Tigo yasherehekea wiki ya huduma kwa wateja kwa kutoa zawadi kwa wateja wake.

October 08, 2016


Mkuu wa kitengo cha huduma cha wateja Zakheem khan akifurahi pamoja na mteja aliyejipatia zawadi ya simu katika kusherekea wiki ya huduma kwa wateja zilizofanyika katika duka la Tigo  makumbusho mwishoni wa wiki hii
Sehemu ya wateja wa Tigo wakipata huduma.


PichanI  ni sehemu ya wateja wa Tigo wakipata huduma.


Wafanyakazi wa Tigo wakiwa na zawadi kwa ajili ya wateja katika duka la Makumbusho mapema mwishoni wa wiki hii

MSANII CHEGE AADHIMISHA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA KUTOA MSAADA KWA HOSPITALI YA TEMEKE JIJINI DAR

October 08, 2016
 Msanii wa Muziki wa kizazi kipya kutoka kundi la Wanaume Family, Chege Chigunda akiweka sawa baadhi ya zawadi alikuwa ameziandaa kwa ajili ya Wagonjwa Temeke Hospitali.
 Msanii wa Muziki kutoka kundi la Wanaume Family, Chege Chigunda akizungumza jambo na mmoja ya wauguzi wa Temeke Hospitali jijini Dar.
 Chege na Temba wakiteta jambo mara baada ya kuwasili katika Hospitali ya Temeke
 Chege Chigunda akizungumza na Waandishi wa habari
 Chege Chigunda na baadhi ya Wasanii kutoka kundi la Mkubwa na Wanawe wakielekea wodini
 Chege Chigunda akiwasiliana na baadhi ya watu kabla ya kuingia wodini
 Msanii wa Muziki wa Bongofleva Mheshimiwa Temba  akitoa zawadi kwa wagonjwa
 Chege Chigunda akitoa baadhi ya Zawadi kwa wagonjwa
 Mh Temba akiingia wodini  kupeleka zawadi kwa Wagonjwa
 Mhe. Temba akigawa zawadi kwa wagonjwa
 Baadhi wasanii kutoka kundi la Mkubwa na Wanawe akitoa zawadi kwa wagonjwa
 Chege Chigunda akiwa amembeba mtoto Hadija Abdalah akiwa na Mama yake Mwanahawa Juma.
Na Humphrey Shao, blog ya Jamii MSANII wa Muziki wa Bongo Fleva kutoka kundi la Wanaume Family Chege Chigunda , leo ameadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa kutembelea hospitlai ya Rufaa ya Temeke na kugawa zawadi mbalimbali katika wodi ya Watoto waliozwa hapo kutokana na matatizo mbalimbali. Akizungumza na Mwandishi wa blog hii Mapema leo Hospitalini hapo chege alisema kuwa imekuwa tofauti sana kwa watu kupenda kusheherekea katika nyumba za starehe lakini yeye ameamua kukaa na watoto hao wagonjwa hili kurudisha kile ancho kipata kwa jamii. “Chege Chigunda aezaliwa leo hivyo ndio maana nipo hapa motto wa Mama Said kushherekea siku yangu ya kuzaliwa na wagonjwa kwa kutoa zawadi mbalimbali kama mnavyoziona Pampers , Dawa za Mswaki na Dawa kwa ajili ya wagonjwa ambao awana uwezo wa kujijinunuli a hivyo katika siku ya leo wamepata fursa ya kununuliwa madawa na mimi” anasema Chege. Anasema kuwa maisha yamebadilika sana na inapaswa watu kurudi nyuma na kufanya yale yaliyoa mazuri yanayompendeza Mungu kwa kusheherekea siku zao za kuzaliwa na watu ambao wanamatazo na wenye uhitaji hili kuweza kuwapa faraja ambayo wakuwa wameikosa kwa muda kutokana na matatizo yaliyowakuta. Alimaliza kwa kutoa wito kwa wasanii na watu maharufu kuwa na utamaduni wa kuwakumbuka watu wenye mahitaji mablimbali kila wanapopata nafasi na kiasi kidogo kwani kutoa akuhitaji kuwa na utajiri mkubwa bali ni moyo tu.
-- ---- Cathbert Angelo Kajuna, Founder and Mananging Director Kajunason Blog, P.O Box 6482, Dar es Salaam. Tel: +255 787 999 774 Alt: +255 765 253 445 www.kajunason.blogspot.com "Everything is Possible Through Peace & Stability''

