MOROCCO AICHIMBA MKWARA OLJORO JKT.

MOROCCO AICHIMBA MKWARA OLJORO JKT.

August 10, 2013


Na Oscar Assenga, Tanga.
KOCHA Mkuu wa timu ya Coastal Union ,Hemed Morroco amesema watahakikisha wanajipanga vyema ili kuweza kuchukua pointi tatu muhimu kwenye mechi yao ya ufunguzi wa Ligi kuu Tanzania bara dhidi yao na JKT Oljoro itakayochezwa Agosti 24 katika uwanja wa Sheirh Amri Abeid mkoani Arusha.

Morroco alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na blog hii ambapo alisema mechi za majaribio walizocheza zimempa mwanga mzuri wa kujua kikosi chake kinahitaji kitu gani kabla ya kuanza msimu mpya wa ligi kuu.

Alisema kutokana na usajili mzuri ambao ulifanywa na timu hiyo matumaini yake ni kuchukua ubingwa wa ligi hiyo ili kuweza kucheza kombe la shirikisho kwani hayo ni malengo yake ya kucheza kombe hilo siku zijazo.

Morroco alisema wanatarajia kuondoka mkoani hapa siku moja kabla ya mechi yao na Oljoro JKT na kueleza watakachokwenda kukifanya mkoani Arusha ni kufuata pointi tatu muhimu.

Wakati huo huo,Timu ya 3 Pillars ya Nigeria na Coastal Union ya Tanga jana zilishindwa kutambiana baada ya kulazimishana sare ya kutokufungana katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani mjini hapa.

Mchezo huo ulianza kwa kasi ambapo kila timu ilikuwa ikilishambulia lango la mwenzie kwa zamu ambapo mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika timu hizo zilitoka nguvu sawa licha ya Coastal Union kuonekana kukosa mabao ya wazi kutokana na wachezaji wake kukosa umakini.

Wakizungumza baada ya kumalizika kwa mechi hiyo baadhi ya wadau wa soka mkoani hapa waliojitokeza walisifu kiwango kilichoonyeshwa na timu ya Coastal Union ambacho kilicheza vema licha ya kushindwa kufunga mabao.

MATUKIO YA PICHA KATIKA MECHI KATI YA COASTAL UNION NA 3PILLARS YA NIGERIA.

August 10, 2013
WACHEZAJI WA TIMU YA COASTAL UNION WAKIPASHA KABLA YA MECHI YAO NA 3 PILLARS YA NIGERIA MCHEZO WA KIRAFIKI ULIOFANYIKA UWANJA WA MKWAKWANI.

CRISPIAN ODULA AKITAFUTA NAMNA YA KUMTOKA MCHEZAJI WA 3PILLARS YA NIGERIA LEO.


UMATI WA MASHABIKI ULIOJITOKEZA KUSHUHUDIA MCHEZO HUO LEO.



KILIMANI FC NA COASTAL UNION -20 1-1.

KILIMANI FC NA COASTAL UNION -20 1-1.

August 10, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
TIMU ya Kilimani FC ya Zanzibar na Coastal Union U-20 juzi zilishindwa kutambiana baada ya kufungana bao 1-1, katika mchezo wa kirafiki uliofanyika jana kwenye uwanja wa mkwakwani mjini hapa.

Mchezo huo ulikuwa ni miongoni mwa michezo ya maandalizi kwa timu ya Kilimani FC ambayo inashiriki ligi daraja la kwanza visiwani humo kabla ya kuanza msimu mpya.

Timu hiyo ipo mkoani Tanga katika ziara ya kimichezo kwa michezo minne lengo lao likiwa ni kuimarisha undugu kwa timu watakazo cheza nazo wakiwa mkoani hapa kabla ya kuondoka kwenda Mombasa ambapo watacheza mechi nyengine za kirafiki.

Kocha wa timu Kilimani FC ,Bakari Mchunga alisema baada ya kumalizika mechi hiyo ya juzi wataelekea Duga Stars wilayani Mkinga na kuelekea Mombasa kucheza na timu ya Dunga ya Msambweni pamoja na timu ya Nzuri ya Kenya na baadae kurejea mkoani hapa kwenda Maramba wilayani Mkinga kucheza mechi moja ya kirafiki.

