DC MTASIWA AITAKA NSSF KUSHIRIKIANA NA HALMASHAURI KUJENGA VIWANDA KOROGWE.

January 26, 2016
MKUU wa wilaya ya Korogwe,Hafsa Mtasiwa amelitaka Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoani Tanga kushirikiana na Halmashauri kuweka mpango katika ujenzi wa viwanda vya nyama na matunda ambavyo vitaboresha,kuinua kipato na kuongeza ajira kwa wanachama wa mfuko huo.
Mtasiwa aliyasema hayo jana wakati akifungua semina ya wajasiriamali, waajiri na wadau wa Mfuko huo wilayanai Korogwe ambapo alisema ujenzi huo utasaidia kuwakwamua wakulima sambamba na wafugaji ambao wanakabiliwa na soko la uhakika wa kuuzia bidhaa zao.

Alisema kuwa uwepo wa viwanda hivyo utaweza kusaidia kuwapunguzia adha wananchi wanayokumbana nayo wakati mazao yao na mifugo inapokuwa tayari kwa ajili ya kuuzwa na hivyo kukuta baadhi ya bidhaa ikiwemo matunda kuozea mashambana kwa kukosa soko.

Aidha alisema kuwa sambamba na hilo wilaya hiyo ina auhitaji mkubwa wa nyumba kwa ajili ya watumishi na wakazi wa wilaya hiyo hivyo kulitaka shirika hilo kuangalia eneo hilo kwa njia ya uwekezaji na kuwapatia makazi bora kwa bei nafuu wananchi.

  “Katika jambo hili ni matumaini yangu kwamba mtaharakisha taratibu husika ili kuhakikisha uwekezaji huo unafanyika mapema na kwa kiwango cha juu ili kumpa mwanachama wenu Faida na pia kunufaisha jamii ya wakazi wa Korogwe na Taifa kwa ujumla “Alisema DC Mtasiwa.

Hata hivyo alilitaka shirika hilo kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha wanaandikisha wanachama katika maeneo ya vijijini na mijini wanaostahili ili waweze kupata fursa ya kujiunga na kunufaika na huduma za mfuko huo hasa kwa mafao ya matibabu.

   “Nitumie nafasi hii kusisitiza kwamba nyie ambao ni waajiri na
wanachama wa mfuko huu milifanya uchaguzi sahihi na hilo ni jambo la kupongezwa kwani ipo mifuko mingi ambayo mngeweza kujiunga nayo lakini mlipima na kuona NSSF ni mfuko sahihi “Alisema.

Mkuu huyo wa wilaya alitoa wito kwa waajiri kuhakikisha wafanyakazi
wao wanaandikishwa na kupata huduma za mfuko na kutekeleza wajibu wao
kuwasilisha michango sahihi na kwa wakati ili waweze kunufaika kupitia
mfuko huo.

Awali akizungumza, Meneja wa NSSF Mkoani Tanga,Dkt Frank Maguda alisema kuwa shirika hilo limekuwa na mpango madhubuti wa kutoa elimu kwa wanachama na wasio wanachama ili kuweza kuzijua na kuzitumia fursa zilizopo kwenye mfuko wa Taifa ya Hifadhi za Jamii zikiwemo za matibabu,pensheni mbalimbali, mafao ya muda mrefu na muda mfupi.

  “Katika kuwaelezea juu ya fursa pia tunaonyesha wajibu wao ili
kuwapa uwezo wa kukidhi vigezo au sifa za kupata mafao na huduma mbalimbali zitolewazo na shirika hilo vikiwemo pia mikopo,msaada wa mazishi,mafao ya uzazi,kuumia kazini,ulemavu “Alisema Meneja Maduga

STIKA ZA KUTOKOMEZA MAUAJI KWA WATU WENYE UALBINO ZA ZINDULIWA JIJINI DAR LEO.

