MBUNGE WA JIMBO LA SEGEREA BONNAH KALUWA AONGOZA SEMINA YA WANAWAKE WAJASIRIAMALI JIJINI DAR ES SALAAM

September 24, 2016

 Mbunge wa Jimbo la Segerea,Bonnah Kaluwa (katikati) akiingia kwenye ukumbi wa Nyantale kwa ajili ya kufungua semina ya ujasiriamali ya wanawake eneo la Tabata Bima jijini Dar es Salaam leo.

 Wanawake wa Jimbo la Segerea wakiwa kwenye semina ya ujasiriamali ukumbi wa Nyantale eneo la Tabata Bima jijini Dar es Salaam.
 Wanawake wa Jimbo la Segerea wakiwa kwenye semina ya ujasiriamali ukumbi wa Nyantale eneo la Tabata Bima jijini Dar es Salaam.
 Katibu wa Ofisi ya Jimbo la Segerea,Jacqueline,akizungumza na akinamama wa jimbo hilo kwenye semina ya ujasiriamali.
 Mkufunzi wa Elimu ya Utunzaji wa Fedha kutoka Benki ya Equity,Daudi Mwashilindi,akitoa mada ya utunzaji wa fedha na mpangilio wa mapato na matumizi jinsi inavyosaidia kwa wajasiriamali kukua kibiashara kwenye semina hiyo.

DC KIGAMBONI APEWA SIKU MBILI KUHAKIKISHA FUKWE ZOTE ZA KIGAMBONI ZIKO SAFI

September 24, 2016
 Naibu waziri wa Nchi ofis ya makamu wa rais muungano na mazingira Mh.Luhaga Mpina akifanya usafi na wananchi wa wilaya ya kigamboni katika kutekeleza agizo la Mh. rais la kila mwisho wa mwezi kufanya usafi. 
 Naibu Waziri wa Nchi ofis ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh.Luhaga Mpina akiwa na wananchi wa kigamboni waliojitokeza kwaajiri ya kufanya usafi katika fukwe za kigamboni 
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina akiongea na waandishi wa habari,hawapo pichani mara baada ya kumaliza kufanya usafi katika fukwe za wilaya ya kigamboni. 



EVELYN MKOKOI
AFISA HABARI
OFISI YA MAKAMU WA RAIS
STORY – KIGAMBONI
23/9/2016
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Luhaga  Mpina amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Bw. Hashim Mgandilwa kuhakikisha fukwe zote za kigamboni zinafanyiwa usafi na kuwa katika hali ya kuridhisha.
Naibu Waziri Mpima ameseyasema hayo leo katika maeneo ya fukwe za kigamboni aliposhiriki katika siku ya  usafi kitaifa ya mwezi wa September.
Amesema fukwe za kigamboni ni chafu sana na usafi wa mazingira katika mji wa kigamboni hauridhishi, “pamoja na wananchi kujitokeza kwa wingi katika kusafisha mazingira leo fukwe ni chafu na wengine wanatuangalia tunavyosafisha huku wakiendelea na shughuli zao, Angalia wale wavuvi kwenye mitumbwi yao wanaendelea na kazi zao na wao ndo wachafuzi wakubwa huko baharini na nchi kavu. “Alisema.
Mpina amemtaka mkuu wa wilaya hiyo kuwawajibisha viongozi walioko chini yake kwa kosa la uzembe wa ufuatiliaji wa sheria ya mazingira kabla hajawajibishwa yeye. “kiongozi mzembe afukuzwe kazi kabla haujafukuzwa wewe na kuingia kwenye matatizo.” Alisisitiza naibu waziri Mpina.
Hata hivyo Naibu Waziri Mpina alimpongeza mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam  Paul Makonda kwa kuanzisha kampeni ya upandaji miti maarufu kama ‘’MTI WANGU’’ na kuwashauri wakazi wa jiji kushiriki Katika siku ya uzinduzi na kuahidi kuwa pamoja nao siku hiyo.
Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Bw. Hashim Mgandilwa ameelezea jitihada za usafi wa mazingira katika mji wa kigamboni ikiwa ni pamoja na mashindano ya usafi wa mazingira na kuwataka wakazi wa kigamboni kuongeza jitihada za kutosha kuiweka kigamboni safi.
Jumamosi ya Mwisho wa Mwezi ni siku maalum ya usafi ikiwa ni katika kutekeleza agizo la Rais la Usafi wa mazingira ambapo mwezi huu kitaifa imefanyika Kigamboni.

