Showing posts with label elimu. Show all posts
Showing posts with label elimu. Show all posts

UNESCO Yaunga Mkono Juhudi za Serikali Kuboresha Mfumo wa Usimamizi wa Mafunzo Endelevu ya Walimu (MEWAKA)

September 11, 2025 Add Comment


Picture1

Picture2

Picture3

Picture4

Picture5

Na Mwandishi Wetu, Arusha.

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeonyesha dhamira ya dhati Kufanya kazi bega kwa bega na wadau wa maendeleo kuhakikisha uboreshaji wa mfumo wa usimamizi wa mafunzo endelevu wa walimu kazini yaani MEWAKA unaboreshwa na kukamilika kwa wakati na kwa ufanisi ili kuwezesha mahitaji ya walimu wa Sekondari.


Akizungumza wakati wa kuhitimisha warsha  iliyofanyika kwa muda ya siku mbili ya tarehe 28 na 29 Agosti 2025, ya mapitio ya mfumo wa MEWAKA ulioboreshwa Mratibu wa Mradi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bi. Lina Rujweka, alitoa shukrani kwa juhudi na muda uliowekezwa na wadau wote, ikitambua mchango wao muhimu unaotarajiwa kuleta mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mradi huu hasa UNESCO na Jamhuri ya Korea kupitia mradi wa ‘’KFIT III wa Transforming Education through ICT in Africa’’ kwa kuendelea kutoa msaada wa kifedha.


Shirika la UNESCO Dar es Salaam, kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), inaendelea na juhudi za uboreshaji mfumo wa MEWAKA ili kuzingatia mahitaji ya walimu wa shule za sekondari.

Ushirikiano huu ulitokana na tathmini ya mahitaji iliyoonyesha kuwa mfumo wa sasa ulikuwa umeundwa mahsusi kwa ajili ya kuwa jukwaa la mafunzo ya maendeleo ya kitaaluma kwa walimu wa shule za msingi.

Hivyo, wadau walikutanishwa ili kupitia toleo la awali la mfumo wa MEWAKA kwa lengo la kuhakikisha umuhimu, ubora, na uendelevu wa muda mrefu wa jukwaa hilo.


Wadau hao walikuwa kutoka  wizara ya elimu, sayansi na Teknolojia , Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Taasisi ya Elimu Tanzania, Tume ya Kitaifa ya UNESCO na baadhi ya walimu wa shule za sekondari.


Katika hotuba yake ya ufunguzi, mwakilishi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ally Mape alisema majukwaa ya kidijitali ni nyenzo yenye nguvu ya maendeleo ya kitaaluma, yanayochangia kwa kiasi kikubwa kuwawezesha walimu kupata ujuzi na kujiamini ili kufanikisha kazi zao katika Dunia ya sasa.


Kwa upande wake mkuu wa Sekta ya Elimu kutoka Ofisi ya UNESCO Dar es Salaam, Dkt. Faith Shayo, ameeleza kuwa lengo kuu ni kupanua upatikanaji wa mafunzo endelevu ya kitaaluma kupitia majukwaa ya kidijitali, hivyo itasaidia kuboresha matokeo ya ufundishaji na ujifunzaji kote nchini.


Hata hivyo Dkt. Shayo aliwahimiza wadau kutoa maoni na mitazamo yao kusaidia kuhakikisha toleo la mwisho la mfumo huu sio tu kuwa la kisasa bali pia rahisi kutumia na lenye matokeo chanya.

Mpango huu unalingana na juhudi za Serikali za kuunganisha TEHAMA katika elimu, kama inavyoonekana katika sera na mikakati muhimu ya kitaifa ikiwemo Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 toleo la 2023, Mkakati wa Kitaifa wa Elimu ya Kidijitali 2025 – 2030, Dira ya Maendeleo ya 2050, Mitaala ya Elimu ya Msingi na ya Ualimu, pamoja na mipango ya kimataifa kama vile Malengo ya Maendeleo Endelevu hasa lengo namba nne.