January 26, 2016

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Naibu Kamishna, Simon Sirro, akizungumza na wadau mbalimbali juu ya kufanisha uzinduzi wa Stika maalumu yenye ujumbe wa kutokomeza mauaji ya watu wenye Albinism,leo jijini Dar es Salaam.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Naibu Kamishna, Simon Sirro, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Stika maalumu yenye ujumbe wa kutokomeza mauaji ya watu wenye Albinism jijini Dar es Salaam,kulia ni Mwenyekiti wa Albno Enteprises of Dar es Salaam Michael Lugendo.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Naibu Kamishna, Simon Sirro, akupokea tuzo kutoka kwa Mwenyekiti wa Albino kutoka Enteprises of  Dar es Salaam, Michael Lugendo leo jijini Dar es Salaam.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Naibu Kamishna, Simon Sirro, akionesha Stika mara baada ya uzinduzi wa wa Stika maalum yenye ujumbe wa kutokomeza mauaji ya watu wenye Albinism,leo jijini Dar es Salaam.
 Sehemu ya maofisa mbalimbali wa Jeshi la Polisi waliofika katika uzinduzi wa Stika maalum yenye ujumbe wa kutokomeza mauaji ya watu wenye Albinism,leo jijini Dar es Salaam.

Waandishi wa habari wakimsikiliza Kamanda wa Polisi Kanda Maalimu ya Dar es Salaam, Naibu Kamishna, Simon Sirro, leo jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globul ya jamii)

KAMANDA wa Polisi Kanda Maalimu ya Dar es Salaam, Naibu Kamishna, Simon Sirro, leo amezindua stika za kutokomeza mauaji kwa watu wenye albinism.

Kamanda Sirro amesema lengo la stika hizo ni kutoa elimu maeneo yote hasa katika mikoa ya Kanda ya ziwa ambapo mauaji ya albino yamekithiri.

Amesema stika hizo zitasambazwa nchi nzima kwasababu ipo mikoa mbalimbali bado ina mila potofu za kishirikina ambapo watu wanaamini kuwa akipata viungo vya albino atakuwa tajiri.

Amesema kuwa kusudi ni kutotoa elimu kwa njia ya stika ni kwamba zitabandikwa katika majumba, maofisini, kwnye magari, madukani, mashuleni, vyuoni, kwenye bodaboda na bajaji na elimu hiyo itamfikia hata yule mtanzania ambaye hana redio na runinga.

“Tuna kila sababu kuhakikisha kuwa kila mmoja anaishi kwa amani na kuwalinda ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi(Albino.

“Sisi kama jeshi la Polisi na vyombo mbalimbali vya dola tunawajibika kupata taarifa za wale wanaotafuta viungo vya albino tutahakikisha tunapata taarifa kabla ya tukio halijafanyika,” alisema Kamanda Sirro.

Amesema jeshi hilo litashirikiana na Viongozi wa Serikali za mtaa, viongozi wa dini zote pamoja na taasisi mbalimbali zenye kutetea haki za binadamu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya AlbinoInterprises Dar es Salaam, Michael Lugendo, alisema lengo la stika hizo ni kutokomeza mauaji lwa watu wenye albinism na kazi hiyo inahitaji ushirikishwaji wa kila mtu.

Amesema hapa nchini albino wanakabiliwa na mauaji ya aina tatu ambayo ni mauaji ya kisaikolojia yanayomgusa kila mtu mwenye albinism ambayo yalianza pale vitendo vya kukata viungo vya albino vilipoibuka.

Kugendo amesema mauaji mengine ni yale yanayosababishwa na saratani ya ngozi ambayo hutokana na ukosefu wa mafuta ya ngozi na vikingia jua kulingana na mabadiliko ya tabia nchi, pamoja na mauaji ya kukatwa viungo ambavyo jamii jamii kubwa inawatambua hadi sasa wanaofanya vitendo hivyo.

Hata hivyo aliwataka viongozi wa dini, wanasiasa, wafanyabiashara kuwasaidia michango ili kuwezesha zoezizima la usambazaji stika hizo.

Pia taasisi hiyo ilimtunuku Kamanda Sirro tuzo ya amani na upendo pamoja na kutoa cheti cha kujali jamii kwa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).




Kamanda Sirro amesema kuwa tuzo hiyo ni mwanzo mzuri kwake na ina mpa moyo wa kuendelea kushirikiana na albino katika kutokomeza mauaji.

MATUKIO MBALIMBALI BUNGENI MJINI DODOMA.