WAZEE WASTAAFU WANAWEZA KUWA MABILIONEA NA KUIBADILISHA NCHI

October 08, 2016



 Kaimu Mkuu wa wilaya ya Lushoto ambaye ni Afisa Tarafa ya Lushoto,Asha Kikoti akifungua mkutano wa uzinduzi wa chama cha wazee wastaafu wilayani Lushoto kushoto ni MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF hapa nchini, Adam Mayingu kulia kwake ni Mwenyekiti wa Chama cha Wazee wilayani humo Paul Kirua. 
MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF hapa nchini, Adam Mayingu akizungumza na wazee wastaafu wilayani Lushoto


MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF hapa nchini, Adam Mayingu akizungumza na wazee wastaafu wilayani Lushoto 
Meneja Matekelezo wa PSPF Franscis Mselemu akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa chama hicho kulia kwake ni MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF hapa nchini, Adam Mayingu       
MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF hapa nchini, Adam Mayingu wa kwanza kuhoto katikati ni Kaimu Mkuu wa wilaya ya Lushoto,Asha Kikoti kulia ni Katibu wa chama cha wazee wastaafu wilayani Lushoto(Chawasewili)Paul Kirua
MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF hapa nchini, Adam Mayingu akimkabidhi Katibu Mkuu wa Chama cha wazee Wastaafu wilayani Lushoto (Chawasewili) Paul Kirua katiba ya Chama hicho mara baada ya kukizundua kushoto ni Kaimu Mkuu wa wilaya ya Lushoto,Asha Kikoti

Katibu Mkuu wa Chama cha wazee Wastaafu wilayani Lushoto (Chawasewili) Paul Kirua akionyesha juu katiba ya Chama hicho mara baada ya kukizunduawilayani humo kushoto ni MKURUGENZI  Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF hapa nchini, Adam Mayingu





Wazee Wastaafu wilayani Lushoto wakimsikiliza kwa umakini Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF hapa nchini, Adam Mayingu


Mmoja kati ya Wazee Wastaafu wilayani Lushoto,Yohana Wiliamu akiuliza swali katika mkutano huo wa uzinduzi wa chama hicho

Mzee  Mstaafu wilayani Lushoto,Judica Mandia akiuliza swali kwenye mkutano huo

Juma Rashidi ambaye ni miuongoni mwa wazee wastaafu wilayani Lushoto akiuliza swali kwa mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF,Adam Mayingu



