizungumza aliyekuwa Meneja wa uwanja wa CCM Mkoa wa Tanga Akida Machai alisema changamoto ya uhaba wa nguvu kazi ndio imepelekea kukwamisha viti hivyo kufungwa .

Alisema kwamba walikuwa wakihitaji kuongezewa nguvu kazi yeye anashukru CCM kwa nafasi waliompatia na wanamtakia kilala heri Meneja Mpya huku akieleza wakati viti vilipokuja walipeleka Bajeti ya kufunga viti CCM na vitu vinavyohusika na hawezi kutoa fedha zake kufungwa viti.

Mwisho.

WANAWAKE WA UWT KIBAHA MJI WAANZA KUTEMA CHECHE BAADA YA USHINDI WA KISHINDO KATIKA UCHAGUZI MKUU

March 11, 2026 Add Comment


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA

Jumuiya ya umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini katika kukiimarisha chama imeamua kufanya ziara maalumu yenye lengo la kuwashukuru na kuwapongeza wanawake kwa umoja wao na mshikamao waliouonyesha katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kupelekea chama cha mapinduzi (CCM) kuweza kushinda kwa kishindo katika nafasi za Udiwani, Ubunge pamoja na Urais.

Akizungumza katika ziara hiyo ambayo imefanyika katika Kata mbili za Visiga pamoja na Misugusugu Mwenyekiti wa (UWT) Wilaya ya Kibaha Elina Mgonja amesema kwamba wameamua kufanya ziara hiyo ambayo itaweza kuwapa fursa ya kukutana na wanawake hao ambao ndio walikuwa mstari wa mbele katika kukipigania chama kiweze kushinda na kupata viongozi wa CCM katika nafasi mbali mbali.'

Katika ziara hiyo ambayo imeongozwa na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha pamoja na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utekelezaji ambapo pia wametumia fursa ya kutembelea zahanati ya Misusugu pamoja na kuendesha zoezi la upandaji wa miti.

Mwenyekiti huyo amebainisha kwamba wameamua kufanya ziara hiyo kwa lengo la kuweza kutoa shukrani kwa wanawake ikiwa pamoja na kuhamasiha viongozi wa matawi mbali mbali kuwezaa kushikamana kwa pamoja ili kuimalisha uwahi wa jumuiya pamoja na chama kuanzia ngazi za chini.

"Tumeanza ziara yetu ya jumuiya ya wanawake Wilayaa ya Kibaha ambapo tumetembeleakata mbili za visiga pamoja na kata ya Misugusugu lakini kitu kikubwa ni kwa ajili ya kuwashukuru wanawake wote wa chama cha mapinduzi pamoja na jumuiya wa UWT kwa kuweza kuwachagua viongozi kwa kura nyingi za kishindo katika nafasi ya Udiwani, Ubunge, pamoja na nafasi ya Urais,"amebainisha Elina

Kadhalika Mwenyekiti huyo amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita kwa kuweza kutekeleza ilani ya cchama kwa vitendo ikiwemo kutenga fedha nyingi ambazo zimekwenda kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya afya, eilimu, maji, nishati ya umeme pamoja na huduma za kijamii.

Kwa upande wake Katibu wa UWT Wilaya ya Kibaha Cesilia Ndalu amesema kuwa ziara hiyo pia imelenga kuanzisha vikundi vya uchumi ambavyo vitaweza kuwasaidia kwa kiasi kukubwa kupambana na wimbii la umasikini.

Diwani wa kata ya Misugusugu Ally Simba amewahimiza wanawake wa UWT kuhakikisha wanachangamkia fursa za mikopo mbali mbali ambayo inatolewa na Halmashauri kwa lengo la kuweza kujikwamua kiuchumi pamoja na kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo katika nyanja tofauti.