WAASTAAFU WA JESHI LA MAGEREZA WAAGWA JIJINI DAR

September 24, 2016


Wastaafu wa Jeshi la Magereza wakiwasili katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji, Ukonga, Dar es Salaam wakiwa wameongozwa na Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile wakielekea Jukwaa Kuu kupokea Salaam ya Heshima. Hafla ya kuwaaga wastaafu wa Jeshi la Magereza imefanyika leo Septemba 23, 2016.
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile akiwa katika Jukwaa Kuu akipokea Salaam ya Heshima kutoka kwenye Gwaride Maalum la kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza.
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile akikagua Gwaride Maalum la kuwaaga Wastafu wa Jeshi la Magereza lililoandaliwa na Maofisa wa Jeshi la Magereza.
Gwaride M aalum likipita mbele ya Jukwaa kwa Heshima.
Viongozi Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakipiga Saluti wakati Gwaride Maalum likipita mbele ya Jukwaa kwa heshima. Wa kwanza kulia ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile akiwa pamoja na Wastaafu wengine wa Jeshi la Magereza wakitoa Salaam za mwisho wakiwa kwenye magari wakati Gwaride Maalum likiwa limeunda Umbo la OMEGA.
Maofisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakipunga mikono ikiwa ni ishara ya kuwaaga Wastaafu hao wakati wakipita katika magari Maalum (hawapo pichani).
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile akipita kwenye gari Maalum akipunga mkono ikiwa ni ishara ya kuwaaga Watumishi wa Jeshi la Magereza baada ya kustaafu rasmi Utumishi wa Umma kwa mujibu wa Sheria.
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wastaafu wa Jeshi la Magereza pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Airtel yaipongeza Kilimanjaro Queens

September 24, 2016


Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imeipongeza Timu ya wanawake Tanzania ya Kilimanjaro Queens kufatia ushindi wa walioupata katika michuano ya Challenge Afrika Mashariki na Kati 2016 maarufu kama CECAFA 
 Timu ya kili Queen iliyosheheni vijana kutoka Airtel Rising Stars imeibuka washindi wa michuano hiyo baada ya kuichapa harambee Queens ya Kenya bao 2-1 akiongea wakati wa timu hiyo ilipotembelea ofisi za Airtel leo , Mwenyekiti wa soka la wanawake Tanzania , Bi Amina Karuma alisema" Tumekuja hapa Airtel leo na kuleta kombe hili kwani tunathamini sana mchango mkubwa unaofanywa na Airtel kupitia program ya Airtel Rising Stars ambayo imetuwezesha kupata wachezaji mahiri na waliotuwezesha kuleta ubingwa huu nchini. 
"Tunajisikia faraja kuona Airtel iko bega kwa bega na sisi katika kuhakikisha soka la wanawake linaendelezwa na kukua kwa kasi, juhudi hizi zilizofanywa kwa miaka sita sasa zimezaa matunda kwa timu ya wanaume ya Serengeti boys na sasa kwa timu yetu ya Kilimanjaro Queens. 
"Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza na kuwaomba waendelee kushirikiana nasi katika kukuza, kulea na kubaini vipaji chini ya mpango wa Airtel Rising Stars ambao umekuwa tija skwa maendeleo ya soka nchini", alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Bwana Sunil Colaso aliwapongeza wachezaji wa Kili Queens kwa ushinid wa kishindo kikubwa na kuahidi kuendelea kudhamini michuano ya Airtel Rising Stars ili kubaini vipaji vipya zaidi na kuwawezesha vijana kuzifikia ndoto zao ili kutimiza dhamira ya kampuni yake chini ya Mpango wake kabambe wa Airtel FURSA.
Kufatia ushindi huo Airtel imewazawadia wachezaji hao kila mmoja kiatu cha mpira ikiwa ni motisha kwa wachezaji kuchezea na kuendelea kufanya vizuri na kupata vifaa bora vya michezo wachezaji wa 
Kili Queens wanane walitoka katika michuano ya Airtel Rising Stars ambao ni pamoja na Stumai Abdallah, Sherida Boniface, Anna Ezron , Anastazia Antony, Amina Ally, Donisia Daniel, Najiat Abbasi na Maimuna Khamis




 Afisa uhusiano wa Airtel, Jane Matinde akiwapokea wachezaji  wa Kili Queens  wakati timu hiyo ilipotembelea ofisi za Airtel makao makuu leo

MIRADI 45 KUZINDULIWA NA MWENGE WA UHURU MKOANI TABORA

September 24, 2016
Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Mhandisi Methew Mtigumwe akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey D.J Mwanri (Kulia)
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Mhandisi Methew Mtigumwe akisoma Risala wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru
Baadhi ya wakuu wa Wilaya za mkoa wa Tabora wakiulaki mwenge wa Uhuru mara baada ya kuwasili Mkoani humo