CHADEMA MUHEZA YAJITENGA NA ALIYEKUWA KATIBU WAO
siasaNa Mwandishi Wetu, Tanga
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Muheza mkoani Tanga kimesema hakihusiki na vitendo vinavyodaiwa kufanywa na aliyekuwa Katibu wa chama hicho wilayani humo, Joseph Mwakidasi, huku kikiwataka wanachama kuendelea kudumisha mshikamano na kuepuka makundi yanayoweza kukigawa chama.
Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Katibu wa CHADEMA Jimbo la Muheza, Michael Mhina, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matukio yaliyojitokeza ndani ya chama katika siku za hivi karibuni.
Mhina alisema Julai 8 mwaka huu viongozi wa chama waliona kupitia vyombo vya habari taarifa za Mwakidasi akimtuhumu Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, kutumia vibaya fedha zinazochangwa na wanachama kupitia kampeni ya "Tone Tone".
Alisema kutokana na uzito wa tuhuma hizo, Kamati Tendaji ya Wilaya ilikutana kwa dharura Julai 9 na kumuita Mwakidasi ili afafanue chanzo cha madai yake, lakini hakufika wala wanachama wa CHADEMA. Alisema waliingia ofisini baada ya kuchukua funguo kutoka kwa m hayo, Julai 21 tuliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili vifanye uchunguzi kuhusu kilichotokea. Sisi kama CHADEMA Muheza hatuhusiki kwenye kikao hicho wala kutoa maelezo.
Mhina alidai kuwa Julai 20, Mwakidasi aliwasili katika ofisi za CHADEMA Wilaya ya Muheza akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi kutoka wilaya nyingine pamoja na watu ambao, kwa mujibu wa chama hicho, si viongozi wala wanachama wa CHADEMA. Alisema waliingia ofisini baada ya kuchukua funguo kutoka kwa mweka hazina wa chama.
Kwa mujibu wa Mhina, watu hao walifanya kikao ndani ya ofisi hizo na baadaye kurekodi na kusambaza taarifa mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii, jambo alilodai lilisababisha taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa Muheza.

"Baada ya matukio hayo, Julai 21 tuliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili vifanye uchunguzi kuhusu kilichotokea. Sisi kama CHADEMA Muheza hatuhusiki na yaliyofanywa na watu hao," alisema Mhina.
Alisema viongozi wa chama wilayani humo wanaendelea kumuunga mkono Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, pamoja na Mwenyekiti wa chama, Tundu Lissu.
Pia aliomba vyombo vya dola kuchunguza madai ya kuwahamasisha wananchi kuhudhuria mkutano kwa ahadi ya kulipwa fedha, akisisitiza kuwa CHADEMA haina utaratibu wa kuwalipa wanachama kushirikiio yote yaliyotokea katika ofisi za chama, akidai hatua zilizochukuliwa na Mwakidasi na wenzake zilichangia taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa shughuli za chama.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Muheza, Ally Mahanyu, alisema chama kinapinga vitendo vinavyodaiwa kufanywa na Mwakidasi kwa madai kuwa vilikiuka taratibu za chama.
Mahanyu alisema viongozi walimuita Mwakidasi mara kadhaa kwenye vikao vya Kamati Tendaji ili kutoa maelezo, lakini hakuitikia wito huo.
Aidha, alivitaka vyombo vya dola kuchunguza matukio yote yaliyotokea katika ofisi za chama, akidai hatua zilizochukuliwa na Mwakidasi na wenzake zilichangia taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa Muheza.
Aliwataka wanachama wa CHADEMA kuendelea kuwa watulivu, kuwaamini viongozi wao na kushiriki shughuli za ujenzi wa chama kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa.
Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CHADEMA Wilaya ya Muheza, Isa Mwaikani, alisema baraza hilo pia lilimuita Mwakidasi kutoa maelezo kuhusu tuhuma alizozielekeza kwa Heche, lakini hakuitikia wito huo.
Mwaikani alisema viongozi wa chama walishangazwa na tuhuma hizo kwa kuwa, kwa mujibu wa muundo wa uongozi wa chama, Makamu Mwenyekiti hahusiki na usimamizi wa fedha.
"Hatuelewi amepata wapi ujasiri wa kumtuhumu kiongozi wa juu wa chama bila kuwasilisha ushahidi kwenye vikao halali vya chama," alisema.
Aliongeza kuwa wanachama wengi wa CHADEMA Muheza wameendelea kubaki ndani ya chama na hali ya kisiasa wilayani humo ni tulivu.

