MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) RAIS DKT. MAGUFULI AHUTUBIA MKUTANO MKUU WA TISA WA CCM KATIKA UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE CONVETIONAL CENTRE MJINI DODOMA

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) RAIS DKT. MAGUFULI AHUTUBIA MKUTANO MKUU WA TISA WA CCM KATIKA UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE CONVETIONAL CENTRE MJINI DODOMA

December 18, 2017

1
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia kwa kugonga mkono pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM kwa upande wa Zanzibar, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein wakati wakijiandaa kupiga kura za kumchagua Mwenyekiti wa CCM katika Mkutano Mkuu wa Tisa wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convetional Centre Mjini Dodoma
4
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Makamu Mwenyekiti wa CCM kwa upande wa Zanzibar, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein wakati wakipiga kura ya kumchagua Mwenyekiti wa CCM katika Mkutano Mkuu wa Tisa wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convetional Centre Mjini Dodoma
5
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan wa tatu kutoka (kushoto), Makamu Mwenyekiti wa CCM kwa upande wa Zanzibar, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein wa nne kutoka (kushoto), Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete wa kwanza (kushoto), Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi wa pili kutoka (kushoto), Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa wa pili kutoka kulia wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya kufungua mkutano wa Tisa wa Chama cha Mapinduzi CCM uliofanyika mjini Dodoma.
6
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM pamoja na wageni mbalimbali katika Mkutano Mkuu wa Tisa wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convetional Centre Mjini Dodoma
8
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kufungua mkutano wa Tisa wa CCM uliofanyika mjini Dodoma.
9
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Philip Mangula mara baada ya kufungua mkutano wa Tisa wa CCM uliofanyika mjini Dodoma.
10
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa na Rais mstaafu  wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa.
11
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akizungumza katika mkutano huo wa tisa uliofanyika mjini Dodoma.
12
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao katika mkutano huo wa tisa.
14
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akipiga kura kwa moja ya wagombea katika mkutano huo wa tisa.
15
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Philip Mangula mara baada ya kupiga kura zao kwa ajili ya uchaguzi wa viongozi hao.
16
Wanachama wa CCM wakiburidika kwa kucheza nyimbo mbalimbali katika mkutano huo wa tisa.
17
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimsalimia Mke wa Hayati Baba wa taifa, Mama Maria Nyerere katika mkutano huo wa Tisa wa CCM uliofanyika mjini Dodoma.
PICHA NA IKULU

VIONGOZI WA KIJIJI CHA MSOSA WILAYANI KILOLO WAVULIWA MADARAKA KWA NGUVU

December 18, 2017
Mtendaji wa kata ya Ruaha Mbuyuni Maiko Chabili akiwafafanulia jambo wananchi wa kijiji wakati wa mkutano wa hadhara ulikuwa na lengo la kuwafukuza kamati ya mipango na fedha ya kijiji kwa matumizi mabaya ya pesa zao
 Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha msosa kilichopo tarafa ya ruaha mbuyuni walihudhuria mkutano wa hadhara wa kijiji

Na Fredy Mgunda,Iringa.


Wananchi wa kijiji cha msosa kilichopo tarafa ya ruaha mbuyuni wameifukuza kamati ya mipango na fedha kwa tuhuma za kufanya ubadhilifu wa mali za kijiji na kuunda kamati mpya itakayoleta maendeleo katika kijiji hicho.

Wakizungumza wakati wa mkutano wa hadhara ulifanyika katika kijiji hicho wanachi waliutaka uongozi wa kamati hiyo kuachia ngazi kutokana na tuhuma zinazowakabili.

 Kwa upande wake mtendaji wa kata MAIKO CHABILI ameafiki kuvuliwa madaraka kwa viongozi wa kamati ya mipangano na fedha kutokana na tuhuma zinazowakabili.

