Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Peter
Ngota akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani (kushoto)
hati ya makubaliano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya
Dawa Tanzania. Hafla hiyo ya makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo
kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania imefanyika leo Makao Makuu ya Ofisi
za MSD Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani akizungumza katika hafla ya
makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa
Tanzania inayotolewa na kampuni ya TTCL. Ofisi za Kanda za MSD
zimeunganishwa na Makao Makuu na huduma za mkongo wa mawasiliano ili
kufanya kazi zake kwa haraka na ufanisi zaidi.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani (kushoto) akisaini hati ya
makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa
Tanzania (MSD) leo Makao Makuu ya Ofisi za MSD Dar es Salaam, kulia ni
Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Peter
Ngota akishuhudia.
Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Peter
Ngota (kulia) akisaini hati ya makabidhiano ya mradi wa huduma za
mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa Tanzania (MSD), kulia ni Mkurugenzi
Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani akishuhudia kabla ya kukabidhiwa.
Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Peter
Ngota (wa tatu kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas Mwaifwani (wa
nne kushoto waliokaa) katika picha ya pamoja na baadhi ya maofisa wa
kampuni ya Simu Tanzania na Bohari ya Dawa Nchini katika hafla ya
makabidhiano ya mradi wa huduma za mkongo kwa ofisi za Bohari ya Dawa
Tanzania na kampuni ya TTCL.
KAMPUNI
ya Simu Tanzania (TTCL) leo imekabidhi mradi mkubwa wa Mkongo wa
Mawasiliano ambao umeyaunganisha matawi yote ya Bohari ya Dawa Nchini
(MSD) na Makao Makuu ili kufanya kazi zake kwa haraka na kwa ufanisi.
Hafla ya kukabidhi mradi huo imefanyika leo Makao Makuu ya Ofisi za MSD
zilizopo jijini Dar es Salaam.
Akikabidhi
mradi huo, kwa niaba ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha
Kazaura, Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Simu Tanzania,
Peter Ngota alisema kampuni hiyo inajisikia fahari kufanikiwa
kuunganisha ofisi zote za kanda za MSD na Makao makuu kupitia mkongo wa
mawasiliano ambao ni salama na wauhakika katika utendaji wa kazi.
Alisema
MSD ni moja ya wateja wake wakubwa ambao wameunganishwa kihuduma
kupitia mkongo wa mawasiliano ambao ufanisi wake ni mkubwa na salama kwa
wateja tofauti na teknolojia nyingine za mawasiliano. Alisema huduma za
mkongo wa mawasiliano zinazotolewa na TTCL kwa wateja wake ni salama na
zenye ubora katika ufanisi jambo ambalo limevuta idadi kubwa ya wateja
kuongezeka kila uchao.
Alisema
kwa sasa TTCL inatoa huduma hizo kwa makampuni ya simu, taasisi
mbalimbali za umma na binafsi, mabenki, hospitali kadhaa, vyombo vya
habari, wateja binafsi pamoja na mataifa kama Rwanda, Burundi, Uganda,
Kenya, Zambia na nchi ya Malawi.
Akizungumza
mara baada ya kukabidhiwa mradi huo, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Cosmas
Mwaifwani alisema MSD ilianza kufungiwa mawasiliano ya mkongo Mwezi Mei,
2011 kwa kuunganisha ofisi za makao makuu na baadaye ofisi mpya za
mauzo zilizopo Muleba zilizounganishwa mwaka 2013.
Alisema
MSD ilifanya uamuzi wa kuhamia kwenye teknolojia ya Mkongo baada ya
kuona uwepo wa matatizo makubwa yaliyokuwepo katika teknolojia ya awali
ambayo ni waya wa jadi yaani shaba ambayo pia ilitolewa na kampuni ya
TTCL.
"...Bohari
ya Dawa iliamua kuhamia katika teknolojia hii baada ya kufanya utafiti
wa kina na kuona faida ambazo zinaweza kupatikana kwa kutumia teknolojia
hii (mkongo) na hivyo kuachana na matatizo yanayosababishwa na
teknolojia ya shaba. Hii ina maana mkongo unaweza kubeba habari zaidi na
kwa ubora mkubwa kuliko waya wa shaba," alisema Mwaifwani.
Alisema
kwa sasa MSD imeanza kupata mafanikio makubwa baada ya kuanza kutumia
huduma za mkongo na tayari TTCL imeyaunganisha Ofisi 10 za MSD ambazo ni
Kanda nane (8) pamoja na vituo viwili vya mauzo; alizitaja Kanda
zilizounganishwa ni pamoja na Dar es Salaam, Moshi, Iringa, Mbeya,
Mwanza, Tabora, Dodoma, Mtwara, Muleba, Tanga, Makao Makuu ya Muda
Jamana na Ofisi za Keko Mwanga.
"...Tunasema
kwamba Bohari ya Dawa imedhamiria kuokoa maisha ya Watanzania kwa
kutumia teknolojia ya Mkongo yenye kasi zaidi, usalama, na gharama nafuu
zaidi katika kuhakikisha dawa zenye ubora zinamfikia kila Mtanzania kwa
wakati na kupunguza kero ya kusubiri huduma zetu kwa muda mrefu kwani
sasa huduma zinapatikana kwa wakati kwa kuwa teknolojia inayotumika ni
ya kisasa na yenye ubora wenye kukidhi viwango vinavyohitajika na bohari
ya dawa," alisema Mkurugenzi Mkuu, Mwaifwani.