January 26, 2016

Spika wa Bunge Job Ndugai (kulia)  akimwapisha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa  , bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016. 
 Spika wa Bunge Job Ndugai (kulia)  akimwapisha Waziri wa  Fedha na Mipango, Dkt.Philip Mpango, bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016.
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Dkt. Abdallah Possi akijibu maswali Bungeni Mjini Dodoma Januari 26, 2016.
 Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama  akijibu swali Bungeni Mjini Dodoma Januari 26, 2016.
 Wabunge wakisikiliza hoja mbalimbali bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016.
  Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Anthony Mavunde  akijibu maswali Bungeni Mjini Dodoma Januari 26, 2016.
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akijibu maswali Bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akitoa hoja ya kutaka Bunge lijadili  Hotuba ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati alipofungua Bunge la Kumi na Moja Novemba 20, 2015.
 Mbunge wa Mvomero, Murad Sadiq akichangia  bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016.
  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
UNESCO YAFANYA KONGAMANO LA KUJADILI MPANGO WA MAENDELEO YA SEKTA YA ELIMU (ESDP) KWA MWAKA 2017 - 2021

UNESCO YAFANYA KONGAMANO LA KUJADILI MPANGO WA MAENDELEO YA SEKTA YA ELIMU (ESDP) KWA MWAKA 2017 - 2021

January 26, 2016
IMG_1467
Mkurugenzi wa Elimu ya Watu Wazima na Elimu iliyo nje ya Mfumo rasmi kutoka Wizara ya Elimu, Salum Mnjagila, kwa niaba ya Kamishna wa Elimu, Prof. Eustella Bhalalusesa akizungumza na waandishi wa habari katika kongamano la kujadili Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (ESDP). Kushoto ni Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues. (Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).
IMG_1499
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusiana na kongamano hilo la siku mbili linalofanyika katika ukumbi wa mikutano wa NACTE jijini Dar es Salaam.
Na Rabi Hume wa Modewjiblog
Katika kuhakikisha elimu ya Tanzania inakua yenye ubora zaidi, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limepanga kuisaidia Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi kuandaa Mpango wa Maendeleo katika Sekta ya Elimu (ESDP), mpango ambao umelenga kusaidia serikali ya Tanzania kutengeneza maudhui na mikakati ya kuendeleza elimu kwa upande wa Tanzania bara.
Akizungumzia mpango huo katika kongamano la siku mbili la kutambua vipaumbele vinavyotakiwa katika kuandaa mpango huo wa elimu, kwa niaba ya Kamishna wa Elimu wa Wizara ya Elimu, Mkurugenzi wa Elimu ya Watu Wazima na Elimu iliyo nje ya Mfumo rasmi kutoka Wizara ya Elimu, Salum Mnjagila alisema mpango huo unatarajiwa kufanya kazi kwa kipindi cha miaka mitano kwa kuanzia mwaka 2017 – 2021 ili kuona ni jinsi gani utabadili elimu ya Tanzania.
Alisema kupitia kongamano hilo wanataraji kuchagua baadhi ya vipaumbele ambavyo wataona vinaumuhimu zaidi kuanza navyo kwa miaka mitano ya kwanza kwa mpango huo na baadae wataanza utekelezaji wa vipaumbele ambavyo vitakuwa vimepewa kipaumbele na washiriki wa kongamano hilo.
“Tupo hapa kufanya tathimini ya vipaumbele ambavyo vimeletwa mbele yetu ili tufanyie uchambuzi na tuone ni vipaumbele vipi tutaviweka kwenye mpango wa miaka mitano katika kuboresha sekta ya elimu nchini,” alisema Mnjagila.
Nae Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Elimu, Makuru Petro ambaye ameshiriki kufanya uchambuzi wa elimu ya Tanzania kwa kushirikiana na wataalamu kutoka UNESCO alisema katika kuchambua elimu ya Tanzania wamegundua kuwa elimu imekuwa ikishuka na hilo linatokana na kuongezeka kwa wanafunzi wanaosajiliwa kuanza shule huku kukiwa hakuna maboresho ambayo yanafanyika ili kuboresha elimu hiyo.