MAHAFALI YA 11 NELSON MANDELA: WAHITIMU WAPEWA WITO WA KUBUNI, KUBIASHARISHA NA KUITUMIKIA JAMII

MAHAFALI YA 11 NELSON MANDELA: WAHITIMU WAPEWA WITO WA KUBUNI, KUBIASHARISHA NA KUITUMIKIA JAMII

August 29, 2025 Add Comment

 

Wahitimu wa Mahafali ya 11 ya Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) wakiwa tayari kwa ajili ya kutunukiwa shahada zao na Mkuu wa Taasisi, Mhe. Omari Issa (hayupo katika picha).

......

TAASISI  ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imejivunia kutimiza malengo matano ya msingi iliyojiwekea, likiwemo eneo la utafiti na ubunifu, pamoja na usimamizi madhubuti wa programu za uatamizi wa teknolojia.

Akizungumza Agosti 28, 2025 jijini Arusha wakati wa Mahafali ya 11 ya taasisi hiyo, Makamu Mkuu wa Taasisi, Prof. Maulilio Kipanyula, alisema taasisi hiyo imepanua wigo wake wa kitaaluma kwa kutoa Shahada ya Umahiri katika Ubunifu na Usimamizi wa Ujasiriamali kupitia Shule Kuu ya Mafunzo ya Biashara na Sayansi za Jamii (BuSH), ambapo wahitimu wa kwanza kutoka shule hiyo walitunukiwa shahada kwa mara ya kwanza.

Jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada katika mahafali hayo, ambapo 71 walitunukiwa Shahada ya Umahiri na 40 walitunukiwa Shahada ya Uzamivu.

Prof. Kipanyula alieleza kuwa dhana ya kubiasharisha bunifu na teknolojia inayoendelezwa na NM-AIST inalenga kusaidia Serikali katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hususan katika kukuza viwanda na uchumi wa nchi kwa ujumla.

“Tunawataka wahitimu wetu kuwa na mtazamo wa soko katika kila bunifu wanayoanzisha. Hadi sasa, zaidi ya bunifu 35 zimepata hatimiliki. Hatua inayofuata ni kuhakikisha zinabiasharishwa kwa tija na kuwa chanzo cha mapato kwa taasisi na taifa,” alisema Prof. Kipanyula.

Aliongeza kuwa usimamizi wa uatamizi, uhaulishaji wa teknolojia na ubia kati ya watafiti na sekta binafsi ni nguzo muhimu ya kuimarisha uchumi kupitia maarifa yanayotolewa na taasisi hiyo. Hata hivyo, alisisitiza kuwa mafanikio hayo hayawezi kufikiwa bila kushirikisha jamii.

Katika mwaka wa kwanza wa masomo, Prof. Kipanyula alisema NM-AIST imefanikiwa kudahili wanafunzi 250 wa shahada za umahiri na uzamivu, ambapo wengi wao walinufaika na ufadhili wa Samia Scholarship. Kupitia ufadhili huo, wanafunzi 50 wamepata mafunzo katika maeneo ya akili bandia (Artificial Intelligence) na Sayansi ya Takwimu (Data Science).

Aidha, alieleza kuwa taasisi hiyo imenunua vifaa vya kisasa vya maabara na imepata ithibati ya kimataifa, hatua inayowezesha utafiti wa kiwango cha juu kinachokubalika kitaifa na kimataifa, hususan kwa kushirikiana na viwanda.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Taasisi, Balozi Maimuna Tarish, aliwahimiza wahitimu kutumia ujuzi walioupata kutatua changamoto za jamii, kuanzisha ajira na kushiriki kikamilifu katika mageuzi ya kiuchumi.

“Maarifa, ujuzi na ubobezi mlioupata lazima uwe chachu ya mabadiliko chanya kwa taifa. Muwe na moyo wa kujituma, mzingatie uadilifu, na mwe mfano wa kuigwa katika jamii,” alisema Balozi Tarish.

