Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

BUSANDA JIKUMBUSHENI HISTORIA YA JIMBO LENU - DKT. BITEKO

October 25, 2025 Add Comment

Wananchi wa Jimbo Busanda, wilayani Geita wametakiwa kujikumbusha hatua za maendeleo zilizofikiwa katika eneo lao na kujotokeza kupiga kura Oktoba 29 mwaka huu.

Wito huo umetolewa Oktoba 24, 2025 na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa na mgombea wa Ubunge Jimbo la Bukombe, Dkt. Doto Mashaka Biteko wakati akihutubia katika Mkutano wa Kufunga Kampeni Jimbo la Busanda.

“Nawaomba mjikumbushe kuhusu maendeleo yaliyofikiwa katika kipindimcha miaka michache iliyopita. Maendeleo yaliyofikiwa katika sekta ya elimu, sekta ya Afya, miundombinu ya Barabara na maendeleo katika sekta ya umeme makubwa” amesema Dkt. Biteko.

Amesisitiza kuwa wana Busanda watakuwa na haki ya kudai maendeleo zaidi endapo watatimiza haki yao ya kikatiba kwa kujitokeza kupiga kura ifikapo Oktoba 29, mwaka huu.

Aidha amewaomba wananchi kumchagua mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, mbunge na madiwani kutoka CCM ili waendeleze mafanikio yaliyopatikana.

Naye Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Geita, Nicholaus Kasendamila amewataka wananchi kujiandaa na kujipanga kwa ajili ya tukio la upigaji kura ifikapo Oktoba 29, mwaka huu.

“ Jiandae na kujipanga kwa ajili ya kuwachagua viongozi waleta maendeleo ili kufanikisha hilo kila mwana CCM aliyejiandikisha ajitokeze kupiga kura” amesema Kasendamila.


Kwa upande wake, mgombea ubunge Jimbo la Busanda, Dkt. Jafari Seif amewashukuru wajumbe wa chama hicho kwa kumchagua kuwa mgombea wa kiti cha ubunge ili aweze kuwawakilisha.

Pia amemshukuru Dkt. Samia kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni humo.

Dkt. Seif pia amewaomba wana Busanda kumchagua Dkt. Samia, Mbunge na madiwani wa CCM ili waendeleze ushirikiano katika kutekeleza miradi ya maendeleo.

MWANA FA AMHAKIKISHIA MCC RAJAB USHINDI WA CCM ASILIMIA 100 KATA YA NKUMBA

October 24, 2025 Add Comment

 



**📍 Mgombea Ubunge Aahidi Kushughulikia Uzio wa Sekondari kwa Fedha za Mfukoni Ikiwa Serikali Itachelewa**


**📍 Ustadh Rajab Asema CCM Ni Mwalimu wa Siasa, Awataka Wananchi Walinde Amani**


**Na Mwandishi Wetu, Kata ya Nkumba**


MGOMBEA Ubunge Jimbo la Muheza kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), **Hamis Mwinjuma**, maarufu kama **MwanaFA**, amemhakikishia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM (MCC), **Ustadh Rajab Abdulrahaman Abdallah**, kwamba chama hicho kitashinda Kata ya Nkumba kwa asilimia 100.


Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Kijiji cha Nkumba-Kisiwani, MwanaFA alisema ushindi huo unatokana na idadi kubwa ya wanachama wa CCM waliojiandikisha katika kata hiyo.


Alifafanua kuwa katika kata hiyo, idadi ya wanachama wa CCM ni **4,984**, huku idadi ya watu waliojiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ikiwa ni **4,807**.

"Ndugu Mwenyekiti, ukitazama wanachama wetu na watu waliojiandikisha, unaona kabisa tunakwenda kushinda. Nikutoe hofu, hapa tutashinda kwa asilimia 100 kura za Rais, mbunge na diwani, kama tu hatutakuwa tumekwanza wenyewe kwa wenyewe," alisema MwanaFA.


### **Sifa kwa Rais Samia na Miradi Iliyotekelezwa**


Mgombea huyo aliwaomba wananchi wa Nkumba kuhakikisha wanajitokeza kupiga kura na kuwachagua wagombea wa CCM.