Alisema baada ya uchambuzi kufanyika wanafanya tathmini ili kupata matokeo ambayo watajadili kwa pamoja kwa kushirikisha wadau mbalimbali kutoka mashirika ya kiserikali na yasiyo ya serikali ili kupitisha vipaumbele ambavyo vitafanyiwa kazi kati ya vipaumbele ambavyo wao waliwasilisha kwa washiriki hao.
“Elimu ya Tanzania hali sio nzuri tumefanya uchambuzi hata mashuleni hakuna hali nzuri mfano hata Geita tumekuta darasa moja linatumiwa na wanafunzi 80 hadi 100 na hilo ni tatizo na baada ya kuchambua changamoto na kuzifanyia tathmini tunazileta hapa ili tuchague vipaumbele vya kuanza kuvifanyia kazi,” alisema Petro.
Nalo Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kupitia kwa Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa shirika hilo nchini, Zulmira Rodrigues alisema lengo la kuweka mpango huo ni kuboresha elimu ya Tanzania kwa kuifanya kuwa bora na iliyo na usawa kwa makundi yote ya jamii kwa matokeo mazuri ya baadae.
Alisema kuna mambo ambayo yanatakiwa kupewa vipaumbele ikiwepo ni pamoja na ubora wa elimu, fursa za elimu kwa makundi yote katika jamii na kujenga uwezo kwa watendaji ambao wanatoa hiyo elimu kama ni walimu basi wawe wanapewa mafunzo kuendana na wakati uliopo ili kuwa na kitu kipya ambacho kinahitajika kwa wanafunzi kwa wakati huo.
IMG_1506
Mkuu wa kitengo cha Ushirikiano wa Kiufundi kutoka Makao Makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini Ufaransa, Anton De Grauwe akiwasilisha vipengele mbalimbali vinavyotakiwa kujadiliwa na washiriki wa kongamano hilo katika kuandaa Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (ESDP) kwa mwaka 2017 - 2021.
IMG_1683
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues akiwasilisha mambo mbalimbali muhimu yanayotakiwa kuzingatiwa kwenye Ajenda 2030 ya elimu na mpango wa utekelezaji katika kongamano la kujadili Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (ESDP).
IMG_1666 IMG_1683 IMG_1591
Ofisa Mipango ya Elimu wa Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Jennifer Kotta (kushoto) akiteta jambo na Maofisa wenzake kutoka UNESCO, Faith Shayo (katikati) na Leonard Kisenha (kulia) wakati kongamano la kujadili Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (ESDP) kwa mwaka 2017 - 2021 likendelea.
IMG_1570
Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Elimu, Bw. Makuru Petro ambaye akishiriki kufanya uchambuzi wa elimu ya Tanzania kwa kushirikiana na wataalamu kutoka UNESCO kwenye kongamano hilo.
IMG_1642
Mshauri wa Taasisi ya kimataifa ya mipango ya elimu (IIEP)/UNESCO, Barnaby Rooke akielekeza vipaumbele kwenye bajeti ya sekta ya elimu ambayo inahitaji maboresho makubwa ili kuleta mabadiliko kwenye sekta elimu nchini.
IMG_1596
Moja ya 'Papers' zilizowasilisha kwa washiriki.
IMG_1615
Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Elimu, Clifford Tandari akishiriki kwenye kongamano la kujadili Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (ESDP) kwa mwaka 2017 - 2021 linalofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za NACTE jijini Dar es Salaam.
IMG_1738
Mwenyekiti wa Mtandao wa Redio za Jamii nchini (COMNETA), Joseph Sekiku akitoa maoni kuhusiana na udhaifu wa mipango ya sekta elimu nchini ambayo haitekelezeki wakati wa kongamano la kujadili Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (ESDP).
IMG_1784
Bi. Helena Reutersward, kutoka Ubalozi wa Sweden kitengo cha Elimu akitoa maoni wakati wa kongamano la kujadili Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (ESDP) nchini linaloendelea katika ukumbi wa mikutano NACTE jijini Dar es Salaam.
IMG_1654
Pichani juu na chini ni wajumbe walioshiriki kongamano hilo kutoka taasisi mbalimbali za serikali, Wizara ya Elimu, Taasisi za Elimu na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
IMG_1539
IMG_1515 IMG_1533
THE TONY ELUMELU FOUNDATION, UNITED BANK FOR AFRICA PLC AND THE UNITED STATES DEPARTMENT OF COMMERCE PARTNER TO ENABLE ENTREPRENEURSHIP IN AFRICA