Wakati huo huo, mmoja wa wahitimu hao, Isaac Mengele, alishukuru kukamilisha masomo yake katika taasisi hiyo huku akieleza kuwa tafiti yake ilihusu kuenea kwa vinasaba vya kinga kwa ng’ombe wa maziwa dhidi ya ugonjwa wa maziwa, kwenye mashamba madogo ya ufugaji.

“Nitahakikisha matokeo ya tafiti yangu yanawasaidia wafugaji wa ng’ombe wa maziwa kufuga kisasa zaidi, kupunguza magonjwa, na kuongeza tija,” alisema Mengele.

Mlau wa Mahafali ya 11 ya Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Gabriel Shirima, akiongoza maandamano ya wanataaluma kuelekea sherehe za Mahafali, Agosti 28, 2025, katika kampasi ya Tengeru, Arusha. Jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada mbalimbali za Umahiri na Uzamivu.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Maulilio Kipanyula, akisoma hotuba wakati wa Mahafali ya 11 yaliyofanyika Agosti 28, 2025, ambapo jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada mbalimbali za Umahiri na Uzamivu.

Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Mhe. Omari Issa (kulia), akimtunuku mmoja wa wahitimu (kushoto) wa Shahada ya Uzamivu wakati wa Mahafali ya 11 ya taasisi hiyo, Agosti 28, 2025. Jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada mbalimbali za Umahiri na Uzamivu.

Wahitimu wa Mahafali ya 11 ya Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) wakiwa tayari kwa ajili ya kutunukiwa shahada zao na Mkuu wa Taasisi, Mhe. Omari Issa (hayupo katika picha).

 
UDOM YAKUTANA NA WADAU KUCHAMBUA NAFASI YA AKILI UNDE KATIKA UTAWALA BORA

UDOM YAKUTANA NA WADAU KUCHAMBUA NAFASI YA AKILI UNDE KATIKA UTAWALA BORA

August 26, 2025 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kwa kushirikiana na wadau wa teknolojia na wataalamu wa utawala wamekutana leo Jijini Dodoma chuoni hapo kwenye warsha maalumu inayolenga kuchambua nafasi ya akili unde katika kuimarisha misingi ya utawala bora nchini.

Akizungumza mara baada ya kufungua warsha hiyo leo Agosti 25,2025 Naibu Makamu Mkuu Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) - Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi Prof. Razack Lokina amesema wananangazia kuhusu matumizi ya akili Hunde na namna ya kuimarisha utawala bora na kuongeza ufanisi katika utendaji wa Serikali

"Suala kubwa ni katika kungalia matumizi bora ya akili hunde namna ambavyo inaweza kusaidia katika sekta ya Afya na kilimo pamoja na kujadili changamoto zake endapo itatumika vibaya ni wapi inaweza kuharibu lakini ikitumika vizuri inaweza kuongeza ufanisi katika utendaji wa Serikali, "amesema.

Amesema suala hilo kwa wao kama wana taaluma ni muhimu kuliongelea kwasababu tayari lipo duniani na hawawezi kulikwepa kwani changamoto mbalimbali wameanza kuzuiona kutokana na baadhi kuitumia vibaya japo inaweza kuwa vizuri katika kuboresha maisha ya binadamu na kizazi kijacho.

"Huu ni wakati mwafaka wa kuweza kulijadili kwa uwazi na kuweza kuchanganua kila eneo ambalo namna gani akili Hunde inaweza ikatumika kwa ubora zaidi kuliko ambao watu wanaweza kuichukua labda wakatimia vibaya.

Kwa upande wake Msimamizi wa mradi wa Africa Artificial Intelligence Lab (AfriAI Lab), UDOM Dkt. Mohamed Mjahid amesema mradi huo ulianza mwaka 2021, ambapo katika warsha hiyo watajadili namna bora ya uwazi katika mifumo ya Serikali na sekta binafsi.

"Pia kupitia warsha hii tunajidiliana kuhusu matumizi ya akili unde ili kuweza kutoa uaminifu kwa wananchi na wadau wengine kiamini mifumo ya Serikali katika namna nyingine ya matumizi, "amesema.

