NAMBA YA 115 YA M-MAMA YAZINDULIWA KATIKA MKUTANO WA KIMATAIFA WA AFYA KWA LENGO LA KUOKOA VIFO VYA MAMA NA MTOTO.

March 25, 2024

 Na Janeth Raphael - MichuziTv -Dodoma


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt Dotto Biteko amewaelekeza Wakuu wa Mikoa wote Nchini pamoja Wakuu wa wilaya kusimamia vyema utekelezaji huduma ya mama na mtoto kwa kuwaunganisha wadau na wananchi katika kuokoa Maisha ya mama na mtoto.

Dkt Biteko ameyasema hayo Leo machi 25,2024 Jijini Dodoma wakati akifungua mkutano wa kwanza wa Kimataifa wa Afya msingi Nchini uliohudhuriwa na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya Nchi pamoja na Waganga wakuu wa Mikoa na Waganga wakuu wafawidhi wa hospital za halmashauri.

Katika hilo Dkt Biteko ametoa wito kwa wananchi wote kuitumia namba hii kwa kuipiga inapotokea dharula ili kuokoa vifo vya mama na mtoto.

"Nitumie nafasi hii kuwaelekeza wakuu wa mkoa wote Nchini pamoja na wakuu wa wilaya kusimamia vyema utekelezaji wa huduma kwa mama na mtoto kuwafanya wadau na wananchi wote kuwa sehemu ya kuokoa vifo vya mama na mtoto".

"Ninayo furaha kubwa sana kuzindua huduma hii ya mama na mtoto ya mama. Hivyo wito wangu kwa wananchi wote wakike na kiume kutumia namba hii kuwasiliana pale inapotokea dharula ili tusikubali kupoteza maisha ya mama zetu na watoto wetu na hii namba itaendelea kutoa huduma wakati wote"

Aidha Naibu Waziri Mkuu amezitaka Wizara zinazohusika na sekta ya Afya uwekezaji wa miundombinu iliyowekwa na Serikali katika vituo vya afya msingi inatunzwa.

"Niseme kuwa Wizara zinazohusika na sekta ya afya wekeni mpango wa kuhakikisha kuwa uwekezaji wa miundombinu uliofanywa na Serikali katika vituo vya afya msingi inatunzwa,haina maana yeyote kituo kimejengwa leo na baada ya muda kimeharibika miundombinu itunzwe".

Akitoa salamu za wizara ya Afya kwaniaba ya Waziri wa afya Naibu Waziri wa afya Dkt Godwin Mollel amesema kuwa afya ni uchumi kwani bila afya hakuna kitu kitakachosonga mbele mfano upo hata kipindi cha króna hakuna kitu chochote kilichofanyika ikiwemo veranda.

"Ndomana tunasema afya ni uchumi katika kipindi cha korona hakuna kilichoweza kuendelea,hakuna kiwanda kilichofanya kazi,hakuna shughuli yeyote ya kiuchumi iliyosonga mbele na shughuli za kiuchumi zilisimama,manake ukigusa eneo la afya na watu wa afya wakasimama katika nafasi zao basi unaboreshs uchumi".

Naye Naibu Waziri Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia masuala ya afya na lishe Dkt Festo Dugange amesema kuwa hadi February 2024 sekta ya afya msingi nchini Tanzania ina jumla ya vituo vya kutea huduma za afya 6,933 zikiwemo Zahanati, na Hospitali za Halmashauri ukilinganisha na mwaka 2015 ambapo idadi ilikuwa ni 5,270.

"Kufikia February 2024 sekta ya afya msingi Nchini Tanzania ina jumla ya vituo vya kutolea huduma ya afya 6,933 zikiwemo Zahanati 5,887 vituo vya afya 874 na hospital za halmashauri 172. Takwimu hizi zinaonesha kwamba kuna ongezeko kubwa la vituo katika afya msingi ikilinganishwa na idadi ya vituo 5,270 katika mwaka 2015. Hii ni hatua kubwa katika kuendelea kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi wote nchini Tanzania".

Aidha Dkt Dugange ameongeza kwa kutoa idadi ya wateja wa nje (OPD)na wateja wa ndani (IPD) kwa mwaka 2023 waliopata huduma katika vituo vya afya.

"Aidha kwa mwaka 2023 wateja milioni 26.9 walipata huduma katika vituo vya afya msingi kama wagonjwa wa nje yani (OPD) wateja 854,318 walipata huduma ya kulazwa (IPD). Katika eneo la mama na mtoto jumla ya wateja milioni 1.6 walijifungulia katika vituo vya kutolea huduma afya msingi na wakina mama waliokuwa na uzazi pingamizi wakafanyia upasuaji walikuwa ni 125,318".