THE TONY ELUMELU FOUNDATION, UNITED BANK FOR AFRICA PLC AND THE UNITED STATES DEPARTMENT OF COMMERCE PARTNER TO ENABLE ENTREPRENEURSHIP IN AFRICA

January 26, 2016
Group Shot
U.S Secretary of Commerce, Penny Pritzker; Select Tony Elumelu Foundation Entrepreneurs; Kehinde Yinusa, Evans George, Nosakhare Oyegun, Belema Alagun and Founder Tony Elumelu Foundation, Mr. Tony Elumelu during the panel and roundtable discussion between members of the U.S. Presidential Advisory Council on Doing Business in Africa (PACDBIA) and a diverse community of entrepreneurs hosted by Tony Elumelu Foundation and UBA Plc in Lagos yesterday.
PO SEC TOE
Group Managing Director United Bank for Africa (UBA) Plc, Mr. Phillips Oduoza; US Secretary of Commerce, Penny Pritzker; UBA Chairman, Mr. Tony Elumelu during the panel and roundtable discussion between members of the U.S. Presidential Advisory Council on Doing Business in Africa (PACDBIA) and a diverse community of entrepreneurs hosted by Tony Elumelu Foundation and UBA Plc in Lagos yesterday.
The Tony Elumelu Foundation and United Bank for Africa Plc (UBA) partnered with the United States Department of Commerce to host a panel and roundtable discussion between members of the U.S. Presidential Council on Doing Business in Africa (PCDBIA)and a diverse community of African entrepreneurs.
The 11 person U.S. delegation, along with representatives of several U.S. government trade and investment-focused agencies, was led by the Honourable Penny Pritzker – U.S. Secretary of Commerce. The Council visited Lagos as part of a fact-finding mission to help inform their upcoming report to President Obama on how to strengthen commercial engagement between the U.S. and Africa, which will result in mutually-beneficial growth.
The event – titled “Unleashing Africa’s Entrepreneurs: Strengthening the Entrepreneurial Ecosystem to Empower the Next Generation of Africa’s Business Leaders” – brought together American business leaders and Nigerian entrepreneurs to discuss challenges, solutions and innovations in the current African business environment. The event was designed to allow representatives of the U.S. Government to participate in direct and substantive discussions with Africa’s emerging business leaders – an opportunity to engage in a dialogue that has the potential to influence U.S. foreign policy for Africa.
"President Obama believes, as I do, that the American private sector, working in partnership with the African business community, and African entrepreneurs can help address many of the continent’s most pressing challenges, including creating jobs and opportunity for young people across the continent," said U.S. Secretary of Commerce Penny Pritzker. "I am proud to lead our Administration’s effort to support and empower aspiring entrepreneurs, both in the United States and across the globe."
UBA Chairman Tony O. Elumelu, through his eponymous Foundation, hosted the delegation, and expressed gratitude for the collaborative approach the Council and U.S. Commerce Department are taking in engaging local entrepreneurs as part of their deliberations.
“Too often, well-meaning foreign policy-makers develop strategies to help Africans without actually engaging us,” he said. “In order to effectively help or support people, we should ask them what kind of help they want. So, I thank you for doing that with African businesses.”
For the U.S. Government, this trip begins the Road to GES 2016 – the Global Entrepreneurship Summit; an annual gathering of entrepreneurs at all stages of business development, designed to demonstrate the U.S. Government’s commitment to fostering entrepreneurship around the world.
Expressly designed to address the needs of and provide opportunities for the next generation of African entrepreneurs, the entrepreneurs in attendance included SMEs supported by UBA Plc, UNCTAD’s EMPRETEC Nigeria Foundation and those selected for the Tony Elumelu Entrepreneurship Programme (TEEP) – a 10-year, $100 million commitment by the Tony Elumelu Foundation to empower the next generation of Africa’s entrepreneurs with businesses that have the potential to generate income and jobs for their nations.
The Tony Elumelu Entrepreneurs in attendance were selected from the Agriculture, Media & Entertainment, ICT, Transport, Healthcare and Financial Services sectors. Their startups reflect the potential that entrepreneurship holds for spurring Africa's transformation; already, they have begun creating jobs in their local communities and generating tax revenues for governments earning them recognition in both local and international media.

CHAMA CHA WAENDESHA BODABODA JIJINI ARUSHA CHAIOMBA SERIKALI KUONDOA UTATA ULIOPO KATI YAO NA WAENDESHA PIKIPIKI ZA KAWAIDA

January 26, 2016
 Waendesha pikipiki wakiwa mbele ya ofisi ya Mkuu wa mkoa.





Na Vero Ignatus , Arusha.