Hata hivyo kamati ya mipango na fedha ya kijiji cha msosa walikubali kujiudhuru na kulipa pesa ambazo ilibaini kuwa walizitumia vibaya bila ruhusa ya wananchi.
NAIBU WAZIRI MHE.MANYANYA AFUNGUA RASMI MKUTANO WA VIDEO CONFERENCE

NAIBU WAZIRI MHE.MANYANYA AFUNGUA RASMI MKUTANO WA VIDEO CONFERENCE

December 18, 2017

DSC_0011
Naibu Waziri Mhe. Injinia Stella Manyanya afungua rasmi mkutano kwa njia ya Mtandao yaan (Video Conference) wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji na Mamlaka za mikoa na Halmashsauri za Wilaya kuhusu masuala ya sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji pamoja na taasisi zake leo Tarehe 18 – 20 Disemba, 2017 na kuunganisha wadau kutoka mikoa ya Mbeya, Songwe, Kilimanjaro, Ruvuma, Kigoma, Lindi, Singida, Pwani na Dodoma.
Mhe. Naibu Waziri aliwashukuru Makatibu Tawala wa Mikoa, Wasaidizi wao na Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya ambao wameitikia wito pamoja na wataalamu na maafisa mbalimbali.
Wizara ilianza na taasisi yake ya BRELA ambayo ilielezea majukujumu yake na huduma mbalimbali wanazotoa kwa umma na kutoa fursa ya wadau kutoka mikoa yote iliyoshiriki walipata fursa ya kuuliza maswali na kujibiwa papo kwa papo.

SAFARI YA WAZALENDO 47 ILIVYOINGIA SIKU YA PILI WAKATI WAKIELEKEA KILELE CHA UHURU,KATIKA MLIMA KILIMANJARO

December 18, 2017


Baada ya kupumzika katika kituo cha Mandara katika siku ya kwanza ,Mkuu wa Majeshi Mstaafu,Jenerali George Waitara aliongoza Wazalendo 47 kutoka jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ),Wanahabari,Marafiki wa China na Tanzania pamoja na watumishi kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) katika siku ya pili ya kuelekea kilele cha Uhuru kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 56 ya uhuru wa Tanzania.
Miongoni mwao alikuwepo ,Balozi Mstaafu na Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Utalii ,Tanzania ,Charles Sanga.
Safari ya kuelekea kituo cha pili cha mapumziko cha Horombo ili chagizwa na nyimbo mbalimbali ambazo ziliongeza morali kwa wapandaji.
Makao makuu ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) yaliwakilishwa vyema na Meneja wake wa Mawasiliano ,Pascal Shelutete .
Mwanahabri Vicky Kimaro aliwakilisha pia Magazeti ya serikali ya HABARI LEO.
Mwanahabari George Mbara alikiwalisha vyema kituo cha luniknga cha ITV.
Mwanahabari Jamila Omar yeye alifanya uwakilishi wa kituo cha Luninga cha Channel ten.
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) liliwakilishwa na Bertha Mwambela 
Na Safari iliendelea ikiongozwa na Slogan ya “Mdogo Mdogo”
Mapumziko yalikuwepo mara baada ya kutembea sehemu yenye umbali mrefu.
Wengine walitumia mapumziko hayo kwa ajili ya kupata picha za kumbukumbu ya pamoja.
Na baadae Safari iliendelea.
Hali ya hewa katika Hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro haitabiliki ghafla linaweza onekana jua na muda mchache tu mvua ikanyesha ,hivyo wapandaji hua wamejiandaa na aina yoyote ile ya hali kama inavyoonekana hapa wakiwa katika mavazi rasmi ya kuzuia mvua pindi walipowasili eneo la Nusu njia kwa ajili ya kupata chakula.
Wazalendo wakatumia mapumziko ya Nusu njia kupata chakula cha mchana.
Safari ikaendelea kwa kupita katika mito mbalimbali ambayo imekuwa ikitiririsha maji kwa wingi.
Wazalendo walipita katika madaraja mbalimbali wakati wa upandaji wa mlima huo.
Wenye kuhitaji msaada walipata kwa wakati.
Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) Betrita Loibook alihakikisha anaongozana na Wazalendo hao katika safari ya kuelekea kilele cha Uhuru akiwa ndiye mwenyeji wa ugeni huo.
Hatimaye safari iliyoanza saa 2:30 za asubuhi katika kituo cha mapumziko cha Mandara ikahitimishwa majira ya saa 11:00 za jioni katika kituo cha mapumziko cha Horombo kwa ajili ya kujiandaa na safari ya kuelekea kituo cha Kibo kabla ya kuelekea kilele cha Uhuru.
 