Alisisitiza kuwa anasimama kifua mbele kumuombea kura **Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan** kutokana na kazi kubwa aliyoifanya Nkumba. Alibainisha kuwa ndani ya miaka minne na nusu, Rais Samia ameleta jumla ya **Shilingi Bilioni 2.1** kutekeleza miradi mbalimbali:


* **Elimu:** Sh. Milioni 121.9 zilitolewa kwa ajili ya Sekondari ya Nkumba, na Sh. Milioni 115.5 kwa Elimu ya Msingi kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo, na ukarabati.

* **Afya:** Sh. Milioni 49.3 zilitumika kwa ajili ya ujenzi wa zahanati.

* **Maji:** Mradi wa Sh. Milioni 630 uliwezesha uchimbaji wa visima vinane, ambapo kila kitongoji katika vijiji vitano vya kata hiyo kilipata kisima kimoja.

* **Umeme:** Sh. Milioni 345 zimetumika kufikisha Umeme katika vitongoji na vijiji.

* **Huduma za Jamii:** Vikundi vitano vya wajasiriamali vilipata Sh. Milioni 34, na vijiji vyote vimenufaika na TASAF.

### **Ahadi za Miaka Mitano Ijayo**


MwanaFA, ambaye mkutano huo ulikuwa wa mwisho katika kata zote 37 za jimbo lake, aliahidi mambo makuu atakayotekeleza katika miaka mitano ijayo:


1.  **Ujenzi wa Uzio (Fensi):** Ujenzi wa uzio wa Sekondari ya Nkumba, akiahidi kutoa **fedha zake za mfukoni** iwapo Serikali itachelewa kuleta fedha.

2.  **Kipaumbele:** Kushughulikia na kukamilisha miradi yote iliyoanzishwa na serikali katika sekta za Elimu, Afya, Maji, Barabara, na Umeme.

3.  **Maji:** Kuchimba visima katika vijiji vya **Kwemhosi** na **Ubembe**.

### **Ustadh Rajab Atoa Onyo Kuhusu Amani**


Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, **Ustadh Rajab Abdulrahaman Abdallah**, aliwaongoza vijana na wazee kukumbuka historia ya Tanzania tangu ilipoasisiwa.

Alisisitiza kuwa **CCM ni Mwalimu wa vyama vya ukombozi** Kusini mwa Jangwa la Sahara na ndio maana inashinda kila uchaguzi, kutokana na misingi miwili mikuu: **Kutekeleza Ilani yake** na **Kulinda Amani**.


Ustadh Rajab aliwataka wananchi wasiharibu amani iliyopo kwa kisingizio cha uchaguzi, akionya kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee ya kukimbilia katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini.

"Tusifanye utani hata kidogo na amani hii. Twendeni tukachague wagombea wa CCM ili wawaletee maendeleo pamoja na kulinda Amani. Wenzetu wakiuana huko hawana pa kukimbilia isipokuwa nchini kwetu. **Kuchagua CCM ni kuchagua Amani**," alisema, akitaja Burundi, Rwanda, na Msumbiji kama nchi zilizowahi kuhifadhi wakimbizi Tanzania.

### **Viongozi Wengine Wamtia Nguvu MwanaFA**


Naye mgombea Udiwani wa Kata hiyo, **Omar Kidundai**, aliahidi kushirikiana na mbunge na Rais kutatua changamoto zote. Alisema ametumia mikutano 18 kuomba kura na wananchi wameahidi kuwachagua wagombea wa CCM.

Kwa upande wake, **Balozi Adadi Rajab**, aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Muheza (2015-2020), alimtaja MwanaFA kama mbunge mwenye uwezo wa kusukuma maendeleo na anatosha kuendelea kuaminiwa.

"Mimi kule bungeni nilipokuwa nilikuwa naongea sana, lakini niliambulia kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama. Lakini MwanaFA alipoingia kule, ametufanyia kazi nzuri na Rais amempa Uwaziri. Nasema mbele yenu **sitagombea tena ubunge Muheza, MwanaFA anatosha**," alisema Balozi Rajab.


Mratibu wa Kampeni Jimbo la Muheza, **Swahibu Mwanyoka**, aliwataka wananchi kuachana na wagombea wa upinzani kwa kuwa hawana nia ya kuwaletea maendeleo, na akawaonya wasiwe na hofu kwani vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga.