Chama cha waendesha bodaboda Jijini Arusha ( UWAPA) chaiomba serikali kutatatua utata uliopo kati ya waendesha bodaboda na waendesha pikipiki za kawaida kwa kuwawekea alama maalumu ambayo itawatambulisha, hii ni kutokana na maandamano ambayo yamefanyika siku ya tar 25./1 /2016 kwani ni kinyume kwakuwa chama hakina taarifa yeyote kuhusu maandamano hayo. Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa UWAPA bwana Godlight Rugemalila ambapo amesema ametoa taarifa polisi kutokana na maandamano hayo na amesema jambo walilolifanya siyo sahihi kwa hao walioratibu maandamano hayo ,na amewataka waendesha bodaboda wote kama kuna jambo lolote watalipata ofisini wafuate utaratibu wasikurupuke

 Amesema kuwa yapo makundi ya aina mbili kwa waendesha bodaboda,kundi la kwanza ni walimesajiliwa na UWAPA hawana vituo maalum , kundi la pili ni waendesha pikipiki za kawaida hawa hawajasajiliwa na idadi yao ni kubwa ambao huwaharibia wale ambao wanafanya biashara halali ya kubeba abiria Amesema kuwa wao kama UWAPA hawajapanga maandamano walipata taarifa kutoka kwa watu binafsi na walishtushwa kusikia kuna maandamano hayo na ameongeza kuwa wanaendelea kufanya utafiti kwa kushirikiana na jeshi la polisi ili kufahamu ni wakina nani wanahusika kuratibu maandamano hayo . 

Amewataka waendesha bodaboda wafuate sheria za usalama barabarani kama zinavyoelekeza, wawe na leseni, wavae kofia ngumu ,wapaki kwenye vituo vilivyosajiliwa ,amewashauri abiria wanaotumia usafiri huo wachukue bodaboda zilizopo kwenye vituo kwani akipata tatizo lolote ni rahisi yeye kusaidika tofauti na akichukua pikipiki ambayo ameiona barabarani inapita utakosa pa kupeleke malalamiko yako maana kila kituo kina kiongozi. Ameainisha waendesha bodaboda waliosajiliwa na wanaotambulika hadi sasa jumla yao ni 2950 ,vituo vilivyosajiliwa 144 na vituo bubu ambavyo bado na vinatazamia kupata usajili ni 55 hivyo amewataka waendesha pikipiki wote wajisajili kwenye chama hii ni kwa faida yao maana watatambulika watasaidika mara wapatapo tatizo na hii itawaepusha kuingia kwenye lawama za mara kwa mara kuwa waendesha pikipiki ni wakwapuaji na wanatumika kwenye matukio ya uhalifu.

 Amehitimisha kwa kusema kuwa UWAPA ni umoja wa wawaendesha bodaboda jijini Arusha na umoja huu ulisajiliwa marchi 2012 na unatambulika kiserikali,lengo ni kuwaleta pamoja waendesha bodaboda na huwa wanapatiwa mafunzo na RTO chini ya kitengo cha usalama barabarani , hivyo amewataka wananchi wafahamu kuwa wapo waendesha bodaboda hawa wanapaki maeneo yaliyoidhinishwa na ni vituo halali na waendesha pikipiki ni yeyeote yule unayeweza mchukua barabarani hana kituo. Maandamano hayo yalifanyika kuelekea kwa mkuu wa mkoa wa Arusha wakiwa na madai ya wakimtaka mkuu huyo wa mkoa atoe tamko kuhusu kusumbuliwa kwao na askari wa usalama barabarani .
-- Gadiel E.W. U (Gadiola Emanuel) IT/ PR /Photojournalist and Blogger -Based in Arusha, Tanzania. Mob :+255 715 643 633 E-mail: gadiola25@gmail.com WEB: www.wazalendo25.blogspot.com : www.arushapublicity.blogspot.com :www.northernshotstz.blogspot.com

WAZAZI MKOANI MWANZA WASIKITIKA ELIMU BURE KUWABAGUA WANAFUNZI WA ELIMU YA WATU WAZIMA.

January 26, 2016

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Asa Mwaipopo (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi katibu mkuu wa Ambassador FC, Bakari Khalid kwa  ajili ya maandalizi ya ligi daraja la pili mkoa wa Shinyanga..
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Asa Mwaipopo (kushoto) na Bakari Khalid Katibu mkuu wa timu ya Ambassador wakati wa hafla ya kukabidhi msaada kwa timu hiyo.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kukabidhi hundi timu ya Ambassador FC.
Katibu wa timu ya Ambassador FC, Bakari Khalid akizungumza mara baada ya kukabidhiwa hundi na Uongozi wa Mgodi wa Buzwagi.
Baadhi ya wafanyakazi wa mgodi wa Buzwagi katika hafla ya makabidhiano ya hundi kwa timu ya Ambassador kwa ajili ya maandalizi ya ligi daraja la pili mkoa wa  Shinyanga.
Vikosi vya timu za Buzwagi fc na Ambassador vikiwa katika maandalizi wakati wa ukaguzi kabla ya kuanza kwa mhezo.