Akijibu tuhuma hizo, aliyekuwa Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Muheza, Joseph Mwakidasi, alisema madai yanayotolewa dhidi yake hayana ukweli na kwamba anaendelea kutetea nafasi yake ndani ya chama.
Alisema hana mpango wa kuhamia chama kingine cha siasa na anasubiri maamuzi ya vikao vya chama kuhusu nafasi yake.
Kuhusu tuhuma alizomwelekeza John Heche, Mwakidasi alisema suala hilo linatokana na mijadala iliyofanyika katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika Dodoma, akidai baadhi ya taarifa zilizokuwa siri zilivuja kutoka ndani ya chama.
Mwisho.
MBUNGE KILINDI,KITETO WAENDELEZA UJIRANI MWEMA MIRADI YA MAENDELEO
siasaKatika kuonesha ujirani mwema Mbunge wa Kiteto Edward Ole Lekaita na Mbunge wa Kilindi Salehe Mhando wameamua kushirikiana kuhakikisha barabara ya Lengatei- Songe inatengenezwa kwa kiwango cha changarawe na kupitika kwa mwaka mzima.
Mbali ya kushirikiana kusimamia Ujenzi wa barabara hiyo pia Wabunge hao wameshiriki shughuli ya uzinduzi wa shule ya awali na msingi Kijiji cha Lesiot Kata ya Lengatei Kiteto.
RAIS DKT SAMIA SULUHU AHUDHURIA HALFA YA UWASILISHWAJI TAMKO LA PAMOJA LA MARIDHIANO YA KISIASA ZANZIBAR KATIKA VIWANJA VYA IKULU ZANZIBAR
habari siasa![]() |
| Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wakiwasili katika viwanja vya Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kuhudhuria hafla ya uwasilishaji wa Tamko la Pamoja la Muafaka wa Kisiasa baina ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo, tarehe 09 Julai, 2026. |
![]() |
![]() |
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mwenyekiti wa Chama cha
ACT-Wazalendo Taifa Mhe. Othman Masoud Othman pamoja na Marais Wastaafu wa
Zanzibar, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Amani Abeid Karume wakishuhudia utiaji
saini wa ajenda zilizokubaliwa na pande zote mbili kwa ajili ya kufanyiwa kazi
baada ya Tamko la Pamoja la Muafaka wa Kisiasa baina ya Chama cha Mapinduzi
(CCM) na ACT-Wazalendo, katika viwanja vya Ikulu Zanzibar, tarehe 09 Julai,
2026. Kushoto anaye saini ni Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo- Zanzibar Omary
Ally Shehe pamoja na Naibu Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM- Zanzibar Dkt.
Mohammed Said Dimwa
KIGOGO WA CHADEMA TANGA RASHID JUMBE ATANGAZA KUMALIZA SAFARI YA MIAKA 30 UPINZANI,AHAMIA CCM
siasa>Asema kasi ya maendeleo chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amani, uchumi, afya, maji na miundombinu vimemshawishi kubadili msimamo wa kisiasa.
Na Oscar Assenga,TANGA
Baada ya zaidi ya miaka 30 ya kuwa mwanasiasa wa upinzani, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Tanga, Rashid Jumbe, amefanya uamuzi mkubwa wa kisiasa kwa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Jumbe, ambaye kwa muda mrefu alikuwa mmoja wa viongozi mashuhuri wa Chadema mkoani Tanga, amesema uamuzi wake umetokana na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na juhudi za Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha amani, umoja na ustawi wa wananchi.
Akizungumza wakati wa hafla ya kumpokea ndani ya CCM iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, Jumbe alisema hakufanya uamuzi huo kwa papara, bali baada ya kutafakari kwa kina na kujiridhisha kuhusu mwelekeo wa maendeleo ya taifa.
"Nilikuwa mpinzani kwa zaidi ya miaka 30, lakini leo nimeamua kuhitimisha safari hiyo. Kilichonishawishi zaidi ni kazi kubwa inayofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea Watanzania maendeleo na kuhakikisha amani ya nchi inalindwa," alisema.