MKURUGENZI wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF hapa nchini, Adam Mayingu amesema kuwa wazee wastaafu wanauwezo wa kuwa mabilionea na kuibadilisha nchi kwa kutengeneza ajira ,kubuni miradi inayoweza kuwaingizia kipato baada ya kulitumikia taifa katika nafasi mbalimbali walizokuwa nazo.
Alisema kwani asilimia kubwa wanaweza kuanzisha miradi mbalimbali ambayo inaweza kuwasaidia kujiongezea kipato hali itakayopelekea vijana kuweza kuinua maisha yao kitendo ambacho pia kitasaidia kuongeza pato la serikali.
Mayingu aliyasema hayo wakati wa wiki ya huduma kwa wateja Duniani ambapo mfuko huo unakutana na wadau wake ili kuweza kubaini changamoto ambazo ikiwemo kuangalia namna ya kukabiliana nazo.
Wiki hiyo ilikwenda sambamba na uzinduzi wa chama cha wazee wastaafu wilayani Lushoto (Chawisewilu) chenye makazi yake mjini hapa waliokuwa wakifanya kazi na baadae kustaafu waliweza kuhudhuriwa kwa wingi na kutoa mapendekezo yao.
  “Ukiangalia wazee wastaafu wanapokuwa wamepata fedha zao za kiunua mgongo badala ya kwenda kuzitumia katika matumizi yasiyokuwa ya lazima badala yake waone namna ya kuzitumia kubuni miradi itakayokuwa chachu kwao kupitia hatua kubwa za kimaendeleo “Alisema.
“Sisi kama Mfuko wa Pensheni wa PSPF tunaunga mkono chama chenu lakini pia niwaambie Sido wapo tuzungumze nao ikiwemo kuweka utaratibu mzuri ili muweza kuona namna ya kuweza kunufaika na uwepo wao “Alisema.
“Lakini pia msisite kuwatumia wataalamu kwenye masuala mbalimbali ya ujasiriamali kwani hiyo ndio njia ambayo inaweza kuwa chachu ya kuweza kufikia malengo yenu hasa katika kipindi hiki kwa kushirikiana “Alisema.
Aidha pia aliwataka kupitia umoja wao kutumia fursa nyingi zilizopo kwenye maeneo yao kwani wanao umri wa kuishi mkubwa badala yake yaondokana na dhani ya kuwa watu wanapokuwa wakistaafu wanafariki kitendo ambacho sio hakina ukweli wowote.
Lakini pia aliwataka kutumia fursa hiyo waliyoipata kuieli misha jamii huku akiwaomba kupitia chama chao kuwahimiza vijana wao kujiunga ma mfuko wa Pensheni wa PSPF ili waweze kunufaika na mafao yanayotolewa.
Awali akizungumza wakati akifungua kikao hicho,Kaimu Mkuu wa wilaya ya Lushoto,Asha Kikoti aliwataka wazee wastafu kuhakikisha fedha wanazozipata za kiunua mgongo kuweka mpango mzuri wa kuzitumia kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo ili waweze kujiingizia kipato.
  “Kiuhalisia wazee wastaafu wanapopata fedha zao wanaona kama vile ni nyingi na kuzitumia bila kwa haraka bila kufikiria hata kuzianzishia miradi ambayo inaweza kuwasaidia kupambana na ukali wa maisha “Alisema huku akiwasisitizia wabadilike.
Sambamba na hayo aliwataka pia kuwa na mpango mzuri wa matumizi ya fedha zao za kiinua mgongo ili ziweze kuwasaidia kutumiza ndoto zao katika maisha ikiwemo kuwa na maisha mazuri.

Tanzania yashiriki Mkutano wa Mwaka wa Benki ya Dunia unaoendelea jijini Washington DC,nchini Marekani

October 08, 2016
 Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayeshughulikia kanda ya Afrika Louis Rene Peter Larose (hayupo Pichani), makao Makuu ya Benki hiyo Jijini Washington DC, Marekani, kulia kwake ni Katibu Mkuu w Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James.(Picha zote na Wizara ya Fedha na Mipango).
 Ujumbe wa wataalamu wa Fedha, Sera na Uchumi kutoka Tanzania wakifuatilia kwa makini Mazungumzo ya Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Louis Rene Peter Larose (hawapo Pichani), Makao Makuu ya Benki hiyo Jijini Washington DC, Marekani, ambapo unafanyika Mkutano wa Mwaka wa Benki hiyo ambayo Tanzania ni Mwanachama, wa kwanza kushoto ni Kamishna wa Sera Augustine Ollal, Kamishna wa Bajeti John Cheyo na Kaimu Kamishna wa Fedha za Nje Mamelta Mutagwaba.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Louis Rene Peter Larose walipokutana ofisini kwake Jijini Washington DC, Marekani, ambapo wamezungumzia masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya Tanzania na namna Benki hiyo ilivyojipanga kuhakikisha kuwa inaiwezesha Tanzania kufikia ndoto yake ya kuwa nchi yenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025
 Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, wakishikana mikono kuonesha umoja na mshikamano mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya ujumbe huo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Louis Rene Peter Larose, Jijini Washington DC nchini Marekani, ambako ujumbe huo unahudhuria Mkutano wa Mwaka wa Benki hiyo.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Katikati, Akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayeshughulikia kanda ya Afrika mara baada ya viongozi hao kumaliza mazungumzo yaliyogusia Nyanja mbalimbali za kijamii na kiuchumi, Jijini Washington DC, nchini Marekani, ambapo Tanzania inashiriki Mkutano wa Mwaka wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani-IMF.

DC NDEJEMBI AKIFUNGA CHUO CHA UALIMU NKURUMA - MKOKA KWA KUTAPELI WANAFUNZI

October 08, 2016
 MKUU wa Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, Mhe Deogratius Ndejembi

MKUU wa Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, Deogratius Ndejembi amekifunga Chuo cha Ualimu cha Nkuruma kilichopo Mkoka na kuagiza uongozi wa chuo kurudisha fedha zote za ada walizolipa wanafunzi ili ziwasaidie kulipia vyuo vingine.