Kuanzia mwaka 2017 hadi January 2024 hospital za halmashauri zimeongezeka kutoka hospital 50 mpaka kufikia hospital 177.






UBOMOAJI NYUMBA MSIMBAZI BONDENI KUANZA RASMI APRILI 12, 2024

March 25, 2024

 Dar es Salaam


Zoezi la ubomoaji wa nyumba zilizofidiwa na Mradi wa Uendelezaji wa Bonde la Msimbazi linatarajiwa kuanza rasmi Aprili 12, 2024, na litawahusu waathirika 2,155 ambao tayari wamelipwa fidia.

Hayo yamesemwa leo tarehe 25 Machi, 2024 na Mhandisi Humphrey Kanyenye, Mratibu wa Miradi ya Ushirikiano na Benki ya Dunia TARURA alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za mradi zilizopo Millenium Tower-Kijitonyama, Dar es Salaam.

Mhadisi Kanyenye alieleza kuwa kwa mujibu wa makubaliano ya utekelezaji wa zoezi hilo, waathirika wa mradi ambao wameshakwishapokea malipo yao wanatakiwa kuhamisha mali zao na kupisha eneo la mradi ndani ya wiki sita (6) baada ya kupokea fedha hizo kwenye akaunti zao.

“Waathrika wote wa mradi huu wanafahamu kuwa tuliwapa muda wa kuhama kwa makubaliano maalumu ya kimkataba yaliyowataka kuhama ndani ya wiki Sita (6) mara tu baada ya fedha kuingia katika akaunti zao, muda huo sasa umepita hivyo wanatakiwa kuondoka ili kupisha utekelezaji wa mradi,” alisema Mhandisi Kanyenye.

Alieleza pia kuwa walichelewa kuanza zoezi hilo kwa ajili ya kuwapa muda waathirika wa mradi kubomoa wenyewe kwa hiari ili kuokoa baadhi ya mali zao.

Aidha, alisema kwamba kati ya waathirika 2,329 waliopo kwenye orodha ya daftari la kwanza la ulipaji fidia, kufikia tarehe 21 Machi 2024, tayari waathirika 2,151 walikuwa wamelipwa kiasi cha shilingi bilioni 52.6

“Lakini pia kuna wale ambao hawakufikiwa katika uthamini wa awali kwa baadhi yao kugomea ama kutoonekana katika maeneo yao, idadi yao ni 466, hawa wameingizwa katika orodha ya daftari la pili ambalo limeshakamilika na litawasilishwa kwa Mthamini Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kusainiwa siku ya jumanne tarehe 26 Machi 2024 tayari kwa kulipwa fidia,” alisema Mhandisi Kanyeye.

Mradi unatekelezwa kwa muda wa miaka sita (6) (2022-2028) kwa gharama takribani shilingi bilioni 663 na lengo kuu la mradi ni kuimarisha ustahimilivu kwa kuweka mikakati ya kukabiliana na mafuriko na kuwa na matumizi bora ya ardhi katika eneo la chini la bonde la mto msimbazi ikiwa ni pamoja na kurudisha uoto wa asili katika uwanda wa juu wa bonde la mto msimbazi.




KAMATI YA PIC YARIDHISHWA NA UWEKEZAJI WA JENGO LA PSSSF COMMERCIAL COMPLEX

March 25, 2024

 

 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), imeridhishwa na uwekezaji wa jengo la kitega uchumi la PSSSF Commercial Complex, lililoko barabara ya Sam Nujoma, jijini Dar es Salaam.

Jengo hilo la kisasa lenye ghorofa 35 linamilikiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na kwa sasa tayari limekamilika kwa asilimia 100 na limeanza kutumika.

Akizungumza mwishoni mwa wiki wakati wa ziara ya PIC ya kutembeela mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 232, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Kudumu ya Bunge Mhe. Deus Sangu amesema, Kamati imekagua mradi na kujiridhisha kuwa ni mzuri na umetekelezwa kwa viwango vyote vinavyohitajika.

“Sisi kama kamati tumeendelea kuishauri PSSSF kuhakikisha jengo hili ambalo limewekeza fedha nyingi za Mfuko linasimamiwa na tija iliyokusudiwa inapatikana, tumekagua na tumeridhika na uwekezaji huu na tunaiponegza PSSSF.” Amesema.

Amesema Kamati yake imeelekeza katika kipindi cha matarajio ya chumo la uwekezaji (Return of investment) inaleta tija na kupata chumo ndani ya muda iliyojiwekea kisha kuanza kupata faida.

“Na hii itakuwa ni faida kwa Mfuko na kuufanya uweze kuendelea kuwahudumia wananchama bila kutetereka.” Alisema.