DCI MSTAAFU BALOZI ADADI -WATANZANIAA MSIOGOPE OCTOBA 29 AMANI NA UTULIVU VITATAWALA

October 24, 2025 Add Comment





>Awataka watanzania kutoka kwa wingi kupiga kura kumchagua Dkt Samia Suluhu,Wabunge na Madiwani wanaotokana na CCM.

Na Oscar Assenga,MUHEZA.

MKURUGENZI Mstaafu wa Makosa ya Jinai nchini (DCI) Balozi Adadi Rajabu amesema kwamba suala la amani na utulivu ni muhimu Octoba 29 mwaka huu kupiga kura huku akiwataka watanzania kujitokeza kwa wingi na kwamba siku hiyo hakutakuwa na maandamano yoyote kutokana na uimara wa vyombo vya ulinzi hapa nchini.

Balozi Adadi aliyasema hayo wakati wa mkutano wa kampeni wa kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Hamisi Mwinjuma alimaarufu Mwana FA katika halfa ambayo mgeni rasmi alikuwa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhamani ambapo alisema suala la amani ni muhimu sana

Alisema kwamba anasema hayo kutokana na kwamba yeye amekulia kwenye vyombo na anajua vyombo hivyo vinafanya nini vipo kwenye mazoezi kuangalia wale ambao wataleta chokochoko Octoba 29 washughulike nao.

“La mwisho suala la amani na utulivu Octoba 29 ni muhumu kuna watu wametokea wanaleta chochoko kwenye mitandano kwamba kuchafua na maandamano nawahakikishia hakutakuwa na maandamabo vyombo vipo imara”Alisema

“Niwaambie kwamba mimi nimekulia kwenye vyombo na najua vyombo vinafanya nini vipo kwenye mazoezi kuangalia wale ambao wataleta chokochoko Octoba 29 nawaomba mtokea kwa amani ikiwemo misusuru ya kwenda kwenye vituo vya kupigia kura mimi nitapiga kura Kerenge”Alisema

Aidha alisema kwamba baada ya kupiga kura ataangalia hali ya usalama inaende vipi hivyo kuwataka watoke wasiwe na hofu yoyote kwamba kutakuwa na watu gani ambao watawashauri waangamane wewe umeshaona watu wa aina hiyo.

“Vitu vya namna hii havijawahi kutokea sijaona mimi kulikuwa na ndugu zangu Waislamu miaka nipo kazini kulitokea maandamano mengi kule Magomeni kwa hiyo wachache wakafungwa ,wachache wakaenda jela”Alisema

Alisema kwamba lakini wale walivyotoka jela wakasema yale yalikuwa ni mambo ya kipumbavu wenzao waliwauza kuna wenzao waliwauza wao hawakutokea walikaa nyuma nyuma wao walikuwa mbele wakadakwa wakafungwa na kueleza hawarudiii tena hilo ni somo hivyo wapige kura kwa amani na utulivu bila matatizo yotote .

Balozi Adadi aliwambia wana Muheza katika mkutano huo kwamba wana kila sababu ya kumchagua Dkt Samia Suluhu kwa sababu ya mambo ambayo ameyafanya katika kipindi cha miaka minne kipovu haambiwa tazama ukiangalia malengo kila upande samia amegusa na uchumi umeongezekana na upo juu ukiangalia sekta ya miundombu barabara za lami nchi nzima.

Alisema pia ukiangalia ndege ambazo zimekuja zipo zaidi ya 15 pamoja na treli ya SGR watu siku hizi wanalala Dodoma wanakwenda kufanya kazi Dar huku wanalala Morogoro wanakwenda kufanya kazi Dar yote ni uchumi kuongezeka kwa kasi,.

Akizungumzia watalii alisema kwamba yeye alikuwa Balozi nchini Zimbabwe kivutio cha utalii ni kimoja tu Victoria Falls wale walikuwa wanaingiza watalii 2,500 na Samia Suluhu alivyoingia madarakani hapa nchini kuna vivutio vingi sana pamoja na vyote hivyo lakini watalii ambao walikuwa wanaingia walikuwa hawafiki Milioni 1 sasa hivi baada ya Royal Tour na sio raisi kufanya hivyo.

Alisema lakini Dkt Samia Suluhu alivunja rekodi aliingia na kufanya filamu ya hiyo na sasa wanaingiza watalii Milioni 5 na nusu lakini pia amefanya mambo mengi sana na uchumi umepanda kwa kiasi kikubwa sana na hata mfumuko wa bei upo katikati ni kitu cha kujivunia.