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya Kaskazini aliyekuwa katika msafara wa Wazalendo hao.

PANGANI COUNCIL AND OTHER GOVERNMENT ORGANS WARNED AGAINST PUTTING HITCHES ON THE WORK OF UZIKWASA

December 18, 2017
Pangani District Council and other Government organs have been advised against putting hurdles on the work of a non-government organization, UZIKWASA that is spearheading efforts to change traditional mindsets that hinder people, especially women and children form speaking out freely against gender-based violence and other social abuses.

The advice was given by the Deputy Minister for Water and Irrigation, Jumaa Awesso when he spoke at a ceremony to award best performing Village Multisectoral Aids, Gender and Leadership Committees (VMACs) held at Msaraza village in Bushiri Ward of Pangani District.

He said that UZIKWASA is responsible for changing mindsets of the people as regards gender-based violence, early marriages, early pregnancies and other social abuses in the society. “It is very difficult to separate the development of a freedom to speak out on various issues on the people and the work of UZIKWASA,” Awesso, who is also the Member of Parliament for Pangani, pointed out.

He said that he know that the organization has some challenges that hinder its work and called oin the Council and other Government organs to work closely with UZIKWASA which is spearheading the transformation of a society that was previously regarded as having fear of speaking out.

Awesso said that the Pangani society would suffer a heavy loss if it cuts down the work of the organization which has trained village leaderships on responsible and transformative leadership and enabled people to speak out on abuses that have been going for years in the society.

He said the work of the organization has had an impact on increase in reported cases of rape and oithe abuses in the district. He said the number of cases that have been reported this was 58 but 38 out of them have been stalling because culprits have been reported to escape.

Speaking at the occasion, a young person, identified as a Child Ambassador, Athumani Juma commended UZIKWASA for initiating the formation of a ‘Safe System’ in schools which enables school children to report incidences of abuse to authorities.

He told the audience, including members of VMACs from 12 villages that 51 cases of abuse against children have been reported from January this year. Thoruhg the safe system initiated by expanded School Committees trained by the organization.

Reading the children’s message, Juma said that action has been taken against people who perpetrated the incidents against children he mentioned as including harsh penalties, denying food to children by parents and caretakers, missing meals at school, beatings, burning, sexual abuse, rape, sodomy, touching of sensitive body spots and name calling against children.

He mentioned other such incidents to bewildered audience who included members of 12 VMACs as being denied money for various expenses at school, being given hard work and being burned in sensitive spots using being pricked using sharp tools.

Juma said that it was a sad that in some incidences were being perpetrated by those who were supposed to protect children and make sure they get better education sometimes turned against those children by abusing them.

 “Headteachers, patron and matron teachers and big age school children, out of schoo youth, including bodaboda drivers and adults in the streets and homes are all culprits in abusing school children. School girls were the main victims, leading to psychological effects that lead to these children absconding and engage in risky jobs,’ he said

The Child Ambassador called on the Government, private institutions and activists to continue to give awareness education and create an official system that would give school children a chance to be heard as regards to their challenges they face

Msaraza VMAC scooped the first prize of Sh. 700,000 for best performing VMAC for the year 2017, follwed by Mwera which scooped Sh. 600,000 and Mkwajuni Sh. 500,000.

TAARIFA KUTOKA NDANI YA SHIRIKISHO LA SOKA TFF LEO

December 18, 2017
DIRISHA DOGO LA USAJILI.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limesikitishwa kwa hitilafu iliyotokea siku ya mwisho ya usajili usiku wa Desemba 15, mwaka huu kwa kufeli kwa mtandao wa mfumo wa usajili hali iliyosababisha vilabu kushindwa kukamilisha usajili kwa wakati kupitia mfumo huo.
TFF inaendelea na jitihada za kuwasiliana na Mwendeshaji wa mfumo huo waliokasimiwa na Shirikisho la soka la Kimataifa (FIFA) walioko Tunis, Tunisia ili kutatua tatizo hilo la kimtandao  haraka iwezekanavyo ili kuweza kukamilisha usajili wa dirisha dogo. Katika mawasiliano na kampuni hiyo, FIFA na CAF wamekuwa wakipewa Taarifa ya kila hatua inayochukuliwa na TFF.
Wakati huu ambao jitihada hizo zinaendelea, TFF imevitaka vilabu kuwasilisha nyaraka za usajili wa dirisha dogo katika ofisi za Makao Makuu ya TFF Karume, Ilala jijini Dar es Salaam.
TFF imetoa muda hadi Jumamosi Desemba 23, 2017 kwa vilabu kuwasilisha nyaraka hizo za usajili wa dirisha dogo.

