MAY 30 2015 Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid, Arusha ilikuwa siku ambayo Mbunge wa Monduli, Edward Ngoyai Lowassa alitangaza
rasmi kwamba ataomba kibali cha CCM ili agombee Urais wa TZ mwaka
huu.Baada ya hapo watu wakaigeukia stage ya burudani ambapo ilikuwepo
list pia ya mastaa wa Bongo Fleva ambao walipiga show ya nguvu.
KAMPENI YA KUTOKOMEZA MARADHI YA FISTULA YATUA WILAYA YA KIBONDO
Mkazi
wa Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma Esther Batolomea akisoma kipeperushi
chenye ujumbe wa maradhi ya Fistula wakati wa kampeni ya kutokomeza
maradhi hayo iliyofanyika wilayani hapo. Hospitali ya CCBRT kwa
kushirikiana na Vodacom Foundation zinatoa elimu kwa Umma kupitia
kampeni inayozunguka mikoa mitatu nchini kuwasisitiza wanawake
wajitokeze wakatibiwe maradhi hayo kwani yanatibika. Inakadiriwa wastani
ya wanawake 3,000 hupatwa na maradhi hayo kwa mwaka wakati wa
kujifungua.
Wakazi
wa Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma wakisoma vipeperushi vyenye ujumbe
wa maradhi ya Fistula wakati wa kampeni ya kutokomeza maradhi hayo
iliyofanyika wilayani hapo. Hospitali ya CCBRT kwa kushirikiana na
Vodacom Foundation zinatoa elimu kwa Umma kupitia kampeni inayozunguka
mikoa mitatu nchini kuwasisitiza wanawake wajitokeze wakatibiwe maradhi
hayo kwani yanatibika. Inakadiriwa wastani ya wanawake 3,000 hupatwa na
maradhi hayo kwa mwaka wakati wa kujifungua.
Wanafunzi
wa shule ya Sekondari ya Kumwamba iliyopo Wilaya ya Kibondo Mkoa wa
Kigoma walijumwika na wakazi wa wilaya hiyo katika viwanja vya Community
Centre wakimsiliza Meneja Biashara wa Idara ya Uhusiano wa Vodacom
Tanzania,Grace Lyon wakati alipokuwa akiwafafanulia jambo kuhusiana na
maradhi ya Fistula. Wakati wa kampeni ya kutokomeza maradhi hayo
inayoendelea kufanyika katika mikoa mitatu nchini,Kampeni hiyo
inaendeshwa na Hospitali ya CCRBT kwa kushirikiana na Vodacom
Foundation. Inakadiriwa wastani ya wanawake 3,000 hupatwa na maradhi
hayo kwa mwaka wakati wa kujifungua.
Balozi
wa maradhi ya Fistula nchini Msanii Mrisho Mpoto alimaarufu”Mjomba”
akitoa elimu kwa wakazi wa Kibonda kuhusiana na maradhi ya fistula na
kuwasihi wakina baba kuwaruhusu wake zao wakatibiwe maradhi hayo kwani
yanatibika. Alitoa elimu hiyo wakati wa kampeni inayoendeshwa na
Vodacom Foundation kwa kushirikiana na CCBRT ya kutokomeza maradhi hayo
inayoendelea katika mikoa mitatu nchini. Inakadiriwa wastani wa
wanawake 3,000 hupatwa na maradhi hayo kwa mwaka wakati wanapojifungua.
MWANAHABARI DEOGRATIAS MONGELA ALIVYO UKACHA UKAPERA
Mwanahabari Deogratias Mongela wa Kampuni ya Global Publishers Ltd.
Bibi Harusi, Elizabeth Sanga.
Deogratias
Mongela akiwa na mke wake Elizabeth Sanga wakati wa hafla ya ndoa yao
iliyofanyika Hoteli ya Atriums iliyopo Sinza Afrikasana baada ya kufunga
ndoa Katika Kanisa la Katoliki, Parokia ya Mbezi Luis Dar es Salaam
jana.
Maharusi
hao (katikati) wakiwa na wapambe wao kwenye hafla hiyo. Kushoto ni
Cobson Nzige na mke wake Subira Nzige (kulia), 'hakika wamependeza si
mnawaona'.
Bibi harusi Elizabeth Sanga akiteta na mpambe wake Subira Nzige.
Rais Kikwete akutana na Maalim Seif Ikulu Dar es Salaam
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
akizungumza na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff
Hamad ikulu jijini Dar es Salaam
(picha na Freddy Maro)
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
akiwa kwenye picha ya pamoja na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Maalim Seif Shariff Hamad ikulu jijini Dar es Salaam.
AFRICAN SPORTS KUINGIA KAMBINI JUNI 3.