Sanjari na hilo Dkt. Mjahid amesema akili unde isipotumika vizuri inaweza kuharibu mifumo mbalimbali ikiweno kudharirisha watu vitu ambavyo sio sahihi pamoja na utoaji wa taarifa zisizo sahihi.

DC UPENDO WELLA AWAASA WAZAZI KUCHANGIA CHAKULA MASHULENI

August 22, 2025 Add Comment


Na Ashrack Miraji 


Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mheshimiwa Upendo Wella, amewaasa wazazi na walezi wa Kata ya Tambukareli kuchangia fedha za chakula kwa ajili ya watoto wao mashuleni. Amesisitiza kuwa upatikanaji wa chakula shuleni ni jambo la msingi linalochangia kuboresha afya, maendeleo ya akili na ufaulu wa wanafunzi.


Mheshimiwa Wella alitoa wito huo wakati wa ziara yake katika Kata ya Tambukareli, akiwa kwenye ziara maalum ya kutembelea kata kwa kata kwa lengo la kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Wilaya ya Tabora. Alibainisha kuwa lishe bora ni msingi wa elimu bora na ni jukumu la jamii nzima kuhakikisha watoto wanapata huduma hiyo muhimu.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo, wananchi walionyesha kufurahishwa na ujio wa kiongozi huyo na walimpongeza kwa juhudi zake za dhati za kusikiliza na kushughulikia changamoto za wananchi kwa wakati. Walisema kuwa utendaji wake umekuwa wa kipekee na unaleta matumaini mapya kwa wakazi wa wilaya hiyo.

Mmoja wa wananchi, akizungumza kwa niaba ya wenzake, alieleza kuwa Mkuu huyo wa Wilaya amekuwa mkombozi wa kweli kwa watu wa Tabora. Alisema kuwa tangu Mheshimiwa Wella alipoanza kuhudumu katika wilaya hiyo, matatizo mengi ambayo yalikuwa sugu sasa yameanza kupata suluhisho.



"Tunaona tofauti kubwa. Masuala ambayo hapo awali yalikuwa hayaangaliwi kwa uzito sasa yanapewa kipaumbele. Tunamshukuru sana Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea kiongozi kama huyu ambaye ni mchapakazi na mwenye kusikiliza wananchi," alisema mwananchi huyo kwa furaha.



Mheshimiwa Wella aliwahakikishia wananchi kuwa serikali ya wilaya itaendelea kushirikiana nao bega kwa bega katika kutatua changamoto zote zinazowakabili. Alisema dhamira yake kuu ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora na kwamba maendeleo ya wilaya hiyo yanakuwa ya haraka na jumuishi.


Ziara ya Mkuu wa Wilaya inaendelea katika kata mbalimbali za Tabora, ambapo anafanya mikutano ya hadhara, kusikiliza malalamiko ya wananchi, na kutoa majibu au miongozo ya moja kwa moja ili kuhakikisha matatizo yanatatuliwa kwa wakati na kwa tija

MAENDELEO YA ELIMU NI MKOMBOZI WA TAIFA LOLOTE DUNIANI -MAJALIWA

August 06, 2025 Add Comment


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa maendeleo katika sekta ya elimu ndio mkombozi na mafanikio ya Taifa lolote duniani.

 

Amesema kwa kutambua hilo, uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan uliamua kuwekeza katika sekta hiyo ili kuhakikisha watoto wa kitanzania wanapata elimu bora katika ngazi zote.

 


Amesema hayo wakati alipozungumza na wanafunzi na walimu wa shule ya sekondari ya Wasichana ya Lucas Malia iliyopo Ruangwa mkoani Lindi, wakati wa hafla ya kuwapongeza wanafunzi wa kidato cha sita waliofanya vizuri katika mitihani ya kitaifa iliyofanyika mwaka 2025.

 

“Mliopo shuleni na mnaokuja, tambueni kuwa tuna maeneo muhimu ya kuwaelimisha, mtapata elimu iliyobora na imara itakayowapa maarufa na ujuzi ili muweze kukabiliana na changamoto mbalimbali za kijamii na kiuchumi”

 


Amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita imefanya maboresho ya mitaala kwa lengo la kukabiliana na mabadiliko ya kiuchumi yaliyopo duniani ikiwemo mahitaji makubwa ya ajira kwa vijana.