MAADHIMISHO YA SIKU YA POSTA DUNIANI 2016, MKOA WA MWANZA WANG'ARA KWENYE SHINDANO LA UANDISHI WA BARUA KITAIFA.

October 08, 2016
Meneja wa Shirika la Posta mkoani Mwanza, Julius Chifungo, akizunguza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani ambayo kimkoa yamefanyika leo katika Shule ya Saint Mary's Seminary (Nyegezi Sekondari) Jijini Mwanza.

Siku ya Posta duniani huadhimishwa ifikapo Oktoba 09 kila Mwaka ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya Siku ya kuanzishwa kwa Umoja wa Posta Duniani ulioanzishwa mwaka 1874 katika mji wa Berne nchini Switzerland ukijumuisha mataifa 192 duniani.
Na BMG

Maadhimisho hayo yamekwenda sambamba na zoezi la kukabidhi zawadi kwa Washindi wa Uandishi wa barua Kitaifa kutoka mkoani Mwanza ambapo washindi watano kati ya 10 bora kitaifa wametoka Saint Mary's Seminary (Nyegezi Sekondari) Jijini Mwanza.

Washindi hao na nambari walizoshika kwenye mabano ni, Denis Bahati Stephen (01), Samwel Lufungulo Somelo (02), Vitalis Aloo Awasi (03), Kizito Eliakimu Paschal (04) na Fredrick Elias Mayunga (08).

Washindi wa Tano na Sita wametoka Shule ya Mazinde Juu mkoani Tanga, Mshindi wa Saba ametoka Shule ya Lugalo mkoani Iringa, huku Washindi wa Tisa na 10 pia wakitoka Shule ya Mazinde Juu mkoani Tanga.

Meneja wa Posta mkoani Mwanza, Julius Chifungo amesema shindano la uandishi wa barua huwashirikisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wasiozidi umri wa miaka 15 ambapo shule za msingi lugha ya kiswahili na kiingereza hutumika na kiingereza pekee kwa shule za sekondari. 

Amebainisha kwamba wanafunzi huandika barua yenye mane kati ya 500 na 1,000 kulingana na mada iliyotolewa na kwamba mwaka huu mada ilikuwa ni "Jiandikie barua ukiwa na miaka 45" ambapo barua ya mshindi wa kwanza itakwenda kushindanishwa na barua za washindi wengine kutoka nchi 191 wanachama wa Umoja wa Posta Duniani ambapo mshindi wa kwanza nchini ataliwakilisha taifa kwenye shindalo hilo nchini Switzerland.
Katibu Mtendaji wa Idara ya Elimu, Jimbo Kuu la Mwanza, Alex Masasi, ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo akizungumza ambapo amewahimiza wanafunzi kuongeza bidii katika masomo yao hususani kuwa bora kwenye kusoma, kuandika na kuzungumza lugha nyingi tofauti na kiswahili na kiingereza.
Wanafunzi wakimsikiliza kwa umakini Katibu Mtendaji wa Idara ya Elimu, Jimbo Kuu la Mwanza, Alex Masasi, ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho Siku ya Posta yaliyofanyika leo Jijini Mwanza.
Mkuu wa Shule ya Saint Mary's (Nyegezi Sekondari) Jijini Mwanza, akizungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani. Siku ya Posta duniani hufanyika kila mwaka Oktoba 08, hivyo yamefanyika leo Oktoba 07 kutokana na ratiba ilivyopangwa.
Mshindi wa Nane Kitaifa kwenye Mashindano ya Uandishi wa barua, Fredrick Elias Mayunga kutoka Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza akipokea zawadi yake.

Mshindi wa Nane amepokea Cheti cha utambuzi, Tisheti, Kamusi ya Kiingereza, begi la kubebea daftari, Kikokoteo pamoja na fedha Elfu Arobaini (40,000).
Mshindi wa Nne Kitaifa kwenye Mashindano ya Uandishi wa barua, Kizito Eliakimu Paschal, kutoka Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza akipokea zawadi yake.