TFF inasisitiza vilabu vyote kuzingatia kusajili kwa wakati pale inapotokea dirisha la usajili limefunguliwa.

RATIBA MPYA LIGI KUU YA VODACOM


Ligi Kuu ya Vodacom iliyosimama kupisha michuano ya Kombe la Chalenji inaendelea mwishoni mwa mwezi huu kwa mechi za raundi ya 12 zitakazochezwa kati ya Desemba 29 na 31 mwaka huu, na Januari mosi mwakani.

Vilevile mechi 16 kati ya 152 zilizobaki za Ligi hiyo zitachezwa kuanzia saa 8 kamili mchana. Kwa mujibu wa Kanuni ya 14 (45) ya Ligi Kuu, mchezo wowote wa Ligi Kuu unatakiwa kuchezwa kati ya saa 8 kamili mchana, na saa 4 kamili usiku.

Uamuzi huo umefanywa ili kuongeza mechi ambazo zinataoneshwa moja kwa moja (live) na mdhamini wa matangazo, hatua ambayo itaisaidia Bodi ya Ligi kufuatilia kwa karibu uchezeshaji wa waamuzi na pia kutoa nafasi kwa wadhamini wa Ligi pamoja na wa klabu kuonekana zaidi (mileage).

Hivyo, mechi 102 kati ya 152 zitaoneshwa moja kwa moja ikiwemo zile zinazofanyika Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam ambazo kwa kawaida zinachezwa kuanzia saa 1 kamili usiku. 

Mechi za raundi ya 12 ni Desemba 29; Azam vs Stand United (saa 1 usiku), Desemba 30; Lipuli vs Tanzania Prisons (saa 8 mchana), Mtibwa Sugar vs Majimaji (saa 10 jioni), Ndanda vs Simba (saa 10 jioni), Desemba 31; Njombe Mji vs Singida United (saa 8 mchana), Mbao vs Yanga (saa 10 jioni), Januari 1; Mbeya City vs Kagera Sugar (saa 10 jioni), na Mwadui vs Ruvu Shooting (saa 10 jioni).

Baada ya raundi ya 12, Ligi Kuu ya Vodacom itapisha mechi za Kombe la Mapinduzi na raundi ya tatu ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports itakayochezwa kati ya Januari 5 na 7 mwakani kabla ya kuingia raundi ya 13 itakayofanyika kati ya Januari 13 na 17, 2018.

Kwa upande wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL), itaingia raundi ya 10 Desemba 30 kwa mechi za Kundi A na C, wakati mechi za Kundi B zitafanyika Desemba 31.

Ligi Daraja la Pili (SDL) itaanza hatua ya pili Desemba 29 kwa Kundi B, C na D wakati mechi za Kundi A zitafanyika kuanzia Desemba 30, 2017.

KAMPUNI YA ABACUS PHARMA (A) LTD YAZINDUA BIDHAA ZA SUGAR FREE JIJINI DAR ES SALAAM

December 18, 2017
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD, Ramesh Babu (kulia), Daktari Bingwa wa Magonjwa ya homoni na Kisukari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Faraja Chiwanga  na Dk. Mohamed Mohamed wa ugonjwa wa Kisukari katika hospitali hiyo wakikata keki maalumu iliyotengenezwa kwa bidhaa hiyo kuashiria uzinduzi wa bidhaa za Sugar Free uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Muonekano wa keki hiyo
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya homoni na Kisukari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Faraja Chiwanga akikabidhiwa zawadi.
 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD, Ramesh Babu, akipatiwa zawadi.