Hata hivyo aliwaomba wananchi wa Jimbo la Muheza kumchagua Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM) Hamisi Mwijuma alimaarufu Mwana FA kwa sababu ni Mbunge k mwenye uwezo wa kila kitu na hatuwezi kuwa na mbunge anakuwa njaa badala ya yeye kuombwa yeye anaomba.

“Jamani Muheza tunahitaji Mbunge kama huyo ?hatuwezi kuwa na mbunge ambaye anaambiwa zahanati haijapauliwa anagonjea fedha ya Serikali sasa si kichekesho hicho,”Alisema

Balozi Adadi alisema kwamba anamuona mwana FA ndio mbunge ambaye anaweza kuongoza wilaya ya Muheza kutokana na uwezo wake akiingia bungeni sio bubu wala kukaa mjengoni kwani kuna wabunge wana lala miaka 5 hawajafungua mdomo.

“Mimi sikugombea safari hii na sidhani kama nitagombea tena lakini nilimuita mwana FA tukaongea yeye ndio anastahili kushika Jimbo la Muheza yeye ndio mwenye uwezo yeye akiingia bungeni sio bubu wala kukaa mjengoni kuna wabunge wengine wana lala miaka 5 hajafungua mdomo kuzungumza”Alisema

Aliwataka wana Muheza wamuombee ili aweze kuingia tena mjengoni aweze kuchaguliwa kuwa Waziri hiyo ni sifa ya Muheza unapokuwa waziri unakuwa na Faida na una uwezo wa kuongea na Mawaziri wenzake ,makatabu wakuu wowote ili Muheza iweze kupata msaada.

Hata hivyo alisema kwamba hata mbunge anatakiwa awe na nguvu ya kugonga kokote na hawahitaji wabunge waoga waoga hivyo lakini pia chagueni na madiwani ambao ni mahiri ambao wanaendea kutuletea maendeleo.

Mwisho.

MWENYEKITI WA CCM NA RAIS MSTAAFU DKT. KIKWETE AHITIMISHA KAMPENI ZA UCHAGUZI KATIKA MAJIMBO MATANO YA ZANZIBAR

October 23, 2025 Add Comment







Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo amehitimisha rasmi kampeni za uchaguzi kwa majimbo matano ya Zanzibar, akiwataka wananchi wa pande zote mbili za Muungano kujitokeza kwa wingi ifikapo Oktoba 29 kupiga kura kwa amani, umoja na utulivu.

Dkt. Kikwete alihitimisha kampeni hizo katika mkutano mkubwa wa wa hadhara uliofanyikia katika uwanja wa Skuli ya Ghana jimbo la Uzini Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini na Shehia ya Kiboje, na kuhitimisha kampeni za majimbo ya Tunguu, Chwaka na Uzini katika Wilaya ya Kati, pamoja na majimbo ya Paje na Makunduchi, Wilaya ya Kusini Unguja.



Akihutubia mkutano huo, Dkt Kikwete amesisitiza kuwa wananchi hawana sababu ya kuwa na wasiwasi, kwani Tanzania inasifika kwa utamaduni wa uchaguzi wa amani, uliosimama katika misingi ya demokrasia, uadilifu na umoja wa kitaifa.

Dkt. Kikwete amesema ana imani kubwa kuwa wagombea wa CCM wataibuka na ushindi kutokana na utekelezaji wa Ilani wa chama hicho kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 85.

“Asilimia 15 zilizosalia ni miradi ambayo utekelezaji wake unaendelea. Yaani kazi imeshaanza. Hii inathibitisha msemo wetu kwamba ‘CCM ikiahidi, inatekeleza,’” alisema kwa msisitizo, akipigiwa makofi na wananchi.



Amesema Ilani ya CCM imeendelea kudumisha misingi ya uhuru, umoja, amani na utulivu wa nchi, huku akiwataka wananchi kuendelea kuilinda amani hiyo ambayo ni tunu ya taifa.



“Tanzania ni nchi yenye utulivu na usalama. Wapo waliowahi kujaribu kuivuruga amani hiyo, lakini hawakufaulu, na hawatafaulu sasa. Rais na Amieri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan mwenyewe amewahakikishia Watanzania kuwa hakutakuwa na vurugu wala maandamano katika kipindi hiki cha uchaguzi,” aliongeza.



