TRBA kuandaa NBL msimu huu

TRBA kuandaa NBL msimu huu

February 28, 2013
Na Oscar Assenga, Tanga. CHAMA cha Mpira wa Kikapu mkoa wa Tanga (TRBA) kimepokea wa mikono miwili kuteuliwa kuwa mwenyeji wa Mashindano ya Kikapu ya Taifa (NBL) ambayo yatafanyika mkoani Tanga Aprili Mosi mpaka Aprili 7 kwenye uwanja wa Mkwakwani. Akizungumza jana, Mwenyekiti wa Chama hicho, Khamisi Jaffary alisema wanashukuru kutokana na mwaliko huo nakueleza baada ya kufanyika mashindano ya Taifa Cup mwaka jana wakazi wa Tanga watapata fuksa ya kushuhudia mashindano mengine ya NBL mkoani hapa. Jaffari alisema mashindano hayo yanatarajiwa kushirikisha vilabu 15 ambavyo vitakuwa zikihusisha timu za wanawake na wanaume kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini. Aidha aliwataka wadau wadau wa michezo mkoani hapa kujitokeza kwa wingi kukisapoti chama hicho ili kiweze kufanikisha mashindano hayo pamoja na kuzisaidia timu za mkoa wa Tanga ili ziweze kutimiza malengo ya kuwa bingwa wa mashindano hayo msimu huu. Mwenyekiti huyo alisema maandalizi ya mashindano hayo kwa timu za mkoa wa Tanga yanaendelea vizuri ambapo vilabu vya mchezo huo tiyari vimekwisha kuanza mazoezi kwenye viwanja mbalimbali kwa ajili ya ushiriki wao. “Ki ukweli nimekaa na vilabu vya mkoa wa Tanga ambapo tutakuwa na timu mbili ambazo zitashiriki ambapo tulikubaliana ni lazima wahakikishe ubingwa wa mashindano hayo unabaki hapa nyumbani “Alisema Jaffary. Mwisho.