DC MTATURU ASIFU UTENDAJI WA MBUNGE ELIBARIKI KINGU

September 25, 2017
Mbunge wa Jimbo La Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi ulioketi kuchagua viongozi wapya watakaoiongoza jumuiya hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu (Mwenye shati la Njano), Mbunge wa Jimbo la Singida Mgharibi Mhe Elibariki Kingu (Wa Kwanza kushoto Pichani) na viongozi wengine wakifatilia Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana Wilaya ya Ikungi katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Ikungi.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Siasa Wilaya akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi ulioketi kuchagua uongozi wapya watakaoiongoza jumuiya hiyo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi wakimsikiliza mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kabla ya kuchagua uongozi wapya kuongoza jumuiya hiyo ngazi ya Wilaya.

Na Mathias Canal, Singida

Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu ametajwa kama Kiongozi makini anayejali maslahi ya wananchi wa Jimbo, Wilaya, Mkoa na Taifa kwa ujumla katika kipindi kifupi cha utendaji wake tangu alipochaguliwa na wananchi Octoba 25, 2015.


Heko hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi kwenye mkutano ambao ajenda yake kubwa ni uchaguzi wa uongozi wa jumuiya hiyo ngazi ya Wilaya.

WAKURUGENZI MKOANI SINGIDA WAAGIZWA KUNUA CHAKI ZINAZOZALISHWA MKOANI HUMO

September 25, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi akishiriki kazi ya uzalishaji chaki wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea Kiwanda cha usagaji wa unga wa Gypsum na Uzalishaji chaki cha Dober Color Kilichopo katika Kata ya Itigi-Majengo Halmashauri ya Itigi

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi akikagua kiwanda cha usagaji wa unga wa Gypsum na Uzalishaji chaki cha Dober Color Kilichopo katika Kata ya Itigi-Majengo Halmashauri ya Itigi wakati wa ziara ya kikazi

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akimkabidhi boksi tano za chaki Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi mara baada ya kutembelea na kukagua kiwanda cha usagaji wa unga wa Gypsum na Uzalishaji chaki cha Dober Color Kilichopo katika Kata ya Itigi-Majengo Halmashauri ya Itigi wakati wa ziara ya kikazi

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akishiriki kazi ya uzalishaji chaki wakati wa ziara ya kikazi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi kutembelea Kiwanda cha usagaji wa unga wa Gypsum na Uzalishaji chaki cha Dober Color Kilichopo katika Kata ya Itigi-Majengo Halmashauri ya Itigi
    Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi akisalimiana na Meneja wa kiwanda cha Uzalishaji chaki cha Dober Color Ndg Mukhtar Mahamood mara baada ya kuwasili kiwandani hapo

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi akikagua mizinga ya nyuki mara baada ya kutembele kiwanda Uzalishaji chaki, Mafuta ya Alizeti na Asali cha Fahari Kilichopo katika eneo la Tambukareli Halmashauri ya Mji wa Itigi wakati wa ziara ya kikazi, Kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu

Ukaguzi wa kiwanda cha uzalishaji Chaki

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi akikagua eneo la kutunzia Unga wa Gypusm katika kiwanda cha uzalishaji Gypsum cha Sanjaranda, Halmashauri ya Itigi

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi akizungumza kwa njia ya simu na mmiliki wa kiwanda cha uzalishaji unga wa Gypsum cha Sanjaranda Bw Rashid Said Rashid akiwa Dar es salaam ambaye alimuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa mpaka kufikia Januari 2018 uzalishaji wa Gypsum utaanza katika eneo la Sanjaranda, Halmashauri ya Itigi ili kurahisisha huduma hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi akiwa kwenye shamba la Mkulima Juma Patrick na kujionea mikorosho inavyoharibika kwa kukosa dawa ambapo alizungumza kwa njia ya simu na muwakilishi wa Bodi ya Korosho akiwa Dar es salaam ambaye alimuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa dawa za kuua wadudu kwenye Mikorosho zitawasili kati ya Jumanne  Septemba 26 na Jumatano 27, 2017
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi akionyesha chaki bora zinazozalishwa Wilayani Manyoni Mkoani Singida
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi akisalimiana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi Mhe Ally Minja mara baada ya kuwasili Kwa ajili ya kutembelea Kiwanda vya usagaji unga wa Gypsum na uzalishaji chaki.
Miongoni wafanyakazi wa kiwanda cha  Uzalishaji chaki cha Dober Color wakiendelea na kazi wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Dkt Rehema Nchimbi

“HATUWEZI KUJUTA UWEPO WA MBUNGE AMBAYE TUMEMCHAGUA –CUF TANGA”