 Wafanyakazi wa kampuni hiyo wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Uzinduzi ukiendelea.
  Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD, Ramesh Babu, akizungumza wakati wa uzinduzi huo.
 Wadau wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Ni furaha tupu katika uzinduzi huo.
 Uzinduzi huo.
 Makofi yakipigwa katika uzinduzi huo.
 Hii ndiyo timu ya maofisa masoko wa kampuni hiyo.
 Meza kuu ikifuatilia mada katika uzinduzi huo.
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya homoni na Kisukari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Faraja Chiwanga, akizungumza kwenye hafla hiyo.
 Mada zikitolewa kuhusu bidhaa hizo.
 Maelezo kuhusu bidhaa hizo yakitolewa.
 Majadiliano yakifanyika.
 Taswira ya ukumbi wakati wa uzinduzi huo.
Ukumbi ulivyokuwa.

Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya Abacus Pharma (A) LTD imezindua bidhaa za Sugar Free ambazo zitatumika kukabiliana na ongezeko la wagonjwa wa kisukari nchini kutokana na bidhaa hizo kutokuwa na sukari wakati wa matumizi yake.

Akizungumza katika uzinduzi wa bidhaa hizo uliofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika Hoteli ya Best Western, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD, Ramesh Babu alisema bidhaa hizo zimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matumizi makubwa ya sukari katika vyakula. 

Alisema bidhaa hizo zimetengenezwa mahususi ili kukabiliana na ongezeko la sukari mwilini na hivi sasa zinapatikana kwa bei ya chini katika soko la nchi za Tanzania, Uganda, Kenya, Rwanda na Burundi na kuwa bei hizo zipo kuanzia shilingi,4200, 4,500, 5,700, 8,850 na za bei ya juu ni shilingi 13,000 na kuwa zinategemea bidhaa husika.

"Bidhaa hizi zipo za aina mbili za sugar free gold  ambazo hutumika katika chai, uji, na vinywaji baridi tu  na sugar free natura hutumika katika baking, kupikia vyakula vinavyohitaji sukari katika upishi na pia hutumika katika chai, uji na vinywaji baridi na matumizi yake ni rahisi sana," alisema Babu.

Alisema kwa Tanzania bidhaa hizo zimeanza kuchukua soko kubwa baada ya wananchi kuona umuhimu wake na hivyo wanategemea muitikio utaendelea kuwa mkubwa.

Aliongeza kuwa, lengo kubwa la kampuni hiyo kusambaza bidhaa hizo ni kusaidia jamii kuelewa matumizi ya bidhaa hizo ambazo hazina sukari ingawa zina ladha ya sukari kama ile ya kawaida  na kwamba bidhaa hizo zimethibitishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Akizungumza katika uzinduzi huo Daktari Bingwa wa Magonjwa ya homoni na Kisukari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Faraja Chiwanga alisema ugonjwa wa kisukari ni changamoto kubwa kwani Tanzania ni nchi ya tano Barani Afrika kwa kuwa na wagonjwa wengi.

Alisema hali hiyo inatokana na watu wengi hasa vijijini kutojijua mapema kama wameathiriwa na ugonjwa huo ambapo baadhi yao huanza kugundua baada ya kupata upofu, kukatwa miguu na kadhalika.

Aliongeza kuwa, matibabu ya mgonjwa mmoja wa kisukari yanafikia asilimia 25 ya pato la familia fedha ambazo ni nyingi jambo linalowafanya wauguzaji kukata tamaa ya kumtibu mgonjwa na kuamua fedha hizo kuzielekeza katika matumizi mengine.

Dk.Chiwanga alitoa mwito kwa kusema ni vizuri kuzuia kupata kisukari kuliko kutibu.

Akizungumzia bidhaa za sugar free alisema hazitibu ugonjwa wa kisukari isipo kuwa zinamsaidia mgonjwa au mtu mwenye kisukari anapokula vyakula vingine visivyo na sukari kupata radha ile ile.

Alisema mtu mwenye ugonjwa wa kisukari hatakiwi kabisa kuvuta sigara ingawa vitu vingine kama vinywaji na pombe anatakiwa kutumia kwa uangalifu.