 

“Mabadiliko haya yameifanya mitaala yetu itakayofundishwa shuleni kila mwanafunzi akimaliza ana uwezo wa kutumia mazingira alimo na taaluma aliyonayo kuyabadilisha kuwa uchumi”

 

Akisoma matokeo ya kidato cha sita kwa mwaka 2025, Makamu Mkuu wa Shule Amon Chalamila hiyo amesema kuwa shule hiyo ilisajili wanafunzi 188 ambapo wote walifanya mitihani na wanafunzi 90 walipata daraja la kwanza, wanafunzi 95 walipata daraja la pili, wanafunzi watatu walipata daraja la tatu na hakuna mwanafunzi aliyepata daraja na nne na sifuri. “Ufaulu huu ni sawa na GPA ya 2.34”.

BI.SAKINA MWINYIMKUU: JENGENI UTAMADUNI WA UTENDAJI UNAOTEGEMEA MATOKEO

July 25, 2025 Add Comment


*Dodoma, Julai 25, 2025*  

Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Bi. Sakina Mwinyimkuu, amewataka watumishi wa umma kutumia maarifa waliyopata katika mafunzo ya ufuatiliaji na tathmini ili kuongeza uwajibikaji na ufanisi katika kazi zao.

Akifunga rasmi mafunzo hayo ya siku tano yaliyofanyika jijini Dodoma, Bi. Sakina amesisitiza umuhimu wa kujenga utamaduni wa kazi bora unaozingatia matokeo (results-based performance), kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

> “Mafunzo haya si kwa manufaa yenu binafsi pekee, bali yatumike kama nyenzo ya kuleta mabadiliko chanya katika taasisi zenu, sambamba na kuendeleza maadili ya uwajibikaji,” amesema Bi. Sakina.

Ametoa rai kwa washiriki kuwa mabalozi wa kueneza uelewa huo kwa wengine katika maeneo yao ya kazi, ili kuimarisha utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia viwango vya kitaifa vya ufuatiliaji na tathmini ya maendeleo.





KAMPENI YA "TUWAAMBIE KABLA HAWAJAHARIBIWA" YAENDELEA SEKONDARI ROBANDA ,SERENGETI

July 16, 2025 Add Comment

Katika mwendelezo wa kampeni ya kitaifa ya TUWAAMBIE KABLA HAWAJAHARIBIWA, Sajenti Emmanuel kutoka Jeshi la Polisi, kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto, ametembelea Shule ya Sekondari Robanda iliyopo Kijiji cha Robanda, Kata ya Ikoma, Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, na kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na wanafunzi wa kidato cha tano.


Akiwa shuleni hapo, Sajenti Emmanuel amewahimiza wanafunzi hao kujitambua na kuelekeza nguvu zao katika masomo ili kufikia malengo yao ya kitaaluma na maisha kwa ujumla, amesisitiza umuhimu wa kuepuka mahusiano ya kimapenzi wakiwa bado shuleni, akieleza kuwa vitendo hivyo vimekuwa chanzo kikuu cha kukatisha ndoto za wanafunzi wengi nchini.

Aidha, amewataka wanafunzi kuwa mstari wa mbele katika kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kutoa taarifa mapema kwa mamlaka husika, amebainisha kuwa taarifa zinaweza kutolewa katika ofisi ya Dawati la Jinsia na Watoto iliyo katika kituo cha polisi, kwa Afisa wa Ustawi wa Jamii, au kwa viongozi wa serikali ya kijiji na kata.

Kampeni hiyo inalenga kuwafikia vijana walioko mashuleni na katika jamii kwa ujumla, ikiwa ni jitihada za pamoja kati ya serikali, vyombo vya dola, na wadau wa maendeleo katika kutokomeza matukio ya ukatili wa kijinsia na kusaidia vijana kufikia ndoto zao kwa usalama.