Alieleza kuwa pia amevutiwa na utekelezaji wa falsafa ya 4R inayosisitiza maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya, akisema imeongeza mshikamano na kuimarisha mazingira ya maendeleo nchini.
Akizungumzia Mkoa wa Tanga, Jumbe alisema mabadiliko yanayoonekana katika sekta mbalimbali ni ushahidi wa dhamira ya Serikali ya kuufungua mkoa huo kiuchumi.
Alitaja kuongezeka kwa shughuli katika Bandari ya Tanga, ujenzi wa bandari kavu pamoja na utekelezaji wa miradi mingine ya kimkakati kuwa miongoni mwa hatua zilizochochea ukuaji wa uchumi na kuongeza fursa za biashara.
"Nimekuwa nikipaza sauti kwa miaka mingi nikitaka Tanga ifunguliwe kiuchumi. Leo naona hilo limefanyika. Mizigo imeongezeka bandarini, bandari kavu zimejengwa na shughuli za biashara zinaendelea kukua," alisema.
Katika sekta ya afya, Jumbe alisema maboresho yaliyofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na ujenzi wa zahanati katika kata na mitaa mbalimbali vimempa imani kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma kwa wananchi.
Aidha, alisema upanuzi wa huduma za maji na umeme pamoja na utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ni miongoni mwa hatua zinazoonyesha dhamira ya Serikali ya kuinua maisha ya Watanzania.
"Nilijiuliza ni hoja gani itanifanya nibaki upinzani wakati maendeleo yanaonekana wazi. Tanga ina amani, huduma zinaimarika na wananchi wanaendelea kunufaika na miradi ya maendeleo," alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, alisema chama hicho kinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano ili kuongeza uwezo wake wa kusimamia maendeleo na kuwatumikia wananchi.
Alisema tangu alipopewa dhamana ya kuongoza CCM mkoani humo, ameweka mkakati wa kuimarisha chama kupitia ushirikiano na wanachama pamoja na kuwakaribisha viongozi kutoka vyama vingine vya siasa.
Rajab alisema mkakati huo umeendelea kuzaa matunda, akieleza kuwa kujiunga kwa Rashid Jumbe ni ishara ya kuongezeka kwa imani ya baadhi ya viongozi wa upinzani kwa juhudi za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali.
"Jumbe alikuwa mmoja wa viongozi wakubwa wa upinzani katika Wilaya ya Tanga. Tuliahidi kwamba tutamshawishi aje kushirikiana nasi katika kujenga chama na kuwaletea wananchi maendeleo, na leo tumefanikiwa," alisema.
ADO AAHIDI UFANISI, UADILIFU NA UMADHUBUTI USIMAMIZI SEKTA ZA FEDHA NA MIPANGO
siasa“Nimeupokea kwa unyenyekevu na hamasa uteuzi wa kuwa Msemaji wa Sekta ya Fedha, Mipango na Hifadhi ya Jamii wa Kamati ya Wasemaji wa Kisekta ya ACT Wazalendo. Wajibu wangu ni kuzisimamia Wizara za Fedha chini ya Balozi Hamis Mussa Omar na Wizara ya Mipango na Uwekezaji chini ya Prof. Kitila Mkumbo.
Wizara hizi zimebeba taasisi nyeti kama vile Benki Kuu ya Tanzania na Sekta ya Benki kwa Ujumla wake, Hazina, TRA, Taasisi ya Manunuzi ya Umma (PPRA), TISEZA na Taasisi nyinginezo katika tasnia ya fedha na mipango.
Ninamshukuru Kiongozi wa Chama Ndugu Dorothy Semu kwa uteuzi huu. Nitatekeleza wajibu wangu kwa ufanisi, uadilifu na umadhubuti”- Ado Shaibu Ado.
KATIBU MKUU WA CCM AKUTANA NA BALOZI WA UINGEREZA KUJADILI USHIRIKIANO WA MAENDELEO NA DIRA 2050
siasa
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Asha-Rose Migiro, leo Ijumaa Juni 5,2026 amefanya mazungumzo na Mheshimiwa Marianne Young, Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma.