Mwenyekiti huyo amempngeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa namna anavyosukuma mabadiliko ya kiuchumi nchini na uwekezaji huo umeakisi R mbili kati ya zile nne za Mhe. Rais ambazo ni Reforms na Rebuild.

Naye Mjumbe wa Kamati hiyo, Mhe. Dkt. Pius Chaya, licha ya kupongeza uwekezaji huo lakini pia ameishauri serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina kuangalia uwezekano wa taasisi za umma ambazo ziko Dar Es Salaam kutumia jengo hilo.

“Hatuui taasisi binafasi lakini ipo haja ya kujaza nafasi zilizobaki.” Amefafanua Dkt. Chaya.

Akitoa wasifu wa jengo hilo, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Abdul-Razaq Badru amesema jengo la PSSSF Commercial Complex ni jengo refu zaidi na ni moja ya alama za jiji la Dar Es Salaami, ni jengo refu sana katika nchi za Afriak Mashariki na Kusini mwa Afrika.

Amesema jengo hilo lina minara mmitatu (towers) moja ni Commercial Complex ambalo ni refu zaidi lenye ghorofa 35 Executive tower lenye ghorofa 14 na eneo la maegesho lenye ghorofa 6.

“Hapa ndio panaitwa PSSSF Commercial Complex, kuna Executive tower ambako ni maalum kwa shughuli za maofisi, commercial complex linahusisha mabenki, ofisi mchanganyiko na kumbi za mikutano na shughuli nyingine za kijamii, lakini pia kuna ene la maegesho ya magari.” Amefafanua.

Amesema jengo hilo limeendelea kuwavutia wapangaji wengi zaidi kadiri muda unavyokwenda na matarajio ya Mfuko, kufikia desemba mwaka huu 2024, kiwango cha upangishaji kinatarajiwa kupanda na kufikia asilimia 70.

Amesema, miongoni mwa wapangaji mashuhuri kwenye jengo hilo ni pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa (UNDP) na taasisi zake, kampuni kubwa ya mitandao ya simu Tigo, taasisi za umma, mabenki na wafanyabiashara binafsi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), Mhe. Deus Sangu, akizungumza mara baada ya Kamati yake kukagua mradi wa jengo la kitega uchumi la PSSSF Commercial Complex, lililoko barabara ya Sam Nujoma jijini Dar es Salaam, Machi 21, 2024.

Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Abdul-Razaq Badru, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa jengo la kitega uchumi la PSSSF Commercial Complex barabara ya Sam Nujoma jijini Dar Es Salaam, mbele ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), wakati wa ziara ya wajumbe wa kamati ya PIC kukagua jengo, Machi 21, 2024.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji PSSSF, Bw. Rashid Mtima (Aliyesimama), akizungumza mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), Mhe. Deus Sangu (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Abdul-Razaq Badru, wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), kukagua jengo la kitega uchumi la PSSSF Commercial Complex barabara ya Sam Nujoma jijini Dar Es Salaam Machi 21, 2024.

Wajumbe wa Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), wakiongozwa NA Mwenyekiti wake Mhe. Deus Sangu na Menejimenti ya PSSSF wakitembelea jengo la PSSSF Commercial Complex barabara ya Sam Nujoma jijini Dar Es Salaam Machi 21, 2024.

Taswira ya jengo la kitega uchumi la PSSSF Commercial Complex lililoko barabara ya Sam Nujoma jijini Dar es Salaam. Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), wametembelea jengo hilo Machi 21, 2024, ili kukagua mradi huo uliogharimu Mfuko wa PSSSF, kiasi cha shilingi Bilioni 232.

Eneo la chini la maegesho ya magari
Majenereta ya usaidizi inapotokea umeme wa TANESCO umekatika
Ngazi za umeme na za kawaida ndani ya jengo la Commecial complex
Bwawa la kuogelea eneo la commercial complex
Mwenyekiti akiwa na baadhi ya wajumbe wa Kamati kwenye ghorofa lenye ofisi za UNDP
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) wakipata maelezo kuhusu wapangaji wa jengo hilo

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), Mhe. Deus Sangu (Katikati), akipeana mikono na Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Abdul-Razaq Badru huku Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji PSSSF, Bw. Rashid Mtima akishuhudia, wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), kukagua jengo la kitega uchumi la PSSSF Commercial Complex barabara ya Sam Nujoma jijini Dar Es Salaam Machi 21, 2024.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), Mhe. Deus Sangu (Katikati), akipeana mikono na Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji PSSSF, Bw. Rashid Mtima huku Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF Bw. Abdul-Razaq Badru, akishuhudia, wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee-PIC), kukagua jengo la kitega uchumi la PSSSF Commercial Complex barabara ya Sam Nujoma jijini Dar Es Salaam Machi 21, 2024.