Dkt. Kikwete alieleza kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar, uchaguzi wa viongozi hufanyika kila baada ya miaka mitano, na mwaka huu, Oktoba 29, Watanzania watapiga kura kuchagua Rais wa Muungano, Rais wa Zanzibar, Wabunge, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani.



“CCM ina wagombea katika ngazi zote – kuanzia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Jamhuri ya Muungano, Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa Zanzibar, pamoja na wagombea wote wa ubunge, uwakilishi na udiwani katika kila jimbo, kata na wadi. Hii ndiyo nguvu ya chama chetu,” alisema Kikwete.



Akiendelea kueleza falsafa ya chama hicho, alisema CCM imekuwa na utamaduni wa kutoa Ilani ya Uchaguzi kila baada ya miaka mitano, ikieleza ahadi na vipaumbele vya chama vitakavyotekelezwa na serikali zake endapo kitapewa ridhaa.



“Ilani ndiyo mkataba kati ya CCM na wananchi. Huo ndio mwongozo wa viongozi wetu wanapotekeleza majukumu yao. Hata hivyo, wagombea hawazuiliwi kuongeza mambo mapya kulingana na mahitaji ya wananchi,” alifafanua.



Akitolea mifano, Dkt. Kikwete alisema viongozi mbalimbali wa CCM akiwemo Hayati Rais Benjamin Mkapa, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, na hata yeye mwenyewe, waliwahi kutoa ahadi nje ya Ilani kutokana na maoni ya wananchi waliokutana nao wakati wa kampeni.

“Ahadi ni deni, na wananchi hawasahau. Ni kama msemo ule wa ‘mla kunde husahau, lakini mtupa maganda hasahau,’” alisema kwa tabasamu.



Dkt. Kikwete pia alitoa pongezi maalumu kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoendesha kampeni kwa uwazi, ukweli na ufasaha.



“Wananchi wanapenda kiongozi anayesema ukweli. Anayeonyesha mafanikio yaliyopatikana na kukiri changamoto zilizopo huku akieleza mipango ya kuzitatua. Huyo ndiye Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, mwanamke jasiri, mkweli na mwenye dira ya maendeleo,” alisisisitiza





Aidha, alimpongeza Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kipindi chake cha uongozi, akisema kuwa ametekeleza miradi mingi mipya ambayo haikuwa hata kwenye Ilani ya CCM.



“Dkt. Mwinyi ameleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi, kijamii na kiutawala Zanzibar. Hii ni ishara ya kiongozi mwenye maono na anayejali wananchi wake,” alisema.



Dkt. Kikwete alimaliza kwa kuwataka wananchi wote wa Zanzibar na Tanzania Bara kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi, kupiga kura mapema, na kuhakikisha kuwa amani inatawala katika kila hatua ya zoezi hilo.



Tanzania ni yetu sote, na amani yake ni jukumu letu sote. Tuwaheshimu viongozi, tuwapigie kura kwa utulivu, na tushiriki katika kuimarisha demokrasia yetu,” alihitimisha huku akishangiliwa kwa vifijo na nderemo.



Mwisho

KWAGILWA ATAJA UJENZI MPYA WA SOKO LA CHANIKA AMESEMA STENDI YA KISASA YA GHOROFA CHOGO INAKUJA

October 23, 2025 Add Comment



>Asisitiza safari hii maji yakitoka atakwenda Mahakamani kubadilisha Jina lake.

>Amtaja Dkt Samia Suluhu uwezeshaji wa Maendeleo Jimboni humo.

Na Oscar Assenga, HANDENI

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Handeni Mjini (CCM) Reuben Kwagilwa amesema dhamira ya Serikali ni kulibomoa soko la Chanika wilayani humo na kulijengwa upya ili liwe muonekano na kisasa pamoja na barabara katika mji huo wa Handeni kwa kiwango cha Lami.

Kwagilwa aliyasema hayo Octoba 22 mwaka huu Mjini Handeni katika eneo la Chanika wakati wa mkutano wa hadhara wa Kampeni uliohudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhman ambapo alisema kwamba Serikali ya Dkt Samia Suluhu imewapa kiasi cha Bilioni 15 ambazo Mwenyekiti huyo alisimama na kuzitaja




Alisema fedha hizo zitatumika kwenye ujenzi wa soko hilo ambalo litakuwa la kisasa katika mji huo wa Handeni utakaokwenda sambamba na ujenzi wa barabara za vwango vya lami kata ya Chanika barabara ya kutoka Mahada kwenda Minazini mita 680.