Mazungumzo hayo yalihusu maeneo ya ushirikiano wa maendeleo kati ya Tanzania na Uingereza, kwa kuzingatia vipaumbele vilivyobainishwa katika Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2025–2030, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).
Viongozi hao walijadili fursa za kuendeleza ushirikiano kwenye maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hususan katika kuwawezesha vijana na wanawake kupitia elimu, ujuzi, ubunifu na uwekezaji.

CCM inaendelea kuthamini ushirikiano wa kimataifa unaochangia maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi wa Tanzania.
NLD YAKEMEA WANAOWINDA URAIS 2030
siasaNa Oscar Assenga, Tanga
CHAMA Cha National League for Democracy (NLD),kimeonya wanasiasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kuonyesha nia ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2030 kuelekeza nguvu zao katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi badala ya kuanza harakati za kisiasa mapema.
Onyo hilo limetolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha NLD Doyo Hassani Doyo wakati akizungumza na wabahabari Jijini Tanga baada ya kuhitimisha ziara ya kichama katika Mkoa wa Tanga, akieleza kuwa Taifa kwa sasa linahitaji mjadala unaolenga maendeleo na ustawi wa wananchi kuliko mjadala wa urais ambao muda wake bado haujafika.
Alisema ingawa Katiba na sheria za nchi zinatoa haki kwa kila mwananchi mwenye sifa kugombea nafasi yoyote ya uongozi, ikiwemo urais, si jambo la busara kwa viongozi kuanza kujinadi kisiasa wakati wananchi bado wanakabiliwa na changamoto nyingi za maendeleo.
Aidha alisema ni haki ya kikatiba na kisheria kugombea nafasi yoyote ya uongozi lakini kwa mtazamo wake anaona jambo hilo sio lenye afya kwa Taifa kuanza mijadala ya urais miezi michache tu baada ya uchaguzi mkuu kumalizika,.
Alidai kuwa katika siku za hivi karibuni baadhi ya wabunge wa CCM wamekuwa wakitoa kauli katika Bunge na kwenye mikutano ya hadhara ambazo, kwa tafsiri yake, zinaashiria kuanza kwa harakati za kuwania urais wa mwaka 2030.
Kwa mujibu wa Doyo, viongozi waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wanapaswa kutumia nafasi zao kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuibua hoja zenye tija na kuishauri serikali katika masuala yatakayoboresha maisha ya Watanzania.
“Wananchi waliwachagua wabunge wao kwa matarajio ya kuona changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi. Tungetarajia kuona nguvu nyingi zikielekezwa katika kujadili maendeleo, uchumi, huduma za jamii na ustawi wa wananchi kuliko kujenga mazingira ya kampeni za uchaguzi ambao bado uko mbali,” alisema.
Aliongeza kuwa kuanza kwa siasa za urais mapema kunaweza kuathiri umakini wa viongozi katika utekelezaji wa majukumu yao na hata kupunguza kasi ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya wananchi.
Doyo pia aligusia kauli mbalimbali zilizowahi kutolewa na baadhi ya viongozi wa serikali kuhusu watu wanaotamani nafasi ya urais mapema, akisema hali hiyo inaonyesha dalili za kuanza kujitokeza kwa makundi ya kisiasa ndani ya chama tawala kabla ya wakati wake.
Hata hivyo, alisisitiza kuwa viongozi wa vyama vyote vya siasa wanapaswa kuweka mbele maslahi ya taifa kwa kushirikiana kutafuta suluhisho la changamoto zinazowagusa wananchi katika maisha yao ya kila siku.
Katika hatua nyingine, Doyo aliwataka Watanzania kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan katika juhudi zake za kusimamia maendeleo ya nchi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
“Sasa ni wakati wa kushughulikia changamoto za wananchi, kuimarisha huduma za kijamii na kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya taifa. Wakati wa siasa za urais ukifika, kila mwenye sifa na nia atapata nafasi ya kujitokeza,” alisema.
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa NLD Wilaya ya Tanga amesema bado kuna changamoto nyingi zinazohitaji ufumbuzi wa haraka mkoani humo, hususan katika sekta ya maji na miundombinu ya barabara.
Alisema viongozi wa chama hicho walijionea hali halisi ya baadhi ya maeneo wakati wa ziara yao, ambapo wananchi wengi bado wanakabiliwa na uhaba wa maji safi na salama pamoja na miundombinu duni inayokwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii.
Alitaja baadhi ya barabara zinazounganisha maeneo ya Maramba, Mashewa, Korogwe, Mwakijembe na Lushoto kuwa miongoni mwa miundombinu inayohitaji maboresho ya haraka kutokana na hali yake kuwa mbaya.
“Tulipita katika maeneo mbalimbali na kujionea changamoto wanazokabiliana nazo wananchi. Bado kuna maeneo mengi yenye matatizo ya maji na miundombinu ambayo yanahitaji kipaumbele kutoka kwa mamlaka husika,” alisema.
Viongozi hao wa NLD walihitimisha kwa kuitaka serikali, viongozi wa kisiasa na wadau wa maendeleo kuelekeza nguvu katika kutatua kero za wananchi na kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo, wakisisitiza kuwa wananchi wanahitaji kuona matokeo ya maendeleo kuliko kushuhudia mijadala ya uchaguzi ambao bado uko miaka kadhaa mbele.
MWISHO
MWENYEKITI WA CCM TANGA YAKABIDHI MILIONI 500 KUKAMILISHA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI WAKE
siasa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimeongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wake wa ujenzi wa nyumba 36 za watumishi baada ya Mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo, Rajab Abdulrahman, kukabidhi shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo unaotekelezwa katika wilaya tisa za mkoa huo.
Fedha hizo zilikabidhiwa kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, katika hatua inayodhihirisha dhamira ya chama ya kuboresha mazingira ya kazi na makazi kwa viongozi wake wa ngazi za wilaya.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Rajab alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba mwaka huu na kwamba utakuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha utendaji wa watumishi pamoja na shughuli za chama katika maeneo mbalimbali ya mkoa.