Kwa upande wake,Kocha wa timu ya U-20 Coastal Union,Joseph Lazaro alisema mchezo huo ulikuwa ni kukipa makali kikosi hicho ambacho kinajiandaa na msimu mpya wa mashindano ya vijana.
August 10, 2013
MWENYEKITI WA KLABU YA COASTAL UNION YA TANGA AKIIKAGUA TIMU YA KILIMANI FC YA ZANZIBAR JANA ANAYEMFUATIA NI SALIMU BAWAZIRI.



MWENYEKITI WA COASTAL UNION YA TANGA AKIIKAGUA TIMU YA COASTAL UNION U-20 JANA KABLA YA KUANZA MCHEZO HUO.
KIKOSI CHA COASTAL UNION U-20 AMBACHO JANA KILITOKA SARE NA KILIMANI FC MCHEZO ULIOCHEZWA UWANJA WA MKWAKWANI.

KIKOSI CHA KILIMANI FC YA ZANZIBAR ILIYOCHEZA NA COASTAL UNION JANA.

PICHA ZA BARAZA LA IDDI MKOA WA TANGA AMBALO LILIFANYIKA SHULE YA SEKONDARI JUMUIYA.

August 10, 2013







NUNDU:AWAASA WAISLAM MKOANI TANGA KUENDELEA KUTENDA MEMA.

August 10, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
MBUNGE wa Jimbo la Tanga, Omari Nundu amewataka waislamu mkoani kuendelea kudumisha amani iliyopo hapa nchini pamoja na kuilinda kwa kufanya mambo mema yanayompendeza mwenyezi mungu ikiwemo kuacha kufanya yale yote yaliyokatazwa.

Nundu alitoa kauli hiyo wakati akitoa hotuba yake kwenye baraza la Iddi lililofanyika ukumbi wa shule ya sekondari Jumuiya mkoani Tanga ambalo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini  akiwemo Meya wa Jiji la Tanga Omari Guledi ambapo alisema waislamu hawana budi kuendelea kutenda mema ili kuweza kupata dhawabu.

Alisema waislamu wanapaswa kuwa na tahadhari kwa kuepuka kuwa na vikundi ambavyo vinalenga kuleta chokochoko ya kidini kwenye jamii zinazowazunguka kwani kufanya hivyo kunapelekea uvunjifu wa amani badala yake waishi kwa kutii na kuheshimu sheria zilizopo hapa nchini.

Mbunge huyo alitumia nafasi hiyo kuwaasa waislamu kutilia mkazo elimu ya dunia kwa sababu ugunduzi mwingi unaotumika hivi sasa umeelemea sana kwenye maandiko yatokanayo na kuruhan hivyo kuwataka kuzingatia suala hilo kiumakini. 

  “Ndugu zangu waislamu wenzangu tumemaliza mwenye mtukufu wa ramadhani kwa amani,basi nawashauri tuendeleze sifa tulizokuwa nazo kwenye mwezi huo kwa kuacha kufanya maovu badala yake tuelekeze nguvu zetu kwenye kutenda mambo mema “Alisema Nundu.

Aidha aliwataka kuepuka mivurugano ambayo haina tija kwenye jamii zao kwa kuishi kwa amani ikiwamo kushirikiana  na watu wengine malengo yakiwa ni kutimiza nguzo kuu ya uislamu ya kufanya ibada mara kwa mara ili kuweza kuwa karibu na mwenyezi mungu.

Awali akizungumza katika baraza hilo,Sheikh wa Mkoa wa Tanga,Ally Juma Luwuchu alisisitiza suala la waislamu kuendelea kutenda mambo mema  ikiwemo kuendelea kuonyesha ustawi mzuri kwa jamii kitu kitakachopolekea kupata radhi za Mwenyezi Mungu na kujenga umoja ulio imara katika uislamu hapa nchini

Sheikh Luwuchu aliwaomba  waslam kuondoa tofauti zao za kiimani na wawe wamoja , wasikivu kwa viongozi wao  wakuu wa kidini hasa inapofikia wakati wa kupata tamko kutoka kwa viongozi hao kitu kitakachowapelekea kuonyesha umoja wetu na mshikamano katika maswala yote yanayohusu uislam.