Mshindi wa Nne amepokea Cheti cha utambuzi, Tisheti, Kamusi ya Kiingereza, begi la kubebea daftari, Kikokoteo pamoja na fedha Laki Moja na Elfu Ishirini (120,000).

Mshindi wa tatu Kitaifa kwenye Mashindano ya Uandishi wa barua, Vitalis Aloo Awasi, kutoka Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza akipokea zawadi yake.


Mshindi wa Tatu amepokea Cheti cha utambuzi, Tisheti, Kamusi ya Kiingereza, begi la kubebea daftari, Kikokoteo pamoja na fedha Laki Mbili (200,000)

Mshindi wa Pili Kitaifa kwenye Mashindano ya Uandishi wa barua, Samweli Lufungulo Somelo, kutoka Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza akipokea zawadi yake.


Mshindi wa Pili amepokea Cheti cha utambuzi, Tisheti, Kamusi ya Kiingereza, begi la kubebea daftari, Kikokoteo pamoja na fedha Laki Tatu (300,000)

Mshindi wa Kwanza Kitaifa kwenye Mashindano ya Uandishi wa barua, Denis Bahati Stephen, kutoka Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza akipokea zawadi yake.


Mshindi wa kwanza amepokea Cheti cha utambuzi, Tisheti, Kamusi ya Kiingereza, begi la kubebea daftari, Kikokoteo pamoja na fedha Laki Nne (400,000)

Mkuu wa Shule ya Saint Mary's Seminary, Maximillian Buluma, akipokea zawadi ya shule hiyo baada ya kuwa shule iliyotoa washindi kitaifa pamoja na washiriki wengi. Amepokea mpira pamoja na Cheti kutoka Shirika la Posta.
Kulia ni Meneja wa Posta Mwanza, Julius Chifungo, akimkabidhi mgeni rasmi zawadi
Washindi wa shindano la kuandika barua nchini, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la Posta Mwanza, Waalimu wa Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza, Mgeni Rasmi pamoja na Wazazi.
Washindi wa shindano la kuandika barua nchini kutoka shule ya Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wazazi wao.
Washindi wa shindano la kuandika barua nchini, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la Posta Mwanza.
Washindi wa shindano la kuandika barua nchini, wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa shule ya Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza, Mgeni Rasmi pamoja na Meneja wa Posta Mwanza.
Washindi wa shindano la kuandika barua nchini kutoka shule ya Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza.
Washindi wa tatu bora katika shindano la kuandika barua nchini kutoka shule ya Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza
Afisa Masoko, Shirika la Posta mkoani Mwanza, Julius Mponda, akizungumza kwenye maadhimisho hayo
Mwalimu Victor Mgisha anayefundisha somo la Kiingereza shule ya Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza akizungumza kwenye Maadhimisho hayo.
Waalimu wa Shule ya Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza wakielezea furaha yao baada ya wanafunzi wa shule hiyo kuibuka washindi wa shindano la uandishi wa barua linaloandaliwa na Umoja wa Posta duniani na kufanyika kwa nchi wanachama 191 kote duniani.
Mwalimu wa Shule ya Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza, akisoma barua iliyompa ushindi, mshindi wa kwanza kwenye shindano la uandishi wa barua nchini.
Meneja wa Shirika la Posta mkoani Mwanza, Julius Chifungo, akizunguza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani ambayo kimkoa yamefanyika leo katika Shule ya Saint Mary's Seminary (Nyegezi Sekondari) Jijini Mwanza.
Mshindi wa kwanza Kitaifa kwenye shindano ya uandishi wa barua, Denis Bahati Stephen, kutoka Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza akizunguza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani ambayo kimkoa yamefanyika leo katika Shule ya Saint Mary's Seminary (Nyegezi Sekondari) Jijini Mwanza.
 Mshindi wa pili Kitaifa katika shindano ya uandishi wa barua, Samweli Lufungulo Somelo, kutoka Saint Mary's Seminary Jijini Mwanza akizunguza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani ambayo kimkoa yamefanyika leo katika Shule ya Saint Mary's Seminary (Nyegezi Sekondari) Jijini Mwanza.
Bonyeza HAPA Kutazama Mwanza walivyoibuka kidedea kwenye Shindano la Uandishi wa barua mwaka 2015 Kitaifa.