Na Masanja Mabula ,Zanzibar.
Makamu wa Kwanza wa
Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, ametembelea uwanja wa Amaan
Mjini Zanzibar kukagua maendeleo ya zoezi la uwekaji wa nyasi bandia katika
uwanja huo.
Meneja wa uwanja huo
Khamis Ali Mzee, amesema zoezi hilo linaendelea vizuri, huku wakiendelea
kukusanya vifaa zaidi kwa ajili ya kukamilisha zoezi hilo kwa wakati muafaka.
Amesema vifaa
vinavyoendelea kukusanywa kwa sasa ni pamoja na mchanga maalum ambao unakwenda
sambamba na uwekaji wa nyasi hizo ili kuweka umadhubuti zaidi wa uwanja huo.
Kwa upande wake
mkandarasi wa uwekaji wa nyasi hizo bw. Ben Mushi kutoka kampuni ya EKIKA ya
Dar es Salaam, amesema mvua zinazoendelea kunyesha zinazorotesha zoezi hilo.
Hata hivyo amesema watafanya kila juhudi kuona kuwa zoezi hilo linakamilika kwa wakati, ili uwanja huo uweze kutumika kwa sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi, zinazotarajiwa kufika kilele chake tarehe 12 Januari, 2014. |
Tamasha la Handeni Kwetu ni balaa, mambo yote burudani kabisa, chini ya Shirika la NSSF
MSIMU wa kwanza wa
Tamasha la Utamaduni Handeni, lililokuwa
likisubiriwa kwa hamu hatimaye lilifanyika Juzi, wilayani Handeni
Tanga ambapo kama ilivyokuwa ikitarajiwa, Shirika la Taifa la
mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) lilijitokeza na kubeba tamasha
hilo.
Meneja wa NSSF mkoani Tanga, Frank Maduga |
Shirika hilo, likiwa limejitokeza dakika za mwisho katoa udhamini wake
katika tamasha hilo kubwa na la kwanza kuwahi kufanyika katika Ardhi
ya wilaya ya Handeni linalojumuisha vijiji zaidi ya kumi, lilichangia
fedha taslimu shilingi milioni mbili, fedha ambazo kwa kiasi kikubwa
ukiacha mchango wa wahisani wengine zilichangia kufanikiwa kwa
Tamasha hilo.
Akizungumza wakati wa kutambulisha wadhamini na wahisani mbalimbali waliofanikisha kufanyika kwa Tamasha hilo, mratibu wa Tamasha la utamaduni Handeni 2013, Kambi Mbwana alisema kukiwa na dalili zote za tamasha kushindwa kufanyika kama ilivyotarajiwa, NSSF kupitia Ofisi ya kanda ya Tanga ilijitolea kunusuru Jahazi.
Akizungumza wakati wa kutambulisha wadhamini na wahisani mbalimbali waliofanikisha kufanyika kwa Tamasha hilo, mratibu wa Tamasha la utamaduni Handeni 2013, Kambi Mbwana alisema kukiwa na dalili zote za tamasha kushindwa kufanyika kama ilivyotarajiwa, NSSF kupitia Ofisi ya kanda ya Tanga ilijitolea kunusuru Jahazi.
Mratibu wa Tanmasha la Utamaduni Handeni-Kambi Mbwana akitambulisha Wadhamini wa Tamasha hilo lililofanyika Juzi katika uwanja wa Azimio, wilaya ya Handeni, Mkoani Tanga. |
Mkuu wa wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu akimkaribisha mmoja wa wahudhuriaji wa Tamasha la Handeni Kwetu 2013. |
Mkurugenzi wa Grace Products akitoa neno la Shukrani kwa Waandaji wa Tamasha |
“Awali ya yote napenda kutanguliza shukurani zangu zote kwa wahisani
wa Tamasha hili, Vodacom, Grace products pamoja a wadhamini wengine
kwa kufanikisha Tamasha hili la kwanza kuwahi kuwakutanisha watu wa
kadhia mbalimbali,
JKT walikuwepo wakafanya yao jukwaani
ilikuwa ni noma saaaana
|
DC Muhingo Rweyemamu |
Shukurani kubwa
ziende kwa NSSF, kwa kweli hawa watu wanajali utu,
tunaomba watusamehe kwa mapungufu yetu lakini kwa kweli wanastahili
kuitwa mfuko wa Hifadhi,” alisema Kambi
Awali akizungumza baada ya kuzindua Tamasha hilo ambalo lengo lake lilikuwa ni kuwakutanisha watu wa Handeni kusherekea utamaduni wao pamoja na kukumbusha umuhimu wa kujenga Handeni, Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, alisema kwa kuwa na Matamasha kama hayo jamii inaweza kuwa katika nafasi nzuri ya kupata Maendeleo wanayoyataka.
Muhingo alisema ili mafanikio yapatikane katika kila jambo ni lazima watu wa eneo Fulani wawe na utayari wa kukutana na kujadili mambo yao kwa sauti kama waratibu wa Tamasha hilo walivyofanya.
Awali akizungumza baada ya kuzindua Tamasha hilo ambalo lengo lake lilikuwa ni kuwakutanisha watu wa Handeni kusherekea utamaduni wao pamoja na kukumbusha umuhimu wa kujenga Handeni, Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, alisema kwa kuwa na Matamasha kama hayo jamii inaweza kuwa katika nafasi nzuri ya kupata Maendeleo wanayoyataka.
