KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA NCHINI AWASILI JIJINI MWANZA KWA ZIARA YA KIKAZI MAGEREZA MKOA WA MWANZA

KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA NCHINI AWASILI JIJINI MWANZA KWA ZIARA YA KIKAZI MAGEREZA MKOA WA MWANZA

June 26, 2014

 image 
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini akiwasili uwanja wa Ndege wa Mwanza leo Juni 26, 2014 kwa ziara ya kikazi Magereza Mkoa wa Mwanza. Aidha Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza atahudhuria pia Kikao cha 26 cha Bodi ya Taifa ya Parole ambacho kimeanza leo katika Ukumbi wa Mwanza Hoteli, Jijini Mwanza(kushoto) ni Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Goleha Masunzu.
image_1 
Afisa Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Remegius Pesambili(wa pili kulia) akimlaki Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(Kaunda Suti nyeusi) alipowasili leo Juni 26, 2014 katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza kwa ziara ya Kikazi Magereza Mkoa wa Mwanza. photo 
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akisaini kitabu cha Wageni mapema leo jioni Juni 26, 2014 alipowasili Jijini Mwanza kwa ziara ya Kikazi(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Waziri Simba Azinduwa Mkutano Kujadili Utokomezaji Ukeketaji Tanzania

Waziri Simba Azinduwa Mkutano Kujadili Utokomezaji Ukeketaji Tanzania

June 26, 2014

Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Sophia Simba akizungumza kabla ya kufungua rasmi mkutano wa Kitaifa wa Kujadili Utokomezaji wa Ukeketaji Nchini Tanzania.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Sophia Simba akizungumza kabla ya kufungua rasmi mkutano wa Kitaifa wa Kujadili Utokomezaji wa Ukeketaji Nchini Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), Valerie Nsoka akizungumza katika mkutano huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), Valerie Nsoka akizungumza katika mkutano huo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, akizungumza katika mkutano wa Kitaifa wa Kujadili Utokomezaji wa Ukeketaji Nchini Tanzania.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, akizungumza katika mkutano wa Kitaifa wa Kujadili Utokomezaji wa Ukeketaji Nchini Tanzania.
MATOKEO YA SENSA YA IDADI YA TEMBO KATIKA MFUMO WA IKOLOJIA WA SELOUS-MIKUMI NA RUAHA-RUNGWA

MATOKEO YA SENSA YA IDADI YA TEMBO KATIKA MFUMO WA IKOLOJIA WA SELOUS-MIKUMI NA RUAHA-RUNGWA

June 26, 2014


tembo tembo2
Wizara ya Maliasili na Utalii inapenda kuujulisha umma matokeo ya sensa ya tembo iliyofanyika mwezi Oktoba na Novemba mwaka huu ili kuiwezesha Serikali kutambua hali ya rasilimali ya wanyamapori ndani na nje ya maeneo yaliyohifadhiwa.
Wizara kwa kushirikiana na wataalamu wa ndani na nje ya nchi imefanya sensa katika Maeneo ya Mfumo ikolojia wa Selous – Mikumi na Ruaha – Rungwa pekee kwa kuwa ni maeneo yenye tembo wengi nchini.
Matokeo ya sensa hii yanaonyesha kwamba Mfumo wa ikolojia wa Selous-Mikumi kwa sasa una tembo wapatao 13,084 na Ruaha–Rungwa una tembo wapatao 20,090. Takwimu hizi zinaonesha kupungua kwa idadi ya tembo na hasa katika mfumo ikolojia wa Selous-Mikumi ikilinganishwa na Sensa za awali.