KIKWETE NA MALALA WAONYA: BAJETI ZA ELIMU ZISIPUUZWE WAKATI WA MISUKOSUKO YA KIUCHUMI NA KISIASA DUNIANI

July 15, 2025 Add Comment

 Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai, wameonya juu ya mwenendo hatarishi duniani wa kupunguza au kupuuza bajeti za elimu hasa wakati wa misukosuko ya kiuchumi na kisiasa.


Wakizungumza kwenye mjdala kuhusu elimu uliofanyika Jumapoili usiku katika hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam, viongozi hao wawili waliwataka viongozi wa serikali, wafadhili na washirika wa maendeleo kulinda na kuendeleza uwekezaji kwenye elimu, wakisisitiza kuwa elimu ndiyo msingi wa maendeleo ya kudumu.


“Elimu haipaswi kuwa mhanga wa kwanza wakati wa janga. Si anasa—ni uhai wa maendeleo,” alisema Dkt. Kikwete. “Tukiacha kuwekeza katika elimu leo, tunajitengenezea matatizo makubwa kesho.”


Malala aliongeza kuwa madhara ya kupunguzwa kwa bajeti ya elimu huathiri zaidi wasichana. “Kila matatizo yanapotokea, wasichana ndiyo huathirika kwanza—hutolewa shule, ndoto zao hukatizwa. Hili si tu dhuluma, bali ni upumbavu wa kisera,” alisema.


Katika ziara yao katika Shule ya Sekondari Kibasila siku ya Jumatatu, Dkt. Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya GPE, alitangaza kuwa Tanzania itapokea msaada wa dola milioni 88 za Kimarekani kuanzia mwakani. 


Dkt. Kikwete alisema tangu kujiunga na GPE mwaka 2013, Tanzania imepokea zaidi ya dola milioni 344 zilizowezesha ujenzi wa zaidi ya madarasa 3,000, vyoo 7,600, nyumba za walimu 64, shule mpya 18, vituo vya walimu 252, na usambazaji wa vitabu milioni 36.


Kwa upande wake, Malala alitangaza msaada wa dola milioni 3 kutoka kwenye Malala Fund kusaidia wasichana waliokatishwa masomo kutokana na ujauzito au sababu nyingine za kijamii.


Malala pia alipongeza hatua ya serikali ya Tanzania ya mwaka 2021 ya kuruhusu wasichana waliopata ujauzito kurejea shule. 


“Uamuzi huu ulikuwa wa kishujaa na wa kibinadamu,” alisema. “Wasichana sasa wanaweza kurudi shule ndani ya miaka miwili au kujiunga na vituo vya elimu mbadala.”


Hata hivyo, wote walikiri changamoto bado zipo, na kwamba chini ya asilimia 50 ya wasichana wanaokamilisha shule ya msingi, na ni asilimia 16 pekee wanaoendelea hadi sekondari ya juu, sababu kubwa  zikiwa ni umaskini, mila kandamizi, na uhaba wa miundombinu.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh. Omary Kipanga, alieleza kuwa kupitia Mpango wa Samia Scholarship ulioanzishwa 2023, wasichana 1,320 tayari wamenufaika kwa kusomea kozi za sayansi vyuo vikuu.


“Mpango huu pamoja na sera ya re-entry ni silaha muhimu kuhakikisha wasichana hawapotei kwenye mfumo wa elimu,” alisema.


Dkt. Neema Mwakalinga, mchambuzi wa elimu, alisema ushirikiano na GPE na Malala Fund umeinua hadhi ya Tanzania kimataifa. “Sio tu fedha—ni pia ushauri wa kitaalamu, uraghibishaji, na dhamira ya kisiasa ya kweli.”

Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai wakiwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh. Omary  Kipanga, walipotembelea shule ya sekondari ya Kibasila wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam siku ya Jumatatu. 

Mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai akivishwa skafu alipowasili kutembelea  shule ya sekondari ya Kibasila wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam siku ya Jumatatu. 

Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai wakiwa katika moja ya madarasa walipotembelea shule ya sekondari ya Kibasila wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam siku ya Jumatatu. 

Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai wakiwa katika moja ya madarasa walipotembelea shule ya sekondari ya Kibasila wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam siku ya Jumatatu. 

Mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai  akiwa na baadhi ya wanafunzi wanamichezo alipotembelea  shule ya sekondari ya Kibasila wilaya ya Temeke jijini Dar es salaamsiku ya Jumatatu. 

  

Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai wakimwagilia mti baada ya Malala Kuupanda, walipotembelea shule ya sekondari ya Kibasila wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam siku ya Jumatatu. Kushoto  ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh. Omary Kipanga

Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati yeye na mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai walipotembelea shule ya sekondari ya Kibasila wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam siku ya Jumatatu. 

 Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai wakiwa katika mazungumzo ofisini kwa Rais Mstaafu siku ya Jumatatu

Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai baada ya mazungumzo ofisini kwa Rais Mstaafu siku ya Jumatatu
Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete akimpa zawadi ya kitabu cha  Global Partnership for Education (GPE)  mwanaharakati wa elimu wa kimataifa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai baada ya mazungumzo ofisini kwa Rais Mstaafu siku ya Jumatatu
 

NISHATI SAFI YA KUPIKIA NI AGENDA YA DUNIA,WIZARA INAITEKEKEZA KWA VITENDO - DKT.KAZUNGU

July 04, 2025 Add Comment


*📌Apokea Magari Mawili kutoka Umoja wa Ulaya kwa ajili ya kuanza kampeni ya kutoa elimu ya uhamasishaji wa nishati safi ya kupikia nchi nzima*


*📌 Amshukuru Dkt Samia kwa kuwa kinara wa nishati safi na kuibeba ajenda hiyo*


*📌 Umoja wa Ulaya waridhishwa na jitihada za Tanzania kwenye kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia*


*📌UNCDF yaahidi kushirikiana na Wizara kuhakikisha watanzania wanafikiwa na elimu ya nishati safi*


Naibu katibu Mkuu Wizara ya Nishati anayeshughulikia umeme na nishati Jadidifu, Dkt Khatibu Kazungu leo 04 Julai, 2025 amepokea magari mawili yatakayotumika kwa ajili ya kampeni ya kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia chini ya kampeni ya nishati safi ya kupikia Okoa Maisha na Mazingira itakayoendeshwa nchi nzima na Wizara ya nishati kwa kushirikiana na UNCDF.

‘’ Ajenda ya Nishati safi ya kupikia ni ajenda ya Dunia na sisi Wizara ya Nishati tuko tayari kwa utekelezaji ili kumuunga mkono Mhe. Rais Samia’’ Amesema Dkt. Kazungu

Aidha, ameishukuru Umoja wa Ulaya, na UNCDF kwa kutekeleza mradi wa nishati safi ya kupikia chini ya mfuko wa Cook fund kwa kuwa umesaidia kubadili maisha na mitazamo ya wananchi kuhusu  utekelezaji wa miradi ya Nishati safi.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo,  Balozi wa Umoja wa Ulaya Mhe. Balozi Christine Grau amesema umoja wa Ulaya uko tayari kuendelea kuisaidia Tanzania kwenye utekelezaji wa Nishati safi ya kupikia na tayari EU imetoa kiasi cha Euro Milioni 19.4 sawa na shilingi Bilioni 59 kutekeleza miradi ya nishati safi ya kupikia kwa mikoa ya Dar es salaam, Dodoma, Pwani, Morogoro  na Mwanza. 

Kuhusu magari amesema magari hayo mawili yana thamani ya Euro 130,000 na amewataka wizara ya Nishati kuhakikisha wananchi wa vijijini wanafikiwa na nishati safi ya kupikia

Tanzania inajipanga kutekeleza kwa vitendo mkakati wa Taifa wa Nishati safi ya kupikia chini ya mkakati wa Mawasiliano wa Taifa ili kutoa elimu kwa wananchi na kufikia lengo la Serikali la asilimia 80 ya watanzania kuanza kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.