KLABU ya African Sports “Wanakimanumanu”inatarajiwa
kuingia kambini Juni 3 mwaka huu kwa ajili ya kujiwinda na Michuano ya Ligi kuu
Tanzania Bara msimu ujao baada ya kupanda kucheza daraja hilo.
Akizungumza jana, Katibu wa timu hiyo, Khatib
Enzi aliliambia gazeti hili kuwa wameamua kuingia kambini mapema ili kuhakikisha
wanakiandaa vema kikosi chao kwa ajili ya kuhimili mikimiki ya Ligi kuu ikiwemo
kupata matokeao mazuri.
Enzi alisema kuwa wachezaji wa timu
hiyo waliopo nje ya mkoa wa Tanga kwa sasa watalazimika kutua mkoani hapa Juni
Mosi mwaka huu tayari kuungana na wenzao katika kambi yao itakayokuwepo Kata ya
Usagara jijini Tanga.
“Kuanza kambi mapema ni miongoni mwa mipango yetu ya kuhakikisha
tunakiandaa kikosi chetu vyema kwani Ligi kuu sio lelemama hivyo inahitajika
kujipanga vema “Alisema Enzi.
Katika hatua nyengie,Enzi alisema
kuwa usajili ambao wataufanya kabla ya kuanza michuano hiyo utakuwa ni katika nafasi
za mlinda mlango, kiungo wa kati na washambualiaji ambao tayari kamati ya
usajili ya timu hiyo imeshaanza kazi ya kuhakikisha nafasi hizo zinapata
wachezaji makini watakaoiletea maendeleo.
Alisema kuwa msimu ujao wamepania
kufanya usajili wa nguvu ambao utawawezesha kurudisha enzi zao za zamani wakati
walipopanda daraja na kuchukua ubingwa wa Ligi kuu soka Tanzania bara.
Hata hivyo alisema kuwa klabu hiyo
imekwisha kuwafungashia virago wachezaji sita ambao ni Gerary Samburu, Khasim
Mkele, Eddy Zaharani, Nyanda Kazioba, Shingwa na Evarist Mujwahuki ambao wapo
huru.
SERIKALI YAKARIBISHA WAWEKEZAJI BINAFSI KWENYE SEKTA YA UCHUKUZI
Waziri wa Uchukuzi Mhe. Samuel Sitta akiwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2015/2016 bungeni mjini Dodoma leo.
Mbunge wa Kisarawe (CCM) Bw. Suleiman Jafo akichangia mjadala wa bajeti ya wizara ya uchukuzi leo bungeni mjini Dodoma.
…………………………………………………………….
Na Fatma Salum – Maelezo
Serikali kupitia Wizara ya
Uchukuzi imesema inakaribisha wawekezaji binafsi kwenye miradi
mbalimbali ili kuboresha sekta za uchukuzi na hali ya hewa hapa nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa
Uchukuzi Mhe. Dkt. Charles Tizeba wakati akijibu hoja mbalimbali za
wabunge zilizowasilishwa kwenye mjadala wa bajeti ya wizara hiyo leo
bungeni mjini Dodoma.
“Serikali inawakaribisha
wawekezaji binafsi kuwekeza kwenye miradi ya kuboresha miundombinu ya
uchukuzi na hali ya hewa kwa kuwa Serikali peke yake haiwezi kukamilisha
miradi yote bila ya ushirikiano na wengine”
Dkt. Tizeba alisema Serikali ina
mipango madhubuti ya kuboresha miundombinu nchini ikiwemo reli, bandari
na barabara na kupitia dhana ya ushirikiano wa Serikali na sekta binafsi
(Public Private Partnership) itaweza kufanikisha mipango hiyo kwa
ufanisi na kwa wakati.
Aidha Dkt. Tizeba aliongeza kuwa
kupitia juhudi za Serikali baadhi ya miradi ipo katika hatua za awali
ikiwemo uboreshaji wa viwanja vya ndege 11 kwenye mikoa mbalimbali
nchini ambapo wataalamu wameshafanya upembuzi yakinifu (Feasibility
Study) na fedha zikipatikana vitafanyiwa matengenezo mara moja.
Akizungumzia upanuzi wa bandari
ya Dar es Salaam Dkt. Tizeba alibainisha kuwa taratibu za kumpata
mzabuni zinaendelea na akipatikana ujenzi wa gati namba 13 na 14 za
bandari hiyo utaanza.
Leo Waziri wa Uchukuzi Mhe.
Samuel Sitta aliwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya
wizara hiyo kwa mwaka 2015/2016 ambapo bunge lilikubali kupitisha zaidi
ya shilingi bilioni 452.9.
Subscribe to:
Posts (Atom)