Picha ya pamoja


Jennifer Dickson: Mwanzilishi wa maktaba ya kijamii wilayani Mwanga atunukiwa tuzo ya Malkia wa Nguvu Ajaye 2024

March 25, 2024
Mwanzilishi wa maktaba ya kijamii wilayani Mwanga, Jennifer Dickson akifurahia tuzo ya Malkia wa Nguvu ajaye katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
------
Nyota ya Mwanafunzi wa Kike wa kitanzania Jennifer Dickson na mwanzilishi wa maktaba ya kijamii wilayani Mwanga anayesoma elimu ya Chuo Kikuu mwaka wa pili nchini Rwanda katika Chuo cha Global Health Equity, akisomea fani ya Udaktari, inazidi kung’aa ambapo ametunukiwa tuzo ya Malkia wa Nguvu Ajaye 2024 katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.Tuzo hizo hutolewa na Clouds Media Group.

Maktaba aliyoianzisha Jennifer, inayojulikana kama maktaba ya kijamii ya Martha Onesmo, ilizinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwaka huu ipo katika kata ya Msangeni kwa ajili ya kuwahudumia watu wote. Mgeni rasmi katika uzinduzi wake alikuwa ni Waziri wa Elimu, Profesa Adolf Mkenda.

Akiongea muda mfupi baada ya kupokea tuzo hiyo, alisema kuwa amefarijika kwa kiasi kikubwa kuona mchango wake katika jamii umetambuliwa na tuzo hiyo imezidi kumtia moyo wa kuendelea kufanya kazi za kijamii zenye mwelekeo wa kunufaisha watu wengi.

Alitoa shukrani kwa wazazi wake,marafiki zake na wa familia,na wafadhili mbalimbali ambao wamemsaidia kufanikisha ndoto yake ya kufungua maktaba ya kijamii ambayo imepelekea apate tuzo ya Malkia wa Nguvu ajae inayotolewa na kampuni ya habari ya Clouds.

Pia alitoa shukrani wa waandaaji wa tuzo hizo kwa kuona mchango wake katika jamii pia alitoa ushauri kwa vijana wenzake hususani watoto wa kike kujiamini na kupambana ili kufanikisha ndoto zao katika maisha na kuhakikisha hawabaki nyuma.

Kwa upande wa wazazi wake, walisema wamefurahi kuona kijana wao anapata mafaniko “Tuzo hii ni kielelezo kikubwa kwamba mtoto wa kike anaweza kama akiwezeshwa. Jennifer ni matokeo ya juhudi zake na ushirikiano wa jamii nzima inayomzunguka ukiaanza na sisi wazazi wake, ndugu zake wengine wa karibu hasa bibi yake mama Cecilia Ezekiel na jamii nzima ambayo ilishirikiana naye kwa hali na mali kuhakikisha anatimiza ndoto yake. Ni watu wengi wanamchango wao wa hali na mali katika kufikia hapa tulipo leo” Alisema Dk. Linda Ezekiel.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya maktaba hiyo, Profesa Bonaventure Rutinwa, ambaye pia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amempongeza Jennifer kwa kufikia mafanikio hayo,”Ni jambo la kufurahisha kuona kijana wa umri wake anakuwa na ubunifu wa mradi ambao unaleta athari chanya kwa jamii hususani katika maeneo ya vijijini ,natoa wito kwake aendelee kupambana ili aweze kufanya mambo makubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla”. Alisisitiza.

Wakati wa uzinduzi wa maktaba hiyo ya kijamii ya Martha Onesmo, mwanzilishi wake Jennifer alisema ndoto ya kuanzisha maktaba hiyo alikuwa nayo yangu anasoma kidato cha sita kwa ajili ya kuwezesha wakazi wa vijijini kupata maarifa.

Picha ya pamoja ya wanafamilia ya Jennifer na marafiki wa familia.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Dk. Kitila Mkumbo (kulia) akimpongeza mshindi wa tuzo la Malkia wa Nguvu ajaye,Jennifer Dickson katika hafla ya kutunuku tuzo hizo iliyofanyika jijini Dar es Salaam,katikati ni mwenyekiti wa bodi ya maktaba ya kijamii ya Mwanga iliyoanzishwa Jennifer, Profesa Bonaventure Rutinwa, ambaye pia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Wanafamilia ya Jennifer na mwenyekiti wa maktaba ya Martha Onesmo wakifuatilia matukio katika hafla hiyo.
Jennifer akiwa na wazazi wake.
Jennifer akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya maktaba ya Martha Onesmo,Profesa Bonaventure Rutinwa.