Mbunge wa Jimbo La Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu akizungumza
na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya
ya Ikungi ulioketi kuchagua viongozi wapya watakaoiongoza jumuiya hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne
Mtaturu (Mwenye shati la Njano), Mbunge wa Jimbo la
Singida Mgharibi Mhe Elibariki Kingu (Wa Kwanza kushoto Pichani) na
viongozi wengine wakifatilia Mkutano Mkuu wa Umoja wa
Vijana Wilaya ya Ikungi katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Ikungi.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne
Mtaturu ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Siasa Wilaya akizungumza
na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya
ya Ikungi ulioketi kuchagua uongozi wapya watakaoiongoza jumuiya hiyo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya
ya Ikungi wakimsikiliza mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne
Mtaturu kabla ya kuchagua uongozi wapya kuongoza jumuiya hiyo ngazi ya Wilaya.
Na
Mathias Canal, Singida
Mbunge wa Jimbo la
Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu ametajwa kama Kiongozi makini anayejali
maslahi ya wananchi wa Jimbo, Wilaya, Mkoa na Taifa kwa ujumla katika kipindi
kifupi cha utendaji wake tangu alipochaguliwa na wananchi Octoba 25, 2015.
Heko hiyo imetolewa na Mkuu
wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati akizungumza na wajumbe wa
Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi
kwenye mkutano ambao ajenda yake kubwa ni uchaguzi wa uongozi wa jumuiya hiyo
ngazi ya Wilaya.