September 25, 2017
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku akizungumza na waandishi wa habari kulia ni Katibu wa CUF wilaya ya Tanga,Thobias Haule
Naibu Meya wa Jiji la Tanga (CUF) Mohamed Haniu akizungumza kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Tanga,Alhaj Mussa Mbaruku kulia ni Katibu wa CUF wilaya ya Tanga,Thobias Haule
Diwani wa viti maalumu (CUF) akizungumza
 Sehemu ya wanachama wa chama hicho wakifuatilia mkutano huo

 CHAMA cha Wananchi CUF wilaya ya Tanga kimekanusha uvumi unaoonezwa kuwa wanajuta uwepo Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku huku kikiwataka wananchi kuwapuuza wanaoeneza taarifa hizo.

Hata hivyo amesema wamesikitishwa na kauli zinazoelezwa kuwa chama
  hicho kinawaomba radhi wananchi wa Jiji hilo kutokana na mbunge huyo kutokuwa na uwakilishi mzuri bungeni kwani tokea apewe nafasi hiyo amekuwa hodari na shupavu kusimamia maendeleo ya Jimbo hilo.

Hayo yalibainishwa leo na Katibu wa Chama cha CUF wilaya ya

Tanga,Thobias Haule wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari uliofanyika jana mjini hapa uliohudhuriwa na mbunge huyo na wanachama wa chama hicho ambapo alisema kuna mambo yanayofanyika ni yasiyokuwa na tija ndani ya chama hicho.

Alisema wao wamechaguliwa kuhakikisha wanawatumikia wananchi na sio
  kutunishia misuli jambo ambalo linaweza kupelekea kushindwa kuwatumikia wananchi.

“Ndugu zangu waandishi kuna mambo yanafanyika ya kihuni na ndani ya
  CUF Uhuni hauna nafasi nisema Jiji la Tanga limetulia na Mbunge anafanya kazi na madiwani nao pia ….sisi tumechaguliwa kwa maslahi ya Tanga na sio vyenginevyo “Alisema.

“Kwanza hatujakaa kikao chohote na hatujasema tunaomba radhi wakazi wa
  Jiji la Tanga eti Mbunge Mussa hana uwezo  ...eti hafai tumeshuhudia wabunge wengi wa miaka ya nyuma ambao walikuwa hawaeleze changamoto za  wananchi kwenye vikao vya bunge lakini huyu tunaona namna anavyopambana.

Naye Mwanachama wa chama hicho,Jumbe Zahoro alisema wamesikitishwa
  sana na kauli kuwa wao wanasikitika kwa sababu hawawezi kusikitika kwa kiongozi ambaye wamemteua na baadae kumpigana mpaka atachaguliwa kuliongoza jimbo hilo.

“Nimesikishwa kuona mtu anasimama na kueleza maneno anayoyataka  kwa
  sababu chama hicho kina kanuni na katiba  haiwezekani mtu anasimama na kusema tunasikitika kwa mbunge ambaye tumemchagua bila kuangalia chama hicho ni cha watu hilo jambo sio kweli “Alisema.

Alisema sio kweli wao CUF wanasikitika kwa mtu ambaye tumeanza kumteua
  na baadae kuanza kumchagua jambo ambalo haliwezi kuwaingia akilini watu.

Awali akizungumza,Mbunge Mussa alisema hivi sasa dhamira kubwa ni
  kuhakikisha anawatumikia wananchi kwa moyo mmoja ili kuweza kusogeza mbele gurudumu la maendeleo kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.

“Tanga imerudisha heshima yake kwa kuanza kupokea miradi mbalimbali
  mikubwa ambayo kwa namna moja au nyingine itakuwa mkombozi kwa wakazi wa Tanga hata mikoa ya jirani hii ni ishara tosha sasa tunarudi kwenye enzi zetu za viwanda “Alisema.

Alisema matarajio hayo hivi sasa yanakwenda sambamba na ujio wa miradi
  ya Bomba la mafuta,ujenzi wa kiwanda cha saruji eneo la Amboni kitakachomilikiwa na Wachina,ujenzi wa barabara ya
Tanga-Pangani-Saadan hadi Bagamoyo.

Alisema miradi hiyo itafungua fursa za kiuchumi kwa mkoa wa Tanga huku
  akiwataka wananchi kujiandaa kuchangamkia fursa hizo kwa ili kuweza kujikomboa kwa kuanzisha shughuli mbalimbali ikiwemo ujasiriamali.