Muhingo alisema ili mafanikio yapatikane katika kila jambo ni lazima watu wa eneo Fulani wawe na utayari wa kukutana na kujadili mambo yao kwa sauti kama waratibu wa Tamasha hilo walivyofanya.
Vyakula vya Asili hapa palikuwa ni mahala pakee |
“Tunajivunia kuwa na vijana wenye mawazo mapana kama haya, naambiwa
tamasha hili ni matokeo ya mawazo ya kimaendeleo ya vijana wetu,
Hongereni sana,” alisema Rweyemamu.
Kwa upande wake, Meneja wa NSSF, mkoani Tanga, Frank Maduga alisema shirika hilo limedhamiria kuendelea kushirikiana na waaandaaji wa Tamasha hilo kwa lengo la kuhakikisha Utamaduni wa Mtanzania unatumika kulitangaza Taifa.
Kwa upande wake, Meneja wa NSSF, mkoani Tanga, Frank Maduga alisema shirika hilo limedhamiria kuendelea kushirikiana na waaandaaji wa Tamasha hilo kwa lengo la kuhakikisha Utamaduni wa Mtanzania unatumika kulitangaza Taifa.
Mamia ya Waandamanaji wakielekea katika Viwanja vya Azimio |
Taem Tamasha la Utamaduni Handeni....chezea |
Msanii kutoka katika kundi la Okalandima, akionesha uwezo wa kutafuna Moto, hii ni moja ya Vyakula vyetu huku Handeni hasa Kwamsisi, karibu Handeni Kwetu..... |
Katika tamasha hilo,kulikuwa na vionjo mbalimbali vya Utamaduni wa Wanahandeni, ikiwa ni Pamoja na Ngoma za asili kutoka katika Vijiji vya wilaya ya Handeni kama vile, Kweingoma, Kwamatukutu, Kwediamba, Kwachaga pamoja na vikundi vingine vya Handeni Mjini.
Burudani kali na ya kuvutia iliyoonesha asili kamili ya Mtanzania ilitoka kwa Kundi la Sanaa la Jeshi la JKT Mgambo, Azimio Jazz band bila kusahau msanii wa kundi la Fataki, Machenja ambaye alipiga onesho
la kukata kiu akiwa na wana okalandima.
Tamasha la Utamaduni Handeni ambalo linafanyika kwa mara ya Kwanza lilidhaminiwa na NSSF, Clouds fm, Vodacom, Plan B, gazeti la Mwananchi, MICHUZI BlogKajunason Blog, Chichi Local Wear, Katomu Solar specialist, Dullah Tiles and Construction, Anesa Company Limited, Country Business directory, Jiachie Blog na TAIFA LETU.com.
MAKATIBU UVCCM TANGA WAASWA.
imewekwa desemba 16,2013 saa 11:56 asubuhi.
Na Oscar Assenga, Korogwe.
Na Oscar Assenga, Korogwe.
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga
(UVCCM),Abdi Makange amewataka makatibu umoja huo ngazi ya wilaya na kata kuachana
na makundi ya uchaguzi mwaka 2014-2015 kwani hali hiyo itawafanya kushindwa
kutimiza wajibu wao ipasavyo na kuleta mpasuko ndani ya umoja huo.
Kauli hiyo aliitoa wakati wa kikao cha baraza la Vijana
wilaya ya Korogwe ambacho kilihusisha wajumbe kutoka wilaya ya Korogwe mjini na
Vijijini ikiwa ni ziara ya siku ya pili ya Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo mkoa wa
Tanga,Abdi Makange ya kukagua uhai wake na kusikiliza kero za wananchi maeneo
mbalimbali mkoani Tanga.
“WAZEE WA NGWASUMA KUZINDUA "CHUKI YA NINI"MZALENDO PUB DESEMBA 21.
IMEWEKWA DESEMBA 16,2013.
Na Raisa Said, Tanga.
BENDI ya FM Academia “Wazee
wa Ngwasuma” inatarajiwa kufanya uzinduzi wa Album yao
ya 10 iitwayo “Chuki ya Nini”Desemba 21 mwaka huu kwenye ukumbi wa Mzalendo Pub
jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Tanga Raha Blog kwa njia ya
simu, Rais wa Bendi hiyo, Nyoshi El Sadat alisema uzinduzi huo utaanza majira
ya moja usiku ambalo Utakwenda sambamba na burudani toka kwa bendi mahiri hapa nchini ya Mashujaa.
Sadat alisema bendi hiyo
imejipanga kikamilifu kuhakikisha inatoa burudani ya aina yake kwa wapenzi na
mashabiki wake hasa ukizingatia uzinduzi huo unafanyika siku chache kabla ya
kuuaga mwaka 2013.
Aidha alisema uzinduzi wa
Album hiyo umedhaminiwa na Kinywaji cha Wind Hoek Lager ambacho kitatoa bia
moja kwa kila mshabikiwa wa bendi hiyo ambaye atahudhuria siku hiyo.
Katika uzunduzi huo viingilio
vinatarajiwa kuwa kati y ash.20,000 kwa VIP n ash.15000 kwa viti vya kawaida
lengo likiwa ni kuwapa fuksa wapenzi wa mziki wa dansi kujitokeza kwa wingi
kushuhudia.
Subscribe to:
Posts (Atom)