Alieleza kuwa mradi huo una thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.5, huku fedha zote zinazohitajika kwa ajili ya utekelezaji wake zikiwa tayari zimepatikana kupitia michango ya wanachama, viongozi na wadau mbalimbali wa chama.
"Mradi huu unagharimu jumla ya shilingi bilioni 2, milioni 500 na laki 250. Fedha hizi zimepatikana kupitia michango mbalimbali ikiwemo milioni 56 zilizotolewa awali, milioni 10 kutoka kwa MNEC pamoja na michango iliyokusanywa kutoka wilaya zote za mkoa," alisema Rajab.

Mwenyekiti huyo alibainisha kuwa kukamilika kwa nyumba hizo kutasaidia kutatua changamoto za makazi kwa baadhi ya viongozi wa chama katika ngazi ya wilaya, jambo litakaloongeza utulivu wa kazi, uwajibikaji na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Alisema nyumba hizo si tu kwamba zitakuwa makazi ya viongozi, bali pia ni uwekezaji wa muda mrefu wa chama katika kujenga taasisi imara yenye uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuendelea kuwahudumia wanachama wake.

"Tunajenga misingi ya chama kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Viongozi wanaweza kubadilika, lakini miundombinu tunayojenga leo itaendelea kulitumikia chama kwa miaka mingi ijayo," alisisitiza.
Rajab aliongeza kuwa ujenzi wa chama ni jukumu endelevu linalohitaji mshikamano wa wanachama wote, akisisitiza kuwa maendeleo ya chama hayawezi kupatikana bila ushiriki wa pamoja wa wanachama wake.

Kutokana na hilo, aliwataka wana-CCM wa Mkoa wa Tanga kuendelea kuchangia kwa hali na mali, kutumia elimu na uzoefu wao pamoja na nguvu kazi katika kukiimarisha chama.
Kwa upande wake, Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, alisema mradi huo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa chama wa kuimarisha utendaji wake katika ngazi za wilaya kwa kuhakikisha viongozi wanapata mazingira bora ya kazi na makazi.
Alifafanua kuwa kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo zitatumika na viongozi muhimu wa chama na jumuiya zake.

"Kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo ni nyumba ya Katibu wa CCM wa Wilaya, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Vijana, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi pamoja na nyumba ya Katibu wa UWT," alisema Kizigo.

Alieleza kuwa uwepo wa nyumba hizo utasaidia kupunguza gharama za upangaji wa makazi, kuimarisha upatikanaji wa viongozi katika maeneo yao ya kazi na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za chama na jumuiya zake.
Kwa mujibu wa Kizigo, kukamilika kwa mradi huo kutakuwa hatua muhimu katika kuijengea CCM Mkoa wa Tanga miundombinu imara itakayosaidia kuendeleza shughuli zake za kisiasa, kiutawala na kijamii kwa ufanisi zaidi katika miaka ijayo.



