NAIBU SPIKA ATOA ZAWADI YA PIKIPIKI NA PESA TASLIMU KWA WASHINDI WA TAMASHA LA TULIA TRADITIONAL FESTIVAL 2017

September 25, 2017
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson (wa tatu kulia) akimkabidhi funguo ya Pikipiki Kiongozi wa Kundi la Ngoma la Kannengwa Rungwe, Nolbert Mwandinga, baada ya kundi lake kuibuka mshindi wa kwanza katika kundi la Ingoma Kituli, wakati wa hafla ya kutoa zawadi kwa washindi wa Tamasha la Tulia Traditional Dances Festival 2017, lililomalizika mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya. Katika Tamasha hilo jumla ya washindi 10 wa kwanza kutoka kila kundi walizawadiwa Pikipiki.
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson akicheza ngoma ya asili ya kundi la  Banyampulo ya kabila la Wanyakyusa, wakati wa Tamasha la Tulia Traditional Dances Festival 2017, lililomalizika mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya. Katika Tamasha hilo jumla ya washindi 10 wa kwanza kutoka kila kundi walizawadiwa Pikipiki.



 Wacheza Bao Gabriel Mwasankinga wa timu ya CCM (kushoto) akichuana na Pascal Mbwelembweta wa timu ya Kawechele, kutafuta mshindi wa tatu katika mchezo wa fainali za mchezo huo kuadhimisha Tamasha la Tulia Traditional Dances Festival 2017, lililomalizika mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.
 Wacheza Bao Kocha Lufingo wa timu ya Stendi Kuu (kushoto) akichuana na Six Willson wa timu ya Soko Kuu, kutafuta mshindi wa kwanza na wapili katika mchezo wa fainali za mchezo huo kuadhimisha Tamasha la Tulia Traditional Dances Festival 2017, lililomalizika mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akipokea michango ya hela kutoka kwa wananchi wa Tukuyu kwa ajili ya harambee ya kuichangia timu ya Tukuyu Stars ''Changia Tukuyu Stars irudi Ligi Kuu'' wakati wa  Tamasha la Tulia Traditional Dances Festival 2017, lililomalizika mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya. Katika Tamasha hilo jumla ya washindi 10 wa kwanza kutoka kila kundi walizawadiwa Pikipiki. 
Picha na Muhidin Sufiani

RAIS DKT MAGUFULI AHITIMISHA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TANO YA ARUSHA LEO

September 25, 2017
: Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi wa Singisi kata ya Akeri nje kidogo ya jiji la Arusha kwenye njia panda ya KIA waliosimamisha msafara wake akiwa njiani kurejea Dar es salaam leo asubuhi Septemba 25, 2017 baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano mkoani Arusha.
Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisindikizwa na wakuu wa mikoa ya Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira na wa Arusha Mhe Mrisho Gambo akati akielekea kupanda ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)  kurejea  Dar es salaam leo asubuhi Septemba 25, 2017 baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano mkoani Arusha.
Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mkuu wa mikoa ya Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira kabla ya  kupanda ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)  kurejea  Dar es salaam leo asubuhi Septemba 25, 2017 baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano mkoani Arusha.
Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisindikizwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo kabla ya kupanda ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)  kurejea  Dar es salaam leo asubuhi Septemba 25, 2017 baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano mkoani Arusha.

Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungiwa mikono na  Mkuu wa mikoa ya Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira na Mkuu wa Mkoa wa Arusha wakati ndege yake ikiondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)  kurejea  Dar es salaam leo asubuhi Septemba 25, 2017 baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano mkoani Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo na Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo wakiondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)  baada ya kumsindikisza Rais Dkt John Pombe Magufuli leo asubuhi Septemba 25, 2017 baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano mkoani Arusha.


Picha na IKULU

RUTAINURWA ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA JUMUIA YA WAZAZI WILAYA YA ILALA

September 25, 2017
NA BASHIR NKOROMO
Lucas Rutainurwa ametawazwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ilala baada ya kuibuka mshindi katika uchaguzi wa Jumuiya hiyo uliofanyika jana.

Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Lugano Mwafongo, amesema katika Uchaguzi huo uliofanyika Segerea, Rutainurwa (pichani), alipata kura 278 dhidi ya Mohamed Honelo aliyepata kura 148 baada ya hao wawili kuingia katika kinyang'anyiro kwa mara ya pili kufuatia kutopatikana mshindi aliyepata zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa  katika uchaguzi wa awali.

Wakati katika awamu ya kwanza  Lutainurwa alipata kura 277 Honelo alipata kura 243 huku Celestine Nyalusi akipata kura 67.

Nafasi ya Mjumbe wa Halimashauri Kuu aliyeshinda ni George MJtambalike ambaye amepata kura 195 dhidi ya Edward Haule aliyepata kura 181. PICHA ZA UCHAGUZI HUO/>BOFYA HAPA