Alizitaja Barabara nyengine kuwa ni ya Rexona mita 130,Barabara ya Melini 110,Barabara ya Shehe Haditi mita 180 ambapo alisema wakimaliza hapo watahamia Kata ya Mdoe watakwenda kuivunja stendi ya Chogo na kujenga stendi ya Kisasa yenye ghorofa juu na chini na inakwenda kuwa stendi bora kuliko stendi zote mkoa wa Tanga na kusini mwa Tanzania.

Akziungumzia mradi wa Mradi wa Maji wa Miji 28 wa (HTM ) alisema kwamba ni mradi wa Kitaifa ambapo kwa upande wa handeni mradi huo umekakamilika kwa asilimia 71 na miezi minne ijayo unakwenda kukamilishwa asilimia 29 iliyobakia na tayari wameshajenga tenki kubwa ambalo limezamishwa chini ya mto pale Mswaha wanapokuchukulia maji wameshalaza mabomba kutoka juu ya mlima wa kilele cha Muhandeni.



Alisemamahali hapo wamejenga tenki kubwa la ukombozi la lita milioni 2 limekamilika kwa asilimia 100 wamelaza maji kutoka Kata ya Mlimani kwenda Kata ya Konje wamelaza kutoa mabomba mpaka Sindeni - Tabora kwenye machujio mpaka Mswaha mahali ambapo wanachukulia maji na tayari wameshakamilisha kazi kwa asilimia 71.

“Mgeukie mwenzako mwambie miezi minne ijayo maji yatatiririka kutoka juu ya kilele cha Mlima Mhandeni yataanzia kwenye Kata ya Chanika maji yatanzia Azimio,Changove,Kivesa,Kwamgumi na yatakwenda mitaa mitano kata ya Chanika, na miezi mine ijayo yatakwenda kata mzima ya Mdoe”Alisema

Alisema kwamba hawataishia hapo maji hayo yatatiririka baada ya hapo yatatiiika na kuifikia kata ya Kibaoni na miezi minne ijao kutoka juu ya Kilele cha Mlima Mhandeni yatakwenda Kata ya Konje wataaanzia Kitulwe na maeneo yote itakapata maji na hatimaye kuendelea kutiririka mpaka Kata ya Kwamagome.


Aliongeza kwamba pia maji hayo yatiririka katika Kata ya Kibeleko Kata, kata ya Kwediamba,Kata ya Kwenjugo,Kata ya Msasa,Kata ya Mlimani mahali ambapo wamejenga tenki kubwa la ukombozi mitaa yote 60 kata zote za Jimbo la Handeni mjini na siku hiyo miezi mine ijayo maji yatakapofika kwenye mitaa yote 60 na kata zote 12.

“Nimewahaidi wana Handeni siku hiyo miezi minne ijayo maji yakifika kwenye mitaa yenu nitaoga hadharani na hicho mnachokishangilia kukiona hamtakiona kwa sababu nitaoga na nguo na mara ya mwisho Handeni mjini na Handeni kwa ujumla kupata mradi mkubwa wa maji ilikuwa mwaka 1974”Alisema

Alisema kwamba enzi hizo mbunge alikuwa Musa Masomo imepita miaka 50 amekuja Rais ambaye kwa leo ni Mgombea Urais wa CCM Dkt Samia Suluhu amekuja ametuwekea mradi mkubwa huo na wanakwenda kuwaletea maji miezi minne.

“Miaka 50 ilyopita baada ya Mbunge Musa Masomo nimefuata mimi Kwagilwa Reubeni “Mamba Lwegwanani”Longwisho naweka nadhiri ya pili nasema miezi mine ijayo maji yakitiririka kwenye maeneo yetu nitakwenda mahakamani kubadilisha jina langu na kutokea siku hiyo nitaitwa Kwagilwa Reuben Santagwa Mamba Laigwanani Longisho Mussa Masomo “Alisema

Awali kizungumza katika Mkutano huo wa Kampeni ambapo alikuwa mgeni rasmi,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman aliwataka wananchi wa Handeni na Taifa kwa ujumla kuwachagua wagombea wanaotokana na chama hicho kutokana na kwamba ndio wazalendo watakaowaletea maendeleo